Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, January 26, 2015

Kauli Kumi Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Mahatma Gandhi.

Mahatma Gandhi alikuwa mpigania uhuru wa nchi ya India. Aliweza kuongoza harakati za kuipatia India uhuru kutoka kwa waingereza na alikuwa akitumia njia za amani katika harakati zake.

Mahatma Gandhi amekuwa akiwahamasisha wengi sana kwa maisha aliyoishi na harakati alizofanya na jinsi alivyoleta mabadiliko makubw akwenye nchi yake na dunia kwa ujumla.

Leo hapa utazipitia kauli kumi za kukuhamasisha kutoka kwake.

1. Happiness is when what you think, what you say, and what you do are in harmony.
Furaha ni pale ambapo mawazo yako, maneno yako na matendo yako yanaendana.

2. You must be the change you wish to see in the world.
Kuwa mabadiliko unayotaka kuyaona duniani.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

3. We may stumble and fall but shall rise again; it should be enough if we did not run away from the battle.

Tunaweza kukwama na kuanguka lakini tutainuka tena; na inatosha kama hatutayakimbia mapambano.

4. It is health that is real wealth and not pieces of gold and silver.

Afya ndio utajiri wa kweli, sio sarafu na dhahabu.

5. First they ignore you, then they laugh at you, then they fight you, then you win.

Kwanza wanakudharau, kisha wanakucheka, halafu wanakupinga, mwisho unashinda.

6. I suppose leadership at one time meant muscles; but today it means getting along with people.

Kuna kipindi uongozi ulikuwa ni nguvu; ila leo uongozi ni uwezo wa kuweza kushurikiana na watu.

SOMA; Dalili Kumi Kwamba Tayari Wewe Ni Kiongozi. 

7. You can chain me, you can torture me, you can even destroy this body, but you will never imprison my mind.

Unaweza kunifunga, unaweza kuniumiza, unaweza kuharibu mwili wangu, lakini huwezi kufunga akili yangu.

8. Live as if you were to die tomorrow. Learn as if you were to live forever.

Ishi kama utakufa kesho. jifunze kama utaishi milele.

9. You must not lose faith in humanity. Humanity is an ocean; if a few drops of the ocean are dirty, the ocean does not become dirty.

Usipoteze imani kwenye ubinadamu. Ubinadamu ni bahari, kama matone machache ya bahari hii ni machafu haimaanishi bahari nzima ni chafu.

10. The best way to find yourself is to lose yourself in the service of others.

Njia bora ya kujijua ni kujipoteza kwenye kuwahudumia wengine.

Soma kauli hizo kumi na zitumie katika maisha yako na shughuli zako za kila siku ili uweze kuboresha maisha yako.

SOMA;
Vitu VITATU Vinavyoathiri Kipato Chako Na Jinsi Ya Kukiongeza.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment