Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, January 21, 2015

UKURASA WA 21; Weka Vipaumbele Kwenye Maisha Yako.

Kuna mambo mengi sana ambayo unatamani kuyafanya kwenye maisha yako, ila kwa bahati mbaya sana huwezi kuyafanya yote.

Huwezi kufanya mambo yote unayotamani kufanya kwa sababu kuu mbili;

1. Huna muda wa kuweza kuyafanya yote hayo, una masaa 24 tu kwa siku na bado una malengo ya kuyafanyia kazi.

2. Huwezi kuwa ma nguvu ya kufanya kila kitu, una mwili ambao unachoka pia hivyo huwezi kufanya kila kitu.

Njia pekee ya kutumia muda wako na nguvu zako vizuri ni kufanya yale ambayo ni muhimu kwako kufikia malengo yako, kuboresha maisha yako na kufikia mafanikio makubwa.

Ili uweze kujua ni yapi muhimu ya wewe kufanya tengeneza vipaumbele vyako na kisha vifanyie kazi.

TAMKO LA LEO;

Kuanzia leo vipaumbele vyangu ni hivi(orodhesha vipaumbele hivyo). Sitatumia muda na nguvu zangu kufanya jambo lolote ambalo halitaniletea mafanikio ninayotarajia. Nitawekeza muda, nguvu na akili zangu zote kwenye vipaumbele hivi mpka pale nitakapopata ninachotaka.

Tukutane kwenye ukurasa wa 22 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment