Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, January 18, 2015

Acha Kuifanya Hali Mbaya Kuwa Mbaya Zaidi.

Mara kwa mara kwenye maisha tunakutana na matatizo.
Baadhi ya matatizo haya yanaweza kuwa makubwa sana kiasi cha kutukatisha tamaa.
Lakini mara nyingi matatizo haya huanza kidogo na sisi wenyewe kuyafanya kuwa makubwa zaidi.
Moja ya njia tunayotumia kufanya hali mbaya kuwa mbaya zaidi ni kutumia hisia wakati unapokutana na hali mbaya.
Hisia hutufanya tuache kuangalia ukweli ni upi na kuishia kuona kwamba kwa nini sisi tunapata matatizo.
Acha sasa kutumia hisia pale unapokutana na matatizo. Tatizo lolote linapotokea, tulia na chambua tatizo hilo kwa kina kujua nini chanzo na unawezaje kulitatua.
Ila ukiingiza hisia utaona njia rahisi kwako ni kukata tamaa au hata kujiua.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment