Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, January 28, 2015

UKURASA WA 28; Kwa Nini Nisiwe Mimi…

Kama kuna watu ambao walianzia chini sana na leo wana mafanikio makubwa, kwa nini nisiwe mimi?

Kama kuna watu ambao hawakupata elimu kubwa ila wameweza kuleta mabadiliko makubwa, kwa nini nisiwe mimi?

Kama kuna watu ambao wametoka familia za kimasikini kabisa ila leo wameweza kutengeneza biashara kubwa, kwa nini nisiwe mimi?

Kama kuna watu ambao hawana viungo vyote vya mwili, ila leo wameweza kufanya mambo makubwa, kwa nini nisiwe mimi?

Kama kuna watu ambao waliweza kufungwa jela miaka mingi, ila walipotoka wakaleta mabadiliko, kwa nini nisiwe mimi?

Husemi hivi kwa sababu unawaonea wivu wale ambao wameweza kufanya makubwa, ila unawatumia wao kama chachu ya wewe kufikia mafanikio.

SOMA; Unataka Kujifunza Kitu Chochote Unachoona Ni Kigumu? Fanya Hivi...

Kuwepo kwa watu ambao wameweza kufanya makubwa licha ya kuwa na changamoto, inatudhibitishia kwamba hakuna kisichowezekana.

TAMKO LA LEO;

Kama kuna watu ambao wameanzia chini zaidi yangu, wameanza na hali mbaya zaidi yangu na wamepitia changamoto nyingi zaidi yangu ila wameweza kufikia mafanikio makubwa, ni ushahidi tosha kwamba inawezekana. Najua nikiweka juhudi na maarifa na kama sitakata tamaa lazima na mimi nitafikia mafanikio makubwa.

Tukutane kwenye ukurasa wa 29 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; USHAURI ADIMU; Usijenge Nyumba Kwenye Uwanja Wa Kukodi.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment