Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Showing posts with label NILICHOJIFUNZA LEO. Show all posts
Showing posts with label NILICHOJIFUNZA LEO. Show all posts

Tuesday, October 14, 2014

Viongozi 100 Walioibadili Dunia.

Hii hapa ni orodha ya viongozi 100 walioibadili dunia kutokana na falsafa zao na misimamo yao. Viongozi hawa wako katika kada mbalimbali ikiwemo siasa, biashara, taaluma, dini na hata wanaharakati. Unaweza kubonyeza majina yao ili kujifunza zaidi.

christ1. Jesus Christ (c.5BC – 30AD) Spiritual Teacher, central figure of Christianity.

Jefferson2. Thomas Jefferson (1743- 1826) 3rd President of US. Principle author of Declaration of Independence

Gorbachev3. Mikhail Gorbachev (1931 – ) Leader of Soviet Union. Oversaw transition from Communism in Eastern Europe.

christ4. Martin Luther King (1929 – 1968) Non-violent civil rights leader.

mandela5. Nelson Mandela (1918 – 2013) Anti-apartheid leader. First President of democratic South Africa in 1994.

buddha6. Lord Buddha (c 563 – 483BC) Spiritual Teacher and founder of Buddhism.

Churchill7. Winston Churchill (1874 – 1965) Prime Minister of Great Britain during Second World War.

Shakespeare8. William Shakespeare (1564- 1616) English poet and playwright.

Hitler9. Adolf Hitler (1889 – 1945) Dictator of Nazi Germany.

Lincoln10. Abraham Lincoln (1809 – 1865) President of US during civil war, helped end slavery.

  1. Prophet Muhammad – (570 – 632) Prophet of Islam
  2. St Paul (5 – AD 67) – Christian missionary
  3. George Washington (1732 – 1799) – 1st President of US
  4. Sri Krishna (c. BC) – Spiritual Teacher of Hinduism
  5. Emperor Constantine (272 – 337) First Roman Emperor to embrace Christianity
  6. Martin Luther (1483 – 1546) – Key figure in Protestant Reformation.
  7. Socrates (469 BC–399 BC) – Greek philosopher
  8. Karl Marx (1818 – 1883) – German philosopher, founder of Marxism
  9. Charles de Gaulle (1890- 1970) French politician.
  10. Franklin D. Roosevelt (1882 – 1945) US President 1932-1945
  11. Charles Darwin (1809 – 1882) – Developed theory of evolution
  12. Sir Isaac Newton (1642-1727) – English mathematician and scientist.
  13. Akbar (1542 – 1605) – Moghul Emperor
  14. Queen Victoria (1819 – 1901) – Queen of Great Britain during Victorian age.
  15. Konrad Adenauer (1876-1967) – German Chancellor post WWII.
  16. Jawaharlal Nehru (1889-1964) – First Indian Prime Minister
  17. Ramses II (1279 – 1213 BC) – Powerful Egyptian king.
  18. Benjamin Franklin (1706 – 1790) – US writer and polymath
  19. Confucius (551 – 479 BC) – Chinese philosopher.
  20. Alexander the Great (356 – 323 BC) – King of Macedonia.
  21. Woodrow Wilson (1856 – 1924) – President of US during WWI
  22. William Wilberforce (1759 – 1833) – Campaigner against slavery
  23. Christopher Columbus (1451 – 1506) – Italian explorer landed in America
  24. Marcus Aurelius (121 – 180) – Roman Emperor and philosopher
  25. Galileo Galilei (1564 -1642) – Astronomer and physicist
  26. Mahatma Gandhi (1869 – 1948) – Indian nationalist and politician
  27. Joan of Arc – (1412-1431) – French saint
  28. Charlemagne (742 – 814) – King of Franks and Emperor of the Romans
  29. Aristotle (384 BC – 322 BC) – Greek philosopher
  30. Mother Teresa – (1910-1997) – Nun who served the poor
  31. Saladin (1138 – 1193) – Leader of Arabs during Crusades.
  32. Simon Bolivar (1783 – 1830) – Liberator of Latin American countries
  33. Babur (1483 – 1531) – Founder of Moghul Empire
  34. Sir Walter Raleigh (1552 – 1618) – English explorer.
  35. Voltaire (1694 – 1778 – French philosopher.
  36. Samuel Johnson (1709 – 1784) – British author and creator of dictionary.
  37. Catherine the Great (1729 – 1796) – Russian Queen
  38. Mozart (1756 – 1791) – Austrian Music composer.
  39. Princess Diana (1961 – 1997) – Humanitarian
  40. Oscar Wilde (1854 – 1900) – Irish writer.
  41. Napoleon Bonaparte (1769 – 1821) – French military and political leader
  42. Beethoven (1770 1827) – German composer
  43. Benjamin Disraeli (1804 – 1881) – British Prime Minister.
  44. Leonardo da Vinci ( 1452 – 1519) – Italian scientist, artist, polymath.
  45. Louis Pasteur (1822 – 1895) – French chemish and Biologist.
  46. Leo Tolstoy (1828 – 1910) – Russian writer and philosopher
  47. Albert Einstein (1879 – 1955) – German physicist.
  48. Ataturk (1881-1938) – founder of the Turkish Republic.
  49. Pablo Picasso (1881-1973) – Spanish painter and sculptor
  50. Pope John Paul II (1920 – 2005) – Polish Pope from 1978-2005
  51. Margaret Thatcher (1925 – ) – British Prime Minister
  52. Mohammed Ali (1942 – ) American boxer
  53. Aung San Suu Kyi (1945 – ) Burmese opposition leader
  54. John F. Kennedy (1917 – 1963) – US President.
  55. Lord Nelson (1758 – 1805) – Admiral in British navy
  56. Boris Yeltsin (1931 – 2007) – Russian President
  57. Lyndon Johnson (1908 – 1973) – US President 1963-69
  58. Indira Gandhi (1917 – 1984) – Third Prime Minister of India.
  59. Eva Peron (1919 – 1952) – First Lady of Argentina
  60. William Tyndale (1494 – 1536) – Translated Bible into English
  61. Tim Berners Lee (1955 – ) Credited with founding World Wide Web
  62. Rosa Parks (1913-2005) – Civil Rights activist
  63. Benazir Bhutto (1953 – 2007) – Prime Minister of Pakistan
  64. Schubert (1797 – 1828) – Austrian Composer
  65. Kofi Annan (1938 – ) United Nations Secretary General
  66. 14th Dalai Lama (1938 – ) Spritual and political leader of Tibetans
  67. Barack Obama (1961 – ) 44th President of United States
  68. Albert Schweitzer (1875 – 1965) – Humanitarian, philosopher.
  69. Malcolm X (1925 – 1965) Black nationalist leader
  70. Lech Walesa (1943 – ) Leader of Polish solidarity movement.
  71. John M Keynes (1883 – 1946) Influential economist.
  72. Mary Wollstonecraft (1759-1797) – Feminist, author
  73. Marie Curie (1867 – 1934) – Chemist and Physicist
  74. Elvis Presley (1935 – 1977) – Rock star.
  75. Oliver Cromwell (1599 – 1658) – British Parliamentarian
  76. Oprah Winfrey (1954 – ) US media celebrity.
  77. Boudicca ( c20 – 60) – British leader against Roman rule
  78. Jesse Owens (1913-1980) US Sprinter
  79. Bill Gates (1955 – ) Founder of Microsoft
  80. Ernest Hemingway ( 1899 – 1961) US writer
  81. John Lennon (1940 – 1980) British popstar and Beatle
  82. Henry Ford (1864-1947) US Industrialist
  83. Genghis Kahn (1162 – 1227) – Leader and creator of Mongol Empire.
  84. Haile Selassie (1892 – 1975) – Ethiopian Leader
  85. George Orwell (1903 – 1950) – English author
  86. Thomas Edison (1847 – 1931) – Inventor and businessman.
  87. Dwight Eisenhower (1890 – 1969) – Supreme Allied Commander
  88. Queen Elizabeth II (1926 – ) British Queen
  89. Plato (424 – 348 BC) – philosopher.
  90. Johann Gutenberg (1395 – 1468) – Inventor of printing press.

Chanzo cha makala hii ni mtandao wa  Biography Online

Monday, October 13, 2014

Maswali Matatu Kwa Anayetaka Kuwa Mjasiriamali Kujiuliza Kutoka Kwa Richard Branson.

Richard Branson ni bilionea mwingereza ambae anamiliki makampuni ya VIRGIN. Chini ya virgin kuna makampuni karibu 400 na yote yako chini ya Richard.

branson

Richard Branson ni mmoja wa mabilionea ninaowakubali sana kwa sababu pamoja na utajiri mkubwa alionao bado anapata muda wa kuwafundisha watu wengine kupitia makala zake na vitabu vyake.

Leo nakushirikisha maswali matatu ambayo Richard anasema kila anayetaka kuwa mjasiriamali ni lazima ajiulize ili aweze kuwa na safari yenye mafanikio.

1. Je elimu ya juu ni muhimu kwangu?

Richard anasema ujiulize swali hilo kwa sababu pamoja na kwamba elimu ni muhimu bado haiwezi kuchukua nafasi ya kazi kubwa unayotakiwa kufanya unapoanza ujasiriamali. Hivyo kama unaendelea na elimu ya juu ili kupata ujuzi zaidi ni vizuri ila kama unataka kurudi shule ili kukwepa maamuzi magumu unayotakiwa kufanya kama mjasiriamali unapoteza muda wako.

2. Je napenda kuwa na bosi?

Richard anasema alianza biashara biashara akiwa mdogo sana kwa sababu hakuwahi kufikiria kufanya kazi chini ya mtu. Hivyo kama unaona huwezi kufanya kazi chini ya mtu basi ujasiriamali ndio njia yako.

3. Wanaonizunguka wanafikiriaje?

Richard anasema kama huwezi kuamua, omba ushauri kwa wale wanaokuzunguka. Wanaweza kukupa ushauri mzuri sana wa nini unaweza kufanya.

Angalizo; kwa mazingira yetu kuwa makini sana maana watu wako wa karibu wanaweza kuwa nao ni waoga kwenye ujasiriamali hivyo wakakuogopesha na wewe.

Kwa msaada zaidi tafuta mlezi (mentor) ambaye amewahi kufanya unachotaka kufanya na yeye atakuongoza.

Jiulize na kujibu maswali hayo matatu ili uweze kufikia mafanikio makubwa kwenye ujasiriamali.

Nakutakia kila la kheri.

TUKO PAMOJA.

Saturday, October 11, 2014

Hotuba ya Nyerere kuhusu Rushwa.

Katika kumbukumbu ya miaka 15 tokea kufariki kwa rais wa kwanza wa Tanzania, angalia na kusikiliza video hii ya hotuba yake kuhusu rushwa.
https://www.youtube.com/watch?v=92mpI-ablNM&feature=youtube_gdata_player

Tuesday, September 23, 2014

Watu Watatu(3) Waliofukuzwa Kwenye Kampuni Walizoanzisha Wenyewe.

Unaweza kufikiri kuingia kwenye biashara na kujiajiri mwenyewe ndio njia nzuri ya wewe kuwa na uhuru kwa kile unachofanya. Inaweza isiwe kweli kwa sababu kwa jinsi hali ya biashara za kisasa ilivyo unaweza kujikuta kwenye hali ngumu sana.

Tena pale unapofikia kampuni ikawa kubwa na kuanza kuuza hisa, wenye hisa nyingi wanaweza kufanya maamuzi hata ya kukufukuza wewe japo wewe ndiye uliyeanzisha.

Hapa ni orodha ya watu watatu ambao walifukuzwa kwenye kampuni walizoanzisha wenyewe;

1. Steve Jobs, Apple

Steve Jobs alianzisha kampuni ya apple ila baadae alifukuzwa kwenye kampuni hiyo. Alikuja kurudishwa kwenye kampuni hiyo na kuleta mapinduzi makubwa ya kiteknolojia.

2. Ted Tunner, CNN

Ted Tunner alianzisha CNN, shirika la habari la marekani lakini baadae alikuja kufukuzwa kwenye shirika hilo.

3. Jack Dorsey, Twitter

Jack Dorsey ni mmoja wa waanzilishi wa mtandao wa kijamii unaoitwa twitter ila kwa sasa anaonekana hayupo tena kwenye mtandao huo kwani ameanzisha kampuni nyingine ya teknolojia.

Kuwa makini pale unapoanzisha kampuni yako yasije kukutokea mambo ambayo hukutarajia.

Nakutakia kila la kheri.

Friday, September 19, 2014

PICHA; Nchi Zilizotawaliwa Na Uingereza Na Miaka Zilipopata Uhuru.

UK

NILICHOJIFUNZA LEO; Sababu Za Kihistoria Kwa Nini Scotland Ilitaka Kujitenga Na Uingereza.

Jana tarehe 18/09/2014 wananchi wa Scotland walipiga kura ya kuamua kama Scotland ijitenge na kuwa na mamlaka yake kamili au iendelee kuwa sehemu ya Uingereza(United Kingdoms). Matokeo ya kura hiyo yaliyotangazwa leo asubuhi yanaonesha kwamba asilimia 55.3 wamekataa kujitenga na asilimia 44.7 walipiga kura ya kutaka kujitenga. Kwa matokeo hayo Scotland inaendelea kuwa sehemu ya Uingereza.

 

Nilitaka kujifunza zaidi juu ya muungano huu wa Scotland na England.

Mwaka 1602 malkia Elizabert I wa England alifariki dunia bila ya kuacha uongozi kwa watu wa familia yake. Mfalme James I wa Scotland alikuwa msimamizi wa ncho zote mbili lakini kila nchi ilikuwa na uhuru wake.

Mwaka 1707 viongozi wa Scotland walikubali kuungana moja kwa moja na England kutengeneza United Kingdoms. Baadhi ya wananchi wa Scotland hawakufurahishwa na maamuzi haya ni hivyo yalitokea maandamano mengi kupinga muungano huo. Kwa miaka mingi baadhi ya wananchi wa Scotland wamekuwa wanajaribu kujitoa ila wanashindwa.

Mwaka 1999 Scotland waliweza kuwa na bunge lao. Uingereza waliruhusu Scotland kuweza kufanya maamuzi yao juu ya mambo kama afya, nyumba na elimu, lakini bajeti walipangiwa na Uingereza.

Bado wananchi wengi wa Scotland hawakufurahishwa na hili na hivyo manunguniko ya chini chini yalikuwa yakiendelea. Chama cha upinzani kiliposhika nafasi ya kuongoza bunge la Scotland viongozi wake walipendekeza ipingwe kura ya kuamua kuendelea kuwepo chini ya Uingereza au kujitegemea wenyewe.

Haya yote ndiyo yaliyopelekea kwenye kura iliyofanyika jana. Na kama tulivyoona kwenye matokeo asilimia 44 ya wanaotaka kujitenga sio ndogo na hivyo huenda chokochoko zikaendelea.

Tunaweza kujifunza nini hapa kwenye muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar? Karibu kwa maoni.

Monday, September 8, 2014

NILICHOJIFUNZA LEO; Viongozi Mashuhuri Walioibadili Dunia.

Karibu kwenye kipengele hiki cha mambo niliyojifunza kwa siku husika. Kwa siku zinazokuja nitakuwa nakushirikisha yale ninayojifunza kuhusu uongozi kupitia kitabu WORLD FAMOUS LEADERS WHO RESHAPED THE WORLD.

Hiki ni kitabu kilichoeleza kwa kifupi baadhi ya viongozi ambao walifanya mambo makubwa duniani. Unaweza kujipatia kitabu hiki na ukaendelea kujifunza zaidi. Kava lake naweka kwenye picha hapo chini;

viongozi

Viongozi hawa kuna waliofanya makubwa kwa wema kama Nelson Mandela na wengineo na kuna waliofanya makubwa kwa ubaya kama Adolf Hitler aliyesababisha vifo vya zaidi ya wayahudi milioni sita.

Kuna mengi ya kujifunza kupitia maisha na uongozi wa watu hawa.

Nakukaribisha katika safari hii ya kujifunza.

TUKO PAMOJA.

NILICHOJIFUNZA LEO; Viongozi Mashuhuri Walioibadili Dunia.

Karibu kwenye kipengele hiki cha mambo niliyojifunza kwa siku husika. Kwa siku zinazokuja nitakuwa nakushirikisha yale ninayojifunza kuhusu uongozi kupitia kitabu WORLD FAMOUS LEADERS WHO RESHAPED THE WORLD.

Hiki ni kitabu kilichoeleza kwa kifupi baadhi ya viongozi ambao walifanya mambo makubwa duniani. Unaweza kujipatia kitabu hiki na ukaendelea kujifunza zaidi. Kava lake naweka kwenye picha hapo chini;

viongozi

Viongozi hawa kuna waliofanya makubwa kwa wema kama Nelson Mandela na wengineo na kuna waliofanya makubwa kwa ubaya kama Adolf Hitler aliyesababisha vifo vya zaidi ya wayahudi milioni sita.

Kuna mengi ya kujifunza kupitia maisha na uongozi wa watu hawa.

Nakukaribisha katika safari hii ya kujifunza.

TUKO PAMOJA.

Tuesday, September 2, 2014

NILICHOJIFUNZA LEO; Vita Kubwa Kuwahi Kutokea Afrika Ukiacha Vita Vya Pili Vya Dunia.

Ukiacha vita vya pili vya dunia vita kubwa ambayo imewahi kutokea Afrika ni vita ya pili ya Congo(Second Congo War)
Vita hii ilianza August 1998 na kutangazwa kumalizika July 2003 baada ya serikali ya mpito kushika madaraka.
congo war
Pamoja na kutangazwa kumalizika kwa vita hii bado mapigano na choko choko zinaendelea katika majimbo ya Kivu na Ituri.
Ni katika vita hii ambapo raisi wa Congo Laurent Kabila aliuawa na mtoto wake Joseph Kabila kushika madaraka ya kuongoza nchi.
Vita hii ilihusisha mataifa tisa ya Afrika na vikundi zaidi ya 20 vya wapiganaji.

Sababu ya vita hii.

Sababu kubwa iliyochangia vita hii ni mgogoro wa kimaslahi katika uchimbaji na biashara ya madini.

Madhara ya vita hii.

Vita hii ndio vita kubwa zaidi kutokea barani Afrika ukiacha vita vya pili vya dunia. Mpaka kufika mwaka 2008 zaidi ya watu milioni 5.4 walikuwa wamepoteza maisha kutokana na vita hii. Vifo vingi vilitokana na mauaji ya kuvita, huduma mbovu za afya na ukosefu wa chakula.
Kuna mengi sana ya kujifunza katika vita hii. Kwa kifupi nimeweza kukuandalia haya kwa leo.
Tukutane tena wakati mwingine. Usisahau kuweka email yako ili upate makala hizi moja kwa moja.

Vyanzo;

WIKIPEDIA; Second Congo War.

NILICHOJIFUNZA LEO; Vita Kubwa Kuwahi Kutokea Afrika Ukiacha Vita Vya Pili Vya Dunia.

Ukiacha vita vya pili vya dunia vita kubwa ambayo imewahi kutokea Afrika ni vita ya pili ya Congo(Second Congo War)
Vita hii ilianza August 1998 na kutangazwa kumalizika July 2003 baada ya serikali ya mpito kushika madaraka.
congo war
Pamoja na kutangazwa kumalizika kwa vita hii bado mapigano na choko choko zinaendelea katika majimbo ya Kivu na Ituri.
Ni katika vita hii ambapo raisi wa Congo Laurent Kabila aliuawa na mtoto wake Joseph Kabila kushika madaraka ya kuongoza nchi.
Vita hii ilihusisha mataifa tisa ya Afrika na vikundi zaidi ya 20 vya wapiganaji.

Sababu ya vita hii.

Sababu kubwa iliyochangia vita hii ni mgogoro wa kimaslahi katika uchimbaji na biashara ya madini.

Madhara ya vita hii.

Vita hii ndio vita kubwa zaidi kutokea barani Afrika ukiacha vita vya pili vya dunia. Mpaka kufika mwaka 2008 zaidi ya watu milioni 5.4 walikuwa wamepoteza maisha kutokana na vita hii. Vifo vingi vilitokana na mauaji ya kuvita, huduma mbovu za afya na ukosefu wa chakula.
Kuna mengi sana ya kujifunza katika vita hii. Kwa kifupi nimeweza kukuandalia haya kwa leo.
Tukutane tena wakati mwingine. Usisahau kuweka email yako ili upate makala hizi moja kwa moja.

Vyanzo;

WIKIPEDIA; Second Congo War.

Nilichojifunza Leo.

Nilichojifunza Leo ni kipengele kipya kitakachokuwa kinakujia mara kwa mara kupitia blog hii Makirita Amani. Ningependa kipengele hiki kiwe kinakujia kila siku ila siwezi kuahidi hilo kwa sasa.
Kupitia kipengele hiki utajifunza mambo mengi kuhusiana na UONGOZI, SIASA, UCHUMI, MAENDELEO na hata HISTORIA za nchi yetu Tanzania, bara letu Afrika na hata Dunia kwa ujumla.
Tutajifunza mambo mengi yatakayotusaidia kuelewa zaidi nchi yetu na dunia kwa ujumla wakati tunajiandaa kuwa viongozi bora wa nchi yetu.
Kupitia kipengele hiki mimi na wewe tutajifunza mambo yatakayotuandaa kuweza kuisaidia nchi yetu, wakati huo mimi naendelea kujiandaa kuwa raisi wa nchi yetu Tanzania.
Karibu sana katika blog hii maalumu kwa maswala ya uongozi na kuhakikisha hukosi machapisho yanayowekwa, weka email yako kwenye box hapo juu na utapokea makala moja kwa moja kwenye email yako kila zinapowekwa.
Naamini tutaendelea kuwa pamoja kwenye safari hii.
Nakutakia kila la kheri.

Nilichojifunza Leo.

Nilichojifunza Leo ni kipengele kipya kitakachokuwa kinakujia mara kwa mara kupitia blog hii Makirita Amani. Ningependa kipengele hiki kiwe kinakujia kila siku ila siwezi kuahidi hilo kwa sasa.
Kupitia kipengele hiki utajifunza mambo mengi kuhusiana na UONGOZI, SIASA, UCHUMI, MAENDELEO na hata HISTORIA za nchi yetu Tanzania, bara letu Afrika na hata Dunia kwa ujumla.
Tutajifunza mambo mengi yatakayotusaidia kuelewa zaidi nchi yetu na dunia kwa ujumla wakati tunajiandaa kuwa viongozi bora wa nchi yetu.
Kupitia kipengele hiki mimi na wewe tutajifunza mambo yatakayotuandaa kuweza kuisaidia nchi yetu, wakati huo mimi naendelea kujiandaa kuwa raisi wa nchi yetu Tanzania.
Karibu sana katika blog hii maalumu kwa maswala ya uongozi na kuhakikisha hukosi machapisho yanayowekwa, weka email yako kwenye box hapo juu na utapokea makala moja kwa moja kwenye email yako kila zinapowekwa.
Naamini tutaendelea kuwa pamoja kwenye safari hii.
Nakutakia kila la kheri.