Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, July 13, 2015

UKURASA WA 194; Utaanza kuona fursa nzuri pale utakapofanya hivi.

Hivi ulishawahi kununua nguo ambayo uliona ni nzuri na ya kipekee ila kila ulipopita mtaani ukaanza kuona karibu kila mtu anayo?
Au labda unafikiria kununua kitu fulani mfano gari au vifaa, mara ghafla ukiwasha tv unaona kitu kile, ukipita mtaani unaona kitu kile?
Au umewahi kufikiria kufanya biashara fulani mara ghafla ukaanza kuona kila unapopita unaona watu wanafanya biashara ile?
Je unafikiri vitu hivyo nimeanza kutoke kwa sababu wewe unafikiria kufanya? Jibu ni hapana, vitu hivyo vilikuwepo kila siku, ila kwa sababu hujawahi kuvifikiria na kuvizingatia basi umekuwa huvioni. Ila unapoanza kuvifikiria au kuvizingatia sana macho yako yanafunguka na unaanza kuona vizuri zaidi.
SOMA; Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha Huponi.
Kuna fursa nyingi sana ambazo zinakuzunguka hapo ulipo. Ila kwa sasa huzioni kwa sababu hujazingatia kuzifikiria. Anza kufikiria kitu fulani na utaanza kuona kwamba kuna njia nyingi sana za kuweza kukipata au kukifanya kitu hiko?
Unataka kuona fursa zaidi? Fungua akili yako, fungua mawazo yako na macho yako yataanza kuona.
TAMKO LA LEO;
Najua nimekuwa sioni fursa nyingi kwa sababu macho yangu hayajafunguliwa kuona. Nitayafungua sasa macho yangu kwa kuzingatia vitu ninavyotaka, kuviweka kwenye akili yangu na macho yangu yatanionesha njia za kufanya au kupata vitu hivyo.
Tukutane kwenye ukurasa wa 195 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment