Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, July 17, 2015

Tangazo muhimu kuhusiana na blog zinazoendeshwa na AMKA CONSULTANTS.

Habari za leo mpenzi msomaji wa blog mbalimbali zinazoendeshwa na AMKA CONSULTANTS. Naamini unaendelea vizuri na harakati zako za kuboresha maisha yako. Na pia naamini TUPO PAMOJA ukiendelea kujifunza na kuhamasika kupitia makala mbalimbali zinazopatikana kwenye blog zako zinazoendeshwa na AMKA CONSULTANTS.
Kama unavyojua lengo kubwa la AMKA CONSULTANTS ni kukuwezesha wewe kuishi maisha bora sawa sawa na uwezo wako. Hapo ulipo una uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo makubwa zaidi ya unavyofanya sasa. Ila mfumo wa elimu uliopitia na malezi uliyokulia vimekufanya ushindwe kufikia uwezo wako mkubwa.
Kama umekuwa unafuatilia blog zetu mbali mbali na ukawa unafanyia kazi yale ambayo umekuwa unajifunza, utakubaliana nami kwamba maisha yako umeona yanabadilika, hata kama ni kwa kiasi kidogo. Kama hiki ndio kinachotokea kwenye maisha yako basi nakusihi endelea kufanyia kazi na utazidi kuona mabadiliko makubwa zaidi.
AMKA CONSULTANTS ilianza na blog ya AMKA MTANZANIA na baadae zilianzishwa blog nyingine kutokana na mahitaji tofauti ya wasomaji wetu. Blog hizo ni KISIMA CHA MAARIFA, ambayo unalipia kuwa mwanachama, MAKIRITA AMANI na JIONGEZE UFAHAMU.
Kupitia blog hizi umekuwa unajifunza mambo mengi na mazuri sana. Kwa sababu makala zinazowekwa kwenye blog hizi zinatofautiana na zinalenga maeneo tofauti tofauti ya maisha yako ikiwemo kazi, biashara na hata maisha kwa ujumla.
Napenda kuchukua nafasi hii kuwajulisha wasomaji wote kwamba kutakuwa na mabadiliko kwenye blog hizi zinazoendeshwa na AMKA CONSULTSNTS. Makala ambazo zilikuwa zinawekwa kwenye JIONGEZE UFAHAMU sasa zitahamishiwa kwenye AMKA MTANZANIA na makala zilizokuwa zinawekwa kwenye MAKIRITA AMANI sasa zitahamishiwa kwenye KISIMA CHA MAARIFA. Na blog hizi mbili, MAKIRITA AMANI na JIONGEZE UFAHAMU zitafutwa.
Kwa nini mabadiliko haya?
Kama umekuwa msomaji mzuri wa blog hizi utakuwa uliona tatizo ambalo lilijitokeza kama mwezi mmoja uliopita. Wasomaji ambao walikuwa wanapokea makala za blog moja wapo kwa email ghafla waliacha kupata makala. Wakati huo makala zilikuwa zinatumwa kama kawaida. Kutokana na tatizo hili ilibidi kutafuta suluhisho la haraka ili wasomaji waendelee kupata makala zetu nzuri. Tulipata suluhisho la muda lakini halitadumu kwa muda mrefu, siku zio nyingi tutaingia tena kwenye tatizo kama lile. Na hii inatokana na sababu ya pili ya kuondoka kwenye blog hizi ambayo ni kuwa zimekuwa zinaendeshwa bure.
Blog inapokuwa imehifadhiwa bure na kutumia jina la bure, kuna baadhi ya vitu huwezi kuvibadili. Sasa hili linakwenda tofauti na kile ambacho nataka wewe msomaji ukipate. Kuna wakati nataka kufanya kitu ambacho ni cha tofauti lakini nashindwa kwa sababu blog imehifadhiwa bure na hivyo huwezi kubadili baadhi ya vitu.
Sababu nyingine ni kwamba nina sehemu kubwa ya kuhifadhi blog hizi ambayo ninailipia kila mwaka ambayo kwa sasa imehifadhi KISIMA CHA MAARIFA, sasa ni vyema kutumia sehemu hii ambayo tunailipia gharama kubwa kuweka mafunzo ambayo yataendelea kuboresha maisha yako.
Na sababu ya mwisho tunayoweza kujadili hapa ambayo imepelekea kufanya mabadiliko haya ni wewe msomaji uweze kupata makala zote nzuri kwenye blog chache. Ni kweli kuna umuhimu wa kutenganisha mambo lakini ni vyema wewe kama msomaji ukijua unapata makala zako zote nzuri kwenye sehemu chache ambazo unaweza kuzitembelea kila siku na kutumia muda wao vizuri.
KISIMA CHA MAARIFA ni kulipia, je sisi tuliokuwa tunapata makala bure ndio mwisho?
Ni kweli kabisa ili uweze kusoma makala kwenye KISIMA CHA MAARIFA inabidi uwe umejiunga na ulipie. Ila kwa sasa kwa kipengele hiki cha KURASA 365 ZA MWAKA 2015 wasomaji wote wataendelea kuzipata hata kama hawajajiunga na kulipia. Ila nakusihi sana kama bado hujajiunga na KISIMA CHA MAARIFA ufanye hivyo mara moja kwani unakosa mengi na utaendelea kukosa mengi. Bonyeza maandishi haya KUJIUNGA NA KISIMA CHA MAARIFA. Kuendelea kupata makala za KURASA 365 hakikisha unatembelea KISIMA CHA MAARIFA kila siku, na pia jiunge kwa kuweka email yako unapokuw akwneye KISIMA na utatarifiwa kila makala inapokwenda hewani.
Asante sana kwa kuendelea kujifunza na kufanyia kazi yale ambayo yanawekwa kwenye mitandao hii. Tunaendelea kukuahidi kwamba tutakuletea makala bora kabisa zitakazo boresha na kubadili maisha yako.
TUPO PAMOJA.
Makirita Amani,
makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment