Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, July 12, 2015

UKURASA WA 193; Ushabiki Unavyokuzuia Kufikia Mafanikio.

Ushabiki umekuwa kikwazo kwa watu wengi sana kuweza kufikia mafanikio makubwa. Watu wamekuwa wakijikuta wanalazimika kuacha mambo yao ya msingi kwa sababu hataki kupitwa na kitu ambacho anashabikia.
Kuna watu ambao ni mashabiki wa mpira kiasi kamba hawezi kuacha kuangalia timu yake inacheza hata kama kutakuwa na kitu gani anachofanya. Kuna wengine ni mashabiki wa muziki, mashabiki wa tamthilia, mashabiki wa matamasha mbalimbali na pia mashabiki wa siasa.
Sina tatizo na wewe kuwa shabiki, ila kama kweli lengo lako ni kuwa na maisha bora na yenye mafanikio basi unatakiwa kufikiria mara mbili kuhusu ushabiki wako.
Fikiria kile unachoshabikia na jiulize, je kinakuongezea maarifa? Je kinakuongezea kipato? Je kinafanya maisha yako na ya wengine kuwa bora zaidi/ kama jibu ni hapana basi ushabiki huo usiwe kipaumbele kwenye maisha yako.
SOMA; Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha Huponi.
Mimi nilikuwa mshabiki wa tamthilia mpaka siku moja mtu akaniambia(kupitia kitabu nilichokuwa nasoma), unapoangalia tv, kuna mambo mawili yanatokea. Yule unayemwona kwenye kioo cha tv analipwa kwa wewe kumwangalia na wewe unalipa kumwangalia mtu huyo. Je unataka kuwa upande upi? Kulipa uangalie maisha ya wengine au kulipwa kwa watu kuangalia maisha yako? Kuanzia hapa nilikata shauri la kutoangalia tamthilia tena, sijaziangalia tangu mwaka 2012 na hakuna nilichokosa zaidi ya maisha yangu kuwa bora zaidi.
Achana na ushabiki ambao hautaboresha maisha yako na anza leo kuwa shabiki wako mwenyewe. Mimi ni shabiki namba moja wa Makirita Amani, huwa sikosi chochote alichopanga kufanya na nitaahirisha vingine vyote ili kuhakikisha namshabikia. Je shabiki wako namba moja ni nani?
Una muda mfupi sana kuanza kuugawa kwa kushabikia vitu ambavyo havina msaada mkubwa kwenye maisha yako, hasa ambavyo unaweza kuvipata baadae. Kwa mfano kama unashabikia timu ya mpira, badala ya kukesha ukiangalia mpira na kesho yake ukashindwa kufanya kazi zako vizuri kwa nini usilale mapema na kesho yake utayajua tu matokeo? Hakuna tofauti yoyote kuona magoli mawili yakifungwa na kuja kuyaona kesho yake. Tena siku hizi mipira inarekodiwa kwa hiyo unaweza kuangalia kwa muda wako.
Narudia tena, usikubali ushabiki uharibu ratiba zako, una mengi yakufanya, yape kipaumbele.
TAMKO LA LEO;
Najua ushabiki wangu umekuwa unanifanya nishindwe kufikia mafanikio makubwa. Nimekuwa nashabikia mambo mengi sana. Nimekuwa naahirisha mipango yangu kwa sababu tu nisipitwe na ushabiki. Leo naamua kwamba mtu wa kwanza kumshabikia ni mimi mwenyewe. Sitakatisha ratiba zangu kwa sababu kuna kitu nakishabikia. Nitaendelea na mipango yangu na ninajua nitafahamishwa kila kinachoendelea.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment