Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Showing posts with label UONGOZI. Show all posts
Showing posts with label UONGOZI. Show all posts

Tuesday, May 5, 2015

Kilichotokea Afrika Kusini Na Somo Kubwa La Sisi Watanzania Kujifunza.

Siku za hivi karibuni kumetokea machafuko nchini Afrika Kusini yaliyosababishwa na wananchi ambao ni wazawa wa nchi hiyo, kuwavamia na kuwafukuza wananchi ambao ni raia wa nchi nyingine. Machafuko hayo sio ya kwanza kutokea kwa Afrika Kusini na hata kwa Afrika kwa ujumla. Kumekuwepo na maandamano na machafuko ya aina hii tangu nchi hizi zimepata uhuru.

Leo nataka tujifunze kitu kutokana na machafuko ya aina hii na ni kitu gani tunaweza kufanya sisi Watanzania ili tusijikute kwenye hali kama hizo. Sitaangalia sana upande wa kisiasa kwa sababu lengo la andiko langu hili na kama yalivyo maandiko yangu mengine ni kuangalia hatua gani mimi na wewe tunachukua ili tusijikute kwenye hali ambazo hatuzipendi. Sio kulaumu wala kulalamika, bali kuchukua hatua.

Sababu halisi ya ubaguzi wa kiraia(xenophobia).

Kuna sababu nyingi sana ambazo zinaelezwa kusababisha machafuko ya aina hii. Lakini kuna sababu moja kubwa sana ambayo inabeba sababu nyingine zote. Sababu hiyo ni hali ngumu ya maisha na ukosefu wa ajira.

Kadiri siku zinavyozidi kwenda hali ya maisha inakuwa ngumu sana. Jamii inagawanyika kwenye makundi mawili, kundi moja dogo la wenye hali nzuri na kundi jingine kubwa ambalo linaendelea kukua kila siku la watu wenye maisha magumu sana. Hawa wenye maisha magumu mambo yao yanazidi kuwa magumu kutokana na tatizo la ukosefu wa ajira ambalo linasumbua dunia nzima kwa sasa.

Katika hali kama hii wananchi wazawa, wenye hali ngumu na ambao mara nyingi wanaitegemea serikali itatue matatizo yao, wanaendelea kuweka matumaini yao kwa serikali. Lakini wananchi ambao sio wazawa, ambao wanajua serikali haipo kwa ajili yao wanaweka juhudi, wanafanya kazi za ajabu na hatimaye maisha yao yanakuwa bora kuliko ya wale wazawa. Sasa kadiri siku zinavyokwenda, hawa wageni wanaendelea kuweka juhudi na maisha yao yanakuwa bora, huku wazawa wakiendelea kuilalamikia serikali ifanye jambo.

SOMA; ONDOKA NYUMBANI

Unafika wakati sasa wazawa wanazidi kuwa na hali ngumu na wakiangalia wageni wana hali nzuri, hapa ndipo wanageuka na kuona kumbe adui yao ni mgeni. Kwa nini kwenye nchi yao wenyewe wawe na maisha magumu wakati kuna wageni ambao wanaishi kwa starehe. Hiki ni kitu ambacho kinawaumiza na kushinda kujizuia hivyo kuona suluhisho pekee ni kutumia wingi wao kuwaondoa hawa wageni.

Kwa akili za haraka wazawa watakubaliana wanachofanya ni sahihi, ila unapokuja kufikiri kwa kina unaona jinsi gani wazawa wanajipoteza na kumuacha adui halisi kwa kugombana na mtu ambaye sio hata adui.

Watanzania tunajifunza nini katika hili?

Yalipotokea machafuko haya Afrika Kusini, watanzania tulilipuka sana kulaani matendo yale. Kila mtu aliongea kwa uchungu ni jinsi gani kitendo walichofanya waafrika kusini kilikuwa cha kinyama. Ila baada ya hapo kila mtu aliendelea na mambo yake. Sina hakika sana kama kuna somo lolote ambalo tulijifunza kama taifa ili na sisi tusiingie kwenye hali kama ile. Na kwa kutojifunza chochote tunajiweka kwenye hatari kubwa ya kuja kurudia makosa ambayo wenzetu wameyafanya.

Kwa ufupi sana naomba nikushirikishe mambo ambayo watanzania tunapaswa kujifunza kwenye machafuko yaliyotokea Afrika Kusini.

1. Uzawa hautakubeba, juhudi ndio zitakubeba.

Kuna wakati ambapo tunafikiri kwamba sisi tunastahili zaidi kwa sababu ni wazawa. Ndio ni kweli, wewe wa nyumbani unastahili kupewa kipaumbele. Lakini kabla ya kupewa kipaumbele umeonesha nini. Hautabebwa kwa sababu wewe ni mzawa, utabebwa kwa sababu wewe unakitu muhimu kinachotakiwa. Tunaona makampuni mengi yanakwenda kuwekeza Lindi na Mtwara kwa sababu kuna gesi. Kampuni haitakupa wewe kazi kWa sababu tu ni mzawa, itakupa wewe kazi kwa sababu unazo sifa za kufanya kazi husika, Na hata kama kazi haihitaji sifa, basi unaonesha juhudi kwenye kazi unayopewa.

Hakuna kampuni inayopenda kuajiri raia wa kutoka nchi nyingine, kama ingeweza kupata wazawa wenye uwezo wa kufanya kazi husika. Ni gharama zaidi kuajiri raia wa nje kuliko raia wazawa.

Watanzania tujiandae sana kwa hili. Tumekuwa tunaona mambo machache ambayo sasa hivi bado hayajatuumiza ila kama hatutachukua hatua itakuwa tatizo baadae. Kwa mfano walimu wa shule nyingi za chekechea na msingi zinazoendeshwa kwa mchepuo wa wa kiingereza ni wakenya na waganda. Na wengi wao hata hawana taaluma ya ualimu, ila wanaweza kuongea kingereza kilichonyooka na cha kujiamini hata kama wanakosea. Sasa mchukue mhitimu wa chuo wa Tanzania mwambie aongee kingereza mfululizo kwa nusu saa kama hatakuwa bubu. Asilimia kubwa hawawezi hivyo, sasa mtu anayeteka kuwafundisha watoto kiingereza unataka akuajiri wewe kwa sababu tu ni mzawa na wakati huwezi kuongea kiingereza?

Hata tukija kwenye kazi ambazo hazihitaji elimu, bado watanzania sio watu wa kujituma na kuweka juhudi. Ukienda kwenye hoteli kubwa ukikuta wahudumu wa tanzania na wa nchi nyingine utaiona tofauti kabisa. Tunahitaji kuamka watanzania na tuanze kuweka juhudi na tujenge sifa zitakazotuwezesha kupewa upendeleo.

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

2. Dunia inakuwa kijiji, ondoka kwenye zama za mawe.

Ni jambo la kushangaza kama utafurahia kuvaa nguo iliyotengenezwa china, simu iliyotengenezwa china, mswaki uliotengenezwa kenya, chakula kilichoandaliwa ulaya na mengine mengi halafu ukahubiri uafrika kwanza, Utanzania kwanza. Haya mambo yanakufa, mawasiliano yamerahisisha sana biashara na muingiliano wa watu wa nchi mbalimbali. Hatuwezi kutumia nguvu kupinga hili, ila tunatakiwa kujiandaa na kuwa vizuri ili tuweze kupambana.

Kila siku Tanzania tunalaumiwa kukwamisha muungano wa Afrika Mashariki kwa sababu tunasema wananchi hawajawa tayari bado. Sasa sijui tutakuwa tayari lini. Na sisi wenyewe tunajitamba kwamba majirani wanatuonea wivu ndio maana wanakazana tuungane. Sawa, tunawakatalia wakenya na warwanda, huku wachina wakijazana kwenye nchi. Tunahitaji kuona kwamba dunia inakwenda haraka sana, hatuwezi kujifungia hapa tukifanya mambo yetu kwenye zama za mawe na kufikiri tutaweza kwenda na kasi ya dunia. Tutaachwa nyuma tu.

3. Tujue chanzo halisi cha matatizo yetu.

Kwa kutojua chanzo halisi cha matatizo yetu, umasikini wetu, utafika wakati tutaona kila tajiri ni adui yetu. Tutaanza kuwapiga matajiri na wakiisha tutageukiana wenyewe. Tatizo sio mchina aliyekuja hapa kufanya biashara, tatizo sio mkenya anayepata kazi wakati wewe hupati, tatizo linaanzia kwako.

SOMA; Katika Kula Ujana Usifanye Mambo Haya Matano, Utajutia Maisha Yako Yote.

4. Tusitegemee serikali ndio itatutoa hapa tulipo.

Ndio nakubali serikali ina nafasi yake ya kuweka sera bora kwenye nchi ambazo zitawawezesha wanachi kunufaika na rasilimali zinazowazunguka. Ila linabaki kuwa jukumu lako kuchangamkia fursa za kuweza kutumi rasilimali hizo. Katika utawala wa Mwl J K Nyerere waliona hawawezi kuyachimba madini kwa sababu hatukuwa na wataalamu wa kutosha. Ikapita miaka zaidi ya 30 na baadae ikaja sera ya uwekezaji. Migodi ikabinafsishwa kwa wageni, bado hatukuwa na wataalamu wa kutosha na hata leo hii miaka 54 baada ya uhuru bado hatuna wataalamu wa kutosha hasa kwenye sekta hii mpya ya gesi. Ndio unaweza kuilaumu serikali sana, lakini mwisho wa siku swali linarudi kwako, ni jitihada gani ambazo umefanya za kukuwezesha na wewe ukanufaika na rasilimali hizi. Ardhi sasa hivi inaonekana ipo na ya kutosha tu, hakuna anayeweka juhudi kubwa za kuitumia, kuna wajanja wameanza kuinunua kwa kasi, hakuna anayeona. Baada ya muda ardhi nyingi itakuwa mikononi mwa wachache na masikini watakuwa hawana hata kasehemu ka kulima mazao ya chakula, hapa ndio matatizo yatakapoanzia.

Naomba niishie hapa kwa leo, lakini tukubaliane ya kwamba sisi watanzania tunayo kazi kubwa ya kufanya ili tusijekuingia kwenye machafuko yatakayosababiswa na wachache kuwa na hali nzuri huku wengi wakiteseka. Sisi wananchi ndio tuna nguvu hiyo, tuhamasishane, tuelimishane na tuweke serikali ambayo itatuwezesha sisi kwa kutumia juhudi zetu kuwa sehemu ya neema ya nchi hii. Na sio kutegemea kupendelewa kwa sababu tu sisi ni wazawa.

Nakutakia kila la kheri mwananchi mwenzangu.

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Thursday, January 1, 2015

Salamu Za Mwaka Mpya Kutoka Kwa Rais Wa Tanzania Mwaka 2040.

Napenda kuchukua nafasi hii ya kipekee kuwatakia watanzania wenzangu wote kheri na hongera ya kuuona mwaka 2015. Sio watu wote walioanza mwaka 2014 wamepata nafasi ya kuuona mwaka 2015, hivyo ni jambo la kushukuru kwa nafasi hii ya kipekee.

Mwaka 2014 huenda ulikuwa mwaka uliokuwezesha kufanikisha mengi na pia kushindwa mengi. Kikubwa cha kuchukua 2014 na kukileta mwaka 2015 na yale uliyojifunza. Katika kila jambo ulilofanikiwa kuna vitu umejifunza na katika kila jambo uliloshindwa kuna vitu vingi umejifunza. Tumia yote uliyojifunza ili mwaka 2015 uwe bora zaidi kwako.

Kama mwaka 2014 kuna vitu ulipanga kufanikisha ukashindwa, hii ina maana kwamba kuna vitu unafanya kwa makosa au kuna vitu hufanyi kabisa. Hivyo kuendelea hivyo hivyo kwa mwaka 2015 utapata majibu yale yale uliyopata mwaka 2014. Kumbuka ujinga ni kufanya jambo lile lile kwa njia ile ile na kutegemea majibu tofauti. Haiwezekani na utazidi kupoteza muda wako.

Mwaka huu 2015 ni mwaka ambao utakuwa na matukio mengi na makubwa kitaifa. Matukio haya mengi yatakuwa chachu muhimu katika maendeleo ya nchi yetu. Mambo mawili makubwa kabisa yatakuwa;

1. Kupigia kura katiba pendekezwa. Sote tunajua katiba ilivyo muhimu kwenye taifa lolote, hivyo tukio la kupigia kura katiba iliyopendekezwa ni tukio muhimu sana.

2. Uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani. Mwaka huu tutapata nafasi ya kuchagua viongozi watakaofanya maamuzi kwa niaba yetu kwa miaka mitano ijayo. Hivyo ni jambo linalohitaji umakini wetu ili tusijekupata viongozi ambao watafanya taifa likose uelekeo.

Matukio haya mawili na mengine yatakayotokea mwaka huu 2015 yameshika hisia za wananchi wengi. Wananchi wengi tunaamini mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yetu yatatokea baada ya kupata katiba mpya na kufanya uchaguzi mkuu. Natoa tahadhari kwamba tusitegemee sana hili, mabadiliko ya kweli yanaanzia ndani yako wewe mwananchi. Kila mwananchi anatakiwa kubadilika ndio taifa liweze kubadilika. Kila mwananchi anatakiwa kupata maendeleo ndio taifa lipate maendeleo. Na kwa bahati mbaya sana sehemu kubwa ya mabadiliko ya nchi haitokani na kile serikali inachofanya, bali kile ambacho kila mwananchi anafanya.

Kitu kingine kikubwa ninachopenda kukigusia kwenye salamu hizi za mwaka mpya ni matatizo mawili makubwa yanayoturudisha nyuma kama taifa. Matatizo haya yamekuwa ndio chanzo cha uzembe na ufisadi mkubwa unaoendelea kwenye nchi hii kwa sasa. Matatizo hayo ni;

1. Kutokufanya kazi kwa bidii na maarifa. Najua watanzania tunachukia sana pale tunapoambiwa sisi ni wavivu, ila hata tukichukia huo ndio ukweli wenyewe. Sehemu kubwa ya wananchi ni wavivu au hawafanya kazi kwa viwango ambavyo wanategemewa kufanya. Kila mtu anatafuta njia rahisi ya kupata fedha. Kila mtu anataka apate kitu pasi na kutoa kitu. Hatimaye hii imetuletea wizi na ufisadi mkubwa kwenye taifa. Najua nikisema ufisadi utakimbilia kwenye ESCROW na EPA, lakini je vipi kuhusu daktari anayetaka rushwa ili amhudumie mgonjwa?

Vipi kuhusu afisa wa kodi TRA anayetaka rushwa ili kumsaidia mtu asilipe kodi stahiki?

Vipi kuhusu mwenyekiti wa serikali ya mtaa anayetaka shilingi elfu mbili ndio akupe barua ya utambulisho?

Vipi kuhusu muuza maziwa anayeweka maji kwenye maziwa ili apate zaidi?

Vipi kuhusu kondakta anayepandisha nauli kwa sababu tu kuna watu wengi wanaotaka kusafiri na usafiri ni wa shida?

Vipi kuhusu mwalimu aliyepangiwa kituo cha kazi ila haonekani kazini?

Vipi kuhusu askari wa usalama barabarani anayetaka rushwa kuruhusu gari ambalo halina sifa za kuwepo barabarani kuendelea na safari? Na baadae lisababishe ajali?

Tukiangalia matukio yote haya tunaona ni jinsi gani sehemu kubwa ya taifa tumemezwa na vitendo vya wizi na ufisadi. Tunapiga kelele kukemea ufisadi mkubwa lakini sisi sisi ndio wa kwanza kufurahia kutoa rushwa ili tupate huduma tunazozitaka kwa haraka.

2. Tatizo la pili ni uadilifu, hili ndio linatumaliza kama taifa na ndio linazaa tatizo na kwanza la kutokufanya kazi kwa bidii na maarifa na hatimaye kujiingiza kwenye wizi na ufisadi.

Ni lazima sisi kama wananchi tuanze kujimulika wenyewe, tuone je matendo tunayofanya kila siku kama yangefanywa kuwa ndio sheria ya nchi nzima nchi yetu ingefika wapi?

Tunakuwa wepesi kuwalaumu viongozi kwa tabia zao mbaya lakini tunasahau viongozi hawa wametoka katikati yetu sisi na hivyo wanapeleka tabia walizokuwa nazo kwenye ngazi za juu zaidi.

Kwa hayo machache nikutakia mwaka mzuri na wenye mafanikio makubwa. Nakusihi sana mwaka huu simamia nguzo hizi tatu muhimu

1. Kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

2. Kuwa mwaminifu, tekeleza kile unachoahidi.

3. Kuwa muadilifu, usimfanyie mwingine kile usichopenda kufanyiwa.

Mwaka huu 2015 AMKA CONSULTANTS imejipanga vizuri ili kufanya kazi na wewe na uweze kuboresha maisha yako na kufikia mafanikio makubwa.

Kila siku tembelea AMKA MTANZANIA ili kujifunza na kuhamasika na uweze kuboresha maisha yako.

Tembelea na ujiunge na KISIMA CHA MAARIFA ambapo utakutana na jumuiya ya watu ambao wamechoka kuwa wa kawaida na wanataka kufanya na kuwa zaidi ya walivyo sasa.

Pia tembelea blog hii MAKIRITA AMANI ambapo utakuwa unapata chakula cha ubongo, mambo ambayo yatakufanya ufikiri zaidi na kukuhamasisha kuchukua hatua kwenye maisha yako.

Pata picha hii, leo umekabidhiwa kitabu kitupu kabisa chenye kurasa 365 na unaamua uandike nini kwenye kila ukurasa, je ukurasa wa leo umeandika nini? Na wa kesho je?

Mwaka 2015 ukawe mwaka wa mafanikio makubwa kwako.

TUPO PAMOJA.

Makirita Amani,

Rais wa Tanzania mwaka 2040.

Sunday, December 14, 2014

Nenda Kapige Kura, Au Usipige Na Fanya Hivi…

Leo ni siku ya kupiga kura kuwachagua viongozi wa serikali za mitaa, najua unajua hili, ila imebidi niliandike tena ili tupate pa kuanzia. Kama ulikuwa hujui leo ndio siku ya uchaguzi basi tuna tatizo kubwa zaidi.

Kwa takwimu mbalimbali za chaguzi zilizopita tunaona idadi kubwa ya watu waliojiandikisha hawapigi kura. Na laiti kama watu hao wangepiga kura mabadiliko yangekuwa makubwa sana.

kupiga kura

Sasa sitaki kuandika mengi nikucheleweshe kupiga kura, ninachokuambia leo ni;

Nenda kapige kura, au usiende kupiga na usilalamike chochote.

Maana watanzania tumekuwa mafundi wa kulalamika ila hatua hatuchukui. Kama hatua kubwa za kuwawajibisha watu hatuwezi kuchukua, basi tuchukue hatua ya kupiga kura na kuchagua viongozi ambao ni bora.

Wahi kapige kura yako asubuhi hii, na mhamasishe kila unayekutana naye nae akapige kura.

Hapa ndipo mabadiliko ya nchi yetu yanapoanzia.

Sunday, November 23, 2014

Mahitaji Manne Ya Mtu Kuwa Kiongozi.

Ili uweze kuwa kiongozi bora na mwenye mafanikio kuna vitu vinne unavyotakiwa kuwa navyo na uweze kuvisimamia. Kwa kujua na kusimamia vitu hivi kutakuwezesha kufanikiwa sana kama kiongozi.

1. Kuweza kujisimamia mwenyewe.

Kiongozi bora ni yule ambaye anayeweza kujisimamia mwenyewe. Ni lazima uweze kujiwekea malengo na mipango yako mwenyewe na uweze kuifuata bila ya kusimamiwa na mtu mwingine yeyote. Kama unahitaji kusimamiwa ndio uweze kutekeleza majukumu yako basi wewe sio kiongozi bali ni mfuasi. Na kama ukijaribu kuongoza kama unakosa tabia ya kujisimamia mwenyewe utashindwa vibaya sana.

2. Kuweza kutatua matatizo.

Kazi kubwa ya kiongozi ni moja, kutatua matatizo. Ili uweze kuwa kiongozi bora inabidi uweze kuyaangalia matatizo kwa jinsi gani yanaweza kutatuliwa. Kama unaogopeshwa na tatizo na kuona haliwezi kutatuliwa wewe sio kiongozi. Kila tatizo lina utatuzi wake. Ni kazi yako kama kiongozi kuja na njia za kutatua tatizo hilo na hivyo kuboresha hali iliyopo.

3. Kuweza kufanya mawasiliano mazuri.

Kiongozi bora ni yule ambaye anaweza kufikia ujumbe wake kwa watu anaowaongoza na wakauelewa na kuufanyia kazi ujumbe huo. Ili kuweza kufikisha ujumbe wao vizuri ni lazima uwe na mbinu nzuri za mawasiliano. Mawasiliano yanaweza kuwa ya maneno, maandishi au hata vitendo. Jinsi ambavyo unawasilisha ujumbe wako unaweza kuwa na ushawishi mkubwa au ukapuuzwa na wale wanaoupokea. Ni muhimu kujifunza mbinu bora za kufanya mawasiliano ili uweze kufikisha ujumbe wako na ufanyiwe kazi.

4. Kuweza kujenga mahusiano.

Kiongozi ni mtu na anayewaongoza ni watu. Ili uweze kuwa kiongozi bora ni lazima uwe na mahusiano mazuri na wale ambao unawaongoza. Kiongozi sio mtawala kwamba anachokisema yeye ndio mwisho, bali anahitaji kujenga urafiki na watu ambao anawaongoza. Kwa urafiki huu watu anaowaongoza watakuwa tayari kumshauri mambo mengi ambayo yatamsaidia kuongoza vizuri zaidi.

Hayo ndio mambo manne unayohitaji kuwa nayo ili kuwa kiongozi bora. Habari nzuri ni kwamba mambo yote hayo manne unaweza kujifunza na kuyaendeleza kwenye uongozi wako.

Nakutakia kila la kheri kwenye mafanikio yako kama kiongozi.

TUPO PAMOJA.

Sunday, November 9, 2014

Nguzo Kuu Ya Uongozi; Tekeleza Kile Unachoahidi.

Katika kujijenga kuwa kiongozi bora na imara kuna misingi mingi ya uongozi ambayo unatakiwa kuifuata. Kushindwa kufuata misingi hii kutapelekea uongozi wako kushindwa na hata kudharaulika sana.

Moja ya nguzo muhimu za uongozi ni kutekeleza kile unachoahidi. Kuongea ni rahisi sana na hivyo watu wengi hujikuta wakiongea mambo ambayo hawana uhakika kama wanaweza kuyatekeleza. Kwa kuwa kuongea ni rahisi watu hutumia nafasi hii kuongea mambo ambayo yatawafanya waonekane ni viongozi wazuri ila hawana uwezo wa kuyatekeleza.

Madhara ya kuahidi mambo usiyoweza kutekeleza.

1. Inakuondolea uaminifu.

Unapoahidi mambo halafu ukashindwa kuyatekeleza watu huondoa uaminifu kwako. Hivyo wakati mwingine utakapowaahidi hawatakusikiliza na hata wakikusikiliza hawataweka maanani uliyowaambia. Kwa sababu binadamu wana tabia moja kwamba ukishamdanganya mtu mara moja kila wakati atakuwa na wasi wasi na wewe.

2. Itakuondolea ushawishi.

Uongozi ni ushawishi, kama utaahidi mambo ambayo huwezi kuyatekeleza na kufanikiwakuwashawishi watu mara ya kwanza, baadae utapoteza ushawishi huo kama hukutekeleza yale uliyoahidi mara ya kwanza. Unapopoteza ushawishi unapoteza uongozi.

3. Unapoteza heshima yako.

Unapokuwa mtu wa kutekeleza maneno yako unaheshimika na wale unaowaongoza na hata jamii kwa ujumla. Unapoanza kuahidi mambo ambayo unashindwa kuyatekeleza unapoteza heshima yako.

Anza sasa kutekeleza kile unachoahidi kufanya, itakujengea sifa nzuri kama kiongozi na itakuongezea ushawishi na heshima mbele ya jamii.

Kama umeahidi wateja kwamba utawapatia bidhaa au huduma bora tekeleza ahadi yako.

Kama umewaahidi wafanyakazi wako kwamba wakifikia kiwango fulani cha uzalishaji utawaongeza mshahara basi timiza ahadi yako wanapofikia kiwango hiko.

Kama umewaahidi wananchi wakupigie kura ili uweze kuwasaidia kufikia maendeleo, tekeleza ahadi uliyotoa.

Hivi ndivyo unavyoweza kuwa kiongozi bora, TEKELEZA AHADI ZAKO NA IKIWEZEKANA ONGEZA ZAIDI.

Nakutakia kila la kheri katika uongozi wako.

TUPO PAMOJA.

Monday, November 3, 2014

Tukemee Tabia Hii Mbaya Kama Taifa.

Jana tarehe 02/11/2014 kulikuwa na mdahalo wa katiba ulioandaliwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere uliokuwa unafanyika katika ukumbi wa ukumbi wa ubungo plaza.

Katika mdahalo huo waliokuwa wajumbe wa iliyokuwa tume ya katiba walialikwa kuzungumza na baadae wananchi waliohudhuria nao wangepata nafasi ya kuzungumzia katiba pendekezwa.

Lengo kubwa la mdahalo huo na mingine ambayo tuliahidiwa itafuata ilikuwa kuwapa uelewa wananchi juu ya katiba pendekezwa kabla wakati wa kupiga kura haujafika.

Binafsi ninaona kitu hiki ni kizuri sana maana taasisi inayoandaa midahalo hii haina uegemeo wowote wa kisiasa na hivyo itatoa nafasi nzuri ya wananchi kujifunza yaliyomo kwenye katiba pendekezwa.

Katika hali ya kushangaza wakati mdahalo unaendelea na Jaji Warioba akizungumza kiliibuka kikundi cha watu ambao walionesha mabango ya kupinga mdahalo ule na kusema kwamba wanaikubali katiba pendekezwa. Hata walipotakiwa kutulia chini ili mdahalo uweze kuendelea bado hawakusikia na hatimaye ikapelekea vurugu kubwa na mdahalo kuahirishwa.

WARIOBA

Kwanza kabisa hiki ni kitendo cha ajabu sana ambacho kinatakiw akulaaniwa na kila Mtanzania ambaye ana mapenzi mema na nchi hii. Ni kweli kabisa hatuwezi kukubaliana wote, ila kutofautiana kwetu kifikra na kihoja kusifanye tuonanae kama maadui. Hizi ni siasa chafu na za kitoto sana ambazo naona zinanyamaziwa na wanaofanya ujinga huu wanaonekana kama wanaleta manufaa kwa kikundi fulani.

Kama unaona mtu anakushinda kwa hoja njia sahihi ni kuleta fujo na kupigana? Hapana hii sio njia sahihi kabisa na kama tutaendelea kuacha mambo haya yaendelee tutalipeleka taifa kubaya.

Katiba ni kitu ambacho kinamhusu kila mwananchi na hivyo kila mwananchi ana uhuru wa kutoa maoni yake na hisia zake juu ya katiba hii. Lakini katika kutoa maoni hayo na hisia hizo usiingilie uhuru wa mwenzako au kuleta fujo au kumwona anayeamini tofauti na wewe ni adui.

Naomba watanzania wote tulaani kitendo hiki kilichotokea na tusitoe tena nafasi ya kutokea kwa kitendo kama hiki.

Tanzania ni nchi yetu sote, tushirikiane kuijenga.

TUPO PAMOJA.

Sunday, November 2, 2014

Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Ni Muhimu Sana. Tuzingatie Mambo Haya Matano.

Tarehe 14/12/2014 itakuwa siku muhimu sana katika miaka mitano ijayo. Siku hii itakuwa ni siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa. Watu wengi sana hawaupi uchaguzi huu nafasi kubwa na wameelekeza macho na masikio yao kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Hili ni kosa kubwa sana ambalo tunafanya watanzania wenzangu. Uchaguzi wa serikali za mitaa ni muhimu kama ilivyo uchaguzi mkuu. Ni kupitia serikali za mitaa ambapo tunakuwa na demokrasia ya moja kwamoja. Yaani kama kuna jambo lolote la kufanya maamuzi kwenye mtaa au kijiji basi wananchi wote watafanya maamuzi kwenye vikao na mikutano mbalimbali.

Pia serikali hizi za mitaa zina mamlaka ya kutunga sheria ndogo ndogo ambazo zinaweza kuwa na athari chanya au hasi kwetu sisi wananchi.

Serikali za vijiji zina mamlaka makubwa sana kwenye ardhi na hivyo zinaweza kufanya maamuzi ya kuuza ardhi kwa watu mbalimbali. Hivyo unapokuwa na serikali ya kijiji ambayo sio imara mnaweza kujikuta mnapoteza ardhi yenu.

Mwisho kabisa naamini mabadiliko na maendeleo ya nchi hii yanaweza kuanzia kwenye ngazi ya mitaa, vitongoji au vijiji. Hii ni kwa sababu matatizo yoyote tunayokumbana nayo kama taifa yanaanzia katika ngazi ya familia na hatimaye mitaa. Kwa mfano wahalifu wote wanaishi kwenye mitaa yetu, wauzaji wa madawa ya kulevya na hata watumiaji wanakaa kwenye mitaa yetu. Hivyo tukiweza kuwa na serikali zamitaa ambazo zipo imara tunaweza kujenga misingi mizuri kama taifa.

Baada ya kuona umuhimu huo mkubwa wa serikali za mitaa sasa naomba nikushirikishe mambo matano muhimu ya kuzingatia kwenye uchaguzi huu wa serikali za mitaa.

1. Hakikisha unapiga kura na hamasisha wengine nao wapige kura.

Ule utamaduni wetu watanzania wa kutokupiga kura halafu tunakuwa wa kwanza kulalamika kwamba viongozi ni wabovu sio utaratibu mzuri. Hakikisha unapiga kura siku hiyo ya uchaguzi na pia washawishi ndugu jamaa na marafiki zako nao wapige kura siku hiyo. Kura yako moja ina thamani kubwa sana, usiidharau.

uchaguzi

2. Chagua kiongozi mwenye maono na mwenye historia nzuri.

Kwanza kabisa mtu ambaye mtamchagua awe mtu ambaye mnamjua vizuri. Awe ni mtu ambaye amekaa kwenye mtaa huo na mna historia yake nzuri ya namna ambavyo amekuwa akihamasisha mambo mbalimbali kwenye mtaa au kijiji chenu. Awe ni mtu mwenye maono na anayefikiria na kukubali mabadiliko. Kiongozi wa aina hii ataweza kushirikiana nanyi kuleta maendeleo kwenye eneo lenu.

Kujua zaidi kuhusu tabia za viongozi bonyeza maandishi haya.

3. Mtu yeyote atakayotoa rushwa usifikirie mara mbili, usimpigie kura na hamasisha wengine wasimpigie kura.

Uongozi wa serikali za mitaa ni uongozi ambao hauna manufaa makubwa kifedha zaidi ya posho ndogo ndogo. Sasa mtu ambaye anatoa rushwa lili kupata nafasi hiyo, jiulize ananufaikaje? Kwa vyovyote vile atahakikisha akipata nafasi analipa fedha yake aliyowekeza kwa kutoa rushwa hivyo atawaingiza kwenye matatizo.

4. Chagua mtu, usichague chama.

Kwa siasa zetu za Tanzania bado haturuhusu mgombea binafsi hivyo unalazimika kuchagua mgombea anayeletwa na chama fulani. Chama kinaweza kuwa na sera nzuri sana ila kama kitakuwa na mgombea ambaye hana uwezo mzuri wa uongozi sera hizo ni kazi bure. Hivyo hudhuria mikutano ya kampeni, wafatilie vizuri wagombea wote na mchague mtu ambaye unaona anaweza kuleta mabadiliko kwenye mtaa au kijiji chenu. Hata kama wewe ni mkereketwa wa chama fulani ila ukaona mgombea wa chama kingine ana sifa zaidi ya mgombea wa chama chako, mpigie kura. Mwisho wa siku maendeleo yatakuwa ni kwa mtaa wenu na sio chama chenu.

5. Tuoneshe ushirikiano na kuwawajibisha viongozi tuliowachagua.

Baada ya uchaguzi na viongozi kupatikana ni vyema kuweka tofauti za kisiasa pembeni na kupeana ushirikiano ili kiongozi mliyemchagua aweze kutekeleza majukumu yake. Kwa kuonesha ushirikiano mzuri italeta mafanikio makubwa kwa mtaa au kijiji chenu.

Pia pale ambapo kiongozi mliyemchagua anakwenda kinyume na ahadi zake ni vizuri kumwajibisha. Kwenye serikali za mitaa tupo karibu sana na viongozi wetu na hivyo ni rahisi kuhoji mambo mbalimbali ambayo mnaona hayaendi sawa.

Nichukue nafasi hii kuwatakia watanzania wote uchaguzi mwema na twende tukafanye maamuzi sahihi kwa mitaa na vijiji vyetu kwa miaka mitano ijayo.

Tanzania ni yetu sote, tushirikiane kuijenga.

Friday, October 31, 2014

Ushauri Muhimu Kwa Wanafunzi Wa Kidato Cha Nne.

Jumatatu ijayo tarehe 03/11/2014 wanafunzi wa kidato cha nne wanakwenda kuanza mitihani yao ya kuhitimu kidato cha nne. Hii ni hatua muhimu sana kwenye maisha yao kwani ndio itapelekea ndoto zao nyingine kuwa kweli. Kama mwananfunzi ana ndoto ya kuwa injinia, rubani, daktari au mwalimu, mitihani hii ni muhimu kwake kufaulu ili kuweza kuendelea na masomo yako.

Hapa napenda kushauri mambo kumi kwa wnafunzi wa kidato cha nne wanaokwenda kuanza mitihani yao. Kwa yeyote anayesoma hapa fikisha ushauri huu kwa mwanafunzi unayemjua, anaweza kuwa kuwa mtoto wako, mdogo wako, ndugu au hata jirani.

1. Kwanza kabisa nitoe hongera kwa wanafunzi wote waliovumilia miaka yote minne na hatimaye sasa mnakaribia kabisa mitihani yenu ya mwisho. Sio kazi ndogo hivyo unastahili pongezi.

2. Kubuka yale uliyosoma na kufundishwa katika miaka yote minne uliyokuwa shuleni. Maswali ya mtihani yanatoka katika mambo hayo.

3. Jiamini unapokuwa kwenye chumba cha mtihani, usiwe na hofu au wasiwasi kwamba mtihani ni mgumu au utafeli. Jitahidi kadiri ya uwezo wako.

4. Wahi kufika kwenye chumba cha mtihani, jitahidi ufike nusu saa kabla ya mtihani kuanza hii itakufanya upate muda wa kutuliza akili. Ukichelewa nakukuta mtihani umeshaanza una nafasi kubwa ya kutofanya vizuri.

5. Unapopewa mtihani wako soma maswali yote kisha chagua maswali unayoweza kuanza nayo na ukayafanya vizuri. Kumbuka huwezi kufanya maswali yote kabisa kwenye mtihani, hivyo anza na yale ambayo unaweza kuyafanya vizuri. Kabla ya kujibu swali hakikisha umelielewa.

KIDATO

6. Ukisikia kuna habari za mtihani umevuja usijihangaishe nazo, zitakupotezea muda na kujiamini na mara nyingi ni habari za uongo. Jiamini kwa yale ambayo umefundishwa na kujisomea, yanakutosha kufaulu mtihani wako.

7. Usipanick, hata unapoona umekosea swali kata na ufanye kwa usahihi. Kukosea swali kwenye mtihani ni swala la kawaida, ila utakapopanick ndio utaharibu kila kitu. Kama umekosea swali, kata na uanze kulifanya kwa usahihi.

8. Ukitoka kwenye chumba cha mtihani msijadili maswali ya mtihani uliopita, unaweza kukata tamaa na kujiona umeshafeli. Mara nyingi baada ya mtihani utapenda kujua wenzako walijibu vipi swali fulani, bahati mbaya sana hakuna hata mmoja wenu ambaye ana jibu sahihi hivyo usisikilize maongezi ya aina hiyo.

9. Siku za mtihani hakikisha unapata usingizi wa kutosha, usikeshe kusoma, akili itashindwa kufikiria vizuri. Hakikisha unapata angalau masaa nane ya kulala na pia hakikisha unapata kifungua kinywa asubuhi kabla ya kwenda kwenye mtihani. Itafanya akili yako iweze kufikiri zaidi.

10. Mwisho kabisa nikuambie kwamba wewe ni hazina kubwa kwa nchi hii, tunakutegemea wewe kama mzalishaji na hata kiongozi wa nchi hii. Jiamini unaweza na fanya maamuzi sahihi kwenye kila hatua utakayokuwa unapitia.

Nakutakia kila la kheri katika mafanikio na ufaulu kwenye mitihani yako.

TUPO PAMOJA.

Tuesday, October 14, 2014

Viongozi 100 Walioibadili Dunia.

Hii hapa ni orodha ya viongozi 100 walioibadili dunia kutokana na falsafa zao na misimamo yao. Viongozi hawa wako katika kada mbalimbali ikiwemo siasa, biashara, taaluma, dini na hata wanaharakati. Unaweza kubonyeza majina yao ili kujifunza zaidi.

christ1. Jesus Christ (c.5BC – 30AD) Spiritual Teacher, central figure of Christianity.

Jefferson2. Thomas Jefferson (1743- 1826) 3rd President of US. Principle author of Declaration of Independence

Gorbachev3. Mikhail Gorbachev (1931 – ) Leader of Soviet Union. Oversaw transition from Communism in Eastern Europe.

christ4. Martin Luther King (1929 – 1968) Non-violent civil rights leader.

mandela5. Nelson Mandela (1918 – 2013) Anti-apartheid leader. First President of democratic South Africa in 1994.

buddha6. Lord Buddha (c 563 – 483BC) Spiritual Teacher and founder of Buddhism.

Churchill7. Winston Churchill (1874 – 1965) Prime Minister of Great Britain during Second World War.

Shakespeare8. William Shakespeare (1564- 1616) English poet and playwright.

Hitler9. Adolf Hitler (1889 – 1945) Dictator of Nazi Germany.

Lincoln10. Abraham Lincoln (1809 – 1865) President of US during civil war, helped end slavery.

  1. Prophet Muhammad – (570 – 632) Prophet of Islam
  2. St Paul (5 – AD 67) – Christian missionary
  3. George Washington (1732 – 1799) – 1st President of US
  4. Sri Krishna (c. BC) – Spiritual Teacher of Hinduism
  5. Emperor Constantine (272 – 337) First Roman Emperor to embrace Christianity
  6. Martin Luther (1483 – 1546) – Key figure in Protestant Reformation.
  7. Socrates (469 BC–399 BC) – Greek philosopher
  8. Karl Marx (1818 – 1883) – German philosopher, founder of Marxism
  9. Charles de Gaulle (1890- 1970) French politician.
  10. Franklin D. Roosevelt (1882 – 1945) US President 1932-1945
  11. Charles Darwin (1809 – 1882) – Developed theory of evolution
  12. Sir Isaac Newton (1642-1727) – English mathematician and scientist.
  13. Akbar (1542 – 1605) – Moghul Emperor
  14. Queen Victoria (1819 – 1901) – Queen of Great Britain during Victorian age.
  15. Konrad Adenauer (1876-1967) – German Chancellor post WWII.
  16. Jawaharlal Nehru (1889-1964) – First Indian Prime Minister
  17. Ramses II (1279 – 1213 BC) – Powerful Egyptian king.
  18. Benjamin Franklin (1706 – 1790) – US writer and polymath
  19. Confucius (551 – 479 BC) – Chinese philosopher.
  20. Alexander the Great (356 – 323 BC) – King of Macedonia.
  21. Woodrow Wilson (1856 – 1924) – President of US during WWI
  22. William Wilberforce (1759 – 1833) – Campaigner against slavery
  23. Christopher Columbus (1451 – 1506) – Italian explorer landed in America
  24. Marcus Aurelius (121 – 180) – Roman Emperor and philosopher
  25. Galileo Galilei (1564 -1642) – Astronomer and physicist
  26. Mahatma Gandhi (1869 – 1948) – Indian nationalist and politician
  27. Joan of Arc – (1412-1431) – French saint
  28. Charlemagne (742 – 814) – King of Franks and Emperor of the Romans
  29. Aristotle (384 BC – 322 BC) – Greek philosopher
  30. Mother Teresa – (1910-1997) – Nun who served the poor
  31. Saladin (1138 – 1193) – Leader of Arabs during Crusades.
  32. Simon Bolivar (1783 – 1830) – Liberator of Latin American countries
  33. Babur (1483 – 1531) – Founder of Moghul Empire
  34. Sir Walter Raleigh (1552 – 1618) – English explorer.
  35. Voltaire (1694 – 1778 – French philosopher.
  36. Samuel Johnson (1709 – 1784) – British author and creator of dictionary.
  37. Catherine the Great (1729 – 1796) – Russian Queen
  38. Mozart (1756 – 1791) – Austrian Music composer.
  39. Princess Diana (1961 – 1997) – Humanitarian
  40. Oscar Wilde (1854 – 1900) – Irish writer.
  41. Napoleon Bonaparte (1769 – 1821) – French military and political leader
  42. Beethoven (1770 1827) – German composer
  43. Benjamin Disraeli (1804 – 1881) – British Prime Minister.
  44. Leonardo da Vinci ( 1452 – 1519) – Italian scientist, artist, polymath.
  45. Louis Pasteur (1822 – 1895) – French chemish and Biologist.
  46. Leo Tolstoy (1828 – 1910) – Russian writer and philosopher
  47. Albert Einstein (1879 – 1955) – German physicist.
  48. Ataturk (1881-1938) – founder of the Turkish Republic.
  49. Pablo Picasso (1881-1973) – Spanish painter and sculptor
  50. Pope John Paul II (1920 – 2005) – Polish Pope from 1978-2005
  51. Margaret Thatcher (1925 – ) – British Prime Minister
  52. Mohammed Ali (1942 – ) American boxer
  53. Aung San Suu Kyi (1945 – ) Burmese opposition leader
  54. John F. Kennedy (1917 – 1963) – US President.
  55. Lord Nelson (1758 – 1805) – Admiral in British navy
  56. Boris Yeltsin (1931 – 2007) – Russian President
  57. Lyndon Johnson (1908 – 1973) – US President 1963-69
  58. Indira Gandhi (1917 – 1984) – Third Prime Minister of India.
  59. Eva Peron (1919 – 1952) – First Lady of Argentina
  60. William Tyndale (1494 – 1536) – Translated Bible into English
  61. Tim Berners Lee (1955 – ) Credited with founding World Wide Web
  62. Rosa Parks (1913-2005) – Civil Rights activist
  63. Benazir Bhutto (1953 – 2007) – Prime Minister of Pakistan
  64. Schubert (1797 – 1828) – Austrian Composer
  65. Kofi Annan (1938 – ) United Nations Secretary General
  66. 14th Dalai Lama (1938 – ) Spritual and political leader of Tibetans
  67. Barack Obama (1961 – ) 44th President of United States
  68. Albert Schweitzer (1875 – 1965) – Humanitarian, philosopher.
  69. Malcolm X (1925 – 1965) Black nationalist leader
  70. Lech Walesa (1943 – ) Leader of Polish solidarity movement.
  71. John M Keynes (1883 – 1946) Influential economist.
  72. Mary Wollstonecraft (1759-1797) – Feminist, author
  73. Marie Curie (1867 – 1934) – Chemist and Physicist
  74. Elvis Presley (1935 – 1977) – Rock star.
  75. Oliver Cromwell (1599 – 1658) – British Parliamentarian
  76. Oprah Winfrey (1954 – ) US media celebrity.
  77. Boudicca ( c20 – 60) – British leader against Roman rule
  78. Jesse Owens (1913-1980) US Sprinter
  79. Bill Gates (1955 – ) Founder of Microsoft
  80. Ernest Hemingway ( 1899 – 1961) US writer
  81. John Lennon (1940 – 1980) British popstar and Beatle
  82. Henry Ford (1864-1947) US Industrialist
  83. Genghis Kahn (1162 – 1227) – Leader and creator of Mongol Empire.
  84. Haile Selassie (1892 – 1975) – Ethiopian Leader
  85. George Orwell (1903 – 1950) – English author
  86. Thomas Edison (1847 – 1931) – Inventor and businessman.
  87. Dwight Eisenhower (1890 – 1969) – Supreme Allied Commander
  88. Queen Elizabeth II (1926 – ) British Queen
  89. Plato (424 – 348 BC) – philosopher.
  90. Johann Gutenberg (1395 – 1468) – Inventor of printing press.

Chanzo cha makala hii ni mtandao wa  Biography Online

Monday, October 13, 2014

Tabia Tatu Za Viongozi Dhaifu, Na Jinsi Ya Kuepuka Kuwa Mmoja Wao.

Ni vizuri sana kujifunza kutoka kwa viongozi waliofanikiwa maana hapa unapata njia ya vitu gani vya kufanya ili na wewe uweze kufanikiwa kama kiongozi.

Ni vizuri pia kujifunza kutoka kwa viongozi walioshindwa kwa sababu kupitia kushindwa kwao unajua ni vitu gani vimewafanya washindwe na hivyo kuviepuka ili na wewe usiishie kushindwa kama wao.

Leo tutaangalia tabia tatu za viongozi dhaifu na jinsi ya kuepuka kuwa kiongozi dhaifu.

1. Husita kufanya maamuzi magumu.

Viongozi wote hufikia wakati ambao wanahitaji kufanya maamuzi magumu ili kubadili hali ya mambo. Maamuzi haya yanaweza kuwa na madhara fulani ila kutokufanya maamuzi hayo kunaleta madhara makubwa zaidi mbeleni.

Viongozi dhaifu husita na kuchelewa kufanya maamuzi magumu na hivyo kujikuta kwenye matatizo makubwa zaidi.

2. Hulalamika kukosa rasilimali.

Viongozi hafifu hulalamika kila mara kwamba wamekosa rasilimali fulani ndio maana wameshindwa kufanikiwa. Hutumia muda mwingi kulalamikia rasilimali wanazokosa badala ya  kutumia rasilimali walizoko nazo katika kufikia mafanikio.

3. Huepuka majukumu.

Viongozi hafifu hukwepa majukumu yao na kutafuta njia rahisi kwao. Kwa kuepuka huku majukumu wanashindwa kufikia mafanikio na kwa kutafuta njia rahisi wanapata njia ambayo inawapeleka kwenye kushindwa.

Epuka tabia hizi tatu za viongozi hafifu ili uweze kuwa kiongozi bora na uweze kufikia mafanikio makubwa.

Nakutakia kila la kheri,

TUPO PAMOJA.

Sunday, October 12, 2014

Njia Moja Muhimu Ya Kuwa Kiongozi Bora.

Ni muhimu sana wewe kuwa kiongozi na ni muhimu zaidi kuwa kiongozi bora. Tunaposema ni muhimu wewe kuwa kiongozi haimaanishi kuwa kiongozi wa kisiasa au kiserikali bali ni uwe kiongozi kwenye jambo lolote unalofanya.

Iwe umeajiriwa kwenye kitengo fulani, fanya kazi yako kama kiongozi.

Iwe umejiajiri au unafanya biashara, fanya biashara yako kama kiongozi.

Iwe una familia, endesha familia yako kama kiongozi.

Ni viongozi pekee ndio wanaofikia mafanikio makubwa katika jambo lolote wanalofanya.

Hii ndio sababu kubwa imenifanya kuweka blog hii na kuandika kuhusu uongozi kila siku ya jumapili. Hii itatusaidia kujitengeneza na kuwa viongozi bora zaidi. Ili kuhakikisha hukosi makala hizi za uongozi weka email yako hapo juu na utakuwa unazipata makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

Ni ipi njia moja ya wewe kuwa kiongozi bora?

Njia moja ya wewe kuwa kiongozi bora ni kuwa mfuasi bora kwanza. Ni muhimu sana wewe kuwa mfuasi bora ndio wafuasi wako waweze kukuamini wewe kama kiongozi wao. Ni lazima kile unachotaka wafuasi wako wafanye, uanze kukifanya wewe kwanza.

Kumbuka watu hupenda vitendo zaidi ya maneno. Hivyo unavyoweza kufanya kwa vitendo ndio unavyoweza kuwahamasisha wafuasi wako nao kufanya kile unachofanya wewe.

Kuwa mfuasi bora kwa kufanya kile ambacho unataka wafuasi wako wakifanye na hii itakuongezea ushawishi mkubwa kama kiongozi.

Unataka kujenga maadili mazuri kwenye familia yako, hakikisha na wewe unakuwa na maadili mazuri. Unataka wafanyakazi wako wafanye kazi kwa bidii na maarifa, hakikisha na wewe unafanya kazi kwa bidii na maarifa.

Wewe kama kiongozi ni sehemu ya wafuasi wako, hivyo ni lazima uweze kuishi maisha ya wafuasi wako kama unataka kuwa na ushawishi mkubwa.

Nakutakia kila la kheri katika kujijenga kama kiongozi bora.

Usisahau kuweka email yako hapo juu ili kuhakikisha unapata makala hizi nzuri za uongozi.

TUPO PAMOJA.

Sunday, September 14, 2014

Hili Ndilo Kosa Kubwa Tunalokwenda Kufanya Watanzania 2015.

Mwaka 2015 ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu sana na watanzania wengi umekaribia kabisa kufika. Huu ni mwaka ambao uchaguzi mkuu wa nchi yetu utakwenda kufanyika na hivyo wananchi kupata nafasi ya kuchagua diwani, mbunge na raisi ambaye tunaona anatufaa.

Mwaka 2015 umekuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu kwa sababu wananchi wengi tumeaminishwa na kuamini kwamba baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 na chama tawala kuondoka madarakani maisha yetu yatakuwa mazuri sana. Ni imani nzuri sana ambayo tumekuwa nayo hasa ukizingatia hali ya nchi kiuchumi ipo chini sana ukilinganisha na rasilimali tulizonazo.

Pamoja na kuwa na imani hii nzuri, kuna kosa kubwa sana ambalo watanzania tutakwenda kulifanya mwaka huo 2015. Kosa hili litatugharimu tena miaka mingine mitano au hata zaidi ya hapo kama hatutaendelea kujifunza.

Kosa hili kubwa ni kutokuwa na vigezo vya kiongozi tunayemtaka sisi wananchi. Na kwa kukosa vigezo hivi tutarudia makosa ambayo tuliyafanya nyuma kwa kuchagua watu kutokana na umaarufu wao. Kutokana na kuangalia umaarufu tumechagua viongozi wengi ambao wameishia kutuangusha na kushindwa kutimiza ahadi zao wenyewe.

Ni lazima sisi kama wananchi bila hata ya kuambiwa na wanasiasa, tuwe na vigezo vya aina ya kiongozi tunayemtaka. Na hii ni kuanzia udiwani, ubunge na uraisi. Lazima sisi tuwe na vigezo vyetu kisha wale watakaojitokeza kuomba nafasi hizo tuwachuje kwa kutumia vigezo vyetu.

SIASA

Ilivyo sasa ni kwamba wananchi hatuna vigezo vyetu, ila tunatumia vigezo vya wagombea watakavyotuletea na hivyo tunaweza kulinganisha baina ya mgombea na mgombea na kuamua kumchagua mmoja wao. Hapa ina maana kama wagombea wote ni wabovu tutamchagua ambaye ni ahueni. Na hapa ni kwa sehemu ndogo, shemu kubwa itatumia kigezo cha umaarufu.

Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu sasa hivi kuitisha mikutano ya waandishi kila kukicha kutangaza nia zao za kugombea uongozi. Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu kuzunguka huku na kule kutoa misaada ili waonekane wanajali sana.

Sasa watanzania tuache kufanya kosa hili ambalo litaendelea kugharimu maisha yetu.

Katika makala zijazo tutazungumzia ni vigezo gani tunaweza kuvitumia katika kila nafasi ya uongozi ili tuweze kupata viongozi bora.

Tanzania ni nchi yetu sote, unapopata ujumbe huu wajulishe na wenzako wote unaowafahamu ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.

Usisahau kuweka email yako ili upate makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

TUKO PAMOJA.

Hili Ndilo Kosa Kubwa Tunalokwenda Kufanya Watanzania 2015.

Mwaka 2015 ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu sana na watanzania wengi umekaribia kabisa kufika. Huu ni mwaka ambao uchaguzi mkuu wa nchi yetu utakwenda kufanyika na hivyo wananchi kupata nafasi ya kuchagua diwani, mbunge na raisi ambaye tunaona anatufaa.

Mwaka 2015 umekuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu kwa sababu wananchi wengi tumeaminishwa na kuamini kwamba baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 na chama tawala kuondoka madarakani maisha yetu yatakuwa mazuri sana. Ni imani nzuri sana ambayo tumekuwa nayo hasa ukizingatia hali ya nchi kiuchumi ipo chini sana ukilinganisha na rasilimali tulizonazo.

Pamoja na kuwa na imani hii nzuri, kuna kosa kubwa sana ambalo watanzania tutakwenda kulifanya mwaka huo 2015. Kosa hili litatugharimu tena miaka mingine mitano au hata zaidi ya hapo kama hatutaendelea kujifunza.

Kosa hili kubwa ni kutokuwa na vigezo vya kiongozi tunayemtaka sisi wananchi. Na kwa kukosa vigezo hivi tutarudia makosa ambayo tuliyafanya nyuma kwa kuchagua watu kutokana na umaarufu wao. Kutokana na kuangalia umaarufu tumechagua viongozi wengi ambao wameishia kutuangusha na kushindwa kutimiza ahadi zao wenyewe.

Ni lazima sisi kama wananchi bila hata ya kuambiwa na wanasiasa, tuwe na vigezo vya aina ya kiongozi tunayemtaka. Na hii ni kuanzia udiwani, ubunge na uraisi. Lazima sisi tuwe na vigezo vyetu kisha wale watakaojitokeza kuomba nafasi hizo tuwachuje kwa kutumia vigezo vyetu.

SIASA

Ilivyo sasa ni kwamba wananchi hatuna vigezo vyetu, ila tunatumia vigezo vya wagombea watakavyotuletea na hivyo tunaweza kulinganisha baina ya mgombea na mgombea na kuamua kumchagua mmoja wao. Hapa ina maana kama wagombea wote ni wabovu tutamchagua ambaye ni ahueni. Na hapa ni kwa sehemu ndogo, shemu kubwa itatumia kigezo cha umaarufu.

Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu sasa hivi kuitisha mikutano ya waandishi kila kukicha kutangaza nia zao za kugombea uongozi. Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu kuzunguka huku na kule kutoa misaada ili waonekane wanajali sana.

Sasa watanzania tuache kufanya kosa hili ambalo litaendelea kugharimu maisha yetu.

Katika makala zijazo tutazungumzia ni vigezo gani tunaweza kuvitumia katika kila nafasi ya uongozi ili tuweze kupata viongozi bora.

Tanzania ni nchi yetu sote, unapopata ujumbe huu wajulishe na wenzako wote unaowafahamu ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.

Usisahau kuweka email yako ili upate makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

TUKO PAMOJA.

Sunday, September 7, 2014

Je Vijana Wanaoingia Kwenye Siasa Wanaweza Kuwa Wakombozi Wetu?

Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana hapa Tanzania ambao wanaingia kwenye siasa. Na kwanzia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambapo baadhi ya vijana waliogombea ubunge walipata kuchaguliwa kumekuwa na mwamko mkubwa sana wa vijana kuingia kwenye siasa.

Na hata kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 vijana wengi wameonesha nia ya kugombea nafasi mbalimbali za udiwani na ubunge katika maeneo mbalimbali. Na kwa kuwa mpaka sasa hatuna sheria inayoruhusu mgombea binafsi, vijana hawa wote ambao wana nia ya kugombea inawalazimu kupitia vyama vya siasa. Kwa sasa tuna vijana wengi sana ambao wameingia kwenye vyama mbalimbali vya siasa na wengine wamepata nafasi kubwa kwenye vyama hivi.

siasa

Swali kubwa la kujiuliza ni je vijana wengi kuingia kwenye siasa wanaweza kuwa wakombozi wa nchi yetu Tanzania? Natumia neno ukombozi kwa sababu naamini nchi yetu inahitaji ukombozi ili kutoka hapa ilipo. Inahitaji ukombozi kwa sababu tumefika hapa tulipo kutokana na uongozi mbovu na siasa na sera mbovu zilizowekwa na viongozi hawa wabovu. Na ukiangalia viongozi hao umri wao umekwenda sasa na hivyo vijana ndio watakwenda kuchukua nafasi zao siku za mbeleni.

Najiuliza swali hili kwa sababu tumeona baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye siasa hizi wakiishia kutumiwa na baadhi ya watu na hivyo kujikuta wakishindwa kuleta mabadiliko yoyote. Tumeona baadhi ya vijana ambao walikuwa wakilalamikia uongozi mbovu ila wamepewa uongozi kwenye sehemu mbalimbali na kushindwa kuleta mabadiliko yoyote. Na vibaya zaidi wanaishia kuwa sehemu ya kitu walichokuwa wanakipinga.

Sina tatizo na kijana ambaye ameingia kwenye chama chochote cha siasa alichopenda yeye. Iwe ameingia CCM, CHADEMA, CUF au hata CHAUSTA. Kikubwa ambacho wananchi wanataka kuona ni mabadiliko ya kweli katika siasa zetu na hatimaye uongozi wa nchi yetu. Naamini mabadiliko haya yanawezekana kupitia vijana kama watajua ni kitu gani wanakwenda kufanya kwenye siasa hizi na kuepuka kutumika na wale ambao wapo kwenye mifumo hii kwa muda mrefu.

Wewe kama ni kijana ambaye umeingia kwenye siasa jiulize swali hili mara kwa mara na hakikisha unakuwa sehemu ya mabadiliko popote unapokuwepo.

Nakutakia kila la kheri katika harakati za kuleta mabadiliko katika taifa letu Tanzania.

TUKO PAMOJA.

Hakikisha hukosi makala mpya kila inapowekwa kwenye blog hii. Weka email yako hapo juu ili upate makala moja kwa moja kwenye email yako.

Je Vijana Wanaoingia Kwenye Siasa Wanaweza Kuwa Wakombozi Wetu?

Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana hapa Tanzania ambao wanaingia kwenye siasa. Na kwanzia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambapo baadhi ya vijana waliogombea ubunge walipata kuchaguliwa kumekuwa na mwamko mkubwa sana wa vijana kuingia kwenye siasa.

Na hata kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 vijana wengi wameonesha nia ya kugombea nafasi mbalimbali za udiwani na ubunge katika maeneo mbalimbali. Na kwa kuwa mpaka sasa hatuna sheria inayoruhusu mgombea binafsi, vijana hawa wote ambao wana nia ya kugombea inawalazimu kupitia vyama vya siasa. Kwa sasa tuna vijana wengi sana ambao wameingia kwenye vyama mbalimbali vya siasa na wengine wamepata nafasi kubwa kwenye vyama hivi.

siasa

Swali kubwa la kujiuliza ni je vijana wengi kuingia kwenye siasa wanaweza kuwa wakombozi wa nchi yetu Tanzania? Natumia neno ukombozi kwa sababu naamini nchi yetu inahitaji ukombozi ili kutoka hapa ilipo. Inahitaji ukombozi kwa sababu tumefika hapa tulipo kutokana na uongozi mbovu na siasa na sera mbovu zilizowekwa na viongozi hawa wabovu. Na ukiangalia viongozi hao umri wao umekwenda sasa na hivyo vijana ndio watakwenda kuchukua nafasi zao siku za mbeleni.

Najiuliza swali hili kwa sababu tumeona baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye siasa hizi wakiishia kutumiwa na baadhi ya watu na hivyo kujikuta wakishindwa kuleta mabadiliko yoyote. Tumeona baadhi ya vijana ambao walikuwa wakilalamikia uongozi mbovu ila wamepewa uongozi kwenye sehemu mbalimbali na kushindwa kuleta mabadiliko yoyote. Na vibaya zaidi wanaishia kuwa sehemu ya kitu walichokuwa wanakipinga.

Sina tatizo na kijana ambaye ameingia kwenye chama chochote cha siasa alichopenda yeye. Iwe ameingia CCM, CHADEMA, CUF au hata CHAUSTA. Kikubwa ambacho wananchi wanataka kuona ni mabadiliko ya kweli katika siasa zetu na hatimaye uongozi wa nchi yetu. Naamini mabadiliko haya yanawezekana kupitia vijana kama watajua ni kitu gani wanakwenda kufanya kwenye siasa hizi na kuepuka kutumika na wale ambao wapo kwenye mifumo hii kwa muda mrefu.

Wewe kama ni kijana ambaye umeingia kwenye siasa jiulize swali hili mara kwa mara na hakikisha unakuwa sehemu ya mabadiliko popote unapokuwepo.

Nakutakia kila la kheri katika harakati za kuleta mabadiliko katika taifa letu Tanzania.

TUKO PAMOJA.

Hakikisha hukosi makala mpya kila inapowekwa kwenye blog hii. Weka email yako hapo juu ili upate makala moja kwa moja kwenye email yako.

Sunday, August 31, 2014

Sababu Mbili Kwa Nini Tanzania Ni Nchi Masikini.

Kwa nini Tanzania ni nchi masikini? Pamoja na rasilimali nyingi tulizonazo, mlima mrefu, mbuga za wanyama, madini na hata ardhi kubwa kwa nini tunaendelea kuwa masikini?
Hili ni swali gumu sana maana hata raisi wa nchi mheshimiwa Jakaya Kikwete alikiri kwamba hajui kwa nini nchi yetu ni masikini. Sasa leo nataka tujadiliane nini kinatufanya tuendelee kuwa kati ya nchi masikini sana duniani licha ya rasilimali nyingi tulizonazo.
Katika moja ya vitabu vyake Mwalimu Nyerere aliwahi kuandika kwamba ili tuendelee tunahitaji vitu vinne. Vitu hivyo ni WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UONGOZI BORA. Katika vitu hivi vinne kuna viwili ambavyo tunavyo vya kutosha na viwili ambavyo tumekosa na ndio maana tunaendelea kuwa masikini.

Vitu viwili tulivyonavyo.

Katika vitu hivi vinne tunavyohitaji ili kuendelea, viwili tayari tunavyo, vitu hivyo ni;
1. Ardhi. Tunayo ardhi kubwa sana ya kutosha. Sehemu kubwa ya ardhi ya tanazania bado haijatumika kabisa. Na sehemu kubwa ya ardhi yetu ina rutuba na hivyo inafaa kwa kilimo cha kila aina. Nenda katika kila mkoa utakuta kuna mazao fulani yanayokubali sana. Hata maeneo ya katikati ya nchi ambayo yana asili ya ukame bado kuna mazai yanakubali vizuri.
Lakini ardhi hii sasa iko hatarini kutoweka kutokana na ukosefu mwingine tutakaouona baadae.
2. Watu. Katika sensa ya mwaka 2012 tanzania ina watu zaidi ya milioni 45. Na wengi katika watu hawa ni vijana. Kwa watu wote hawa tulionao, kama wangeweza kutumiaka vizuri tungeweza kufikia maendeleo makubwa sana.

Vitu viwili ambavyo tumekosa.

1. Siasa safi. Kila nchi duniani inaendeshwa kwa siasa. Tanzania tuliwahi kuwa na siasa ya UJAMAA NA KUJITEGEMEA, ambayo ilikwenda vizuri sana mpaka pale ilipouliwa, tumewahi pia kuwa na SIASA NI KILIMO ambapo kilimo kilipewa kipaumbele kwa sababu ndio sehemu kubwa ya wananchi wanategemea kilimo. Lakini nayo haikudumu muda mrefu. Tuliwahi pia kuwa na SIASA YA UWEKEZAJI NA UBINAFSISHAJI ambapo tulishuhudia mashirika ya umma yakipewa watu binafsi na wengi wao kutoka nje ya nchi. Sasa hivi sina hakika tunaendeshwa na siasa gani.
Tumekosa siasa safi na ndio maana tumeshindwa kutumia rasilimali zetu na hata watu wengi tulionao kuweza kufikia maendeleo kama taifa.
2. Uongozi bora. Hili ndio tatizo kubwa sana na ndio linazaa matatizo mengine yote. Tumekosa uongozi bora ambao unaweza kuwatengeneza na kuwatumia watu tulionao kuweza kufikia mafanikio. Tumekosa uongozi bora ambao utatengeneza siasa safi ambayo itatuwezesha kutumia watu wetu na rasilimali zetu vizuri.
Tunao watu wengi ambao wanashikilia nafasi za uongozi ila wamekosa sifa za uongozi. Watu hawa ndio wanafanya maamuzi mabovu na hivyo kutufanya tuendelee kuwa masikini.
Hii ndio sababu kubwa iliyonifanya niwe naandika kuhusu uongozi kwenye blog hii kila siku ya jumapili. Kama umekosa kusoma makala za uongozi zilizopita, bonyeza maandishi haya ili uweze kuzisoma.

Tufanye nini ili kuondoka kwenye umasikini huu?

Kwa kuwa tumeshajua mambo mawili muhimu tunayokosa ili kufikia maendeleo na kwa kuwa tumeshajua ukosefu wa uongozi bora ndio tatizo kubwa zaidi nashauri sisi wananchi tuchukue hatua ya kujua na kuchagua viongozi bora. Na nashauri hasa vijana tujifunze sana kuhusu uongozi na kisha tugombee nafasi mbalimbali za uongozi ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.
Kukaa tu na kulalamika kila siku hakutakuwa na msaada kwetu binafsi na hata kwa vizazi vijavyo. Kuna chaguzi zinakuja mwaka huu na mwaka ujao, tutumie nafasi hii kujua ni viongozi wapi wanaotufaa na wapi wasiotufaa. Tukiendelea kufanya makosa haya katika uchaguzi wa viongozi tutaendelea kuwa masikini siku zote.
TANZANIA NI NCHI YETU SOTE, TUSHIRIKIANE KUIJENGA.

Sababu Mbili Kwa Nini Tanzania Ni Nchi Masikini.

Kwa nini Tanzania ni nchi masikini? Pamoja na rasilimali nyingi tulizonazo, mlima mrefu, mbuga za wanyama, madini na hata ardhi kubwa kwa nini tunaendelea kuwa masikini?
Hili ni swali gumu sana maana hata raisi wa nchi mheshimiwa Jakaya Kikwete alikiri kwamba hajui kwa nini nchi yetu ni masikini. Sasa leo nataka tujadiliane nini kinatufanya tuendelee kuwa kati ya nchi masikini sana duniani licha ya rasilimali nyingi tulizonazo.
Katika moja ya vitabu vyake Mwalimu Nyerere aliwahi kuandika kwamba ili tuendelee tunahitaji vitu vinne. Vitu hivyo ni WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UONGOZI BORA. Katika vitu hivi vinne kuna viwili ambavyo tunavyo vya kutosha na viwili ambavyo tumekosa na ndio maana tunaendelea kuwa masikini.

Vitu viwili tulivyonavyo.

Katika vitu hivi vinne tunavyohitaji ili kuendelea, viwili tayari tunavyo, vitu hivyo ni;
1. Ardhi. Tunayo ardhi kubwa sana ya kutosha. Sehemu kubwa ya ardhi ya tanazania bado haijatumika kabisa. Na sehemu kubwa ya ardhi yetu ina rutuba na hivyo inafaa kwa kilimo cha kila aina. Nenda katika kila mkoa utakuta kuna mazao fulani yanayokubali sana. Hata maeneo ya katikati ya nchi ambayo yana asili ya ukame bado kuna mazai yanakubali vizuri.
Lakini ardhi hii sasa iko hatarini kutoweka kutokana na ukosefu mwingine tutakaouona baadae.
2. Watu. Katika sensa ya mwaka 2012 tanzania ina watu zaidi ya milioni 45. Na wengi katika watu hawa ni vijana. Kwa watu wote hawa tulionao, kama wangeweza kutumiaka vizuri tungeweza kufikia maendeleo makubwa sana.

Vitu viwili ambavyo tumekosa.

1. Siasa safi. Kila nchi duniani inaendeshwa kwa siasa. Tanzania tuliwahi kuwa na siasa ya UJAMAA NA KUJITEGEMEA, ambayo ilikwenda vizuri sana mpaka pale ilipouliwa, tumewahi pia kuwa na SIASA NI KILIMO ambapo kilimo kilipewa kipaumbele kwa sababu ndio sehemu kubwa ya wananchi wanategemea kilimo. Lakini nayo haikudumu muda mrefu. Tuliwahi pia kuwa na SIASA YA UWEKEZAJI NA UBINAFSISHAJI ambapo tulishuhudia mashirika ya umma yakipewa watu binafsi na wengi wao kutoka nje ya nchi. Sasa hivi sina hakika tunaendeshwa na siasa gani.
Tumekosa siasa safi na ndio maana tumeshindwa kutumia rasilimali zetu na hata watu wengi tulionao kuweza kufikia maendeleo kama taifa.
2. Uongozi bora. Hili ndio tatizo kubwa sana na ndio linazaa matatizo mengine yote. Tumekosa uongozi bora ambao unaweza kuwatengeneza na kuwatumia watu tulionao kuweza kufikia mafanikio. Tumekosa uongozi bora ambao utatengeneza siasa safi ambayo itatuwezesha kutumia watu wetu na rasilimali zetu vizuri.
Tunao watu wengi ambao wanashikilia nafasi za uongozi ila wamekosa sifa za uongozi. Watu hawa ndio wanafanya maamuzi mabovu na hivyo kutufanya tuendelee kuwa masikini.
Hii ndio sababu kubwa iliyonifanya niwe naandika kuhusu uongozi kwenye blog hii kila siku ya jumapili. Kama umekosa kusoma makala za uongozi zilizopita, bonyeza maandishi haya ili uweze kuzisoma.

Tufanye nini ili kuondoka kwenye umasikini huu?

Kwa kuwa tumeshajua mambo mawili muhimu tunayokosa ili kufikia maendeleo na kwa kuwa tumeshajua ukosefu wa uongozi bora ndio tatizo kubwa zaidi nashauri sisi wananchi tuchukue hatua ya kujua na kuchagua viongozi bora. Na nashauri hasa vijana tujifunze sana kuhusu uongozi na kisha tugombee nafasi mbalimbali za uongozi ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.
Kukaa tu na kulalamika kila siku hakutakuwa na msaada kwetu binafsi na hata kwa vizazi vijavyo. Kuna chaguzi zinakuja mwaka huu na mwaka ujao, tutumie nafasi hii kujua ni viongozi wapi wanaotufaa na wapi wasiotufaa. Tukiendelea kufanya makosa haya katika uchaguzi wa viongozi tutaendelea kuwa masikini siku zote.
TANZANIA NI NCHI YETU SOTE, TUSHIRIKIANE KUIJENGA.

Sunday, July 27, 2014

Uongozi Ni Watu, Na Sio Vinginevyo.

Kama nikikuuliza swali ni nani muhimu kati ya kiongozi na mwananchi anayeongozwa?

Kwa hali ya kawaida na mazoea tuliyonayo sisi, unaweza kufikiri kiongozi ni bora zaidi ya mwananchi. Lakini huu sio ukweli hata kidogo.

Sio ukweli kwa sababu bila ya mwananchi anayeongozwa hakuna kiongozi, kiongozi ni mwakilishi wa wale waliompa nafasi ya kuwawakilisha. Sasa inakuwaje mtu huyu aliyepewa nafasi awe bora zaidi ya wale waliompa nafasi hiyo?

Kuna utamaduni ama mazoea mabaya ambayo yamejengeka kwenye jamii yetu yanayowafanya viongozi kujiona ni bora kuliko wale wanaowaongoza. Au kujiona ni muhimu zaidi ya wale ambao wamewapa nafasi ya kuwawakilisha.

Haya ni mazoea mabaya sana ambayo yalipata nafasi kutokana na watu wengi kutokuwa na uelewa mzuri kwenye mambo ya uongozi. Ila kwa sasa asilimia kubwa ya watu wana uelewa mzuri sana juu ya wajibu wao na wajibu wa viongozi wao.

Hivyo kwa kizazi kipya cha viongozi ni vyema tukafahamu huu mtazamo wa zamani wa uongozi umekufa na hautoweza kukusaidia. Wewe kama kiongozi unayejitengeneza jua watu ni muhimu kama ulivyo wewe kiongozi. Watu wana nafasi kubwa sana kwenye mafanikio ya uongozi wako.

Ule utamaduni wa viongozi kutaka kupata huduma bora kwa sababu wao ni viongozi hauwezi kukujenga na kukupa mafanikio. Kwa kusema hivi pia sisemi kiongozi apate huduma mbovu ili aonekane yuko na wananchi. Bali kiongozi ahakikishe wananchi wanapata huduma bora kama anazopata yeye.

Lakini hili halitokei kwa sababu baada ya kiongozi kupata huduma bora anasahau kwamba wananchi wanapata huduma mbovu. Na hata akiambiwa haoni uzito sana kwa sababu huduma hizo mbovu hazimuumizi moja kwa moja.

Ni mara ngapi tumeona mtu akiwa na uchungu sana kabla ya kuwa kiongozi ila anapokuwa kiongozi anasahau yale aliyokuwa anayalalamikia? Wanasema madaraka matamu, ila usianguke kwenye shimo hili. Jua watu unaowaongoza ni muhimu sana kama ulivyo wewe na baada ya kujua hili hakikisha unafanya kila juhudi kulinda umuhimu wao.

Karibu katika darasa letu la uongozi ambapo kila jumapili unapata makala nzuri inayohusu uongozi. Tembelea mtandao huu kila mara ili kujifunza mengi zaidi. Karibu tujenge kizazi kipya cha uongozi ambao utaleta tija kwenye nchi yetu Tanzania.

Uongozi Ni Watu, Na Sio Vinginevyo.

Kama nikikuuliza swali ni nani muhimu kati ya kiongozi na mwananchi anayeongozwa?

Kwa hali ya kawaida na mazoea tuliyonayo sisi, unaweza kufikiri kiongozi ni bora zaidi ya mwananchi. Lakini huu sio ukweli hata kidogo.

Sio ukweli kwa sababu bila ya mwananchi anayeongozwa hakuna kiongozi, kiongozi ni mwakilishi wa wale waliompa nafasi ya kuwawakilisha. Sasa inakuwaje mtu huyu aliyepewa nafasi awe bora zaidi ya wale waliompa nafasi hiyo?

Kuna utamaduni ama mazoea mabaya ambayo yamejengeka kwenye jamii yetu yanayowafanya viongozi kujiona ni bora kuliko wale wanaowaongoza. Au kujiona ni muhimu zaidi ya wale ambao wamewapa nafasi ya kuwawakilisha.

Haya ni mazoea mabaya sana ambayo yalipata nafasi kutokana na watu wengi kutokuwa na uelewa mzuri kwenye mambo ya uongozi. Ila kwa sasa asilimia kubwa ya watu wana uelewa mzuri sana juu ya wajibu wao na wajibu wa viongozi wao.

Hivyo kwa kizazi kipya cha viongozi ni vyema tukafahamu huu mtazamo wa zamani wa uongozi umekufa na hautoweza kukusaidia. Wewe kama kiongozi unayejitengeneza jua watu ni muhimu kama ulivyo wewe kiongozi. Watu wana nafasi kubwa sana kwenye mafanikio ya uongozi wako.

Ule utamaduni wa viongozi kutaka kupata huduma bora kwa sababu wao ni viongozi hauwezi kukujenga na kukupa mafanikio. Kwa kusema hivi pia sisemi kiongozi apate huduma mbovu ili aonekane yuko na wananchi. Bali kiongozi ahakikishe wananchi wanapata huduma bora kama anazopata yeye.

Lakini hili halitokei kwa sababu baada ya kiongozi kupata huduma bora anasahau kwamba wananchi wanapata huduma mbovu. Na hata akiambiwa haoni uzito sana kwa sababu huduma hizo mbovu hazimuumizi moja kwa moja.

Ni mara ngapi tumeona mtu akiwa na uchungu sana kabla ya kuwa kiongozi ila anapokuwa kiongozi anasahau yale aliyokuwa anayalalamikia? Wanasema madaraka matamu, ila usianguke kwenye shimo hili. Jua watu unaowaongoza ni muhimu sana kama ulivyo wewe na baada ya kujua hili hakikisha unafanya kila juhudi kulinda umuhimu wao.

Karibu katika darasa letu la uongozi ambapo kila jumapili unapata makala nzuri inayohusu uongozi. Tembelea mtandao huu kila mara ili kujifunza mengi zaidi. Karibu tujenge kizazi kipya cha uongozi ambao utaleta tija kwenye nchi yetu Tanzania.

Sunday, April 20, 2014

Dalili Kumi Kwamba Tayari Wewe Ni Kiongozi.

Kwenye makala zilizopita tumeona ni muhimu sana kwa kila mmoja wetu kuwa kiongozi. Pamoja na umuhimu huo sio watu wote ni viongozi na sio watu wote wataweza kuwa viongozi. Na hata ambao ni viongozi sio wote ni viongozi bora wanaotoa matokeo mazuri.

Pia tumejifunza kwamba kiongozi anaweza kuzaliwa au kutengenezwa. Kutegemea na mazingira na uhitaji wa mtu, mtu yeyote anaweza kuendeleza tabia za uongozi ndani yake.

Leo tutaona dalili kumi za sifa ya uongozi. Kama wewe una sifa hizi tayari wewe ni kiongozi na unahitaji kujiendeleza zaidi ili kuweza kufanya makubwa zaidi kwenye uongozi wako. Kama huna dalili hizi kuna habari nzuri na mbaya kwako.

Habari mbaya kwako ni kwamba utaendelea kuwa mfuasi maisha yako yote na kwa nafasi kubwa utashindwa kuonesha uwezo wako wa kweli na kuleta tofauti kubwa kwenye jamii yako na dunia kwa ujumla.

Habari nzuri ni kwamba unaweza kujifunza tabia hizi na ukawa kiongozi bora sana. Uzuri ni kwamba kila kitu unaweza kujifunza, ni utayari wako na juhudi zako ndivyo vitakufanya uweze kujua kile unachotaka kujua. Njia bora ya kujifunza uongozi ni kujua vitu na kuvifanyia kazi. Hutakuwa kiongozi kwa kusoma tu hapa, bali soma na utumie yale unayojifunza kwenye maisha yako ya kila siku.

Kwa kifupi sana naomba nitaje dalili kumi zinazoonesha kwamba wewe ni kiongozi. Kwa maelezo zaidi tunaweza kujadiliana kwenye maoni hapo chini.

1. Unapenda kuleta mabadiliko.

2. Una ndoto kubwa sana mpaka wengine wanaona haziwezekani.

3. Husubiri kuambiwa nini cha kufanya,

4. Unapenda kutatua matatizo yanayowasumbua wengine.

5. Hupendi kulalamika au kulaumu wengine.

6. Unajali sana na kukuza mahusiano.

7. Matendo yako na maneno yako vinaendana.

8. Hukubaliani na mifumo isiyo na tija.

9. Uko tayari kukiri makosa na kuomba radhi.

10. Unapenda kujifunza mambo mapya na kuhusu uongozi.

Kama una dalili hizo kumi hongera wewe ni kiongozi. Kama huna usikate tamaa bado una nafasi kubwa ya kujijengea uongozi.

Uongozi unaanza na kuchagua kuwa kiongozi, baada ya hapo unaendelea kujifunza na kupata uzoefu. Karibu kwenye mafunzo ya kuongozi kupitia blog hii. Ili kuhakikisha hukosi mafunzo haya weka email yako hapo juu kwenye blog ili upate makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

TUKO PAMOJA.