tag:blogger.com,1999:blog-55922481177367493372024-02-19T10:08:34.096+03:00Makirita AmaniLisha Ubongo Wako, Badili Fikra Zako, Boresha Maisha yako.Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.comBlogger736125tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-10423048193059011482015-07-18T20:05:00.001+03:002015-07-18T20:05:11.312+03:00Nakukumbusha Kwamba Tumeshahama hapa.<p dir="ltr">Habari za leo mpenzi msomaji wa blog hii.<br>
Napenda kukumbusha kwamba blog hii sasa imehama na makala zotye zinapatikana kwenye <a href="http:// www.kisimachamaarifa.co.tz">www.kisimachamaarifa.co.tz</a><br>
Kwa wale ambao walikuwa wanapokea makala kwa email, unapoenda kwenye KISIMA CHA MAARIFA kuna sehemu ya kuweka email yako ili uendelee kupata makala kila zinapotoka.<br>
Nakutakia kila la kheri.<br>
TUPO PAMOJA.</p>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-47484193579292592802015-07-17T18:37:00.000+03:002015-07-17T18:37:03.406+03:00UKURASA WA 198; Tuko Upande Mmoja.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Katika shule moja kulikuwa na kundi la wanafunzi watukutu ambao
walikuwa wakionea wanafunzi wenzao. Wanafunzi hao walikuwa wakikuta mwanafunzi
mwingine wanamlazimisha achague wa kupigana naye na akikataa wanampiga
wote.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Siku moja kundi hili walikutana na mwanafunzi mmoja aliyeonekana
kuwa mnyonge sana. Wakamwambia achague wa kupigana naye. Yule mwanafunzi
akachora mstari na kusema yule ambaye anajiona ndio mbabe kuliko wote avuke huu
mstari. Yule ambaye ndio alikuwa mbabe alivuka mstari ule na alipofika upande wa
pili yule mwanafunzi mnyonge alimwambia sasa tupo upande mmoja, tuungane
kupambana na hao wengine.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Maisha ndivyo yalivyo, sisi wote tuko upande mmoja. Na watu wote
wanaokuzunguka mpo nao upande mmoja. Sema watu hatuelewi hili na ndio maana
tumekuwa tunashindana lakini hatufiki mbali.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama wanandoa wangejua kwamba wapo upande mmoja, wa kutaka
maisha yao wote kuwa bora basi matatizo mengi sana ya ndoa yasingekuwepo na ndoa
zingedumu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama mwajiri na mwajiriwa wangejua wapo upande mmoja, kunufaisha
kazi yao na maisha yao kwa ujumla, basi kungekuwa na ufanisi mkubwa sana kwenye
eneo la kazi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama mfanyabiashara na mteja wake wangejua kwamba wapo upande
mmoja basi biashara zingeendeshwa kwa mafanikio makubwa kwa wote wawili.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Lakini mara nyingi tunafikiri kwamba tuko pande tofauti na hivyo
kuishia kushindana, mashindano ambayo hayamfaidishi hata mmoja wetu.</span>
<br />
<blockquote class="tr_bq">
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua kwamba wale wote ambao wamenizunguka tupo upande mmoja.
Mwenza wangu, wateja wangu, mwajiri/mwajiriwa wangu wote tupo upande mmoja. Kila
mara nitajitahidi kuelewa upande tuliopo ili iweze kutusaidia kuboresha maisha
yetu sote.</span>
</blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 199 kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-32802803694999635912015-07-17T07:33:00.002+03:002015-07-17T07:33:35.114+03:00Tangazo muhimu kuhusiana na blog zinazoendeshwa na AMKA CONSULTANTS.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Habari za leo mpenzi msomaji wa blog mbalimbali zinazoendeshwa
na <a href="http://amkaconsultants.blogspot.com/" target="_blank">AMKA
CONSULTANTS</a>. Naamini unaendelea vizuri na harakati zako za kuboresha maisha
yako. Na pia naamini TUPO PAMOJA ukiendelea kujifunza na kuhamasika kupitia
makala mbalimbali zinazopatikana kwenye blog zako zinazoendeshwa na AMKA
CONSULTANTS.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama unavyojua lengo kubwa la AMKA CONSULTANTS ni kukuwezesha
wewe kuishi maisha bora sawa sawa na uwezo wako. Hapo ulipo una uwezo mkubwa
sana wa kufanya mambo makubwa zaidi ya unavyofanya sasa. Ila mfumo wa elimu
uliopitia na malezi uliyokulia vimekufanya ushindwe kufikia uwezo wako
mkubwa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama umekuwa unafuatilia blog zetu mbali mbali na ukawa
unafanyia kazi yale ambayo umekuwa unajifunza, utakubaliana nami kwamba maisha
yako umeona yanabadilika, hata kama ni kwa kiasi kidogo. Kama hiki ndio
kinachotokea kwenye maisha yako basi nakusihi endelea kufanyia kazi na utazidi
kuona mabadiliko makubwa zaidi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">AMKA CONSULTANTS ilianza na blog ya <a href="http://www.amkamtanzania.com/" target="_blank">AMKA MTANZANIA</a> na baadae
zilianzishwa blog nyingine kutokana na mahitaji tofauti ya wasomaji wetu. Blog
hizo ni <a href="https://www.blogger.com/www.kisimachamaarifa.co.tz">KISIMA CHA MAARIFA</a>, ambayo
unalipia kuwa mwanachama, <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/" target="_blank">MAKIRITA AMANI</a> na <a href="http://www.jiongezeufahamu.blogspot.com/" target="_blank">JIONGEZE
UFAHAMU</a>.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kupitia blog hizi umekuwa unajifunza mambo mengi na mazuri sana.
Kwa sababu makala zinazowekwa kwenye blog hizi zinatofautiana na zinalenga
maeneo tofauti tofauti ya maisha yako ikiwemo kazi, biashara na hata maisha kwa
ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Napenda kuchukua nafasi hii kuwajulisha wasomaji wote kwamba
kutakuwa na mabadiliko kwenye blog hizi zinazoendeshwa na AMKA CONSULTSNTS.
Makala ambazo zilikuwa zinawekwa kwenye JIONGEZE UFAHAMU sasa zitahamishiwa
kwenye AMKA MTANZANIA na makala zilizokuwa zinawekwa kwenye MAKIRITA AMANI sasa
zitahamishiwa kwenye <a href="https://www.blogger.com/www.kisimachamaarifa.co.tz">KISIMA CHA
MAARIFA</a>. Na blog hizi mbili, MAKIRITA AMANI na JIONGEZE UFAHAMU
zitafutwa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>Kwa nini mabadiliko haya?</strong></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama umekuwa msomaji mzuri wa blog hizi utakuwa uliona tatizo
ambalo lilijitokeza kama mwezi mmoja uliopita. Wasomaji ambao walikuwa wanapokea
makala za blog moja wapo kwa email ghafla waliacha kupata makala. Wakati huo
makala zilikuwa zinatumwa kama kawaida. Kutokana na tatizo hili ilibidi kutafuta
suluhisho la haraka ili wasomaji waendelee kupata makala zetu nzuri. Tulipata
suluhisho la muda lakini halitadumu kwa muda mrefu, siku zio nyingi tutaingia
tena kwenye tatizo kama lile. Na hii inatokana na sababu ya pili ya kuondoka
kwenye blog hizi ambayo ni kuwa zimekuwa zinaendeshwa bure.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Blog inapokuwa imehifadhiwa bure na kutumia jina la bure, kuna
baadhi ya vitu huwezi kuvibadili. Sasa hili linakwenda tofauti na kile ambacho
nataka wewe msomaji ukipate. Kuna wakati nataka kufanya kitu ambacho ni cha
tofauti lakini nashindwa kwa sababu blog imehifadhiwa bure na hivyo huwezi
kubadili baadhi ya vitu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sababu nyingine ni kwamba nina sehemu kubwa ya kuhifadhi blog
hizi ambayo ninailipia kila mwaka ambayo kwa sasa imehifadhi KISIMA CHA MAARIFA,
sasa ni vyema kutumia sehemu hii ambayo tunailipia gharama kubwa kuweka mafunzo
ambayo yataendelea kuboresha maisha yako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Na sababu ya mwisho tunayoweza kujadili hapa ambayo imepelekea
kufanya mabadiliko haya ni wewe msomaji uweze kupata makala zote nzuri kwenye
blog chache. Ni kweli kuna umuhimu wa kutenganisha mambo lakini ni vyema wewe
kama msomaji ukijua unapata makala zako zote nzuri kwenye sehemu chache ambazo
unaweza kuzitembelea kila siku na kutumia muda wao vizuri.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;"><strong>KISIMA CHA MAARIFA ni kulipia, je sisi tuliokuwa
tunapata makala bure ndio mwisho?</strong></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ni kweli kabisa ili uweze kusoma makala kwenye <a href="https://www.blogger.com/www.kisimachamaarifa.co.tz">KISIMA CHA MAARIFA</a> inabidi uwe umejiunga
na ulipie. Ila kwa sasa kwa kipengele hiki cha KURASA 365 ZA MWAKA 2015 wasomaji
wote wataendelea kuzipata hata kama hawajajiunga na kulipia. Ila nakusihi sana
kama bado hujajiunga na KISIMA CHA MAARIFA ufanye hivyo mara moja kwani unakosa
mengi na utaendelea kukosa mengi. Bonyeza maandishi haya <a href="http://www.kisimachamaarifa.co.tz/karibu-kwenye-kisima-cha-maarifa/">KUJIUNGA
NA KISIMA CHA MAARIFA</a>. Kuendelea kupata makala za KURASA 365 hakikisha
unatembelea <a href="https://www.blogger.com/www.kisimachamaarifa.co.tz">KISIMA CHA MAARIFA</a> kila
siku, na pia jiunge kwa kuweka email yako unapokuw akwneye KISIMA na utatarifiwa
kila makala inapokwenda hewani.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Asante sana kwa kuendelea kujifunza na kufanyia kazi yale ambayo
yanawekwa kwenye mitandao hii. Tunaendelea kukuahidi kwamba tutakuletea makala
bora kabisa zitakazo boresha na kubadili maisha yako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Makirita Amani,</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-41410721179228386652015-07-16T18:36:00.001+03:002015-07-16T18:36:20.079+03:00UKURASA WA 197; Una Sababu Moja Tu, Nyingine Zote Ni Kuchagua.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Umekuwa ukisikia mara nyingi kwamba kosa sio kutenda kosa, bali
kosa ni kurudia kosa. Hii ikiwa na maana kwamba unapofanya jambo kwa mara ya
kwanza na ukapata majibu ambayo hukutegemea kupata, tunaweza kukusamehe. Ila
tunatarajia kwamba uwe umejifunza kwamba njia uliyotumia mwanzo haileti majibu
unaotaka.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sasa kama wewe utarudia tena kufanya vile vile na ukapata majibu
yale yale ambayo hukuyataka ndio tunasema kwamba wewe unafanya makosa. Nafikiri
tumeelewana vizuri hapo kwenye kosa, na unajua ni makosa gani ambayo umechagua
kuwa unayafanya tena na tena.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sasa leo nataka nikuambie kitu kingine kizuri ambacho kinaweza
kuendana na hiko. Una sababu moja tu, nyingine zote ni kuchagua mwenyewe. Kwa
maana nyingine unaweza kuwa na kisingizio mara moja tu, baada ya hapo umeamua
mwenyewe na huna sababu au kisingizio chochote.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa mfano; kwa nini kila siku unasema utaanza biashara ila
huanzi? Sababu ya kweli, sina mtaji. Swali hilo tena miaka mitano baadae, kwa
nini mpaka sasa hujaanza biashara... hapa ukisema tena huna mtaji sio sababu
tena, maana yake unajua kabisa kwamba huna mtaji na hufanyi jitihada zozote
kutafuta mtaji huo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Usipende kutafuta sababu(visingizio), ila kama haikwepeki, basi
sababu iwe mara moja tu. Kama utaendelea kutuambia sababu ile kila siku sio
sababu tena bali umeamua kuishi maisha hayo. Hivyo tafadhali sana, usitupigie
tena kelele, tumeshasikia sababu yako na umeshatuambia kwamba umekubali kuishi
nayo.</span>
<br />
<blockquote class="tr_bq">
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua nina nafasi moja tu ya kuwa na sababu au kisingizio. Ila
baada ya hapo siwezi tena kutumia kisingizio hiko kwa sababu nitakuwa nimeamua
mwenyewe. Kuanzia leo nitakwepa kutoa sababu na kama sababu haikwepeki nitatoa
mara moja tu.</span>
</blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-72094236794056603102015-07-15T12:00:00.000+03:002015-07-15T12:00:03.227+03:00UKURASA WA 196; Kama Huwezi Kujibu Swali Hili Hujui Maisha Yako Yanakoelekea.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Siku zote huwa nasema kwamba kuna ‘emergency’ chache sana kwenye
maisha. Ile hali kwamba jambo limetokea na watu wanashangaa limetokeaje ni
kuamua tu kutumia unafiki wetu wenyewe.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Ni sawa na shimo ambalo lipo njiani kwa muda mrefu lakini watu
wanaliangalia tu, siku moja linasababisha vifo watu wanasema ni ajali. Hapana
sio ajali, ni watu wamechagua kufa kwa njia hiyo. Kwa sababu shimo lilikuwa
linaonekana siku zote, lakini hakuna aliyejali.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hivyo hivyo kwenye maisha yako, kuna vitu vingi sana ambavyo
unavipuuzia kwa sasa lakini kuna siku vitakukaba sana. Na wakati huo ndio
utaanza kuhangaika, utaanza kusumbua wengine kwamba kwa nini hawachukulii hali
yako kwa tahadhari. Bila ya wewe kujua na kukubali kwamba hakuna tahadhari kubwa
ila ni kitu ulichotengeneza wewe mwenyewe.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kila siku inayoanza jiulize swali hili muhimu sana, je mambo
haya ninayofanya leo hayatengenezi tahadhari siku ya kesho? Au siku zijazo?
Mambo ninayoyapuuza leo hayajitengenezi na kuwa makubwa halafu siku moja
yakanizidi?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ni kawaida ya binadamu kufanya vitu kwa mazoea ila mambo
yanapokuwa magumu tunasahau kwamba tumeyatengeneza wenyewe. Na kama wewe ni mtu
wa kulaumu utaanza kulaumu na uzuri ni kwamba hutakosa mtu wa kumlaumu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hakuna kitu kinachokea kwa ajali kwenye maisha yako, kila kitu
kinasababishwa na wewe mwenyewe ndiye unayesababisha. Kuwa makini na yale yote
unayofanya, yanaweza kukusababishia matatizo makubwa siku za mbeleni.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua chochote ninachofanya leo kina madhara kwenye maisha yangu
siku za baadae. Madhara haya yanaweza kuwa chanya au kuwa hasi. Nitahakikisha
maamuzi ninayofanya hayanipelekei kwenye madhara hasi ili niepuke kuwa na
dharura zisizo za msingi kwenye maisha yangu.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 196 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-88611471916763976492015-07-14T19:53:00.003+03:002015-07-14T19:53:51.827+03:00UKURASA WA 195; Dunia Inapenda Washindi, Usiumizwe Na Hilo.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Wakati unaweka juhudi za ziada zaidi ya wengine hakuna
atakayekutukuza, na wengine wengi watakukatisha tamaa.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Wakati wewe unafanya kazi wakati wengine wamepumzika,
wanastareheka hakuna atakayekuwa anakumulika, na wanaojua watakuwa wanakubeza na
kukuona hujui unachofanya.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama utaendelea kung’ang’ana na kuweka juhudi licha ya watu
kukususa na wengine kukukatisha tamaa, unajua ni nini kitatokea?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Mambo yako yatakuwa mazuri, utaanza kupata majibu tofauti na
wengine wanayopata, kila mtu ataanza kuona mafanikio yako. Na wakati huu unajua
ni kitu gani kitatokea?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kila mtu ataanza kukutukuza, kukusifu, huyu hakukata tamaa. Na
wanaokujua wataanza kusema tulijua tu atafika mbali, wakati hakuna hata siku
moja wamekutia moyo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Je utawachukia watu hawa kwa sababu ni wanafiki, wanakusifia
wakati tu umefikia mafanikio? Hapana usifanye hivyo, sio kosa lao, ndivyo dunia
ilivyowatengeneza. Dunia inapenda washindi, dunia haina muda na wanaoteseka,
wanaokazana na ukishindwa ndio kabisa utakuwa mfano wa kuwatisha wengine.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ufanye nini sasa? Endelea kuweka juhudi, endelea kushinda. Hata
pale wanapokusifia usione ndio umefika mwisho, wacha wao waendelee kutoa sifa,
na wewe endelea kuweka juhudi.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua dunia inapenda washindi. Hainisumbui kama sasa hivi hakuna
anayeniona pamoja na juhudi kubwa ninazoweka. Na hata nitakapofikia mafanikio na
waliokuwa wa kwanza kunicheka wakawa ndio wa kwanza kusema walijua nitafanikiwa
pia halitakuwa tatizo kwangu. Mimi nitaendelea kuweka juhudi bila ya kujali watu
wanasema nini.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 196 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-18088672550294563542015-07-13T15:01:00.003+03:002015-07-13T20:30:10.861+03:00UKURASA WA 194; Utaanza kuona fursa nzuri pale utakapofanya hivi.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Hivi ulishawahi kununua nguo ambayo uliona ni nzuri na ya
kipekee ila kila ulipopita mtaani ukaanza kuona karibu kila mtu anayo?</span><br />
<span style="font-size: medium;">Au labda unafikiria kununua kitu fulani mfano gari au vifaa,
mara ghafla ukiwasha tv unaona kitu kile, ukipita mtaani unaona kitu
kile?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Au umewahi kufikiria kufanya biashara fulani mara ghafla ukaanza
kuona kila unapopita unaona watu wanafanya biashara ile?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Je unafikiri vitu hivyo nimeanza kutoke kwa sababu wewe
unafikiria kufanya? Jibu ni hapana, vitu hivyo vilikuwepo kila siku, ila kwa
sababu hujawahi kuvifikiria na kuvizingatia basi umekuwa huvioni. Ila unapoanza
kuvifikiria au kuvizingatia sana macho yako yanafunguka na unaanza kuona vizuri
zaidi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/07/ukurasa-wa-190-huwezi-au-hutaki-kabla.html" target="_blank">Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha
Huponi.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuna fursa nyingi sana ambazo zinakuzunguka hapo ulipo. Ila kwa
sasa huzioni kwa sababu hujazingatia kuzifikiria. Anza kufikiria kitu fulani na
utaanza kuona kwamba kuna njia nyingi sana za kuweza kukipata au kukifanya kitu
hiko?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Unataka kuona fursa zaidi? Fungua akili yako, fungua mawazo yako
na macho yako yataanza kuona.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua nimekuwa sioni fursa nyingi kwa sababu macho yangu
hayajafunguliwa kuona. Nitayafungua sasa macho yangu kwa kuzingatia vitu
ninavyotaka, kuviweka kwenye akili yangu na macho yangu yatanionesha njia za
kufanya au kupata vitu hivyo.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 195 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-12123502808139114592015-07-12T08:15:00.001+03:002015-07-12T08:15:35.769+03:00UKURASA WA 193; Ushabiki Unavyokuzuia Kufikia Mafanikio.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Ushabiki umekuwa kikwazo kwa watu wengi sana kuweza kufikia
mafanikio makubwa. Watu wamekuwa wakijikuta wanalazimika kuacha mambo yao ya
msingi kwa sababu hataki kupitwa na kitu ambacho anashabikia.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuna watu ambao ni mashabiki wa mpira kiasi kamba hawezi kuacha
kuangalia timu yake inacheza hata kama kutakuwa na kitu gani anachofanya. Kuna
wengine ni mashabiki wa muziki, mashabiki wa tamthilia, mashabiki wa matamasha
mbalimbali na pia mashabiki wa siasa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sina tatizo na wewe kuwa shabiki, ila kama kweli lengo lako ni
kuwa na maisha bora na yenye mafanikio basi unatakiwa kufikiria mara mbili
kuhusu ushabiki wako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Fikiria kile unachoshabikia na jiulize, je kinakuongezea
maarifa? Je kinakuongezea kipato? Je kinafanya maisha yako na ya wengine kuwa
bora zaidi/ kama jibu ni hapana basi ushabiki huo usiwe kipaumbele kwenye maisha
yako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/07/ukurasa-wa-190-huwezi-au-hutaki-kabla.html" target="_blank">Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha
Huponi.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Mimi nilikuwa mshabiki wa tamthilia mpaka siku moja mtu
akaniambia(kupitia kitabu nilichokuwa nasoma), unapoangalia tv, kuna mambo
mawili yanatokea. Yule unayemwona kwenye kioo cha tv analipwa kwa wewe
kumwangalia na wewe unalipa kumwangalia mtu huyo. Je unataka kuwa upande upi?
Kulipa uangalie maisha ya wengine au kulipwa kwa watu kuangalia maisha yako?
Kuanzia hapa nilikata shauri la kutoangalia tamthilia tena, sijaziangalia tangu
mwaka 2012 na hakuna nilichokosa zaidi ya maisha yangu kuwa bora zaidi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Achana na ushabiki ambao hautaboresha maisha yako na anza leo
kuwa shabiki wako mwenyewe. Mimi ni shabiki namba moja wa Makirita Amani, huwa
sikosi chochote alichopanga kufanya na nitaahirisha vingine vyote ili
kuhakikisha namshabikia. Je shabiki wako namba moja ni nani?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Una muda mfupi sana kuanza kuugawa kwa kushabikia vitu ambavyo
havina msaada mkubwa kwenye maisha yako, hasa ambavyo unaweza kuvipata baadae.
Kwa mfano kama unashabikia timu ya mpira, badala ya kukesha ukiangalia mpira na
kesho yake ukashindwa kufanya kazi zako vizuri kwa nini usilale mapema na kesho
yake utayajua tu matokeo? Hakuna tofauti yoyote kuona magoli mawili yakifungwa
na kuja kuyaona kesho yake. Tena siku hizi mipira inarekodiwa kwa hiyo unaweza
kuangalia kwa muda wako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Narudia tena, usikubali ushabiki uharibu ratiba zako, una mengi
yakufanya, yape kipaumbele.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua ushabiki wangu umekuwa unanifanya nishindwe kufikia
mafanikio makubwa. Nimekuwa nashabikia mambo mengi sana. Nimekuwa naahirisha
mipango yangu kwa sababu tu nisipitwe na ushabiki. Leo naamua kwamba mtu wa
kwanza kumshabikia ni mimi mwenyewe. Sitakatisha ratiba zangu kwa sababu kuna
kitu nakishabikia. Nitaendelea na mipango yangu na ninajua nitafahamishwa kila
kinachoendelea.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-84742823008566938732015-07-11T16:53:00.002+03:002015-07-11T16:53:22.166+03:00UKURASA WA 192; Tatizo La Kuweka Kipimo Cha Furaha, Na Kwa Nini Hukifikii.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kuna watu ambao huwa wanaweka furaha kwenye kipimo. Mtu
anafikiri nikishapa kitu fulani basi nitakuwa na furaha sana.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa hiyo huwa inaanza hivi;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Uko mtoto mdogo unatamani sana kwenda shule unasema nikianza
darasa la kwanza nitafurahi sana. Unaanza na unagundua hakuna kitu cha tofauti
sana. </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Unaendelea na shule kwa miaka saba, unapokaribia mwisho
unasubiri kwa hamu sana ukisema nikimaliza darasa la saba tu, nitakuwa na raha
sana. Unamaliza na unaona kumbe kilikuwa kitu cha kawaida sana.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Unaanza sekondari unasoma na kufikiria nikimaliza tu, nitakuwa
na raha, unamaliza na maisha ni yale yale.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://www.amkamtanzania.com/2015/07/ndege-wa-angani-hawalimi-ila-wanakula.html" target="_blank">Ndege Wa Angani Hawalimi Ila Wanakula, Kuna Mambo Haya Matano(5)
Pia Wanakuzidi Ujanja.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hivyo hivyo mpaka unaingia chuoni, unafikiria nikimaliza na
nikapata kazi, maisha yangu yatakuwa ya furaha sana. Unamaliza na labda unapata
kazi na unakuta ni kawaida tu na huenda ukakutana na changamoto nyingi
zaidi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hivyo pia inakuwa kwenye kila kitu unachofanya kwenye maisha
yako, unafikiri ukipata kitu fulani utakuwa na furaha, ila unakifanya na
unagundua kuna kingine zaidi cha kufanya.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ni vigumu sana kupima furaha kwa vipimo hivi hasa pale
unaposogeza kipimo kila unapokifikia.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Wakati sahihi kwako kuwa na furaha ni sasa hivi, hapo ulipo na
unaposoma hii. Na utakapotoka hapo kila wakati kuwa na furaha. Kama unafikiria
utaipataje furaha chukua kalamu na karatasi na andika vitu kumi unavyoshukuru
kuwa navyo hapo ulipo. Huenda ni kazi au biashara inayokupatia fedha za
kuendesha maisha, huenda ni familia inayokupenda, huenda ni marafiki mnaopendana
na kadhalika.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Huwezi kupima furaha na ukaipata, furaha ipo ndani yako, ni wewe
kuifikia na kuiishi.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuanzia sasa naacha kupima furaha kwa sababu nimegundua kwamba
kuweka kipimo kwenye furaha ni sababu namba moja ya kushindwa kuifurahia. Hapa
nilipo nina furaha kwa sababu nina vitu hivi vifuatavyo(soma orodha yako ya vitu
kumi). </span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-29239667663364750102015-07-10T14:03:00.002+03:002015-07-10T14:03:52.115+03:00UKURASA WA 191; unalipwa kwa sababu unaonekana au kwa sababu unatoa thamani?<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Swali muhimu sana hilo kujiuliza kama hujawahi kufanya hivyo.
Ngoja nikuulize tena vizuri ili twende sawa,</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Je unalipwa mshahara kwa sababu unaonekana kazi au kwa sababu
una thamani unayotoa kwenye kazi yako? </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Je mteja wa biashara yako ananunua kutoka kwako kwa sababu
amekuona na wewe unafanya biashara au kwa sababu kuna thamani anaifuata?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Jipe muda wa kujibu swali hili, maana ndio msingi wako wote wa
mafanikio umelala hapo.</span>
<br />
<b><span style="font-size: medium;">Kulipwa kwa kuonekana.</span></b>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hapa ni pale unapotegemea malipo kwa sababu tu umeonekana
kazini, au kwa sababu tu na wewe unauza. Hivyo kinachotokea ni wewe kujionesha
kwamba na wewe upo. Kama ni kazini basi unahakikisha unaonekana una kazi nyingi
na upo bize kumbe hakuna thamani kubwa unayotengeneza. Ukiwa mtu wa aina hii
inakubidi uonekane una juhudi sana kumbe ukweli sio hivyo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama ni biashara unakazana kutangaza ili uonekane na wewe
upo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Tatizo la kutegemea kipato kwa njia hii ni kwamba huwezi kupata
kipato kizuri na huwezi kujiamini.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/05/ukurasa-wa-146-ukiendelea-na-maisha.html" target="_blank">Ukiendelea Na Maisha Haya Watu Watakunyanyasa Sana…</a></span>
<br />
<b><span style="font-size: medium;">Kulipwa kwa kuongeza thamani.</span></b>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hiki ndio wanachofanya watu wote wenye mafanikio. Hawaendi
kazini ili waonekane na wao wamekuja, ila wanakwenda pale kuleta mabadiliko.
Kuongeza thamani kwenye kile wanachofanya na hivyo kuwanufaisha wengi
zaidi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama ni wafanyabiashara wanakazana kutatua matatizo
yanayowasumbua wengi. Na kwa kuwa suluhisho lao ni bora watu wanakuwa
wanawatafuta wenyewe.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Na kwa upande wa kipato, watu hawa wao wenyewe ndio wanaamua
walipwe kiasi gani, wakitaka kuongezwa kipato wanaongeza thamani
wanayotoa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Je umeshajua uko wapi? Kazana kuongeza thamani na sio kukazana
kuonekana. Unapokazana kuonekana maana yake unapiga kelele. Unapokazana kuongeza
thamani umuhimu wako pia unaongezeka. Na kila mtu atataka kufanya kazi na wewe.
Na utaanza kupanga ulipwe kiasi gani.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua njia bora ya kutengeneza kipato sio kwa kuonekana bali kwa
kuongeza thamani. Kuanzia sasa nitakuwa nakazana kuongeza thamani na sio
kuwapigia watu kelele ili wajue kama nipo. Najua nitakapotoa thamani kubwa na
kipato changu pia kitaongezeka.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 192 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-63808584727497030672015-07-09T15:23:00.002+03:002015-07-09T15:23:58.328+03:00UKURASA WA 190; Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha Huponi.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Mpaka sasa umeshajifunza mambo mengi sana kuhusu mbinu za
kuboresha kazi yako, biashara yako na hata maisha yako kwa ujumla. Lakini mbona
bado huchukui hatua yoyote ili kuweza kunufaika na yale ambayo
unajifunza?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Mpaka sasa unajua kabisa ya kwamba kwa kufanya kile ambacho kila
mtu anafanya utaendelea kupata matokeo ambayo kila mtu anayapata na ambayo sio
mazuri sana. Lakini mbona unaendelea kufanya hivyo?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/06/ukurasa-wa-167-maisha-ni-mchezo-na.html" target="_blank">Maisha Ni Mchezo Na Sheria Za Kuushinda.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Mpaka sasa unajua kabisa kulalamika au kulaumu wengine
hakutakupatia wewe chochote unachotaka, sana sana kutakufanya ujione kama yatima
ambaye hana msaada wowote. Lakini bado unaendelea kulalamika na kulaumu, kwa
nini?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa sababu huwezi!! Hili ndio jibu ambalo unajiridhisha nalo.
Kwamba siwezi kufanya tofauti, kila mtu ameshazoea vile nilivyo. Kwamba siwezi
kuweka muda zaidi kwenye kujifunza, kwa sababu nina mambo mengi ya kufanya.
Kwamba siwezi kuacha kuangalia tv kila siku, nitapitwa na mambo mengi. Kwamba
siwezi kuacha kukaa na jamaa zangu kila siku jioni tukipata moja moto na moja
baridi ili nifuatilie zaidi biashara na kazi zangu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama haya ndio majibu yako, kwanza wewe mwenyewe unayaamini
kweli? Ni kweli kwamba huwezi kufanya mambo hayo ambayo yatabadili kabisa maisha
yako? Vipi kama maisha yako ndio yangekuwa yanategemea hivyo ndio uweze kuishi.
Kwa mfano unaambiwa kuchagua kuishi ila usiangalie tv au uangalie tv halafu
unakufa, ungechagua nini?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua ungechagua kutokuangalia tv, safi sana, una maamuzi
mazuri. Na ndio maana mimi siamini kwamba yale yote unayosema huwezi ni kwamba
huwezi kweli, bali ni kwamba hutaki tu kufanya.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa hiyo mambo yote unayosema kwamba huwezi, ukweli ni kwamba
hutaki tu kufanya. Na kwa maana hii basi nakuomba kuanzia leo usiseme tena
SIWEZI, sema SITAKI.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Siku nyingine kabla hujaniambia huwezi hakikisha kwamba ukifanya
kitu hiko unakufa, vinginevyo ni sitaki.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua hakuna kitu kizuri na cha kubadili maisha yangu ambacho
siwezi kufanya. Vingi ninavyoona siwezi kufanya ni kwamba sitaki tu kufanya. Kwa
sababu kama maisha yangu yangekuwa yanategemea vitu hivyo ni lazima ningefanya.
Hakuna kinachonishinda kufanya, na kuanzia sasa nitaacha kutumia sababu hii
kwamba siwezi.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 191 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-22433704047588826592015-07-08T13:36:00.002+03:002015-07-08T13:36:59.686+03:00UKURASA WA 189; Matatizo Yote Ya Mahusiano Yanaanzia Hapa... Sehemu Ya Pili(2)<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Jana nilikushirikisha sababu kubwa ya matatizo kwenye mahusiano
yetu sisi na watu wengine. Na kama ukiweza kuondokana na chanzo kile basi
utapunguza sehemu kubwa sana ya matatizo kwenye mahusiano yako iwe ya kikazi,
kibiashara, kindugu au kimapenzi. Kama hukupata nafasi ya kusoma kile
tulichojadili jana basi kisome hapa; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/07/ukurasa-wa-188-matatizo-yote-ya.html" target="_blank">Matatizo Yote Ya Mahusiano Huanzia Hapa.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Leo nataka tugusie kitu kingine kikubwa sana kinacholeta
matatizo kwenye mahusiano yetu. Najua eneo la mahusiano ndio eneo gumu sana
kuelewana na watu kwa sababu moja kubwa, inapokuja swala la mahusiano watu
hawatumii akili kufikiri, bali wanatumia hisia kufikiri. Na pale hisia
zinapojiongoza zenyewe bila akili basi hapo ni majanga. Ndio maana ni vigumu
sana kuweza kumweleza mtu kuhusu mahusiano hasa ya mapenzi akakuelewa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sasa sababu nyingine kubwa ambayo inasababisha matatizo kwenye
mahusiano ni watu kuvaa visanamu mwanzoni mwa mahusiano. Watu wanapokutana ili
kujenga uhusiano, wengi wanadanganya, wanasema vitu ambavyo vitawafanya
wakubalike au kupendwa na wale wanaotaka kuwa na mahusiano nao. Hii ni kwenye
mahusiano yote, iwe ya kazi, biashara au hata mahusiano mengine ya
karibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://jiongezeufahamu.blogspot.com/2014/10/katika-kula-ujana-usifanye-mambo-haya.html" target="_blank">Katika Kula Ujana Usifanye Mambo Haya Matano, Utajutia Maisha Yako
Yote.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Mtu anadanganya kwenye usaili wa kazi ili aonekane ni bora na
kupewa kazi. Labda hudanganyi vitu vikubwa, ni vitu vidogo vidogo tu kama
kuahidi vitu ambavyo unajua kabisa huwezi kufanya kwa muda mrefu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Au kwenye biashara unamdanganya mteja kwamba unaweza kufanya
kitu fulani ili akubali kufanya biashara na wewe. </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwenye mapenzi sasa, ndio mtu atadanganya vitu vingi sana,
atabadili mpaka mfumo wa maisha, kuacha baadhi ya vitu na kadhalika.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Mambo yangekuwa rahisi sana kama kila mtu angeweza kuishi na
hiki alichoahidi anaweza kufanya. Lakini kama tulivyoona jana, watu
hawabadiliki, tena kwa haraka hivyo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa hiyo mtu atafanya kile alichosema kwa muda mfupi baada ya
hapo anachoka na hivyo kurudia maisha yake ya zamani. Hapa ndio utasikia siku
hizi fulani kabadilika. Hapana hajabadilika, amechoka kuvaa kile kisanamu na
sasa ameanza kuonesha ukweli wake.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuwa makini usivae kisanamu wakati unataka kujenga mahusiano
ambayo yatadumu. Kuwa mkweli, kama mtu hawezi kukukubali kwa ukweli wako hata
ukimdanganya huo uhusiano hautadumu. Nasisitiza tena hii sio kwa mapenzi tu,
bali kwenye mahusiano ya kazi, biashara na hata maisha ya kawaida. Kuwa mkweli
na utawavutia wale wa kweli. Vaa kisanamu na utavutia visanamu vingine.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua kwamba kudanganya mwanzoni mwa mahusiano ni kujenga kifo
cha mahusiano hayo. Hakuna uongo unaoweza kudumu kwa muda mrefu. Nitakuwa mkweli
siku zote ili niweze kujenga mahusiano bora na yatakayoniletea mafanikio. Hata
kama kuwa kwangu mkweli kutanikosesha baadhi ya mahusiano, najua kutanijengea
mahusiano ambayo ni bora.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-42441102291166683032015-07-07T14:09:00.001+03:002015-07-07T14:09:53.768+03:00UKURASA WA 188; Matatizo Yote Ya Mahusiano Huanzia Hapa.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kama kuna kazi ngumu hapa duniani basi ni kuishi. Ndio maisha ni
mazuri na ndio maisha ni matamu ila ni kazi kubwa sana kuweza kuyaishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ni kazi kubwa kuyaishi kwa sababu huwezi kuishi maisha ya peke
yako. Umezungukwa na watu wengi na watu hawa wana tabia tofauti tofauti. Watu
wote hawafanani tabia.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuna wakati unafikiri kama watu wote wangekuwa kama fulani basi
mambo yangekuwa mazuri sana. Saa nyingine unafikiria kama wateja wote wangekuwa
kama mteja fulani basi biashara ingekuwa nzuri sana. Au wakati mwingine
unafikiria kama bosi wako angekuwa na roho ya tofauti na aliyonayo sasa basi
maisha yako ya kazi yangekuwa mazuri sana.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Lakini ukweli ndio huo kwamba watu hatufanani na pamoja na
tofauti zote hizo bado unahitaji kushirikiana na watu wote hao.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://jiongezeufahamu.blogspot.com/2015/01/tabia-saba-za-watu-wasiokuwa-na.html" target="_blank">Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Matatizo yote ya kwenye mahusiano, yawe ya kindugu, ya
kibiashara, ya kikazi au hata ya kimapenzi yanaanzia pale mtu mmoja anapotaka
kumbadilisha mwingine. Yaani ikishafikia hatua hii kwamba mtu mmoja anataka
mwingine abadilike, ndio matatizo makubwa sana yanaibuka.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Unajua ni kwa nini? Kwa sababu mwanadamu atafanya kitu chochote
kile kinachowezekana ili mradi tu asibadilike. Watu hawapendi kubadilishwa na
wanapenda kuendelea kuwa vile walivyo. Tena kama ndio mtu mzima, ndio basi
kabisa, atahakikisha anakataa kubadilika hata kama kufanya hivyo kunagharimu
maisha yake.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Wakubali watu vile walivyo, au kama huwezi kuwakubali walivyo
achana nao. Kama wataona wewe ni wa muhimu sana na hawawezi kukupoteza basi
watabadilika wao wenyewe. Na mtu anapoamua yeye mwenyewe kubadilika inakuwa
rahisi kwake kubadilika hata kwa kiasi kidogo. Ila kama wewe ndio unamlazimisha
mtu abadilike, okoa nguvu zako.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua matatizo makubwa kwenye mahusiano ya watu huwa yana anza
pale watu wanapojaribu kuwabadilisha wengine. Najua ya kwamba binadamu hawapendi
kubadilishwa. Sitapoteza nguvu zangu kutaka kumbadilisha mtu. Nitamkubali mtu
kama alivyo na kama siwezi nitaachana naye iwe ni mteja, bosi, ndugu au mwingine
wa karibu. Muda wangu ni wa thamani sana siwezi kuupoteza kwa kufanya kazi
ambayo haileti matunda.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-12028585372531818382015-07-06T12:00:00.000+03:002015-07-06T12:00:01.798+03:00UKURASA WA 187; Usikubali jua lizame leo kabla hujafanya kitu hiki muhimu.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Siku ya leo kuna watu wengi sana watakaokuudhi. Kuna watu wengi
watakukasirisha na wengine watakufanya ujisikie vibaya sana. Kwa hasira
inayotokana na watu hawa unaweza kufanya maamuzi ambayo sio mazuri sana kwao na
kwako pia.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ila kumbuka mara nyingi unapokuwa na hasira huwezi kufanya
maamuzi ambayo ni sahihi. Na hata kama mtu atakuchukiza kiasi gani, hata kama
atakuudhi kiasi gani kwa wewe kuwa na hasira, kwa wewe kuendelea kuwa na
kinyongo naye haimuumizi yeye bali inakuumiza wewe mwenyewe.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/01/jicho-kwa-jicho-tutabaki-na-dunia-ya.html" target="_blank">JICHO KWA JICHO; Tutabaki Na Dunia Ya Vipofu.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sasa leo nataka nikupe kitu kimoja muhimu cha kufanya kabla jua
halijazama. Hakikisha jua linapozama umemalizana na kitu hiki ili siku yako ya
kesho iwe bora sana.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kabla jua halijazama leo hakikisha umewasamehe wote waliokukosea
leo. hakikisha umeondokana na vinyongo vyote ambavyo unaweza kuwa
umejitengenezea kwa siku ya leo. Acha mambo haya yote yazame na jua la leo, ili
jua linapochomoza kesho uanze siku yako ukiwa vizuri na uweze kufanya
makubwa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Usikubali jua lizame ukiwa bado na hasira au kinyongo. Vitu hivi
havikusaidii chochote zaidi ya kufanya maisha yako kuwa magumu na hata kuharibu
afya yako.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sitakubali siku ya leo na siku nyingine yoyote ipite nikiwa na
kinyongo au hasira kwenye moyo wangu. Jua litakapozama nitahakikisha nimeachia
yote niliyokumbana nayo siku ya leo. kama kuna mtu ameniudhi, amenikasirisha au
amefanya chochote ambacho kimenifanya niwe na kinyongo nitamsamehe. Maisha yangu
ni muhimu zaidi ya chuki ninazotaka kutengeneza na watu.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 188 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-44173530096054987722015-07-05T16:05:00.001+03:002015-07-05T16:17:48.828+03:00UKURASA WA 186; Kama Utashindwa Kufanya Chochote Utakachojifunza, Basi Fanya Hiki Kimoja Tu, Na Maisha Yako Yatagusa Wengine.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Nimekuwa nakushirikisha mambo mengi sana ambayo unahitaji
kuyafanya ili kuboresha maisha yako. Mambo haya yanahitaji wewe ubadilike, uanze
kufanya tofauti na ulivyozoea kufanya na sio kitu rahisi sana.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuacha kuangalia tv na kujisomea mambo yatakayokuweka mbele
zaidiinahitaji kujitoa kweli.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuacha kukaa na jamaa zako kila jioni mkipata moja moto na moja
baridi ili upate muda mwingi zaidi wa kuweka kwenye kazi au biashara yako sio
kitu rahisi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuacha kulalamika pale unapoona kabisa kwamba umeonewa au
umeumizwa inahitaji nguvu ya ziada.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuacha usingizi na kuamka asubuhi na mapema sana ili uweze
kujifunza na kuipangilia siku yako sio kitu rahisi kama unavyoweza
kufikiria.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Tuseme labda wewe umeona kwamba mambo haya yote huwezi, kwa
sababu tu una uvivu uliopitiliza au kwa kifupi basi tu hutaki kujihangaisha. Leo
nataka nikuambie kitu kimoja muhimu sana cha kufanya.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/02/kauli-kumi-za-marcus-aurelius.html"><span style="font-size: medium;">Kauli KUMI Za Marcus Aurelius Zitakazokufanya Uyaone Maisha Kwa
Utofauti.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Tafadhali sana hata kama una uvivu kiasi gani, jitahidi ufanye
kitu hiki kimoja na maisha yako yatagusa wengine kwa kiasi kikubwa sana.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kitu chenyewe ni kuishi maisha mazuri kwako na kwa
wanaokuzunguka. Kuwa mtu mwema, usimwibie mtu, usisengenye mtu, usijihusishe na
majungu. Saidia wengine kadiri ya uwezo wako. Yaani kuwa tu mtu mwema na wengine
waone wewe ni mfano wa kuigwa. Na hata kama kuna mtu amekosa tumaini kwa kuyaona
maisha yako atapata tumaini kwamba dunia bado ina watu wema waliomo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hili ni jambo muhimu kwetu sote kufanya hata kama unafanya hayo
mengine yote unayojifunza kila siku.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Nitahakikisha naishi maisha ambayo yatakuwa mfano mzuri kwa watu
wengine. Nitajiepusha na mambo ambayo sio mazuri kwangu na kwa wale
wanaonizunguka. Sitoiba wala kumdhulumu mtu, sitosengenya wala kushiriki majungu
na nitasaidia wengine kadiri ya uwezo wangu.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-29193145237758087952015-07-04T20:45:00.001+03:002015-07-04T20:45:34.792+03:00ONGEA NA KOCHA; Epuka Vipimo Hivi Viwili Ambavyo Jamii Inakupima Navyo.<p dir="ltr">#ONGEA_NA_KOCHA <br>
Kwa miaka mingi dunia imekuwa inatupima kwa mambo haya mawili makuu...<br>
Wanawake wamekuwa wakipimwa kwa kuonekano wao. Ni mzuri au sio mzuri?<br>
Wanaume wamekuwa wakipimwa kwa umiliki wao. Je ana hela au hana hela, ana mali au hana mali?<br>
Jamii nzima tumekuwa tukifanya hivi japo kwa unafiki tunaweza kukataa.<br>
Vipimo hivi vimekuwa vinawazuia watu wengi kushindwa kufikia mafanikio kwa sababu tu wanatengwa na vipimo hivi.<br>
Kama jamii inasema mwanamke mzuri ndio anaweza kuwa na maisha mazuri, kuna makabila mwanamke mweupe mahari yake ni kubwa kuliko mweusi, yule ambaye anakosa sifa hii atajiona hawezi kuwa na maisha mazuri.<br>
Kama jamii inasema mwanaume mwenye hela ndio wa maana, kwenye jamii zetu wanaosikilizwa ni wenye hela hata kama hawana mawazo mazuri, ambaye anakosa sifa hii atajiona yeye sio wa maana na hivyo kujiondoa kabisa kwenye njia ya mafanikio.<br>
Sasa mimi kama kocha wako nakutangazia rasmi kwamba achana kabisa na vipimo hivi vya hovyo.<br>
Wewe ni zaidi ya vipimo hivi vilivyowekwa na jamii. Haijalishi una uzuri au ubaya, wewe ni bora sana. Haijalishi una fedha au huna fedha wewe ni mtu wa kipekee.<br>
Endelea kuweka juhudi kwenye kile unachofanya na usikubali jamii ikuyumbishe na vipimo vyao visivyo na maana.<br>
Wewe ni wewe, ni wa kipekee, ni bora na una mengi yaliyo mbele yako. Yaendee.<br>
Makirita Amani,<br>
www.amkamtanzania.com<br>
</p>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-16173732330381461652015-07-04T19:46:00.001+03:002015-07-04T19:46:13.959+03:00UKURASA WA 185; Bila Kuwajua Watu Hawa Watatu Na Kumalizana Nao, Sahau Kuhusu Mafanikio.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kuna watu watatu ambao kwa wewe kujua au kutokujua wamekuwa
wanakuzuia kufikia mafanikio.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sio kwamba wao wanakuja na kukuzuia wewe kufikia mafanikio, ila
kwa sababu yao wewe mwenyewe umeshindwa kufikia mafanikio kwenye maisha
yako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Aina ya kwanza ya watu hawa ni watu ambao unataka kuwalinda.
Kuna watu ambao wewe unataka kuwalinda na hivyo unajizuia kufikia mafanikio ili
uendelee kuwalinda. Kuna baadhi ya watu wanaogopa kufikia mafanikio kwa sababu
wanataka kuendelea kuwa na watu wanaowazunguka. Kuna wafanyakazi ambao wanaogopa
kuonesha ubora wao kwenye kazi zao kwa sababu wanaogopwa kuchukiwa na wenzao au
kuonekana ni hatari kwa mabosi zao.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://www.amkamtanzania.com/2013/11/wajue-watu-hawa-na-waepuke-kwenye.html" target="_blank">Wajue Watu Hawa na Waepuke Kwenye Maisha Yako.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Aina ya pili ni watu ambao unajaribu kuwaadhibu. Kuna watu ambao
unaweza kuwa unataka kuwaadhibu na hivyo ukajizuia wewe kufikia mafanikio. Labda
wazazi wako hawakukupatia kile ulichofikiri kingekuwa bora kwako. Na hivyo
unataka uwaoneshe kwamba walikosea na hivyo wewe huwezi kufikia mafanikio kama
ya wengine.... kwa sababu ya kutojali kwao.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Aina ya tatu ni watu ambao unataka kuwafurahisha. Hawa ni watu
ambao unataka kuwafurahisha ili waendelee kukuona kama wanavyopenda kukuona na
hivyo kujizuia kufikia mafanikio. Kuna watu ambao wanalazimika kuvaa mavazi ya
bei ghali, kuendesha magari ya bei ghali na hata kuishi maeneo fulani ili tu
waonekane. </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Wajue watu hawa watatu kwenye maisha yako na malizana nao,
hakikisha unaishi maisha uliyochagua wewe mwenyewe, yatakayokufikisha kwenye
mafanikio unayotaka na sio kuwalinda watu, kuwaadhibu au kuwafurahisha.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Nimeamua sasa kwamba sitaki tena kuwalinda watu, kuwaadhibu au
kuwafurahisha. Nahitaji kuishi maisha ambayo yatanipa furaha na kunifikisha
kwenye mafanikio na sio maisha ambayo yatanirudisha nyuma. Nitaweka juhudi na
maarifa ili niweze kuwa bora zaidi ya nilivyo sasa.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-31915081702388610022015-07-03T12:00:00.000+03:002015-07-03T12:00:03.386+03:00UKURASA WA 184; Ni Ruhusa Kwako Kubadili Mawazo.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kwa mfano umeshakubaliana na mtu mtafanya kitu fulani halafu
dakika za mwisho anakuambia nimebadili mawazo, sitafanya tena kama
nilivyokuambia. Unajisikiaje? Unachukuliaje hali kama hiyo?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Labda ni biashara na umeshakubaliana na mteja ila baadae
anakuambia nimebadili mawazo. Au ni kwenye ajira na umeshakubaliana kitu fulani
na mwajiri wako, umeshajiandaa kabisa na anakuambia nimebadili mawazo, hutafanya
tena hivyo. Au ni kwenye maisha yako ya kawaida, ulipanga muoane na mtu na
dakika za mwisho anakuambia nimebadili mawazo? Au umeshaona na mtu na kati kati
ya safari anakuambia nimebadili mawazo?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua kama wewe ndio umeambiwa hivi unaweza kujisikia vibaya
sana. Unaweza kuona aliyebadili mawazo hafai na ameharibu maisha yako. Lakini
ukweli ni kwamba yeye ametumia haki yake ya msingi, kuruhusu mawazo yake
yamchagulie kile ambacho anaona ni bora kwake. Hakuna jinsi unaweza kuzuia
hilo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://jiongezeufahamu.blogspot.com/2015/07/kabla-hujakubali-kila-unachoambiwa.html" target="_blank">Kabla Hujakubali Kila Unachoambiwa, Kumbuka Jambo Hili Moja Muhimu
Sana.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Badala ya wewe kulalamika kwamba kwa nini hakukwambia mapema au
kwa nini alikubali mwanzoni, furahi kwamba umejua mapema kabla hata hujapoteza
muda mwingi. Shukuru kwamba umejua ni mtu wa aina gani na jifunze wakati
mwingine kuangalia vitu muhimu kabla hujaingia kwenye makubaliano na mtu ambayo
ni muhimu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Jipe ruhusa ya kubadili mawazo, wape wengine ruhusa ya kubadili
mawazo na usitake kuishi maisha ya kufungwa au kuwafunga wengine kwa sababu tu
wanaogopa kubadili mawazo. Maisha yanapaswa kufurahiwa na sio kuishi kwa ajili
ya kuwaridhisha wengine.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua nina ruhusa ya kubadili mawazo hata kama nilishakubaliana
na mtu. Najua pia kwamba watu wana ruhusa ya kubadili mawazo yao hata kama
walishaniahidi kitu. Naheshimu uhuru wangu na wa kila mtu na ni kwa uhuru huu
ndio naweza kuishi maisha ninayoyafurahia na yenye faida kwa wengine
pia.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 185 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-19687561280072218042015-07-02T17:51:00.000+03:002015-07-02T17:51:01.935+03:00UKURASA WA 183; Hakuna Anayekuchukia Wewe, Bali Wanahamisha Chuki Zao Kutoka Hapa.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Leo naomba tujadili kidogo kuhusu mtu kumchukia mwingine.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Labda tuseme wewe kuna mtu anakuchukia, na amekuwa akikuonesha
wazi wazi kwamba anakuchukia. Na hapa wewe huna tatizo lolote na mtu huyu.
Unajaribu kuishi maisha yako bila hata ya kuingilia maslahi yao wala kuwavurugia
chochote ambacho ni chao, lakini mtu anachagua tu kukuchukia. </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Unajisikiaje katika hali kama hii? Unaumia kwa sababu
ulitegemewa mtu ambaye ni wa karibu kwako awe pamoja na wewe badala yake
anakuchukia? Unajaribu kumbadili mtu labda akupende?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Leo nataka nikupe sababu kwa nini mtu anaweza kukuchukia na njia
bora ya kuondokana na chuki hiyo.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwanza kabisa mtu anapokuchukia sio kwamba anakuchukia wewe, ila
anajichukia yeye binafsi. Ni hivyo tu. Mtu kuna kitu ambacho kinamsumbua kwenye
maisha yake na hataki kukikubali, hivyo anayachukia maisha yake, kwa sababu
hataki kukubali hilo pia anatafuta mtu wa kumchukia ili angalau aone tatizo sio
lake. Si unajua tabia za wakwepa majukumu?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hivyo atajipa kila sababu kwa nini anakuchukia wewe, lakini wewe
huna tatizo lolote na yeye kukuchukia, hakuna chochote ambacho umemharibia.
Labda umeamua tu kubadili maisha yako na kwa kuwa huyo anayekuchukia hawezi
kubadilika basi anakuchukia. Kwa mfano ulikuwa na marafiki wa karibu kila siku
mnakunywa pamoja, wewe ukakaa chini na kuona kunywa kwenu hakuna faida yoyote,
hivyo ukaamua kuacha utaratibu huu wa kukutana baa kila siku na ukaanza
kujifunza na kujishughulisha na vitu vya pembeni(fanya hivi kama bado una
utaratibu wa kuhudhuria vikao vya baa kila siku). Unafikiri ni nini kitatokea
kwa marafiki zako hao? Watakuchukia. Sasa hebu jiulize wanakuchukia kwa sababu
wewe umeamua kuacha kukaa vikao hivyo kila siku? Hapana, wanakuchukia kwa sababu
wewe unaanza kuwa bora kuliko wao. Kwa mfano ingetokea huna tena kazi na hivyo
huna fedha ya kwenda baa kila siku unafikiri wangekuchukia? Hawawezi kukuchukia,
watakuonea huruma tu na wataendelea na utaratibu wao.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hivyo kama kuna mtu yeyote ambaye anakuchukia, wala usijiumize
kichwa ufanye nini ili aache kukuchukia, endelea kufanya unachofanya na mwache
ajiue mwenyewe na chuki zake. Maisha ni mafupi sana mpaka uanze kupata muda wa
kumfurahisha kila mtu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Usikubali uhusiano wowote wa kindugu au kirafiki uwe kikwazo
kwako kuishi maisha unayotaka kuishi wewe, kama huvunji sheria. Hata kama kuna
atakayekuchukia hawezi kukuchukia zaidi ya miaka 100 ijayo, kwa sababu wote
mtakuwa mmekufa na hakuna atakayekuja kukukumbusha kwamba nilikuchukia sana
duniani, kama mtakutana peponi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2014/12/hiki-ndio-kitakachotokea-miaka-100-ijayo.html" target="_blank">Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Maisha ni yako chaguo ni lako, kama kuna mtu anakuchukia muonee
huruma na achana naye, wala hata usimfikirie, wewe endelea kuweka juhudi kwenye
kile unachofanya na unachotaka kuwa bora.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua kwamba mtu yeyote anayenichukia sio kwa sababu ananichukia
kweli, ila ni kwa sababu anajichukia yeye mwenyewe. Mimi sina muda wa kuanza
kufikiria kuhusu anayenichukia, ni bora nikatumia muda huo vizuri kujiendeleza
kuwa bora zaidi kwenye hiki ninachofanya.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 184 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-20126266084403370052015-07-01T12:00:00.000+03:002015-07-01T12:00:00.874+03:00UKURASA WA 182; Urahisi Wa Kutengeneza Tabia Mbaya Na Ugumu Wa Kuishi Nazo.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kuna jambo moja muhimu sana kwenye maisha ambalo unatakiwa kuwa
unalijua. Na sio kulijua tu bali kulifanyia kazi kila siku maana kwa jambo hili
moja ndio watu wanafanikiwa au wanashindwa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Jambo hilo ni kwmaba, tabia mbaya ni rahisi sana kutengeneza ila
ni ngumu sana kuishi nazo. Na kwa upande wa pili, tabia nzuri ni ngumu sana
kutengeneza ila ni rahisi sana kuishi nazo. Hivyo ni wewe kuchagua kuwa tayari
kufanya kipi ili uweze kuishije baadae.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Urahisi wa kutengeneza tabia mbaya.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Tabia mbaya ni rahisi sana kutengeneza, kwa mfano ulevi, ni
rahisi sana kuwa mlevi, anza kunywa pombe kila siku na kunywa nyingi uwezavyo,
hata hivyo unasikia raha, hivyo ni rahisi kutengeneza. Ila sasa maisha ya ulevi
ni magumu sana, ni vigumu sana kuweza kufurahia maisha kama tayari wewe ni
mlevi, utajikuta maisha yako yametawaliwa na ulevi na unajiona kama huwezi
kutoka tena huko.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Tabia zote mbaya, iwe ni uvivu, wizi, uongo, kula hovyo zote ni
rahisi sana kutekeleza. Ila kuishi nazo baada ya kuwa zimejijenga ni vigumu
sana.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/02/kama-unataka-kumaliza-matatizo-yako-ya.html" target="_blank">Kama Unataka Kumaliza Matatizo Yako Ya Fedha Fanya Kitu Hiki
Kimoja.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ugumu wa kutengeneza tabia nzuri.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa upande wa pili, tabia nzuri ni vigumu sana kuzitengeneza
lakini ukishakuwa nazo ni rahisi sana kuishi nazo. Kwa mfano tabia ya kujiwekea
akiba, ni vigumu sana mwanzoni, inabidi ujinyime inabidi uonekane huendi na
wakati na wakati mwingine utahitaji kuzishinda tamaa zako. Ila unapokuwa na
tabia hii ni rahisi na vizuri sana kuishi nayo kwa sababu unajua kuna akiba
ambayo inaendelea kukua na hivyo kuvutiwa kuweka zaidi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Unahitaji nguvu ya ziada ili kuweza kufikia mafanikio, ingekuwa
rahisi kila mtu angekuwa nayo. Sio rahisi na ndio maana kuna wakati utaona kama
unajitesa, endelea hivyo hivyo na mambo yatakuwa mazuri sana.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua nina machanguo mawili, nipate raha ya muda mfupi sasa
halafu niteseke kwa muda mrefu au nipate shida ya muda mfupi sasa na kuishi kwa
raha muda mrefu. Mimi nimechagua kuteseka kwa muda mfupi sasa ili niishi kwa
raha muda mrefu ujao. Nitatengeneza tabia ambazo ni nzuri kwa sasa, ambazo ni
ngumu kutengeneza lakini najua baadae nitafurahia kuishi
nazo.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 183 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-74233113428845826742015-06-30T12:00:00.000+03:002015-06-30T12:00:04.984+03:00UKURASA WA 181; Kitu Cha Kufanya Pale Watu Wanapokuwa Hawakuamini Kama Unaweza.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kama unataka kufanya jambo jipya, kama unataka kufanya jambo
tofauti na wengine walivyozoea kufanya, naweza nikakuhakikishia jambo moja, WATU
HAWATAKUAMINI.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Watu hawatakuamini kwamba unaweza kufanya jambo hilo. Watu
hawatakuamini kwamba kuna uwezekano wa jambo hilo kufanyika kwa tofauti. Na hapa
ndipo watu wengi hukata tamaa na kuamua kuacha. Na hivyo watu wale walioshindwa
kuwaamini mwanzo wanakuwa sahihi na wanazidi kupata nguvu ya kuwaambia wengine
kwamba hawawezi au haiwezekani.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Leo nataka nikuulize, je unajua unatakiwa kufanya nini pale
ambapo watu hawakuamini kwamba unaweza? Au umekuwa mtu wa kukatishwa tamaa mara
nyingi na wewe kukubali?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sasa kuna kitu kimoja muhimu sana unachotakiwa kufanya pale
ambapo watu hawakuamini kama unaweza. JIAMINI WEWE MWENYEWE. Wewe ndio umekuja
na mawazo hayo uliyonayo, wewe ndiye ambaye umekuwa unafikiria usiku na mchana
jinsi unavyoweza kubadili hali ya mambo. Wewe ndiye uliyefikiria na kuona kuna
njia mbadala na ambayo inawezekana. Sasa kwa nini ukubali kumsikiliza mtu ambaye
amefikiria kwa upande mmoja tu wa kwamba vitu haviwezekani? </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <b><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/05/ukurasa-wa-134-hukuja-na-maelekezo-kwa.html">Hukuja
Na Maelekezo Kwa Mtumiaji Na Kwa Nini Ufurahie Hili.</a></b></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama utawasikiliza watu hawa utakuwa hujajitendea haki kabisa,
kwa sababu hata watu hawa sio kwamba wana uhakika haiwezekani, ni vile tu
hawajawahi kuona mtu mwingine akifanya hicho unachotarajia kufanya. </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama watu hawaamini kwamba unaweza, huo ndio wakati wa kujiamini
na hata kufurahia sana kwenye maisha yako. Unajua ni kwa nini? Kwa sababu
unapoanza kufanya kitu ambacho wengi wanaona hakiwezekani, jua unafanya kitu
ambacho sio cha kawaida, unafanya kitu kikubwa. Na mafanikio yanakuja kwa
kufanya vitu ambavyo sio vya kawaida.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua ya kwamba pale ninapopanga kufanya jambo kubwa, watu wengi
watashindwa kuniamini. Huu ni wakati muhimu sana wa mimi mwenyewe kujiamini na
kuendelea kuweka juhudi. Hakuna mafanikio yanayokuja kwa kufanya vitu ambavyo ni
vya kawaida. Hivyo ninapoona watu hawaniamini kwa kitu kikubwa ninachotaka
kufanya, najua hapo ndio penye mafanikio.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 182 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-835582953682880862015-06-29T12:00:00.000+03:002015-06-29T12:00:08.017+03:00UKURASA WA 180; Pamoja Na Ushauri Mzuri Utakaopewa, Bado Kitu Hiki Utafanya Wewe Mwenyewe.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<br />
<span style="font-size: medium;">Unapokuwa unahitaji kufanya maamuzi ambayo huenda ni magumu
kwenye kazi yako, biashara yako au hata maisha yako kwa ujumla, huwa unahitaji
kupata ushauri. Unaweza kupewa ushauri mzuri sana kutoka kwa watu mbalimbali
ambao unaweza kuwa unawaamini sana.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Pamoja na ushauri huu muhimu bado wewe mwenyewe ndio utahitaji
kufanya maamuzi ya mwisho. Wewe ndio utakayekaa chini na kufanya maamuzi ambayo
utakuwa tayari kuishi nayo.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Hivyo ni muhimu sana wewe uwe na uwezo wa kufanya maamuzi.
Huwezi kutegemea tu watu watakavyokushauri, kwa sababu watu mbalimbali watakuwa
na ushauri tofauti. Kama hutakuwa na uwezo mzuri wa kufanya maamuzi ambayo
utakuwa tayari kuishi nayo, utaishia kufanya maamuzi ambayo
yatakupoteza.</span><br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/05/ukurasa-wa-148-mambo-kumi10-unayotakiwa.html" target="_blank">Mambo Kumi(10) Unayotakiwa Kubadili Leo Ili Kufikia Mafanikio
Makubwa.</a></span><br />
<span style="font-size: medium;">Nakumbuka siku sio nyingi rafiki yangu mmoja aliniomba ushauri
kuhusiana na maamuzi ya kibiashara aliyokuwa anataka kufanya. Nilimpa ushauri
wangu na mambo muhimu anayohitaji kuzingatia. Baadae alinipigia kuniambia kwamba
ameamua kufanya tofauti na nilivyomshauri. Nilistuka kidogo kwa sababu
alichokuwa anakwenda kufanya ni kosa kubwa sana ambalo mimi binafsi nimewahi
kufanya na likanigharimu na nimekuwa naona wengi wakifanya kosa hilo na
linawagharimu sana. Nilijaribu kumwelewesha, labda kama hakuwa amenielewa
vizuri, lakini alisisitiza kuendelea na kile alichopanga kufanya.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Nilijikumbusha kwamba yeye pekee ndio mwinye kufanya maamuzi ya
mwisho na hivyo nilimwambia kila la kheri kama ndio maamuzi ambayo yuko tayari
kuishi nayo. Siku chache baadae alinipigia na kuniambia hataendelea tena na
mpango ule, hapa nilichanganyikiwa zaidi na sikutaka hata kujua
zaidi.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Katika maisha yako jiandae kuweza kufanya mamauzi ambayo ni
sahihi kwako na sio ya kusukumwa na mtu au kitu chochote.</span><br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span><br />
<span style="font-size: medium;">Najua ya kwamba nitapata ushauri kutoka kwa watu wengi. Najua
ushauri huu utakuwa mzuri sana, lakini mwisho wa siku ni mimi pekee
nitakayehitaji kufanya maamuzi ambayo ni sahihi kwangu na nitakuwa tayari kuishi
nayo. Kila siku nitajijenga ili niweze kufanya maamuzi ambayo yatakuwa bora
kwangu.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 181 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a><br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span><br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a><br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span><br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-6708278396177925442015-06-28T08:24:00.000+03:002015-06-28T08:24:15.847+03:00UKURASA WA 179; Unataka Kuwazidi Wengine? Umeshapotea.<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kwanza kabisa nikiri kwamba mimi huwa napinga sana dhana ya
kushindana. Ndio kuna wakati ushindani unaonekana ni mzuri, lakini tatizo
linakuja kwamba ukishakuwa na akili ya kushindana ndio unadumaa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kama unakuwa na akili ya kushindana maana yake lengo lako kubwa
ni kuwazidi wengine. Kuwa wa kwanza, kuwa bora zaidi ya wengine.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Sasa tuseme labda unafanya biashara eneo ambalo watu wanafanya
biashara kwa mitindo ya kizamani. Mtu akipata faida kidogo siku moja kesho yake
analala, anaona amewini maisha. Na wewe ukawa unashindana nao, unafikiri utafika
wapi?</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Au tuseme unafanya kazi kwenye eneo ambalo kila mtu anakazana
kununua gari na wewe ukawa na akili ya kushindana, unafikiri mafanikio yako
makubwa kwenye maisha yatakuwa nini. Ukishanunua gari bora zaidi ya wengine
tayari umekwisha. Utaonekana wewe ndio wewe na kile kiroho chako cha kushindana
kitafurahi, kitakufanya uone maisha umeyamaliza.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/03/ukurasa-wa-89-sheria-tatu-muhimu-za.html" target="_blank">Sheria Tatu Muhimu Za Kufanikiwa Kwenye Maisha.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Lengo lako sio kuwa zaidi ya wengine, kama unataka kufikia
mafanikio makubwa. Bali lengo lako ni wewe kuwa bora zaidi yako wewe mwenyewe.
Wewe kuwa bora kuliko wewe mwenyewe. Wewe kuwa mbele yako mwenyewe. Hii ina
maana kwamba leo uwe bora zaidi ya ulivyokuwa jana, leo ufanye kazi yako au
biashara yako kwa ubora zaidi kuliko ulivyokuwa unafanya siku zilizopita. Leo
upate kipato kikubwa zaidi ya ulichopata siku zilizopita. Leo upate mteja mpya
tofauti na uliokuwa nao zamani.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Hiki ndio unatakiwa kupigania, hiki ndio unatakiwa kufanya kila
siku. Na sio kuingia kwenye mbio za kundi na kujiingiza kwenye mashindano ambayo
hujui hata yanakupeleka wapi.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua kukazana kuwa bora zaidi ya wengine ni kupoteza muda wangu
na kujizuia kufikia mafanikio makubwa. Kuanzia sasa nitakazana kuwa bora zaidi
yangu mwenyewe, nitakazana kuwa mbele yangu mwenyewe, kwa sababu najua kuna
uwezo mkubwa uliopo ndani yangu ambao bado sijautumia. Nitahakikisha nautumia
sasa ili niweze kufika mbali zaidi ya hapa nilipo sasa.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 180 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-90720195290087264252015-06-27T07:28:00.000+03:002015-06-27T07:28:03.793+03:00UKURASA WA 178; Lakini Nitapitwa.... (Sababu Ya Kijinga Inayokufanya Upoteze Muda)<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Kama umejitoa ili kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako,
unahitaji kujifunza jinsi ya kutumia muda wako vizuri. Na kwa kuwa siku ina
masaa 24 tu na hakuna anayeweza kuyazidisha, hakuna njia ya kuongeza muda ambao
tunao.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa kuwa tunahitaji muda mwingi zaidi wa kufanya kile
tunachofanya kwa ubora, basi tunahitaji kupunguza mambo mengi tunayofanya ili
tuokoe muda mwingi. </span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ili kupata muda mwingi nimekuwa nawashauri watu kufanya
yafuatayo, ambayo hata mimi nafanya; usifuatilie habari, punguza sana muda
unaotumia kwenye mitandao ya kijamii, tenga muda wa kuwa mbali na simu yako pale
ambapo unafanya kazi inayohitaji umakini wako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Watu wamekuwa wakipinga sana baadhi ya mambo haya, hasa
kutokufuatilia habari au kukaa mbali na simu. Watu wamekuwa wakisema lakini
nitapitwa.....</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua na wewe unaona usipoangalia au kusoma habari siku moja
unaona unapitwa. Yaani unapitwa na habari ya mtu aliyejinyonga huko mpanda,
ukishaisikia inakusaidia nini? Utaniambia kuna habari muhimu kuhusu mambo
yanayoendelea. Kama habari ni muhimu kweli zitakufikia tu. Kwa mfano kama nchi
inaingia vitani, utajua hata kama huangalii habari. Lakini mambo ya mgombea gani
kapata wadhamini wangapi sio habari za mtu makini kushabikia, ni kupoteza muda
wako.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/01/ukurasa-wa-04-unacho-kila-unachohitaji.html" target="_blank">Unacho Kila Unachohitaji Ili Kufanikiwa.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Asilimia kubwa ya watu wanaotumia simu ni kama wamefunga ndoa na
simu hizo. Kila dakika mtu upo na simu na hazipiti dakika tano unaangalia kama
kuna mtu katuma ujumbe au kapiga hukusikia. Na hata unapokwenda kulala, unaiweka
pembeni ya kichwa chako, ili usipitwe. Unapoteza muda mwingi sana, ni vigumu
kufanya kazi yenye maana huku unajibu ujumbe wa simu au kupokea simu kila mara.
Ni afadhali uweke simu hiyo kimya kabisa na ufanye kazi yako, bila ya
kuiangalia. Utasema lakini watu watanipigia na kunikosa, nitakosa dili nzuri.
Ukweli ni kwamba, na hapa nakuambia kwa uzoefu, kama mtu ana shida ya
kuwasiliana na wewe kweli, atakutafuta hata mara kumi. Ila anayepiga mara moja
na kuacha, hata ukija kumpigia baadae hakuna jambo kubwa na la haraka sana
alilokuwa anakuambia. Mwingine atasema labda mtoto wangu ataumwa ghafla inabidi
nipate taarifa, sawa umeshazipata unafanya nini? Maana hata kama wewe ni daktari
huwezi kumtibu mtoto wako, itabidi apelekwe tu hospitali. Sisemi usikae na simu
siku nzima, bali masaa machache hivyo taarifa hizi utazipata baadae na utafanya
maamuzi sahihi, huku umeshakamilisha kazi uliyopanga kufanya.</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Nimekuwa najidanganya kwamba nitapitwa na hivyo kuwa karibu na
habari, kuwa karibu na mitandao na kuwa karibu na simu yangu kila mara. Hali hii
imekuwa inanipotezea muda wangu mwingi kwa kufuatilia vitu visivyo na maana na
kukosa muda w akufuatilia yale ambayo yataniletea mafanikio. Kuanzia sasa
natenga muda wangu wa kufanya mambo muhimu na muda huu hautaingiliwa na kitu
kingine chochote.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa 179 kesho, Like page yangu ya
</span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach
Makirita Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha
kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-5592248117736749337.post-88593406520339643812015-06-26T12:33:00.000+03:002015-06-26T12:33:00.963+03:00UKURASA WA 177; Ndio, Kwa Hiyo...<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<span style="font-size: medium;">Ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kwenye biashara, ndio kwa hiyo
unahitaji kujipanga vizuri na kutokukata tamaa ili uweze kufikia mafanikio
unayotarajia.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Umri wangu ni mdogo/mkubwa sana kuweza kuanza kufanya jambo hili
sasa. Ndio kwa hiyo unahitaji kuwa wa tofauti, licha ya umri wako kuwa
usiotegemewa bado unaweza kuweka juhudi na ukafikia kile ambacho unataka.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Nimejaribu mara nyingi sana lakini nimeshindwa. Ndio kwa hiyo
unahitaji kubadili mbinu zako, kuendelea kufanya kitu kile kile na kutegemea
majibu tofauti ni ujinga wa kupindukia.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Napenda sana kuanza biashara ila sina mtaji. Ndio kwa hiyo
unahitaji kufikiria njia ya kuweza kuanza biashara kidogo au kutafuta kitu
kingine cha kukuingizia kipato kwa sasa ili ujiandae na kuingia kwenye biashara
unaotazamia.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">SOMA; <a href="http://makiritaamani.blogspot.com/2015/06/ukurasa-wa-164-vitu-ambavyo-ni-rahisi.html" target="_blank">Vitu Ambavyo Ni Rahisi Kufanya.... Na Madhara Yake.</a></span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Ukweli ni kwamba mtu yeyote anaweza kuja na sababu zaidi ya elfu
moja kwa nini hawezi kufanya kitu fulani. Ila sababu hizi haziwezi kusaidia
chochote.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Watu waliofanikiwa wanakuja na sababu lakini huzipatia sababu
zao suluhisho ambalo hulifanyia kazi na hatimaye kufanikiwa.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Usiwe mtu wa kutafuta au kutoa sababu tu. Hebu anza kuzipa
sababu zako suluhisho na utaona fursa nyingi sana za kukufikisha kwenye kile
unachotaka.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Wakati wowote unapokuja na sababu tafadhali sana mbele yake
ongeza NDIO KWA HIYO....</span>
<br />
<blockquote>
<span style="font-size: medium;">TAMKO LA LEO;</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Najua sababu yoyote ninayojipa haiwezi kunifikisha kule
ninakotaka kwenda. Ila ninapoifanyia kazi sababu ninayoipata ndio natoa nafasi
kubwa kwangu kuweza kupata kile ninachotaka. Najua mjinga yeyote anaweza kuja na
sababu kwa nini hafanikiwi na hii ndio inazidi kumfanya asifanikiwe. Lakini mimi
sio mmoja wa wajinga hawa, kila sababu ninayopata lazima niipatie
ufumbuzi.</span></blockquote>
<span style="font-size: medium;">Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya </span><a href="https://www.facebook.com/MakiritaAmani"><span style="font-size: medium;">Coach Makirita
Amani</span></a><span style="font-size: medium;"> uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi
yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365
</span><a href="https://feedburner.google.com/fb/a/mailverify?uri=MakiritaAmani&amp;loc=en_US"><span style="font-size: medium;">bonyeza hapa na uweke email.</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kusoma makala zilizopita za </span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/search/label/KURASA%20365%20ZA%20MWAKA%202015"><span style="font-size: medium;">KURASA 365 ZA MWAKA 2015</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo
maandishi.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya
facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya
email.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kwa lolote andika email kwenda </span><a href="mailto:makirita@kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">makirita@kisimachamaarifa.co.tz</span></a>
<br />
<span style="font-size: medium;">Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na
</span><a href="http://makiritaamani.blogspot.com/www.kisimachamaarifa.co.tz"><span style="font-size: medium;">KISIMA CHA MAARIFA</span></a><span style="font-size: medium;"> bonyeza hayo maandishi kupata
utaratibu.</span>
<br />
<span style="font-size: medium;">TUPO PAMOJA.</span></div>
Anonymoushttp://www.blogger.com/profile/07389552367879892295noreply@blogger.com0