Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, December 31, 2014

Kozi 1100 Unazoweza Kujifunza Bure Kupitia Mtandao.

Mwaka 2015 ndio huu hapa, una nafasi kubwa ya kuanza kufanya mabadiliko makubwa kwenye maisha yako kuanzia leo.
Ili uweze kubadili maisha yako, elimu ni muhimu sana.
Ni muhimu sana kujifunza na kuongeza maarifa ili kuweza kuwa na utaalamu utakaokufanya ufanye kazi nzuri na ya kipekee itakayokuwezesha kuboresha maisha yako.
Na dunia ya sasa imebadilika sana, kupata elimu sio lazima ukakae darasani siku nzima, ufundishwe na walimu ambao wanakuwa wanakutishia na mtihani na wakati mwingine usome vitu vingi ambavyo hata hutavitumia.
Dunia ya sasa imerahisishwa sana kiasi kwamba hapo ulipo unaweza kupata mafunzo makubwa sana yanayokuwezesha kuwa bora zaidi ya ulivyo sasa.
Hapa nakupatia sehemu ambayo utaweza kujifunza chochote unachotaka bure kabisa. 
Unaweza kujifunza kuhusu kompyuta, mitindo, upishi, biashara, uchumi, uhasibu, historia, lugha, sheria, uandishi wa habari, dini, siasa, falsafa, hesabu, na chochote kile unachohitaji wewe ili kuboresha kazi au biashara zako.
Kitu kizuri zaidi kuhusu elimu hii ni kwamba unaweza kujifunza kwa njia ya video au audio yaani kuangalia au kusikiliza.
Nakushauri sana uchague japo kozi moja na uisome, nakuhakikishia hutakosa kitu cha kukufanya uwe bora zaidi.
Kuzipata kozi hizo BONYEZA MAANDISHI HAYA.

NENO LA LEO; Wazazi Wanavyojenga Au Kubomoa Maisha Ya Watoto Wao

It is not what you do for your children, but what you have taught them to do for themselves, that will make them successful human beings. –Ann Landers
Sio kile unachowafanyia wanao ndio muhimu, bali kile ulichowafundisha kufanya kwa ajili ya maisha yao ndio kitawafanya wafanikiwe.
Umekuwa ni utamaduni wa wazazi kutaka kuwafanyia watoto wao kila kitu ili wawe na maisha bora. Ila pale wazazi wanapoondoka watoto hawa wamekuwa wanapata shida sana.
Ni muhimu kuwafundisha watoto jinsi ya kutengeneza maisha yao wenyewe badala ya wewe mzazi kujaribu kuwajengea maisha, hutawasiadia kwa kuwajengea maisha yao.
Nakutakia siku njema.

Tuesday, December 30, 2014

Kesho Jua Litachomoza Tena...

Kesho asubuhi jua litachomoza tena, kama lilivyochomiza leo, jana na siku zote zilizopita.
 Hii ina maana kwamba haijalishi leo mambo yako yamekwenda vibaya kiasi gani, kesho ni siku mpya na unaweza kubadili maisha yako.
 Kesho jua litachomoza tena hata kama kutakuwa ja mawingu.
 Hii ina maana kwamba hata kama unapitia matatizo mengi kiasi gani, usikubali yakufanye upoteze muelekeo.
 Jifunze kutokana na changamoto unazopitia huku ukifurahia maisha yako.

Matatizo Yote Kwenye Maisha Yako Yanatokana Na Kitu Hiki.

Kila mmoja wetu anapitia matatizo au changamoto mbalimbali kwenye maisha yake. Inawezekana unapitia matatizo ya kuumwa, au mwingine anapitia changamoto ya madeni na pia inawezekana unapitia changamoto ya migogoro kwenye familia.
Sasa matatizo yote haya huwa yanaanza na kitu kimoja.
Kabla sijakuambia kitu hiko naomba nikuoe mfano mmoja mzuri sana.
Ukitaka kumuua chura kwa maji ya moto huwezi kumuua kwa kumweka kwenye maji ya moto. Chura ni mnyama ambaye anavyopata joto kali anakuwa na nguvu ya kuweza kuchukua hatua haraka. Hivyo ukimweka kwenye maji ya moto ataruka haraka sana kuondoka kwenye maji hayo.
Sasa hapa kuna njia rahisi ya kumuua chura kwa maji ya moto. Unachukua maji ya baridi kabisa, tena yenye barafu halafu unamweka chura. Kwenye baridi chura hana nguvu ya kuondoka. Baada ya hapo unaanza kupasha maji yale taratibu, kadiri maji yanapata joto chura anakuwa anafurahia, anaona utamu. Akija kustuka maji yanakaribia kuchemka na mwili mzima umesaishiwa nguvu.
Hivi ndivyo matatizo uliyonayo yalivyoanza;
Hukujikuta siku moja unaumwa tu, bali zilianza dalili ndogo ndogo ukazipuuzia.
Hukujikuta kwenye madeni tu, bali ulianza uzembe mdogo mdogo kwenye fedha na ukapuuzia,
Hukujikuta kwenye mgogoro mkubwa wa kifamilia kwa mara moja tu, bali vilianza vitu vidogo vidogo ukavipuuzia.
Hatimaye mambo yamekuwa mambo na sasa upo katikati ya matatizo.
Kupuuzia dalili ndogo ndogo ambazo zingeweza kushughulikiwa ndio kunakufikisha kwenye matatizo makubwa.
Kama waswahili wanavyosema; usipoziba ufa....

Mambo Kumi Muhimu Kuhusu Maisha

1.Tupo hapa kujifunza, dunia ndio mwalimu wetu.

2. Ulimwengu hauna upendeleo.

3. Maisha yako ni matokeo ya imani yako.

4. Pale utakapoanza kutegemea zaidi vitu, watu au fedha unaharibu kila kitu.

5. Kila unachokiwekea mkazo kwenye maisha yako kinakua.

6. Fuata moyo wako.

7. Mungu hatoshuka kutoka mawinguni na kukuambia “sasa hivi una ruhusa ya kufanikiwa”

8. Unapopigana na maisha maisha siku zote yanashinda.

9. Unawapendaje watu? Kwa kuwakubali.

10. Mpango wetu hapa duniani sio kuibadili dunia bali kujibadili sisi wenyewe.

Kama Hutofanya Chochote…

Kama hutofanya chochote hakuna kitakachotokea…

Kama ukifanya chochote, chochote kinaweza kutokea…

Ndio unaweza kuishia huna kitu, lakini hapo ndio ulipoanzia.

Una nini cha kupoteza?

Fanya kitu kubadili maisha yako sasa.

NENO LA LEO; Njia Isiyokuwa Na Foleni.

There are no traffic jams along the extra mile. –Roger Staubach

Hakuna foleni unapokwenda mbali zaidi.

Unapofanya kile ambacho kila mtu anafanya utakutana na ushindani mkubwa sana.

Unapofanya kitu chenye ubora mkubwa na wa kipekee utakuwa mwenyewe na hakutakuwa na ushindani.

Mara zote nenda maili ya ziada, fanya zaidi ya wengine na utapata zaidi.

Nakutakia siku njema.

Monday, December 29, 2014

Kitu Hiki Kimoja Kitakufanya Uweze Kujiajiri, Uishie Kuwa Mwajiriwa Au Uishie Jela.

Habari za jumatatu rafiki?
Tunaelekea kabisa ukingoni mwa mwaka 2014.
Najua unefanikiwa mengi, umepata changamoto kwenye machache na umejifujza mengi pia.
Najua pia unajiandaa vyema kwa mwaka 2015
Leo nataka tukumbusane kitu muhimu sana ambacho ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuzingatia.
Kitu hiko ni NIDHAMU...
Unapoweza kuwa na nidhamu ya kujisimamia wewe mwenyewe yaani jidhamu binafsi unaweza kujiajiri, kuwa mjasiriamali au kufanya biashara.
Unaposhindwa kuwa na nidhamu ya kujisimamia mwenyewe utahitaji mtu wa kukusimamia na hivyo utapata mtu wa kukuajiri na utakuwa muajiriwa, ukijaribu biashara itakushinda.
Unapokosa Nidhamu kabisa, yaani huna nidhamu kabisa unaishia kukaa jela.
Fanya maamuzi mazuri mwaka 2015, jijengee nidhamu binafsi.
Kama hujui uanzie wapi ili kujijengea nidhamu binafsi jiunge na KISIMA CHA MAARIFA, tumejadili hatua kwa hatua jinsi ya kujijengea tabia hii.
Tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz na ujiunge.
Nakutakia kila la kheri.
TUPO PAMOJA.

Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..

Sio kwamba nimekuwa mtabiri ila nina uhakika miaka mia moja ijayo kitu hiki kitatokea.
Kitu hiko ni kwamba wote tunaosoma hapa tutakuwa tumekufa. Ndio namaanisha hata wewe utakuwa umekufa miaka mia moja ijayo kuanzia leo, yaani mwaka 2114.
Na kwa bahati nzuri sana tutakuwa tumekufa kwa kipindi kirefu sana, kwa miaka zaidi ya trilioni inayokuja tutakuwa tumekufa.
Nakwambia yote haya ili nini, si unayajua?
Nataka ufanye nambo mawili;
1. Ishi maisha yako kwa furaha maana muda unaoishi ni mfupi kuliko ambao utakuwa umekufa.
2. Hakikisha unagusa maisha ya wengine ili utakapoondoka uache kumbukumbu ya kuwepo kwako. Kujua jinsi ya kufanya hivyo soma makala hii; sio wote tunaowazika wamekufa.
Kila la kheri.

NENO LA LEO; Hiki Ndio Unachohitaji Ili Kufanikiwa.

In order to succeed, your desire for success should be greater than your fear of failure. –Bill Cosby

Ili kufanikiwa, hamu yako ya mafanikio inabidi iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.

Kinachokufanya mpaka sasa hujafanikiwa ni hofu ya kushindwa. Una hofu kwamba ukijaribu kitu fulani unachokifikiria utashindwa.

Ili ufanikiwe inabidi uweze kuishinda hofu hiyo na utaweza kuishinda kama kiu yako ya kufanikiwa ni kubwa kuliko hofu ulizo nazo.

Nakutakia siku njema.

Sunday, December 28, 2014

NENO LA LEO; Hapa Ndio Pa Kuanzia, Hasa kwa mwaka 2015…

The way to get started is to quit talking and begin doing. –Walt Disney

Njia ya wewe kuanza ni kuacha kuongea na kuanza kufanya.

Ni rahisi sana kuongea, kila mtu anaweza kuongea..

Ni rahisi sana kupanga, kila mtu anapenda kupanga na kupanga tena baada ya kupanga.

Lakini kuongea na kupanga hakutofanya lolote, hakutokufikisha popote.

Kufanya ndio kutakutoa hapo ulipo, vitendo na sio maneno au mipango.

Acha kupanga na kuongea kila siku, 2015, maneno kidogo vitendo vingi..

Nakutakia siku njema.

Hiki Ndicho Kinachonisukuma…

Imani yangu.
Hiki ndicho ninachokiamini mimi na kinachonisukuma kila siku kufanya kile ambacho ninafanya;
Naamini kila mtu ana uwezo mkubwa ndani yake wa kuweza kuwa bora zaidi ya alivyo sasa.
Naamini kuna fursa nyingi sana zinazomzunguka kila mtu pale alipo ambazo zinaweza kumsaidia kuboresha maisha yake zaidi.
Nafanya kazi na watu kuwawezesha kutumia uwezo mkubwa ulio ndani yao na fursa zinazowazunguka ili kuweza kuboresha maisha yao na kufikia mafanikio makubwa.
Hiki ndio ninachokiamini, hii ndio itakuwa sala yangu kila siku kwa mwaka 2015.
Nataka wale ambao wanahitaji mabadiliko kweli kwenye maisha yao wakaribie kwenye KISIMA CHA MAARIFA ili tufanye kazi pamoja.
Tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz na ujiunge kisha nitumie meail kwenye makirita@kisimachamaarifa.co.tz ili tuanze mpango kazi.

Sunday, December 21, 2014

Ishi na Waache wengine nao waishi...

Ishi na waache wengine nao waishi,
Fanya biashara na waache wengine nao wafanye biashara,
Vua samaki na waache wengine nao wavue samaki,
Kula raha na waache wengine nao wale raha...
Kuna fursa nyingi sana hapa duniani hivyo hakuna haja ya kiwabania wengine.
Kama ilivyo kwamba huweza kulinda bahari na kusema ni yako, ndivyo ilivyo kwa fursa.
Nakutakia kila la kheri.

Saturday, December 20, 2014

Hawa Ndio Watu Unaoishia Kuwa Nao...

Unaishia kuwa na watu ambao unawavumilia...
Marafiki ulionao ni wale ambao unawavumilia, wenye tabia ambazo unazivumilia na hakuna aliyekulazimisha uwe nao.
Wafanyakazi ulionao ni wale ambao unawavumilia, wenye ufanisi ambao unauvumilia na hakuna aliyekulazimisha kuendelea kuwa nao.
Wateja ulionao ni wale ambao unawavumilia, wenye tabia ambazo unazivumilia na hakuna aliyekulazimisha kuendelea kuwa nao.
Mwajiri uliyenaye ni yule unayemvumilia, mwenye tabia unazozivumilia na anayekupa kipato unachokivumilia, hakuna aliyekulazimisha uendelee kuwa naye...
Yote hii ina maana gani?
Maana kubwa ni kwamba MAISHA NI UCHAGUZI, unachagua nani awe rafiki yako, nani awe mwajiri wako, nani awe mfanyakazi wako na nani awe mteja wako.
Kama kuna ambaye unaona hafai kuwa mmoja kati ya hao, unamfukuza, unaachana nae na kujumuika na yule unayeendana nae.
Maisha yako, uchaguzi wako.

Adui Yako Anaanzia Hapo Ulipo Na Anaanza hivi.

Adui yako ni wewe mwenyewe na anaanza na hofu zako...
Una hofu ngapi leo asubuhi?
Una hofu kama utakula leo mchana na jioni?
Una hofu kama mshahara utaingia kabla ya krismas?
Una hofu kama krismasi yako itakuwa nzuri?
Una hofu kama baraza la mawaziri litabadilishwa au halitabadilishwa?
Una hofu kama serikali itafanya maisha kuwa rahisi zaidi?
Una hofu kama 2015 chama unachokipenda kitashika madaraka?
Una hofu kama mpenzi/mwenza wako atakusaliti/atakuacha?
Una hofu kama hofu zako zitaosha??
Karibu hofu zote hapo juu hazina msaada mkubwa kwako au huwezi kuziathiri. Na kuendelea kuziendekeza ndio zinakuzuia ushindwe kufikiria mambo makubwa yatakayokuwezesha kufikia mafanikio makubwa.
Yaani kichwa kimoja chenye hofu zote hizo kitapata wapi nafasi ya kuweka jambo la muhimu?
Hofu hizi ndio adui mkubwa wa mafanikio kwako...
Usizipeleke hofu hizi 2015....

Friday, December 19, 2014

Hiki Ni Kitu Unachotakiwa Kufanya Kila Siku...

Linapokuja swala la kuhamasika/kuhamasishwa sio kitu kinachotokea mara moja halafu ghafla unakuwa mtu uliyehamasika.
Hiki ni kitu ambacho kinatakiwa kutokea kila siku ya maisha yako.
Usifikiri unasoma kitabu kimoja unapata maarifa yote unayohitaji, unatakiwa kujifunza kila siku kila siku, yaani namaanisha KILA SIKU, kama jinsi ambavyo UNAOGA KILA SIKU na kama ambavyo UNAKULA KILA SIKU.
Ndio maana mambo haya sio rahisi, yanahitaji kujitoa, yanahitaji kujikana?
Je upo tayari?
Upo tayari kufanya mabadiliko kwenye maisha yako mwaka 2015?
Kama upo tayari niambie NDIO kwenye maoni hapo chini, halafu tuma email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz ukisema upo tayari halafu nitakupa mpango mzima.
Pia tembelea www.amkaconsultants.blogspot.com ili kujifunza kitu kipya kila siku.
Karibu sana, TUPO PAMOJA.

Wewe Ni Wa Kwanza Kusoma Hapa…

Ndio wewe ni wa kwanza kusoma hapa, yaani ndio unapata habari hii kwa mara ya kwanza na unaipata hapa tu.

Wewe ni wa kwanza kusikiliza wimbo huu mpya, na unausikia kwa mara ya kwanza kwenye kituo hiki cha redio tu.

Wewe ni wa kwanza kupata habari hizi mbaya za ajali, umezisikia hapa tu…

Kuwa wa kwanza kupata kila habari inayotokea, kila linalofanyika, masaa 24 kwa siku, siku saba bkwa wiki.

Swali; je ukishakuwa wa kwanza inabadilisha nini?

Kupenda kuwa wa kwanza kwa vitu ambavyo havina msaada mkubwa kwentu kunatufanya tushindwe kufuatilia yale ambayo ni ya muhimu kwetu.

Kwa mfano unasoma kwenye mtandao; mtu fulani maarufu amekufa, na wewe kwa kuwa unataka kuwa wa kwanza kutoa habari, unakimbilia kusambaza, bila hata ya kudhibitisha kweli kama amekufa.

NENO LA LEO; Hiki Ndio Unachokiishi

Too many of us are not living our dreams because we are living our fears. –Les Brown

Wengi wetu hatuishi ndoto zetu kwa sababu tunaishi hofu zetu.

Acha sasa kuzuiwa na hofu na anza kuishi maisha ya ndoto zako. Hakuna kinachoshindikana kama kweli utakuwa umedhamiria.

Nakutakia siku njema.

Thursday, December 18, 2014

NENO LA LEO; Huwezi Kuanguka Kama Hutafanya Hivi.

You can’t fall if you don’t climb. But there’s no joy in living your whole life on the ground. –Unknown

Huwezi kuanguka kama hutopanda. Lakini hakuna furaha kwenye maisha kama utaishi maisha yako yote ukiwa chini.

Anza sasa kupanda na kuwa bora zaidi, ndio unaweza kuanguka ila utajifunza mengi na utaweza kufikia juu zaidi.

Ukiendelea kuogopa kuanguka, utaendelea kubaki hapo ulipo.

Nakutakia siku njema.

Wednesday, December 17, 2014

Mabadiliko Yanaanzia Hapa...

Mabadiliko yanaanza na yule anayetaka mabadiliko...
Kama unataka watu wakuheshimu anza wewe kuwaheshimu...
Kama unataka watu wakupende anza wewe kuwapenda...
Kama unataka watu wafanye unachotaka anza wewe kufanya kitu hiko.
Ni vigumu sana kumlazimisha mtu afanye kile unachomtaka afanye.
Ila ni rahisi sana mtu kuiga kile unachofanya.
Badala ya kupoteza nguvu nyingi kumwambia mtu kwa nini abadilike, kwa nini usoelekeze nguvu hizo katika kuanzisha mabadiliko yenyewe?

Hili Ndilo Kaburi Unalozika Ndoto Zako Kubwa.

Jana ulipanga leo utaanza kuweka mipango ya kuanza biashara,
Au ulipanga leo utaanza mazoezi,
Au ulipanga leo utaanza kuweka akiba ya kila unachopata,
Au ulipanga utaboresha kazi yako zaidi...
Leo imefika, unajikumbusha kwamba unahitaji kufanya ulichopanga jana, lakini mwili haupo tayari kabisa kufanya.
Nafsi inaanza kukusuta, ulipanga leo utafanya, mbona hufanyi? Kwa haraka linakuja wazo linalotuliza nafsi yako.... NITAFANYA KESHO....
Baada ya wazo hili unaacha kujisuta na kukubali kwamba kesho mambho yataanza rasmi.
Na kweli kesho mambo yanaanza rasmi kweli, ila ni mambo kama uliyofanya leo, kusema utaanza kesho.
NITAANZA KESHO ni kaburi la ndoto kubwa sana. Ndoto nzuri na za kuboresha maisha yako umezizika kwenye kaburi hilo.
Acha sasa kuzika ndoto zako, kama kuna kitu muhimu unataka kufanya kwenye maisha yako, kifanye sasa, sio kesho.

Sunday, December 14, 2014

Nenda Kapige Kura, Au Usipige Na Fanya Hivi…

Leo ni siku ya kupiga kura kuwachagua viongozi wa serikali za mitaa, najua unajua hili, ila imebidi niliandike tena ili tupate pa kuanzia. Kama ulikuwa hujui leo ndio siku ya uchaguzi basi tuna tatizo kubwa zaidi.

Kwa takwimu mbalimbali za chaguzi zilizopita tunaona idadi kubwa ya watu waliojiandikisha hawapigi kura. Na laiti kama watu hao wangepiga kura mabadiliko yangekuwa makubwa sana.

kupiga kura

Sasa sitaki kuandika mengi nikucheleweshe kupiga kura, ninachokuambia leo ni;

Nenda kapige kura, au usiende kupiga na usilalamike chochote.

Maana watanzania tumekuwa mafundi wa kulalamika ila hatua hatuchukui. Kama hatua kubwa za kuwawajibisha watu hatuwezi kuchukua, basi tuchukue hatua ya kupiga kura na kuchagua viongozi ambao ni bora.

Wahi kapige kura yako asubuhi hii, na mhamasishe kila unayekutana naye nae akapige kura.

Hapa ndipo mabadiliko ya nchi yetu yanapoanzia.

Saturday, December 13, 2014

Vitu Vitamu Muhimu Unavyohitaji Ili Kuingia Kwenye Biashara.

Ili kuingia kwenye biashara zama hizi unahitaji vitu vitatu tu;
i. Kidadavuzi mpakato(laptop)
ii. Simu ya mkononi yenye uwezo mkubwa(smartphone)
iii. Wazo.
Na wazo sio lazima liwe kubwa sana, linaweza kuwa wazo la kawaida sana ambalo wengine wanalipuuza.
Kama una vitu hivyo vitatu na hujui uanzie wapi niandikie kwenye makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Angalizo; uwe tayari kufanya kazi, sio lelemama...

Friday, December 12, 2014

NENO LA LEO; Hiki Ndio Chanzo Cha Furaha.

Happiness is not something readymade. It comes from your own actions. –Dalai Lama

Furaha sio kitu ambacho kimetengenezwa tayari. Furaha inatokana na matendo yako mwenyewe.

Kama utakuwa na matendo yenye maana kwako na kwa wanaokuzunguka ni lazima yatakuletea furaha. Furaha hupewi na mtu mwingine.

Soma; HII NI HAKI YAKO YA KUZALIWA, USITEGEMEE KUPEWA NA WENGINE.

Nakutakia siku njema.

Msitu Msituni…

Ukiwa mbali na msitu, yaani kabla hujaingia msituni utauona msitu ni mkubwa sana. Utaona eneo lote la msitu limejaa miti na huwezi kuona hata ardhi. Kwa umbali uliopo unaweza kuamini kwamba hakuna hata sehemu ya kupita kwenye msitu huo.

Ila unapoingia kwenye msitu huo, huoni tena msitu. Yaani unapokuwa msituni huoni tena msitu, bali unaona mti mmoja mmoja na kuna sehemu kubwa ya kupita. Unaweza kuupita mti mmoja baada ya mwingine na kuendelea kufanya yako…

Kabla hujaingia kufanya jambo lolote utaona vikwazo vingi sana, utaona hatari na ilivyo rahisi kushindwa. Ila unapoingia kwenye jambo hilo, vikwazo vilivyokuwa vinakutisha mwanzo unakuta sio vikubwa kama ulivyokuwa unafikiri. Unakuta ni changamoto ndogo ndogo ambazo unaweza kuzimudu.

Usiogope tena kufanya kile unachotaka kufanya, huwezi kuona msitu ukiwa msituni…

Nakutakia kila la kheri.

Wednesday, December 10, 2014

NENO LA LEO; Mlango Mpya Wa Furaha

When one door of happiness closes, another opens, but often we look so long at the closed door that we do not see the one that has been opened for us. –Helen Keller

Mlango mmoja wa furaha unapojifunza, mlango mwingine unafunguka, lakini tunaishia kuangalia mlango uliojifunza kwa muda mrefu na hivyo kushindwa kuona mlango mpya uliofunguka.

Acha kuangalia matatizo yako tuu, angalia pembeni na utaona fursa nyingi za kubadili na kuboresha maisha yako.

Nakutakia siku njema.

Waliofika kileleni…

Watu waliofika kwenye kilele kikubwa sio kwa sababu watu hao waliruka na kujikuta kileleni, ila kwa sababu watu hao, wakati wenzao wamepumzika wao waliendelea kukomaa na kuendelea na safari.

Endelea na safari yako wakati wengine wamelala…

Endelea na safari yako wakati wengine wanastareheka…

Endelea na safari yako wakati wengine wanabishana mambo ambayo hawawezi kuyaathiri…

Watakuona upo kileleni, wakati wao wakiendelea kusota na kushindwa kufika kwenye kilele.

Tuesday, December 9, 2014

Ana Miaka 53 Ila Bado Analishwa Uji…

Kwa kawaida mtu yeyote anayezaliwa huwa anapitia vipindi tofauti kwenye maisha yake.

Kwanza kabisa anaanza kama mtoto ng’aa, ambapo anakuwa anategemea kunyonya maziwa ya mama tu.

Anaendelea kukua na baadae anakuwa analishwa uji, huku akikazana kutambaa na hatimaye kutembea.

Baada ya muda anaanza kula matonge ya ugali na kukimbia mwenyewe..

Baadae kabisa anakuwa mtu mzima anayejitegemea na kuweza pia kuwasaidia wengine.

Mpaka kufika miaka 53, mtu anatakiwa awe ameshapitia vipindi vingi vya ukuaji na maendeleo kwa ujumla. Na huu ndio umri ambao anakuwa ameshakamilisha mambo mengi kwenye maisha yake na anaishi maisha ya furaha.

tz1

Sasa maajabu makubwa ni pale unapomkuta mtu mwenye miaka 53 bado analishwa uji. Yaani yeye tokea atoke kwenye hatua ya kwanza ya kunyonya amekwamba kwenye hatua ya pili ya kunyweshwa uji.

Kama akitishiwa kunyimwa uji huo anaolishwa anaanza kulia sana na kuona maisha yake yatakuwa magumu.

Sio kwamba mtu huyu alizaliwa na ulemavu wa aina yoyote, na wala sio kwamba amekosa nguvu au mbinu nyingine za kujitegemea, yeye amefurahia kulishwa uji na hataki kufikiria zaidi ya hapo.

Ni jambo la kushangaza sana unapomkuta mtu mzima, miaka 53, mwenye afya na nguvu akiendelea kulishwa uji…

NENO LA LEO; Ni Mara Ngapi Unahitaji Kusimama Tena?

Fall seven times and stand up eight. –Japanese Proverb

Anguka mara saba, nyanyuka mara ya nane.

Haijalishi ni mara ngapi umeshindwa, cha msingi ni kuendelea tena.

Kukata tamaa ni mwiko kama kweli unataka kuyafikia mafanikio makubwa.

Nakutakia siku njema.

Monday, December 8, 2014

NENO LA LEO; Jambo Kubwa Na La Kushangaza.

We can easily forgive a child who is afraid of the dark; the real tragedy of life is when men are afraid of the light. –Plato

Tunaweza kumsamehe mtoto mdogo anayeogopa giza; ila jambo kubwa na la kushangaza kwenye maisha ni pale mtu mzima anapoogopa mwanga.

Ni kipi unachokiogopa kukifanya kwenye mwanga? Maana hiko ndio kinachokuzuia wewe kufikia mafanikio makubwa.

Nakutakia siku njema.

Nyasi Za Upande Wa Pili Ni Za Kijani Zaidi…

Angalia zile nyasi za upande wa pili, ni za kijani zaidi ya nyasi zilizopo upande wako…

Hii ni fikra ambayo huwa inamjia kila mtu katika sehemu aliyopo iwe ni maisha, kazi au biashara.

Unaweza kuona wenzako wana maisha mazuri kuliko hayo uliyoko nayo kwa sababu tu unaona wanatembelea magari mazuri au wanaonekana sehemu nzuri nzuri…

Unaweza kuona kazi au biashara wanazofanya wengine ni nzuri na zinawalipa zaidi kuliko kazi au biashara unayofanya wewe…

nyasi

Hii sio kweli kabisa, unaziona nyasi hizo ni za kijani zaidi ya za upande wako kwa sababu hujafika kwenye nyasi hizo. Utakapo pata nafasi ya kufika kwenye nyasi hizo utagundua kwamba hazina tofauti kubwa na nyasi zako.

Thamini kile ulicho nacho na kama unataka kiwe bora zaidi, kiboreshe. Usiyumbishwe kwa kutamani wanayofanya wengine, huenda hata wao wanatamani unayofanya wewe.

Hivyo njia bora sio kuangalia nyasi zipi ni za kijani zaidi, bali zifanye nyasi zako kuwa za kijani zaidi.

Nakutakia kila la kheri.

Sunday, December 7, 2014

Tulikuona Wakati Unakuja Mjini…

Tulikuona wakati unakuja mjini, usijione mjanja leo…

Ulikuja umevaa yeboyebo na nguo umebeba kwenye mfuko wa rambo, leo unajiona unajua sana…

Hayo ni maneno ya hovyo sana yanayotolewa na watu walioshindwa. Watu ambao wamepoteza muda wao kwa kufikiri wao ni wakongwe na anakuja mtu na kuwaacha wakishangaa.

Ili kujifariji kwamba na wao wana kitu fulani wanatumia sababu hiyo ya ukongwe.

joti-mpoki-enzi-hizo

Sikiliza mafanikio hayapimwi kwamba ulizaliwa wapi au umekulia wapi. Mafanikio yanapimwa na nini unachoweza kuonesha watu kwamba umefanya na kimeleta mabadiliko kwenye maisha ya wengine.

Kama wewe ndio unaambiwa wakuja usihofu, endelea kukazana.

Kama wewe ndio unawaambia wenzako ni wakuja soma hapa; ONDOKA NYUMBANI. Itakusaidia sana na utajua ni hatua gani ya kuchukua.

Chukua hatua sasa…

NENO LA LEO; Hapa Ndio Unapoweza Kuanzia Na Hiki Ndio Unachoweza Kufanya.

Start where you are. Use what you have. Do what you can. –Arthur Ashe

Anzia hapo ulipo. Tumia hiko ulicho nacho. Fanya unachoweza.

Usipoteze tena muda kufikiri ni wapi pa kuanzia, uanze na nini au ufanye nini. Unachohitaji ni kuanza kupiga hatua na mambo mengine yote yatakwenda vizuri.

Nakutakia siku njema.

Saturday, December 6, 2014

Maswali matatu muhimu ya kujiuliza leo ili kujua muelekeo wa maisha yako.

Maswali matatu muhimu ya kujiuliza ili kujua ni nini unapaswa kufanya.
i. Ni kitu gani ambacho unajua unataka ukifanye ila bado unakipuuzia kukifanya?
ii. Ni kitu gani unaweza kukisimamia leo?
iii. Ni kitu gani haupo tayari kukiacha/kukiharibu hata kama kungetokea nini?
Kwa kujibu maswali haya utajua ni kipi muhimu kwako na anza kukifanyia kazi.
Kama bado unapata shida ya kujua ni kipi muhimu kwako karibu kwenye ushauri utakaokuwezesha kujijua zaidi. Andika email kwenda ushauri@kisimachamaarifa.co.tz
Nakutakia kila la kheri.

Bado Hujachelewa...

Kuna bwana mmoja alikuwa analalamika ni jinsi gani alikuwa anapenda kujifunza kupiga kinanda ila akakosa muda kwenye maisha yake.
"Kwa nini usianze sasa" rafiki yake alimuuliza.
"Unashangaza wewe" yule bwana alimjibu. "Nina miaka hamsini sasa, nikianza kujifunza leo itanichukua miaka mitano mpaka nijue kupiga kinanda vizuri, wakati huo nitakuwa na miaka hamsini na tano" aliongeza bwana yule.
Rafiki yake alimsikiliza kwa makini kisha akamuuliza, " kama usipoanza kujifunza kinanda leo, miaka mitano ijayo utakuwa na miaka mingapi"?
Katika simulizi hii fupi unaweza kuona ni jinsi gani tunajijengea vikwazo visivyo na msingi sisi wenyewe.
Kama kuna jambo lolote unalotaka kufanya kwenye maisha yako bado hujachelewa kulifanya, ANZA SASA...
Nakutakia kila la kheri,
Kama unahitaji ushauri wa kina juu ya jambo lolote linalokusumbua andika email kwenda ushauri@kisimachamaarifa.co.tz
Karibu sana.

Tunarudia Makosa Yale Yale…

Hakuna makosa mapya, tunarudia makosa yale yale.

Ila kwa kuwa teknolojia imekua basi na kiwango chetu cha kufanya makosa yale yale tuliyokuwa tunayafanya zamani kimebadilika.

Watu wamekuwa wakiambiwa wasiue zaidi ya miaka 4000 iliyopita sasa, lakini mpaka leo bado wanaua.

Usiibe, usizini, bado kila siku tunarudia makosa haya haya.

Hii ni kwa sababu sisi ni binadamu, na tunakosea kila mara. Lakini hii haituzuii kuwa bora zaidi ya tulivyo sasa. Tunaweza, tufanye.

NENO LA LEO; Chochote Unachotaka Kuwa Kipo Huku

Everything you’ve ever wanted is on the other side of fear. –George Addair

Chochote ambacho umewahi kutaka kipo upande wa pili wa hofu.

Acha sasa kuwa na hofu na chukua hatua kupata kile unachotaka.

Kumbuka hakuna kingine zaidi ya kuchukua hatua.

Nakutakia siku njema.

Friday, December 5, 2014

NENO LA LEO; Umepangiwa Kuwa Mtu huyu…

The only person you are destined to become is the person you decide to be. –Ralph Waldo Emerson

Mtu pekee uliyepangiwa kuwa ni yule unayeamua kuwa.

Kama unaamua kuwa na mafanikio utakuwa nayo kweli na kama unaamua kuwa wa hovyo utakuwa wa hovyo.

Maamuzi ni yako, uchaguzi ni wako.

Nakutakia siku njema.

Mwalimu Anakusubiri, Chukua Hatua Sasa…

Mwanafunzi anapokuwa tayari mwalimu hutokea…

Huu ni usemi wa kale kidogo ila unaobeba maana kubwa sana.

Mwanafunzi anapokuwa tayari mwalimu hutokea, sio kwa sababu mwalimu alikuwa anasubiri mwanafunzi awe tayari ndio ajitokeze bali mwalimu alikuwepo muda wote ila mwananfunzi anapokuwa tayari ndio anamuona mwalimu kuwa yupo.

Mambo mengi kwenye maisha ambayo hujayawekea mkazo huwezi kuona umuhimu wake, pale unapoyawekea mkazo ndio unaona umuhimu wake na ndio unaona fursa zaidi.

Hivyo kuwa tayari ili uweze kumuona mwalimu wako na unufaike zaidi.

Walimu wapo wengi na kwa uhakika tu walimu wafuatao wanakusibiria wewe uwe tayari ili waanza kukupa yale kuhimu;

AMKA CONSULTANTS

AMKA MTANZANIA

KISIMA CHA MAARIFA

UWEKEZAJI TANZANIA

Hiyo ni baadhi ya mitandao ambayo utajifunz amambo mengi sana kuhusu mafanikio na maisha kwa ujumla.

Chukua hatua sasa, mwalimu anakusubiri.

Thursday, December 4, 2014

Hii Ndio Ardhi Yenye Utajiri Mkubwa Sana Duniani.

Kuna ardhi yenye utajiri na thamani kubwa sana duniani...
Ardhi hiyo sio yenye visima vya mafuta..
Na wala sio ardhi yenye migodi ya madini...
Bali ardhi hiyo ni makaburi,


Makaburi yamejaa ndoto nyingi sana ambazo hazikutimizwa.
Kuna mawazo makubwa ya kibiashara ambayo hayakutimizwa...
Kuna mawazo na ndoto kubwa za mabadiliko ambazo hazikupata nafasi ya kutekelezwa.
Badala yake watu hawa walikufa na ndoto zao.
Angalia na wewe usijekufa na ndoto yako kabla hujaitekeleza,
Maana utainyima dunia kitu kizuri sana.

NENO LA LEO; Maana Halisi Ya Vikwazo.

Obstacles are those frightful things you see when you take your eyes off the goal. –Henry Ford

Vikwazo ni yale mambo ya kutisha unayoyaona pale unapoondoa macho yako kwenye malengo yako makubwa.

Ukishaweka malengo na mipango yako usiangalie tena pembeni, utaona mambo mengi ambayo yatakukatisha tamaa.

Nakutakia siku njema.

Wednesday, December 3, 2014

Lazima Wakufanye Uendelee Kuwa Mjinga...

Ili uendelee kuwaona wao ni muhimu ni lazima waendelee kukufanya wewe mjinga...
Kwa sababu ukijua wanavyojua hutaona umuhimu wao tena...
Huu ndio ukoloni mpya unaoathiri sehemu kubwa ya watu..,
Kudai uhuru wako, unajua cha kufanya.

NENO LA LEO; Njia Moja Ya Uhakika Ya Kuepuka Kupingwa.

There is only one way to avoid criticism: do nothing, say nothing, and be nothing. –Aristotle

Kuna njia moja pekee ya kuepuka kupingwa; usifanye chochote, usiseme chochote na usiwe chochote.

Vinginevyo chochote utakachofanya lazima kuna mtu atakupinga au kukukosoa.

Fanya kile unachoona ni sahihi kufanya na komaa nacho mapaka ufikie mafanikio.

Nakutakia siku njema.

Tuesday, December 2, 2014

Aina Mbili Za Ujinga.

Kuna aina mbili za ujinga, kulingana na uelewa wa mjinga mwenyewe.
Kuna ujinga wa juu juu ambapo mtu hajui lakini anafikiri kuna mtu anajua.
Na kuna ujinga wa kweli ambapo mtu hajui na anajua hakuna anayejua.
Wanafunzi wana ujinga wa juu juu,
Wataalamu wana ujinga wa kweli.
Hii ndio inatufanya tuwe na kiu ya kutafuta kujua zaidi na hivyo kujifunza zaidi.

Huhitaji Tena Kuomba Ruhusa…

Kuna kipindi ambapo ilikuwa kama unataka kuwa msanii ni lazima uende kwa mzalishaji wa mziki na yeye ndio angeamua kwamba unafaa kuwa msanii au la…

Kuna kipindi ambapo ilikuwa ili uwe mwandishi ungeandika rasimu yako na kuipeleka kwa mhariri na yeye ndio angeamua ichapwe au la…

Nyakati hizo zimepita sasa, huhitaji tena mtu wa kukupa ruhusa kwamba wewe unaweza kuwa msanii au unaweza kuwa mwandishi au hata kitu kingine unachotaka kuwa.

Dunia imebadilika sana kiasi kwamba unaweza kujifunza chochote na kuanza kukifanyia kazi bila ya mtu kukuzuia au kukuruhusu.

Tutumie vizuri mabadiliko haya.

NENO LA LEO; Jinsi Ya Kuua Hofu

If you hear a voice within you say “you cannot paint,” then by all means paint and that voice will be silenced. –Vincent Van Gogh

Kama unasikia sauti ndani yako inayokuambia huwezi kuchora basi kwa njia yoyote ile hakikisha unachora na sauti hiyo itanyamazishwa.

Usikubali kukatishwa tamaa na nafsi yako mwenyewe. Fanya kile unachohofia na hofu itakufa yenyewe.

Natutakia siku njema.

Monday, December 1, 2014

SIKU YA UKIMWI DUNIANI; Mambo Kumi Unayotakiwa Kujua Kuhusu Ukimwi.

Kila tarehe 01/12 ya kila mwaka dunia inaadhimisha siku ya UKIMWI. Siku hii imepewa heshma yake kutokana na madhara yake makubwa kwa watu wanaoupata.

Wakati tukiwa kwenye siku hii ya UKIMWI jiongeze na mambo haya kumi muhimu.

1. UKIMWI HAUUI.

UKIMWI maana yake ni upungufu wa kinga mwilini. Hivyo kinga yako inapopungua unatoa nafasi ya magonjwa mengine kukushambulia. Hivyo kinachowaua wagonjwa wa ukimwi sio ukimwi wenyewe bali magonjwa nyemelezi.

2. UKIMWI ni tofauti na VIRUSI VYA UKIMWI.

Ukiambukizwa virusi vya ukimwi leo, hauna ukimwi. Unawez akukaa na vizsi hivi kwa muda hata wa miaka kumi na pale kinga ya mwili inaposhindwa kukulinda na magonjwa ndio unakuwa na UKIMWI.

3. Wagonjwa watatu wa kwanza wa UKIMWI Tanzania waligunduliwa katika hospitali ya Ndolange mkoani Kagera mwezi November 1983.

4. UKIMWI husambazwa kwa kupitia maji maji ya mwilini. Yanayoongoza ni damu, na yenye kiasi kidogo ni mate, machozi na majimaji ya ukeni.

UKIMWI TZ

5. Njia kuwa ya kusambaza ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine ni kufanya mapenzi bila ya kujikinga. Njia nyingine ni kuchangia vitu vikali kama sindano na pia mama kwenda kwa mtoto.

6. Mpaka leo hakuna tiba wala kinga ya UKIMWI. Baadhi ya tafiti zimeonesha matokeo mazuri ila hakuna ambayo imedhibitishwa kutumiwa kama kinga au dawa.

7. Afrika chini ya jangwa la sahara ndio sehemu yenye maambukizi makubwa ya UKIMWI, asilimia 80 ya watu wenye ukimwi duniani wako Africa chini ya jangwa la sahara. Wakati idadi ya wanachi walioko Afrika chini ya jangwa la sahara ni asilimia 10 tu ya idadi ya watu wote duniani.

8. Wanawake wana hatari mara nane zaidi ya kuambukizwa ukimwi kuliko wanaume.

9. Mikoa inayoongoza kwa UKIMWI Tanzania ni Njombe ukifuatiwa na Iringa na mikoa yenye maambukizi madogo ni Pemba, Unguja na Lindi.

10. Mapambano ya UKIMWI yanaanza na mimi na wewe. Njia nyingine za maambukizi zimeweza kuzuiwa kwa kiasi kikubwa ila njia moja ndiyo yenye changamoto na njia hiyo ni kupitia kufanya mapenzi.

Tushirikiane kuutokomeza UKIMWI.

NENO LA LEO; Kisasi Bora

The best revenge is massive success. –Frank Sinatra

Kisasi bora ni mafanikio makubwa.

Kama mtu amekufanyia jambo baya na unataka kulipa kisasi, kisasi bora kulipa ni kuhakikisha unafanikiwa sana.

Nakutakia siku njema.

Sunday, November 30, 2014

Kesho ni siku muhimu sana kwako, na itumie kufanya jambo hili moja muhimu.

Kesho ni tarehe moja mwezi wa kumi na mbili. Maana yake ni kwamba ni siku ya kwanza ya mwezi wa mwisho wa mwaka huu 2014.
Kuanzia kesho zitakuwa zimebaki siku 30 tu mwaka uishe!
Je mwaka huu 2014 uliendaje kwako?
Je malengo na mipango uliyojiwekea umeyatimiza!
Tumia siku ya kesho kutafakari mwaka huu umekwendaje.
Nakutakia kila la kheri,
TUPO PAMOJA.

Sheria Kumi Za Familia Za Kuzingatia

NENO LA LEO; Uwekezaji Unaolipa Riba Kubwa Sana

An investment in knowledge pays the best interest. –Benjamin Franklin

Uwekezaji kwenye elimu/ujuzi ndio uwekezaji unaolipa riba kubwa sana.

Anza sasa kuwekeza kwenye ujuzi na elimu yako, jifunze mambo mapya na yafanyie kazi.

Jinsi unavyojifunza zaidi ndivyo unavyoongeza thamani yako na hivyo kuongeza kipato chako.

Nakutakia siku njema.

Saturday, November 29, 2014

UMUHIMU WA KUSOMA ZAIDI NA KUSOMA KILA MARA;

i. Jinsi unavyoishi jifunze jinsi ya kuishi, hakuna anayejua kila kitu.
ii. Viongozi bora wa uchumi mpya watakuwa ni wale wanaoweza kufikiri vizuri.
iii. Kufikiri vizuri kunajengwa na kusoma sana.
iv. Unachohitaji ili kubadili maisha yako moja kwa moja ni wazo moja tu kutoka kwenye kitabu sahihi.
v. Beba kitabu popote unapokuwa, ukiwa unamsubiri mtu soma, ukiwa kwenye foleni soma. Usipoteze muda wako kulalamika.
vi. Kama hujasoma kitu kizuri leo, hujaishi siku ya leo. Na kusoma huku sio habari, bali kitu kinachoweza kukusogeza karibu na malengo yako kweny maisha.
Kupata nafasi ya kusoma zaidi tembelea www.voraciousreaderstz.blogspot.com

Mambo matatu yatakayokufanya uishi maisha marefu.

Magonjwa mengi yanayowafanya watu kufa wakiwa na umri mdogo yanatokana na mtindo wa maisha tunaochagua.
Magonjwa kama presha ya juu, kisukari na hata kansa yanatokana na mitindo mbalimbali ya maisha.
Hapa nakushirikisha mambo matatu unayoweza kuanza kuyafanya leo na ukapunguza nafasi ya wewe kupata magonjwa haya na hivyo kuishi miaka mirefu.
1. Kula vizuri.
Naposema kula vizuri namaanisha ule mlo kamili. Kula mafita kidogo na kwa mtu mzima kula wanga kidogo. Kula matunda na mboga ,boga kwa wingi na pia kunywa maji mengi.
2. Fanya mazoezi.
Mazoezi ni muhimu sana kwa afya yako. Na mazoezi sio lazima ulipie gym au kukimbia barabarani japo hiyo ni sehemu nzuri ya mazoezi.
Unaweza kuchagua kutembea kwa miguu badala ya kupanda gari, kupanda ngazi badala ya kupanda lifti na kusimama na kufuata kitu mwenyewe badala ya kuagiza uletewe.
3. Usivute sigara.
Kila unapovuta sigara moja unapunguza dakika 14 za maisha yako. Sigara ina kemikali zaidi ya elfu moja zinazosababisha kansa. Karibu kila kansa inayompata binadamu inaweza kuchochewa na uvutaji wa sigara.
Na sigara sio lazima uvute wewe, hata ule moshi unaovuta kutoka kwa watu wanaovuta sigara una athari kubwa kwa afya yako.
Hayo ndio mambo matatu ambayo unaweza kuanza kuyafanya leo na ukaboresha afya yako na kyongeza siku zako za kuishi.
Nakutakia kila la kheri,
TUPO PAMOJA.
www.kisimachamaarifa.co.tz
www.amkamtanzania.com

NENO LA LEO; Siku Mbili Muhimu Sana Kwenye Maisha Yako.

The two most important days in your life are the day you are born and the day you find out why. –Mark Twain

Siku mbili muhimu sana kwenye maisha yako ni siku uliyozaliwa na siku uliyojua kwa nini ulizaliwa.

Najua wengi tunajua siku tulizozaliwa ila ni wachache sana wanaojua kwa nini walizaliwa.

Kama bado hujajua kwa nini ulizaliwa kwaribu tusaidiane kujua kwa nini ulizaliwa, yaani ni nini hasa unatakiwa kufanya na maisha yako.

Andika email yenye kichwa cha habari KWA NINI NILIZALIWA na maelezo mengine muhimu kuhusu wewe kisha tuma kwenye email ushauri@kisimachamaarifa.co.tz

Nakutakia siku njema.

Friday, November 28, 2014

NENO LA LEO; Kuhusu Kuendesha Siku Au Kuendeshwa na Siku.

Either you run the day, or the day runs you. –Jim Rohn

Kwenye siku yako ni labda unaiendesha siku au siku inakuendesha wewe.

Unaiendesha siku pale ambapo unakuwa na malengo na mipango yako ambayo unaifuata.

Unaendeshwa na siku pale ambapo unafanya kile kinachotokea mbele yako.

NINAJUA UNAJUA UNACHOTAKIWA KUFANYA, FANYA SASA, LEO HII ILI UWEZE KUIENDESHA SIKU YAKO.

Nakutakia siku njema.

Thursday, November 27, 2014

NENO LA LEO; Unachohitaji Ili Kubadili Maisha Yako.

You can never cross the ocean until you have the courage to lose sight of the shore. –Christopher Columbus

Huwezi kuivuka bahari mpaka pale utakapokuwa na ujasiri wa kupoteza taswira ya ufukwe.

Tunapenda vitu vizuri lakini tunaogopa kupoteza tulivyo navyo. Huwezi kupata vitu vipya kama hutaacha hivyo ulivyonavyo sasa.

Nakutakia siku njema.

Wednesday, November 26, 2014

NENO LA LEO; MUDA MZURI WA KUPAMDA MTI.

The best time to plant a tree was 20 years ago. The second best time is now.

Muda mzuri wa kupanda mti ilikuwa miaka 20 iliyopita. Muda mwingine mzuri ni sasa.

Kila kitu kinahitaji maandalizi ya muda mrefu. Hivyo ili kuwa na maisha bora baadae inabidi uanze kufanya mabadiliko sasa.

Nakutakia siku njema.

Tuesday, November 25, 2014

NENO LA LEO; FURSA UNAZOZIKOSA.

You miss 100% of the shots you don’t take. –Wayne Gretzky

Unakosa asilimia 100 ya fursa ambazo hujazichukulia hatua.

Acha kuendelea kusita sita, unapoteza fursa nyingi na muda wako pia.

Wakati wa kuchukua hatua ni sasa.

Nakutakia siku njema.

Monday, November 24, 2014

Hivi ndivyo shauku inavyokufanya kuwa mteja bila ya kupenda.

Sasa hivi tumekuwa watu wa kuendeshwa na shauku inayotokana na hisia. Na hii imetufanya tuwe wateja kwa wanaoweza kuzitumia hisia na shauku zetu.
Kwa mfano;
Kuna tofauti gani kwa anayenunua simu mpya iliyotoka leo kwa kusubiria muda mrefu na atakayekuja kuinunua kesho wakati kumetulia?
Kuna tofauti gani kati ya anayesikia habari mpya leo, BREAKING NEWS na atakayeisikia kesho?
Kuna tofauti gani kwa atakayekuwa wa kwanza kusambaza habari na ambae hatakuwa na haraka hiyo?
Yote haya na mengine mengi hayana tofauti ila yanatufanya tuwe wateja wa matoleo mapya, habari zilizovunjika na mbaya zaidi kusambaza habari ambazo hatuna uhakika nazo ili tu uwe wa kwanza......
Huna haja ya kuwa wa kwanza katika mambo haya, ni kujiongezea tu msongo.

NENO LA LEO; Kuhusu Fedha Kutonunua Furaha.

Watu wote wanaosema fedha haiwezi kununua furaha nao hawana fedha za kuwatosha. Sijawahi kumsikia tajiri akitumia kauli hiyo kwamba fedha haiwezi kununua furaha.

Hivyo basi badala ya kukubali tu kauli hiyo kwa nini usiifanyie majaribio? Kuwa na fedha nyingi halafu uone kama kweli zinaweza kununua furaha au la.

Nakutakia siku njema.

Sunday, November 23, 2014

Mahitaji Manne Ya Mtu Kuwa Kiongozi.

Ili uweze kuwa kiongozi bora na mwenye mafanikio kuna vitu vinne unavyotakiwa kuwa navyo na uweze kuvisimamia. Kwa kujua na kusimamia vitu hivi kutakuwezesha kufanikiwa sana kama kiongozi.

1. Kuweza kujisimamia mwenyewe.

Kiongozi bora ni yule ambaye anayeweza kujisimamia mwenyewe. Ni lazima uweze kujiwekea malengo na mipango yako mwenyewe na uweze kuifuata bila ya kusimamiwa na mtu mwingine yeyote. Kama unahitaji kusimamiwa ndio uweze kutekeleza majukumu yako basi wewe sio kiongozi bali ni mfuasi. Na kama ukijaribu kuongoza kama unakosa tabia ya kujisimamia mwenyewe utashindwa vibaya sana.

2. Kuweza kutatua matatizo.

Kazi kubwa ya kiongozi ni moja, kutatua matatizo. Ili uweze kuwa kiongozi bora inabidi uweze kuyaangalia matatizo kwa jinsi gani yanaweza kutatuliwa. Kama unaogopeshwa na tatizo na kuona haliwezi kutatuliwa wewe sio kiongozi. Kila tatizo lina utatuzi wake. Ni kazi yako kama kiongozi kuja na njia za kutatua tatizo hilo na hivyo kuboresha hali iliyopo.

3. Kuweza kufanya mawasiliano mazuri.

Kiongozi bora ni yule ambaye anaweza kufikia ujumbe wake kwa watu anaowaongoza na wakauelewa na kuufanyia kazi ujumbe huo. Ili kuweza kufikisha ujumbe wao vizuri ni lazima uwe na mbinu nzuri za mawasiliano. Mawasiliano yanaweza kuwa ya maneno, maandishi au hata vitendo. Jinsi ambavyo unawasilisha ujumbe wako unaweza kuwa na ushawishi mkubwa au ukapuuzwa na wale wanaoupokea. Ni muhimu kujifunza mbinu bora za kufanya mawasiliano ili uweze kufikisha ujumbe wako na ufanyiwe kazi.

4. Kuweza kujenga mahusiano.

Kiongozi ni mtu na anayewaongoza ni watu. Ili uweze kuwa kiongozi bora ni lazima uwe na mahusiano mazuri na wale ambao unawaongoza. Kiongozi sio mtawala kwamba anachokisema yeye ndio mwisho, bali anahitaji kujenga urafiki na watu ambao anawaongoza. Kwa urafiki huu watu anaowaongoza watakuwa tayari kumshauri mambo mengi ambayo yatamsaidia kuongoza vizuri zaidi.

Hayo ndio mambo manne unayohitaji kuwa nayo ili kuwa kiongozi bora. Habari nzuri ni kwamba mambo yote hayo manne unaweza kujifunza na kuyaendeleza kwenye uongozi wako.

Nakutakia kila la kheri kwenye mafanikio yako kama kiongozi.

TUPO PAMOJA.

Saturday, November 22, 2014

NENO LA LEO; Tofauti Ya Washindi Na Washindwa.

Winners make goals... losers make excuses!

Washindi wanatengeneza malengo, washindwa wanatengeneza visingizio.

Amua leo kuwa mshindi na weka malengo na mipango mikubwa kwenye maisha yako. Acha sasa kutafuta visingizio.

Nakutakia siku njema.

Thursday, November 20, 2014

NENO LA LEO; Kuhusu Kujitetea.

It will do no good to argue if you're in the wrong. If you're right, you don't need to.

Kama umekosea au uko upande ambao sio sahihi, kujitetea hakuwezi kusaidia. Kama uko sahihi huna haja ya kujitetea.

Nakutakia siku njema.

Tuesday, November 18, 2014

NENO LA LEO; Mwalimu Bora.

The best teachers teach from the heart, not from the
book.

Mwalimu bora anafundisha kutoka moyoni na sio kutoka kwenye vitabu.

Nakutakia siku njema.

Monday, November 17, 2014

Hivi ndivyo unavyoweza kuianza wiki yenye mafanikio.

Habari za asubuhi rafiki?
Ni siku nyingine mpya na mwanzo wa wiki mpya.
Naamini umeipangilia wiki yako vizuri kwa ajili ya kufikia mafanikio makubwa.
Wiki hii fanya kitu hiki kimoja;
Dhibiti kiwango cha taarifa unazopata, hasa kupitia vyombo vya habari. Hii ni kwa sababu taarifa nyingi ni;
i. Zinakula muda wako mwingi
ii. Ni hasi
iii. Hazina uhusiano na malengo yako.
iv. Huwezi kuziathiri, ziko nje ya uwezo wako.
Nakutakia wiki njema na yenye mafanikio makubwa.
TUPO PAMOJA.
Tembelea www.amkaconsultants.blogspot.com kujifunza zaidi.

Saturday, November 15, 2014

NENO LA LEO; Kuhusu Kuamini Uongo.

It is easier to believe a lie that you have heard a
thousand times, than the truth that you have only heard once.

Ni rahisi kuamini uongo uliousikia mara elfu moja kuliko kuamini ukweli uliousikia mara moja.

Ukweli utabaki kuwa ukweli, ukatae au ukubali.

Nakutakia siku njema.

Friday, November 14, 2014

NENO LA LEO; Maana Halisi Ya Machozi

Tears are words the heart can't express.

Machozi ni maneno ambayo moyo hauwezi kuyaeleza.

Machozi ni hisia kubwa sana inayotolewa na mtu, inaweza kuwa furaha au inaweza kuwa huzuni. Hakikisha unaleta machozi ya furaha kwa watu wako wa karibu.

Nakutakia siku njema.

Wednesday, November 12, 2014

NENO LA LEO; Chanzo Cha Mafanikio.

Achieving starts with believing in yourself.

Mafanikio huanza pale unapojiamini mwenyewe.

Anza sasa kujiamini na amini una uwezo mkubwa ulioko ndani yako wa kufikia mafanikio makubwa.

Nakutakia siku njema.

Tuesday, November 11, 2014

NENO LA LEO; Mambo Unayotakiwa Kufanya.

You have to do what others won't. To achieve what others don't.

Unatakiwa kufanya mambo ambayo watu wengine hawafanyi ili kupata vitu ambavyo wengine hawapati.

Kupata mafanikio makubwa unahitaji kuwa tofauti na wengine.

Nakutakia siku njema.

Monday, November 10, 2014

NENO LA LEO; Kuhusu Mtu Anayejua Kila Kitu.

Any man who knows all the answers most likely misunderstood the questions.

Mtu anayejua majibu yote kuna uwezekano mkubwa haelewi maswali.

Katika ulimwengu wa sasa ni vigumu sana kujua kila kitu, chagua vitu vichache unavyotaka kuvijua na vijue vizuri.

Nakutakia siku njema.

Sunday, November 9, 2014

Mambo 21 muhimu ya kiufanya kila siku ili kuwa na maisha yenye mafanikio.

HABARI ZA LEO RAFIKI?
Naomba nikushirikishe Vitu 21 rahisi vya kufanya kila siku ili kuwa na maisha yenye furaha na mafanikio.
i. Lala masaa nane kwa siku.
ii. Kula milo miwili kwa siku.
iii. Usiangalie TV
iv. Usile vyakula vya haraka
v. Usilaumu wala kulalamika
vi. Usisengenye, usishiriki majungu na umbea.
vii. Onesha shukrani kwa marafiki.
viii. Andika orodha ya mawazo bora kila siku.
ix. Iambie nafsi yako unapoamka kwamba utakwenda kusaidia na kuokoa maisha ya watu kwa siku hiyo.
x. Andika mambo unayopanga kufanya kwa siku.
xi. Mshangaze mtu.
xii. Fikiria watu kumi ambao unashukuru kuwa nao kwenye maisha yako.
xiii. Msamehe mtu.
xiv. Panda ngazi badala ya lifti.
xv. Usiseme ndio wakati unafikiria kusema hapana.
xvi. Mwambie mtu kila siku kwamba unampenda.
xvii. Soma sura moja ya kitabu cha mtu anayekuhamasisha.
xviii. Weka mipango ya kutumia muda na rafiki yako.
xix. Pumua kwa kina na taratibu.
xx. Jifunze kitu kipya kila siku, pata walau saa moja ya kujisomea.
xxi. Fikiria watu wawili unaoweza kuwakutanisha na wakasaidiana na kushirikiana.
Kutoka kwa James Altucher - Choose Yourself.
Tembelea www.amkaconsultants.blogspot.com kujifunza zaidi.
TUPO PAMOJA, TUTAKUTANA KILELENI.

Nguzo Kuu Ya Uongozi; Tekeleza Kile Unachoahidi.

Katika kujijenga kuwa kiongozi bora na imara kuna misingi mingi ya uongozi ambayo unatakiwa kuifuata. Kushindwa kufuata misingi hii kutapelekea uongozi wako kushindwa na hata kudharaulika sana.

Moja ya nguzo muhimu za uongozi ni kutekeleza kile unachoahidi. Kuongea ni rahisi sana na hivyo watu wengi hujikuta wakiongea mambo ambayo hawana uhakika kama wanaweza kuyatekeleza. Kwa kuwa kuongea ni rahisi watu hutumia nafasi hii kuongea mambo ambayo yatawafanya waonekane ni viongozi wazuri ila hawana uwezo wa kuyatekeleza.

Madhara ya kuahidi mambo usiyoweza kutekeleza.

1. Inakuondolea uaminifu.

Unapoahidi mambo halafu ukashindwa kuyatekeleza watu huondoa uaminifu kwako. Hivyo wakati mwingine utakapowaahidi hawatakusikiliza na hata wakikusikiliza hawataweka maanani uliyowaambia. Kwa sababu binadamu wana tabia moja kwamba ukishamdanganya mtu mara moja kila wakati atakuwa na wasi wasi na wewe.

2. Itakuondolea ushawishi.

Uongozi ni ushawishi, kama utaahidi mambo ambayo huwezi kuyatekeleza na kufanikiwakuwashawishi watu mara ya kwanza, baadae utapoteza ushawishi huo kama hukutekeleza yale uliyoahidi mara ya kwanza. Unapopoteza ushawishi unapoteza uongozi.

3. Unapoteza heshima yako.

Unapokuwa mtu wa kutekeleza maneno yako unaheshimika na wale unaowaongoza na hata jamii kwa ujumla. Unapoanza kuahidi mambo ambayo unashindwa kuyatekeleza unapoteza heshima yako.

Anza sasa kutekeleza kile unachoahidi kufanya, itakujengea sifa nzuri kama kiongozi na itakuongezea ushawishi na heshima mbele ya jamii.

Kama umeahidi wateja kwamba utawapatia bidhaa au huduma bora tekeleza ahadi yako.

Kama umewaahidi wafanyakazi wako kwamba wakifikia kiwango fulani cha uzalishaji utawaongeza mshahara basi timiza ahadi yako wanapofikia kiwango hiko.

Kama umewaahidi wananchi wakupigie kura ili uweze kuwasaidia kufikia maendeleo, tekeleza ahadi uliyotoa.

Hivi ndivyo unavyoweza kuwa kiongozi bora, TEKELEZA AHADI ZAKO NA IKIWEZEKANA ONGEZA ZAIDI.

Nakutakia kila la kheri katika uongozi wako.

TUPO PAMOJA.

Saturday, November 8, 2014

NENO LA LEO; Kuhusu Kikomo Cha Kasi Kwenye Njia Ya Mafanikio.

There are no speed limits on the road to excellence.

Hakuna kikomo cha kazi kwenye njia ya mafanikio.

Amua leo kwenda kwa kasi kubwa ili uweze kufikia mafanikio makubwa. Hakuna mda wa kupoteza.

Nakutakia siku njema.

Friday, November 7, 2014

NENO LA LEO; Maana Halisi Ya Msamaha

Forgiveness is all about me giving up my right to hurt you for hurting me.

Msamaha ni pale ambapo mimi naamua kupoteza haki yangu ya kukuumiza wewe kwa kuniumiza mimi.

Unaposamehe unaepuka kutengeneza maumivu zaidi.

Amua leo kuwasamehe wote waliokuumiza, maana kuendelea kukaa na kinyongo unazidi kuumia wewe.

Nakutakia siku njema.

Thursday, November 6, 2014

NENO LA LEO; Mambo Mawili Muhimu Sana Kujua Kuhusu Maisha.

Life can either be accepted or changed. If it is not
accepted, it must be changed. If it cannot be changed, then it must be accepted.

Maisha yanaweza kukubaliwa au yanaweza kubadilishwa. Kama hayakubaliwi ni lazima yabadilishwe. Kama hayawezi kubadilishwa ni lazima yakubaliwe.

Usiendelee tena kuteseka na maisha yako, kama kuna kitu hukipendi kibadilishe na kama huwezi kukibadilisha kikubali. Ukiweza kufanya hivi maisha yako yatakuwa ya furaha.

Nakutakia siku njema.

Wednesday, November 5, 2014

NENO LA LEO; Kukolea Kwenye Tabia Mbaya.

Bad habits are like a comfortable bed; they are easy to get into, but hard to get out of.

Tabia mbaya ni kama kitanda kizuri, ni rahisi kuingia ila ni vigumu sana kutoka.

Kama kuna tabia ambayo huipendi fanya jitihada kubwa kuondokana nayo.

Nakutakia siku njema.

Tuesday, November 4, 2014

NENO LA LEO; Mbinu Ya Kufikia Urefu Mkubwa.

To reach a great height a person needs to have great depth.

Kufikia urefu mkubwa mtu anahitaji kuwa na kina kikubwa.

Kiendacho juu kinategemea uimara wa kilichopo chini. Kama ilivyo kwamba ghorofa ndefu ina kina kikubwa na msingi imara.

Nakutakia siku njema.

Monday, November 3, 2014

Tukemee Tabia Hii Mbaya Kama Taifa.

Jana tarehe 02/11/2014 kulikuwa na mdahalo wa katiba ulioandaliwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere uliokuwa unafanyika katika ukumbi wa ukumbi wa ubungo plaza.

Katika mdahalo huo waliokuwa wajumbe wa iliyokuwa tume ya katiba walialikwa kuzungumza na baadae wananchi waliohudhuria nao wangepata nafasi ya kuzungumzia katiba pendekezwa.

Lengo kubwa la mdahalo huo na mingine ambayo tuliahidiwa itafuata ilikuwa kuwapa uelewa wananchi juu ya katiba pendekezwa kabla wakati wa kupiga kura haujafika.

Binafsi ninaona kitu hiki ni kizuri sana maana taasisi inayoandaa midahalo hii haina uegemeo wowote wa kisiasa na hivyo itatoa nafasi nzuri ya wananchi kujifunza yaliyomo kwenye katiba pendekezwa.

Katika hali ya kushangaza wakati mdahalo unaendelea na Jaji Warioba akizungumza kiliibuka kikundi cha watu ambao walionesha mabango ya kupinga mdahalo ule na kusema kwamba wanaikubali katiba pendekezwa. Hata walipotakiwa kutulia chini ili mdahalo uweze kuendelea bado hawakusikia na hatimaye ikapelekea vurugu kubwa na mdahalo kuahirishwa.

WARIOBA

Kwanza kabisa hiki ni kitendo cha ajabu sana ambacho kinatakiw akulaaniwa na kila Mtanzania ambaye ana mapenzi mema na nchi hii. Ni kweli kabisa hatuwezi kukubaliana wote, ila kutofautiana kwetu kifikra na kihoja kusifanye tuonanae kama maadui. Hizi ni siasa chafu na za kitoto sana ambazo naona zinanyamaziwa na wanaofanya ujinga huu wanaonekana kama wanaleta manufaa kwa kikundi fulani.

Kama unaona mtu anakushinda kwa hoja njia sahihi ni kuleta fujo na kupigana? Hapana hii sio njia sahihi kabisa na kama tutaendelea kuacha mambo haya yaendelee tutalipeleka taifa kubaya.

Katiba ni kitu ambacho kinamhusu kila mwananchi na hivyo kila mwananchi ana uhuru wa kutoa maoni yake na hisia zake juu ya katiba hii. Lakini katika kutoa maoni hayo na hisia hizo usiingilie uhuru wa mwenzako au kuleta fujo au kumwona anayeamini tofauti na wewe ni adui.

Naomba watanzania wote tulaani kitendo hiki kilichotokea na tusitoe tena nafasi ya kutokea kwa kitendo kama hiki.

Tanzania ni nchi yetu sote, tushirikiane kuijenga.

TUPO PAMOJA.

LEO KATIKA HISTORIA; TAREHE 03/11/2014

November 3

1493
Christopher Columbus arrives at the Caribbee Isles (Dominica) during his second expedition.

1507
Leonardo da Vinci is commissioned to paint Lisa Gherardini ("Mona Lisa").

1529
The first parliament for five years opens in England and the Commons put forward bills against abuses amongst the clergy and in the church courts.

1794
Thomas Paine is released from a Parisian jail with help from the American ambassador James Monroe. He was arrested for having offended the Robespierre faction.

1813
American troops destroy the Indian village of Tallushatchee in the Mississippi Valley.

1868
Ulysses S. Grant elected the 18th president of the United States.

1883
A poorly trained Egyptian army, led by British General William Hicks, marches toward El Obeid in the Sudan–straight into a Mahdist ambush and massacre.

1883
The U.S. Supreme Court declares American Indians to be "dependent aliens."

1892
First automatic telephone exchange goes into operation in La Porte, Indiana.

1896
William McKinley is elected 25th president of the United States.

1912
The first all-metal plane flies near Issy, France, piloted by Ponche and Prinard.

1918
The German fleet at Kiel mutinies. This is the first act leading to Germany's capitulation in World War I.

1921
Milk drivers on strike dump thousands of gallons of milk onto New York City's streets.

1935
Left-wing groups in France form the Socialist and Republican Union.

1957
The Soviet Union launches Sputnik II with the dog Laika, the first animal in space, aboard.

1964
For the first time residents of Washington, D.C., are allowed to vote in a presidential election.

1964
Lyndon B. Johnson is elected the 36th president of the United States.

1964
Robert Kennedy, brother of the slain president, is elected as a senator from New York.

1967
The Battle of Dak To begins in Vietnam's Central Highlands; actually a series of engagements, the battle would continue through Nov. 22.

1969
US President Richard Nixon, speaking on TV and radio, asks the "silent majority" of the American people to support his policies and the continuing war effort in Vietnam.

1973
NASA launches Mariner 10, which will become the first probe to reach Mercury.

1979
Ku Klux Klansmen and neo-Nazis kill 5 and wound 7 members of the Communist Workers Party during a "Death to the Klan" rally in Greensboro, NC; the incident becomes known as the Greensboro Massacre.

1983
Jesse Jackson announces his candidacy for the office of president of the United States.

1986
The Lebanese magazine Ash-Shiraa reports the US has secretly been selling weapons to Iran in order to secure the release of 7 American hostages being held by pro-Iranian groups in Lebanon.

1992
Arkansas Governor Bill (William Jefferson) Clinton is elected 42nd president of the United States.

1997
US imposes economic sanctions against Sudan in response to human rights abuses and support of Islamic extremist groups.

Born on November 3

1718
John Montague, fourth Earl of Sandwich and inventor of the sandwich.

1794
William Cullen Bryant, poet and journalist.

1801
Karl Baedeker, German publisher, well known for travel guides.

1831
Ignatius Donnelly, American social reformer best known for his book Atlantis: The Antediluvian World.

1901
Andre Malraux, French novelist (Man's Fate).

1903
Walker Evans, photographer.

1909
James "Scotty" Reston, New York Times reporter, editor and columnist.

1918
Russell Long, U.S. senator from Louisiana from 1951 to 1968 and son of Huey P. Long.

1920
Oodgeroo Noonuccal [Kath Walker], Australian Aboriginal poet.

1933
Jeremy Brett, actor; best known for his portrayal of Sherlock Holmes in the Granada TV productions of Sir Arthur Conan Doyle's stories about the detective.

1933
Michael Dukakis, politician; the longest-serving governor in the history of the State of Massachusetts (1975-79, 1983-91); unsuccessful Democratic candidate for US presidency (1988).

1933
Amartya Sen, Indian economist, winner of Nobel Memorial Prize in Economic Sciences (1998) for his work on economic theories of famines and social justice and indexes for measuring the well-being of citizens in developing countries.

1942
Martin Cruz Smith, novelist (Gorky Park).

1949
Larry Holmes, professional boxer known as The Easton Assassin; his 20 successful defenses of his heavyweight title is second only to Joe Louis' record 25.

1952
Roseanne Barr, comedian, actress, producer; best known for her starring role in the TV series Roseanne, for which she won both an Emmy and a Golden Globe.

1952
David Ho, virologist, AIDS researcher.

1956
Gary Ross, film director, screenwriter (The Hunger Games, Seabiscuit).

NENO LA LEO; Kuhusu Dunia Kutokukuzuia.

The whole world steps aside for the man who knows where he is going.

Dunia nzima hukaa pembeni na kumpisha mtu anayejua anakoelekea.

Kuwa na ujasiri wa kujua unakoelekea na hakuna kitakachoweza kukuzuia.

Nakutakia siku njema.

Sunday, November 2, 2014

NENO LA LEO; Sehemu Ambapo Hofu Itakuwahisha.

Perpetual worry will get you to one place ahead of time - the cemetery.

Hofu ya kila mara itakusaidia kuwahi sehemu moja – kaburini.

Ni kweli hofu inaweza kukusababishia kifo.

Kuwa makini.

Nakutakia siku njema.

Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Ni Muhimu Sana. Tuzingatie Mambo Haya Matano.

Tarehe 14/12/2014 itakuwa siku muhimu sana katika miaka mitano ijayo. Siku hii itakuwa ni siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa. Watu wengi sana hawaupi uchaguzi huu nafasi kubwa na wameelekeza macho na masikio yao kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Hili ni kosa kubwa sana ambalo tunafanya watanzania wenzangu. Uchaguzi wa serikali za mitaa ni muhimu kama ilivyo uchaguzi mkuu. Ni kupitia serikali za mitaa ambapo tunakuwa na demokrasia ya moja kwamoja. Yaani kama kuna jambo lolote la kufanya maamuzi kwenye mtaa au kijiji basi wananchi wote watafanya maamuzi kwenye vikao na mikutano mbalimbali.

Pia serikali hizi za mitaa zina mamlaka ya kutunga sheria ndogo ndogo ambazo zinaweza kuwa na athari chanya au hasi kwetu sisi wananchi.

Serikali za vijiji zina mamlaka makubwa sana kwenye ardhi na hivyo zinaweza kufanya maamuzi ya kuuza ardhi kwa watu mbalimbali. Hivyo unapokuwa na serikali ya kijiji ambayo sio imara mnaweza kujikuta mnapoteza ardhi yenu.

Mwisho kabisa naamini mabadiliko na maendeleo ya nchi hii yanaweza kuanzia kwenye ngazi ya mitaa, vitongoji au vijiji. Hii ni kwa sababu matatizo yoyote tunayokumbana nayo kama taifa yanaanzia katika ngazi ya familia na hatimaye mitaa. Kwa mfano wahalifu wote wanaishi kwenye mitaa yetu, wauzaji wa madawa ya kulevya na hata watumiaji wanakaa kwenye mitaa yetu. Hivyo tukiweza kuwa na serikali zamitaa ambazo zipo imara tunaweza kujenga misingi mizuri kama taifa.

Baada ya kuona umuhimu huo mkubwa wa serikali za mitaa sasa naomba nikushirikishe mambo matano muhimu ya kuzingatia kwenye uchaguzi huu wa serikali za mitaa.

1. Hakikisha unapiga kura na hamasisha wengine nao wapige kura.

Ule utamaduni wetu watanzania wa kutokupiga kura halafu tunakuwa wa kwanza kulalamika kwamba viongozi ni wabovu sio utaratibu mzuri. Hakikisha unapiga kura siku hiyo ya uchaguzi na pia washawishi ndugu jamaa na marafiki zako nao wapige kura siku hiyo. Kura yako moja ina thamani kubwa sana, usiidharau.

uchaguzi

2. Chagua kiongozi mwenye maono na mwenye historia nzuri.

Kwanza kabisa mtu ambaye mtamchagua awe mtu ambaye mnamjua vizuri. Awe ni mtu ambaye amekaa kwenye mtaa huo na mna historia yake nzuri ya namna ambavyo amekuwa akihamasisha mambo mbalimbali kwenye mtaa au kijiji chenu. Awe ni mtu mwenye maono na anayefikiria na kukubali mabadiliko. Kiongozi wa aina hii ataweza kushirikiana nanyi kuleta maendeleo kwenye eneo lenu.

Kujua zaidi kuhusu tabia za viongozi bonyeza maandishi haya.

3. Mtu yeyote atakayotoa rushwa usifikirie mara mbili, usimpigie kura na hamasisha wengine wasimpigie kura.

Uongozi wa serikali za mitaa ni uongozi ambao hauna manufaa makubwa kifedha zaidi ya posho ndogo ndogo. Sasa mtu ambaye anatoa rushwa lili kupata nafasi hiyo, jiulize ananufaikaje? Kwa vyovyote vile atahakikisha akipata nafasi analipa fedha yake aliyowekeza kwa kutoa rushwa hivyo atawaingiza kwenye matatizo.

4. Chagua mtu, usichague chama.

Kwa siasa zetu za Tanzania bado haturuhusu mgombea binafsi hivyo unalazimika kuchagua mgombea anayeletwa na chama fulani. Chama kinaweza kuwa na sera nzuri sana ila kama kitakuwa na mgombea ambaye hana uwezo mzuri wa uongozi sera hizo ni kazi bure. Hivyo hudhuria mikutano ya kampeni, wafatilie vizuri wagombea wote na mchague mtu ambaye unaona anaweza kuleta mabadiliko kwenye mtaa au kijiji chenu. Hata kama wewe ni mkereketwa wa chama fulani ila ukaona mgombea wa chama kingine ana sifa zaidi ya mgombea wa chama chako, mpigie kura. Mwisho wa siku maendeleo yatakuwa ni kwa mtaa wenu na sio chama chenu.

5. Tuoneshe ushirikiano na kuwawajibisha viongozi tuliowachagua.

Baada ya uchaguzi na viongozi kupatikana ni vyema kuweka tofauti za kisiasa pembeni na kupeana ushirikiano ili kiongozi mliyemchagua aweze kutekeleza majukumu yake. Kwa kuonesha ushirikiano mzuri italeta mafanikio makubwa kwa mtaa au kijiji chenu.

Pia pale ambapo kiongozi mliyemchagua anakwenda kinyume na ahadi zake ni vizuri kumwajibisha. Kwenye serikali za mitaa tupo karibu sana na viongozi wetu na hivyo ni rahisi kuhoji mambo mbalimbali ambayo mnaona hayaendi sawa.

Nichukue nafasi hii kuwatakia watanzania wote uchaguzi mwema na twende tukafanye maamuzi sahihi kwa mitaa na vijiji vyetu kwa miaka mitano ijayo.

Tanzania ni yetu sote, tushirikiane kuijenga.

Friday, October 31, 2014

Ushauri Muhimu Kwa Wanafunzi Wa Kidato Cha Nne.

Jumatatu ijayo tarehe 03/11/2014 wanafunzi wa kidato cha nne wanakwenda kuanza mitihani yao ya kuhitimu kidato cha nne. Hii ni hatua muhimu sana kwenye maisha yao kwani ndio itapelekea ndoto zao nyingine kuwa kweli. Kama mwananfunzi ana ndoto ya kuwa injinia, rubani, daktari au mwalimu, mitihani hii ni muhimu kwake kufaulu ili kuweza kuendelea na masomo yako.

Hapa napenda kushauri mambo kumi kwa wnafunzi wa kidato cha nne wanaokwenda kuanza mitihani yao. Kwa yeyote anayesoma hapa fikisha ushauri huu kwa mwanafunzi unayemjua, anaweza kuwa kuwa mtoto wako, mdogo wako, ndugu au hata jirani.

1. Kwanza kabisa nitoe hongera kwa wanafunzi wote waliovumilia miaka yote minne na hatimaye sasa mnakaribia kabisa mitihani yenu ya mwisho. Sio kazi ndogo hivyo unastahili pongezi.

2. Kubuka yale uliyosoma na kufundishwa katika miaka yote minne uliyokuwa shuleni. Maswali ya mtihani yanatoka katika mambo hayo.

3. Jiamini unapokuwa kwenye chumba cha mtihani, usiwe na hofu au wasiwasi kwamba mtihani ni mgumu au utafeli. Jitahidi kadiri ya uwezo wako.

4. Wahi kufika kwenye chumba cha mtihani, jitahidi ufike nusu saa kabla ya mtihani kuanza hii itakufanya upate muda wa kutuliza akili. Ukichelewa nakukuta mtihani umeshaanza una nafasi kubwa ya kutofanya vizuri.

5. Unapopewa mtihani wako soma maswali yote kisha chagua maswali unayoweza kuanza nayo na ukayafanya vizuri. Kumbuka huwezi kufanya maswali yote kabisa kwenye mtihani, hivyo anza na yale ambayo unaweza kuyafanya vizuri. Kabla ya kujibu swali hakikisha umelielewa.

KIDATO

6. Ukisikia kuna habari za mtihani umevuja usijihangaishe nazo, zitakupotezea muda na kujiamini na mara nyingi ni habari za uongo. Jiamini kwa yale ambayo umefundishwa na kujisomea, yanakutosha kufaulu mtihani wako.

7. Usipanick, hata unapoona umekosea swali kata na ufanye kwa usahihi. Kukosea swali kwenye mtihani ni swala la kawaida, ila utakapopanick ndio utaharibu kila kitu. Kama umekosea swali, kata na uanze kulifanya kwa usahihi.

8. Ukitoka kwenye chumba cha mtihani msijadili maswali ya mtihani uliopita, unaweza kukata tamaa na kujiona umeshafeli. Mara nyingi baada ya mtihani utapenda kujua wenzako walijibu vipi swali fulani, bahati mbaya sana hakuna hata mmoja wenu ambaye ana jibu sahihi hivyo usisikilize maongezi ya aina hiyo.

9. Siku za mtihani hakikisha unapata usingizi wa kutosha, usikeshe kusoma, akili itashindwa kufikiria vizuri. Hakikisha unapata angalau masaa nane ya kulala na pia hakikisha unapata kifungua kinywa asubuhi kabla ya kwenda kwenye mtihani. Itafanya akili yako iweze kufikiri zaidi.

10. Mwisho kabisa nikuambie kwamba wewe ni hazina kubwa kwa nchi hii, tunakutegemea wewe kama mzalishaji na hata kiongozi wa nchi hii. Jiamini unaweza na fanya maamuzi sahihi kwenye kila hatua utakayokuwa unapitia.

Nakutakia kila la kheri katika mafanikio na ufaulu kwenye mitihani yako.

TUPO PAMOJA.

Ushauri Muhimu Kwa Wanafunzi Wa Kidato Cha Nne.

Jumatatu ijayo tarehe 03/11/2014 wanafunzi wa kidato cha nne wanakwenda kuanza mitihani yao ya kuhitimu kidato cha nne. Hii ni hatua muhimu sana kwenye maisha yao kwani ndio itapelekea ndoto zao nyingine kuwa kweli. Kama mwananfunzi ana ndoto ya kuwa injinia, rubani, daktari au mwalimu, mitihani hii ni muhimu kwake kufaulu ili kuweza kuendelea na masomo yako.

Hapa napenda kushauri mambo kumi kwa wnafunzi wa kidato cha nne wanaokwenda kuanza mitihani yao. Kwa yeyote anayesoma hapa fikisha ushauri huu kwa mwanafunzi unayemjua, anaweza kuwa kuwa mtoto wako, mdogo wako, ndugu au hata jirani.

1. Kwanza kabisa nitoe hongera kwa wanafunzi wote waliovumilia miaka yote minne na hatimaye sasa mnakaribia kabisa mitihani yenu ya mwisho. Sio kazi ndogo hivyo unastahili pongezi.

2. Kubuka yale uliyosoma na kufundishwa katika miaka yote minne uliyokuwa shuleni. Maswali ya mtihani yanatoka katika mambo hayo.

3. Jiamini unapokuwa kwenye chumba cha mtihani, usiwe na hofu au wasiwasi kwamba mtihani ni mgumu au utafeli. Jitahidi kadiri ya uwezo wako.

4. Wahi kufika kwenye chumba cha mtihani, jitahidi ufike nusu saa kabla ya mtihani kuanza hii itakufanya upate muda wa kutuliza akili. Ukichelewa nakukuta mtihani umeshaanza una nafasi kubwa ya kutofanya vizuri.

5. Unapopewa mtihani wako soma maswali yote kisha chagua maswali unayoweza kuanza nayo na ukayafanya vizuri. Kumbuka huwezi kufanya maswali yote kabisa kwenye mtihani, hivyo anza na yale ambayo unaweza kuyafanya vizuri. Kabla ya kujibu swali hakikisha umelielewa.

KIDATO

6. Ukisikia kuna habari za mtihani umevuja usijihangaishe nazo, zitakupotezea muda na kujiamini na mara nyingi ni habari za uongo. Jiamini kwa yale ambayo umefundishwa na kujisomea, yanakutosha kufaulu mtihani wako.

7. Usipanick, hata unapoona umekosea swali kata na ufanye kwa usahihi. Kukosea swali kwenye mtihani ni swala la kawaida, ila utakapopanick ndio utaharibu kila kitu. Kama umekosea swali, kata na uanze kulifanya kwa usahihi.

8. Ukitoka kwenye chumba cha mtihani msijadili maswali ya mtihani uliopita, unaweza kukata tamaa na kujiona umeshafeli. Mara nyingi baada ya mtihani utapenda kujua wenzako walijibu vipi swali fulani, bahati mbaya sana hakuna hata mmoja wenu ambaye ana jibu sahihi hivyo usisikilize maongezi ya aina hiyo.

9. Siku za mtihani hakikisha unapata usingizi wa kutosha, usikeshe kusoma, akili itashindwa kufikiria vizuri. Hakikisha unapata angalau masaa nane ya kulala na pia hakikisha unapata kifungua kinywa asubuhi kabla ya kwenda kwenye mtihani. Itafanya akili yako iweze kufikiri zaidi.

10. Mwisho kabisa nikuambie kwamba wewe ni hazina kubwa kwa nchi hii, tunakutegemea wewe kama mzalishaji na hata kiongozi wa nchi hii. Jiamini unaweza na fanya maamuzi sahihi kwenye kila hatua utakayokuwa unapitia.

Nakutakia kila la kheri katika mafanikio na ufaulu kwenye mitihani yako.

TUPO PAMOJA.

Thursday, October 30, 2014

NENO LA LEO; Kuhusu Hofu.

If you cannot help worrying, remember that worrying cannot help you.

Kama huwezi kuacha kuwa na hofu, kumbuka kwamba hofu haiwezi kukusaidia.

Nakutakia siku njema.

Wednesday, October 29, 2014

JE WAJUA; Kuhusu Ladha Ya Chakula

Bila chakula kuchanganyika na mate huwezi kupata ladha yake.
Mate yanalainisha chakula na kukisambaza kwenye sehemu za ulimi zinazopima ladha.

LEO KATIKA HISTORIA, TAREHE 29/10/2014

October 29

1618
Sir Walter Raleigh is executed. After the death of Queen Elizabeth, Raleigh's enemies spread rumors that he was opposed the accession of King James.

1787
Mozart's opera Don Giovanni opens in Prague.

1814
The Demologos, the first steam-powered warship, launched in New York City.

1901
Leon Czolgosz is electrocuted for the assassination of US President William McKinley. Czolgosz, an anarchist, shot McKinley on September 6 during a public reception at the Temple of Music in Buffalo, N.Y. Despite early hopes of recovery, McKinley died September 14, in Buffalo, NY.

1927
Russian archaeologist Peter Kozloff apparently uncovers the tomb of Genghis Khan in the Gobi Desert, a claim still in dispute.

1929
Black Tuesday–the most catastrophic day in stock market history, the herald of the Great Depression. 16 million shares were sold at declining prices. By mid-November $30 billion of the $80 billion worth of stocks listed in September will have been wiped out.

1945
The first ball-point pen goes is sold by Gimbell's department store in New York for a price of $12.

1949
Alonzo G. Moron of the Virgin Islands becomes the first African-American president of Hampton Institute, Hampton, Virginia.

1952
French forces launch Operation Lorraine against Viet Minh supply bases in Indochina.

1964
Thieves steal a jewel collection–including the world's largest sapphire, the 565-carat "Star of India," and the 100-carat DeLong ruby–from the Museum of Natural History in New York. The thieves were caught and most of the jewels recovered.

1969
The U.S. Supreme Court orders immediate desegregation, superseding the previous "with all deliberate speed" ruling.

1969
First computer-to-computer link; the link is accomplished through ARPANET, forerunner of the Internet.

1972
Palestinian guerrillas kill an airport employee and hijack a plane, carrying 27 passengers, to Cuba. They force West Germany to release 3 terrorists who were involved in the Munich Massacre.

1983
More than 500,000 people protest in The Hague, The Netherlands, against cruise missiles.

1986
The last stretch of Britain's M25 motorway opens.

1998
South Africa's Truth and Reconciliation Commission reports condemns both sides on the Apartheid issue for committing atrocities.

1998
John Glenn, at age 77, becomes the oldest person to go into outer space. He is part of the crew of Space Shuttle Discovery, STS-95.

1998
The deadliest Atlantic hurricane on record up to that time, Hurricane Mitch, makes landfall in Honduras (in 2005 Hurricane Wilma surpassed it); nearly 11,000 people died and approximately the same number were missing.

2004
For the first time, Osama bin Laden admits direct responsibility for the Sept. 11, 2001, terrorist attacks in the US; his comments are part of a video broadcast by the Al Jazeera network.

2008
Delta and Northwest airlines merge, forming the world's largest airline.

2012
Hurricane Sandy devastates much of the East Coast of the US; nearly 300 die directly or indirectly from the storm.

Born on October 29

1882
Jean Giraudoux, French dramatist, novelist and diplomat, famous for his book Tiger at the Gates.

1891
Fanny Brice, comedian, singer and actress.

1897
Joseph G. Göbbels, German Nazi Propaganda Minister who committed suicide in Hitler's bunker.

1905
Henry Green, novelist (Living, Party Going).

1910
A. J. Ayer, English philosopher.

1921
Bill Maudlin, American cartoonist whose GI characters "Willie" and "Joe" appeared in Stars and Stripes newspapers during World War II.

1938
Ralph Bakshi, Palestinian-American director of live films and animated full-length films for adults including 1972's Fritz the Cat (first animated film to be rated X by the Motion Picture Association of America), Wizards (1977) and The Lord of the Rings (1978).

1943
Don Simpson, film producer, screenwriter, actor; (co-producer Flashdance, 1985; Top Gun, 1986).

1945
Melba Moore, disco and R&B singer, actress ("You Stepped into My Life," "Lean on Me").

1946
Peter Green, guitarist, songwriter, founder of the band Fleetwood Mac; regarded as one of the greatest guitarists of all time.

1947
Richard Dreyfuss, actor (American Graffiti, Jaws; won Academy Award for Best Actor for 1977's The Goodbye Girl).

1948
Kate Jackson, actress, director, producer (original Charlie's Angels TV series, Scarecrow and Mrs. King TV series).

1954
Lee Child, author; creator of the Jack Reacher novel series.

1958
David Remnick, journals, author, magazine editor (The New Yorker); won Pulitzer Prize for Lenin's Tomb: The Last Days of the Soviet Empire (1994).

1971
Winona Ryder, actress, producer (Beetlejuice; Girl, Interrupted).

NENO LA LEO; Kuhusu Chakula

Take twice as long to eat half as much.

Tumia muda mrefu zaidi kula chakula kidogo zaidi.

Muda unaotumia kula na kiwango cha chakula unachokula vina madhara kwenye afya yako.

Nakutakia siku njema.

Tuesday, October 28, 2014

LEO KATIKA HISTORIA TAREHE 28/10/2014

October 28

312
Constantine the Great defeats Marcus Aurelius Valerius Maxentius at the Mulvian Bridge.

969
After a prolonged siege, the Byzantines end 300 years of Arab rule in Antioch.

1216
Henry III of England is crowned.

1628
After a fifteen-month siege, the Huguenot town of La Rochelle surrenders to royal forces.

1636
Harvard College, the oldest institution of higher learning in the United States, is founded in Cambridge, Mass.

1768
Germans and Acadians join French Creoles in their armed revolt against the Spanish governor of New Orleans.

1793
Eli Whitney applies for a patent on the cotton gin, a machine which cleans the tight-clinging seeds from short-staple cotton easily and effectively–a job which was previously done by hand.

1863
In a rare night attack, Confederates under Gen. James Longstreet attack a Federal force near Chattanooga, Tennessee, hoping to cut their supply line, the "cracker line." They fail.

1886
The Statue of Liberty, originally named Liberty Enlightening the World, is dedicated at Liberty Island, N. Y., formerly Bedloe's Island, by President Grover Cleveland

1901
Race riots sparked by Booker T. Washington's visit to the White House kill 34.

1904
The St. Louis police try a new investigation method: fingerprints.

1914
The German cruiser Emden, disguised as a British ship, steams into Penang Harbor near Malaya and sinks the Russian light cruiser Zhemchug.

1914
George Eastman announces the invention of the color photographic process.

1919
Over President Wilson's veto, Congress passes the National Prohibition Act, or Volstead Act, named after its promoter, Congressman Andrew J. Volstead. It provides enforcement guidelines for the Prohibition Amendment.

1927
Pan American Airways launches the first scheduled international flight.

1940
Italy invades Greece, launching six divisions on four fronts from occupied Albania.

1944
The first
B-29 Superfortress bomber mission flies from the airfields in the Mariana Islands in a strike against the Japanese base at Truk.

1960
In a note to the OAS (Organization of American States), the United States charges that Cuba has been receiving substantial quantities of arms and numbers of military technicians" from the Soviet bloc.

1962
Soviet Premier Nikita Khrushchev orders Soviet missiles removed from Cuba, ending the
Cuban Missile Crisis.

1965
Construction completed on St. Louis Arch; at 630 feet (192m), it is the world's tallest arch.

1971
Britain launches the satellite Prospero into orbit, using a Black Arrow carrier rocket; this is the first and so far (2013) only British satellite launched by a British rocket.

1982
The Spanish Socialist Workers' Party wins election, giving Spain its first Socialist government since the death of right-wing President Francisco Franco.

2005
Libby "Scooter" Lewis, chief of staff to Vice President Dick Cheney, resigns after being indicted for "outing" CIA agent Valerie Plame.

2007
Argentina elects its first woman president, Cristina Fernandez de Kirchner.

Born on October 28

1875
Gilbert Grosvenor, editor, turned the National Geographic Society's irregularly published pamphlet into a periodical with a circulation of nearly two million.

1896
Howard Hansen, composer, director of the Eastman School of music.

1903
Evelyn Waugh, English novelist who wrote Decline and Fall and Brideshead Revisited.

1909
Francis Bacon, English artist who painted expressionist portraits.

1912
Richard Doll, English epidemiologist who established a link between tobacco smoke and cancer.

1914
Jonas Salk, U.S. scientist who developed the first vaccine against polio.

1926
Bowie Kuhn, Commissioner of Major League Baseball (1969–1984).

1936
Charlie Daniels, country / Southern rock singer, songwriter, musician ("The Devil Went Down to Georgia").

1938
Anne Perry, an author of historical detective fiction, she was herself convicted at age 15 of aiding in the murder of a friend's mother in New Zealand; their crime was the basis for the 1994 film Heavenly Creatures.

1944
Anton Schlecker, founder of the Schlecker Company, which operated retail stores across Europe.

1949
Bruce Jenner, athlete, actor; won gold medal in the Decathlon at the Summer Olympics in Montreal (1976).

1951
Joe R. Lansdale, author ("Hap and Leonard" novel series, "Bubba Ho-Tep"); won World Horror Convention Grand Master Award 2007.

1955
William "Bill" Gates, the chairman and CEO of Microsoft Corporation, the world's largest software firm.

1967
Sophie, Hereditary Princess of Liechtenstein.

1967
Julia Roberts, actress (Pretty Woman, Steel Magnolias; won Academy Award for Best Actress in Erin Brockovich).

1967
John Romero, game designer, developer; co-founded id Software (Doom, Quake).

1972
Brad Paisley, country / Southern rock singer, songwriter, musician ("I'm Gonna Miss Her," "Letter to Me"); his many awards include the Country Music Association's Entertainer of the Year 2010.