Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, December 29, 2014

Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..

Sio kwamba nimekuwa mtabiri ila nina uhakika miaka mia moja ijayo kitu hiki kitatokea.
Kitu hiko ni kwamba wote tunaosoma hapa tutakuwa tumekufa. Ndio namaanisha hata wewe utakuwa umekufa miaka mia moja ijayo kuanzia leo, yaani mwaka 2114.
Na kwa bahati nzuri sana tutakuwa tumekufa kwa kipindi kirefu sana, kwa miaka zaidi ya trilioni inayokuja tutakuwa tumekufa.
Nakwambia yote haya ili nini, si unayajua?
Nataka ufanye nambo mawili;
1. Ishi maisha yako kwa furaha maana muda unaoishi ni mfupi kuliko ambao utakuwa umekufa.
2. Hakikisha unagusa maisha ya wengine ili utakapoondoka uache kumbukumbu ya kuwepo kwako. Kujua jinsi ya kufanya hivyo soma makala hii; sio wote tunaowazika wamekufa.
Kila la kheri.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment