Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Showing posts with label SIASA. Show all posts
Showing posts with label SIASA. Show all posts

Tuesday, May 5, 2015

Kilichotokea Afrika Kusini Na Somo Kubwa La Sisi Watanzania Kujifunza.

Siku za hivi karibuni kumetokea machafuko nchini Afrika Kusini yaliyosababishwa na wananchi ambao ni wazawa wa nchi hiyo, kuwavamia na kuwafukuza wananchi ambao ni raia wa nchi nyingine. Machafuko hayo sio ya kwanza kutokea kwa Afrika Kusini na hata kwa Afrika kwa ujumla. Kumekuwepo na maandamano na machafuko ya aina hii tangu nchi hizi zimepata uhuru.

Leo nataka tujifunze kitu kutokana na machafuko ya aina hii na ni kitu gani tunaweza kufanya sisi Watanzania ili tusijikute kwenye hali kama hizo. Sitaangalia sana upande wa kisiasa kwa sababu lengo la andiko langu hili na kama yalivyo maandiko yangu mengine ni kuangalia hatua gani mimi na wewe tunachukua ili tusijikute kwenye hali ambazo hatuzipendi. Sio kulaumu wala kulalamika, bali kuchukua hatua.

Sababu halisi ya ubaguzi wa kiraia(xenophobia).

Kuna sababu nyingi sana ambazo zinaelezwa kusababisha machafuko ya aina hii. Lakini kuna sababu moja kubwa sana ambayo inabeba sababu nyingine zote. Sababu hiyo ni hali ngumu ya maisha na ukosefu wa ajira.

Kadiri siku zinavyozidi kwenda hali ya maisha inakuwa ngumu sana. Jamii inagawanyika kwenye makundi mawili, kundi moja dogo la wenye hali nzuri na kundi jingine kubwa ambalo linaendelea kukua kila siku la watu wenye maisha magumu sana. Hawa wenye maisha magumu mambo yao yanazidi kuwa magumu kutokana na tatizo la ukosefu wa ajira ambalo linasumbua dunia nzima kwa sasa.

Katika hali kama hii wananchi wazawa, wenye hali ngumu na ambao mara nyingi wanaitegemea serikali itatue matatizo yao, wanaendelea kuweka matumaini yao kwa serikali. Lakini wananchi ambao sio wazawa, ambao wanajua serikali haipo kwa ajili yao wanaweka juhudi, wanafanya kazi za ajabu na hatimaye maisha yao yanakuwa bora kuliko ya wale wazawa. Sasa kadiri siku zinavyokwenda, hawa wageni wanaendelea kuweka juhudi na maisha yao yanakuwa bora, huku wazawa wakiendelea kuilalamikia serikali ifanye jambo.

SOMA; ONDOKA NYUMBANI

Unafika wakati sasa wazawa wanazidi kuwa na hali ngumu na wakiangalia wageni wana hali nzuri, hapa ndipo wanageuka na kuona kumbe adui yao ni mgeni. Kwa nini kwenye nchi yao wenyewe wawe na maisha magumu wakati kuna wageni ambao wanaishi kwa starehe. Hiki ni kitu ambacho kinawaumiza na kushinda kujizuia hivyo kuona suluhisho pekee ni kutumia wingi wao kuwaondoa hawa wageni.

Kwa akili za haraka wazawa watakubaliana wanachofanya ni sahihi, ila unapokuja kufikiri kwa kina unaona jinsi gani wazawa wanajipoteza na kumuacha adui halisi kwa kugombana na mtu ambaye sio hata adui.

Watanzania tunajifunza nini katika hili?

Yalipotokea machafuko haya Afrika Kusini, watanzania tulilipuka sana kulaani matendo yale. Kila mtu aliongea kwa uchungu ni jinsi gani kitendo walichofanya waafrika kusini kilikuwa cha kinyama. Ila baada ya hapo kila mtu aliendelea na mambo yake. Sina hakika sana kama kuna somo lolote ambalo tulijifunza kama taifa ili na sisi tusiingie kwenye hali kama ile. Na kwa kutojifunza chochote tunajiweka kwenye hatari kubwa ya kuja kurudia makosa ambayo wenzetu wameyafanya.

Kwa ufupi sana naomba nikushirikishe mambo ambayo watanzania tunapaswa kujifunza kwenye machafuko yaliyotokea Afrika Kusini.

1. Uzawa hautakubeba, juhudi ndio zitakubeba.

Kuna wakati ambapo tunafikiri kwamba sisi tunastahili zaidi kwa sababu ni wazawa. Ndio ni kweli, wewe wa nyumbani unastahili kupewa kipaumbele. Lakini kabla ya kupewa kipaumbele umeonesha nini. Hautabebwa kwa sababu wewe ni mzawa, utabebwa kwa sababu wewe unakitu muhimu kinachotakiwa. Tunaona makampuni mengi yanakwenda kuwekeza Lindi na Mtwara kwa sababu kuna gesi. Kampuni haitakupa wewe kazi kWa sababu tu ni mzawa, itakupa wewe kazi kwa sababu unazo sifa za kufanya kazi husika, Na hata kama kazi haihitaji sifa, basi unaonesha juhudi kwenye kazi unayopewa.

Hakuna kampuni inayopenda kuajiri raia wa kutoka nchi nyingine, kama ingeweza kupata wazawa wenye uwezo wa kufanya kazi husika. Ni gharama zaidi kuajiri raia wa nje kuliko raia wazawa.

Watanzania tujiandae sana kwa hili. Tumekuwa tunaona mambo machache ambayo sasa hivi bado hayajatuumiza ila kama hatutachukua hatua itakuwa tatizo baadae. Kwa mfano walimu wa shule nyingi za chekechea na msingi zinazoendeshwa kwa mchepuo wa wa kiingereza ni wakenya na waganda. Na wengi wao hata hawana taaluma ya ualimu, ila wanaweza kuongea kingereza kilichonyooka na cha kujiamini hata kama wanakosea. Sasa mchukue mhitimu wa chuo wa Tanzania mwambie aongee kingereza mfululizo kwa nusu saa kama hatakuwa bubu. Asilimia kubwa hawawezi hivyo, sasa mtu anayeteka kuwafundisha watoto kiingereza unataka akuajiri wewe kwa sababu tu ni mzawa na wakati huwezi kuongea kiingereza?

Hata tukija kwenye kazi ambazo hazihitaji elimu, bado watanzania sio watu wa kujituma na kuweka juhudi. Ukienda kwenye hoteli kubwa ukikuta wahudumu wa tanzania na wa nchi nyingine utaiona tofauti kabisa. Tunahitaji kuamka watanzania na tuanze kuweka juhudi na tujenge sifa zitakazotuwezesha kupewa upendeleo.

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

2. Dunia inakuwa kijiji, ondoka kwenye zama za mawe.

Ni jambo la kushangaza kama utafurahia kuvaa nguo iliyotengenezwa china, simu iliyotengenezwa china, mswaki uliotengenezwa kenya, chakula kilichoandaliwa ulaya na mengine mengi halafu ukahubiri uafrika kwanza, Utanzania kwanza. Haya mambo yanakufa, mawasiliano yamerahisisha sana biashara na muingiliano wa watu wa nchi mbalimbali. Hatuwezi kutumia nguvu kupinga hili, ila tunatakiwa kujiandaa na kuwa vizuri ili tuweze kupambana.

Kila siku Tanzania tunalaumiwa kukwamisha muungano wa Afrika Mashariki kwa sababu tunasema wananchi hawajawa tayari bado. Sasa sijui tutakuwa tayari lini. Na sisi wenyewe tunajitamba kwamba majirani wanatuonea wivu ndio maana wanakazana tuungane. Sawa, tunawakatalia wakenya na warwanda, huku wachina wakijazana kwenye nchi. Tunahitaji kuona kwamba dunia inakwenda haraka sana, hatuwezi kujifungia hapa tukifanya mambo yetu kwenye zama za mawe na kufikiri tutaweza kwenda na kasi ya dunia. Tutaachwa nyuma tu.

3. Tujue chanzo halisi cha matatizo yetu.

Kwa kutojua chanzo halisi cha matatizo yetu, umasikini wetu, utafika wakati tutaona kila tajiri ni adui yetu. Tutaanza kuwapiga matajiri na wakiisha tutageukiana wenyewe. Tatizo sio mchina aliyekuja hapa kufanya biashara, tatizo sio mkenya anayepata kazi wakati wewe hupati, tatizo linaanzia kwako.

SOMA; Katika Kula Ujana Usifanye Mambo Haya Matano, Utajutia Maisha Yako Yote.

4. Tusitegemee serikali ndio itatutoa hapa tulipo.

Ndio nakubali serikali ina nafasi yake ya kuweka sera bora kwenye nchi ambazo zitawawezesha wanachi kunufaika na rasilimali zinazowazunguka. Ila linabaki kuwa jukumu lako kuchangamkia fursa za kuweza kutumi rasilimali hizo. Katika utawala wa Mwl J K Nyerere waliona hawawezi kuyachimba madini kwa sababu hatukuwa na wataalamu wa kutosha. Ikapita miaka zaidi ya 30 na baadae ikaja sera ya uwekezaji. Migodi ikabinafsishwa kwa wageni, bado hatukuwa na wataalamu wa kutosha na hata leo hii miaka 54 baada ya uhuru bado hatuna wataalamu wa kutosha hasa kwenye sekta hii mpya ya gesi. Ndio unaweza kuilaumu serikali sana, lakini mwisho wa siku swali linarudi kwako, ni jitihada gani ambazo umefanya za kukuwezesha na wewe ukanufaika na rasilimali hizi. Ardhi sasa hivi inaonekana ipo na ya kutosha tu, hakuna anayeweka juhudi kubwa za kuitumia, kuna wajanja wameanza kuinunua kwa kasi, hakuna anayeona. Baada ya muda ardhi nyingi itakuwa mikononi mwa wachache na masikini watakuwa hawana hata kasehemu ka kulima mazao ya chakula, hapa ndio matatizo yatakapoanzia.

Naomba niishie hapa kwa leo, lakini tukubaliane ya kwamba sisi watanzania tunayo kazi kubwa ya kufanya ili tusijekuingia kwenye machafuko yatakayosababiswa na wachache kuwa na hali nzuri huku wengi wakiteseka. Sisi wananchi ndio tuna nguvu hiyo, tuhamasishane, tuelimishane na tuweke serikali ambayo itatuwezesha sisi kwa kutumia juhudi zetu kuwa sehemu ya neema ya nchi hii. Na sio kutegemea kupendelewa kwa sababu tu sisi ni wazawa.

Nakutakia kila la kheri mwananchi mwenzangu.

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Thursday, January 1, 2015

Salamu Za Mwaka Mpya Kutoka Kwa Rais Wa Tanzania Mwaka 2040.

Napenda kuchukua nafasi hii ya kipekee kuwatakia watanzania wenzangu wote kheri na hongera ya kuuona mwaka 2015. Sio watu wote walioanza mwaka 2014 wamepata nafasi ya kuuona mwaka 2015, hivyo ni jambo la kushukuru kwa nafasi hii ya kipekee.

Mwaka 2014 huenda ulikuwa mwaka uliokuwezesha kufanikisha mengi na pia kushindwa mengi. Kikubwa cha kuchukua 2014 na kukileta mwaka 2015 na yale uliyojifunza. Katika kila jambo ulilofanikiwa kuna vitu umejifunza na katika kila jambo uliloshindwa kuna vitu vingi umejifunza. Tumia yote uliyojifunza ili mwaka 2015 uwe bora zaidi kwako.

Kama mwaka 2014 kuna vitu ulipanga kufanikisha ukashindwa, hii ina maana kwamba kuna vitu unafanya kwa makosa au kuna vitu hufanyi kabisa. Hivyo kuendelea hivyo hivyo kwa mwaka 2015 utapata majibu yale yale uliyopata mwaka 2014. Kumbuka ujinga ni kufanya jambo lile lile kwa njia ile ile na kutegemea majibu tofauti. Haiwezekani na utazidi kupoteza muda wako.

Mwaka huu 2015 ni mwaka ambao utakuwa na matukio mengi na makubwa kitaifa. Matukio haya mengi yatakuwa chachu muhimu katika maendeleo ya nchi yetu. Mambo mawili makubwa kabisa yatakuwa;

1. Kupigia kura katiba pendekezwa. Sote tunajua katiba ilivyo muhimu kwenye taifa lolote, hivyo tukio la kupigia kura katiba iliyopendekezwa ni tukio muhimu sana.

2. Uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani. Mwaka huu tutapata nafasi ya kuchagua viongozi watakaofanya maamuzi kwa niaba yetu kwa miaka mitano ijayo. Hivyo ni jambo linalohitaji umakini wetu ili tusijekupata viongozi ambao watafanya taifa likose uelekeo.

Matukio haya mawili na mengine yatakayotokea mwaka huu 2015 yameshika hisia za wananchi wengi. Wananchi wengi tunaamini mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yetu yatatokea baada ya kupata katiba mpya na kufanya uchaguzi mkuu. Natoa tahadhari kwamba tusitegemee sana hili, mabadiliko ya kweli yanaanzia ndani yako wewe mwananchi. Kila mwananchi anatakiwa kubadilika ndio taifa liweze kubadilika. Kila mwananchi anatakiwa kupata maendeleo ndio taifa lipate maendeleo. Na kwa bahati mbaya sana sehemu kubwa ya mabadiliko ya nchi haitokani na kile serikali inachofanya, bali kile ambacho kila mwananchi anafanya.

Kitu kingine kikubwa ninachopenda kukigusia kwenye salamu hizi za mwaka mpya ni matatizo mawili makubwa yanayoturudisha nyuma kama taifa. Matatizo haya yamekuwa ndio chanzo cha uzembe na ufisadi mkubwa unaoendelea kwenye nchi hii kwa sasa. Matatizo hayo ni;

1. Kutokufanya kazi kwa bidii na maarifa. Najua watanzania tunachukia sana pale tunapoambiwa sisi ni wavivu, ila hata tukichukia huo ndio ukweli wenyewe. Sehemu kubwa ya wananchi ni wavivu au hawafanya kazi kwa viwango ambavyo wanategemewa kufanya. Kila mtu anatafuta njia rahisi ya kupata fedha. Kila mtu anataka apate kitu pasi na kutoa kitu. Hatimaye hii imetuletea wizi na ufisadi mkubwa kwenye taifa. Najua nikisema ufisadi utakimbilia kwenye ESCROW na EPA, lakini je vipi kuhusu daktari anayetaka rushwa ili amhudumie mgonjwa?

Vipi kuhusu afisa wa kodi TRA anayetaka rushwa ili kumsaidia mtu asilipe kodi stahiki?

Vipi kuhusu mwenyekiti wa serikali ya mtaa anayetaka shilingi elfu mbili ndio akupe barua ya utambulisho?

Vipi kuhusu muuza maziwa anayeweka maji kwenye maziwa ili apate zaidi?

Vipi kuhusu kondakta anayepandisha nauli kwa sababu tu kuna watu wengi wanaotaka kusafiri na usafiri ni wa shida?

Vipi kuhusu mwalimu aliyepangiwa kituo cha kazi ila haonekani kazini?

Vipi kuhusu askari wa usalama barabarani anayetaka rushwa kuruhusu gari ambalo halina sifa za kuwepo barabarani kuendelea na safari? Na baadae lisababishe ajali?

Tukiangalia matukio yote haya tunaona ni jinsi gani sehemu kubwa ya taifa tumemezwa na vitendo vya wizi na ufisadi. Tunapiga kelele kukemea ufisadi mkubwa lakini sisi sisi ndio wa kwanza kufurahia kutoa rushwa ili tupate huduma tunazozitaka kwa haraka.

2. Tatizo la pili ni uadilifu, hili ndio linatumaliza kama taifa na ndio linazaa tatizo na kwanza la kutokufanya kazi kwa bidii na maarifa na hatimaye kujiingiza kwenye wizi na ufisadi.

Ni lazima sisi kama wananchi tuanze kujimulika wenyewe, tuone je matendo tunayofanya kila siku kama yangefanywa kuwa ndio sheria ya nchi nzima nchi yetu ingefika wapi?

Tunakuwa wepesi kuwalaumu viongozi kwa tabia zao mbaya lakini tunasahau viongozi hawa wametoka katikati yetu sisi na hivyo wanapeleka tabia walizokuwa nazo kwenye ngazi za juu zaidi.

Kwa hayo machache nikutakia mwaka mzuri na wenye mafanikio makubwa. Nakusihi sana mwaka huu simamia nguzo hizi tatu muhimu

1. Kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

2. Kuwa mwaminifu, tekeleza kile unachoahidi.

3. Kuwa muadilifu, usimfanyie mwingine kile usichopenda kufanyiwa.

Mwaka huu 2015 AMKA CONSULTANTS imejipanga vizuri ili kufanya kazi na wewe na uweze kuboresha maisha yako na kufikia mafanikio makubwa.

Kila siku tembelea AMKA MTANZANIA ili kujifunza na kuhamasika na uweze kuboresha maisha yako.

Tembelea na ujiunge na KISIMA CHA MAARIFA ambapo utakutana na jumuiya ya watu ambao wamechoka kuwa wa kawaida na wanataka kufanya na kuwa zaidi ya walivyo sasa.

Pia tembelea blog hii MAKIRITA AMANI ambapo utakuwa unapata chakula cha ubongo, mambo ambayo yatakufanya ufikiri zaidi na kukuhamasisha kuchukua hatua kwenye maisha yako.

Pata picha hii, leo umekabidhiwa kitabu kitupu kabisa chenye kurasa 365 na unaamua uandike nini kwenye kila ukurasa, je ukurasa wa leo umeandika nini? Na wa kesho je?

Mwaka 2015 ukawe mwaka wa mafanikio makubwa kwako.

TUPO PAMOJA.

Makirita Amani,

Rais wa Tanzania mwaka 2040.

Sunday, December 14, 2014

Nenda Kapige Kura, Au Usipige Na Fanya Hivi…

Leo ni siku ya kupiga kura kuwachagua viongozi wa serikali za mitaa, najua unajua hili, ila imebidi niliandike tena ili tupate pa kuanzia. Kama ulikuwa hujui leo ndio siku ya uchaguzi basi tuna tatizo kubwa zaidi.

Kwa takwimu mbalimbali za chaguzi zilizopita tunaona idadi kubwa ya watu waliojiandikisha hawapigi kura. Na laiti kama watu hao wangepiga kura mabadiliko yangekuwa makubwa sana.

kupiga kura

Sasa sitaki kuandika mengi nikucheleweshe kupiga kura, ninachokuambia leo ni;

Nenda kapige kura, au usiende kupiga na usilalamike chochote.

Maana watanzania tumekuwa mafundi wa kulalamika ila hatua hatuchukui. Kama hatua kubwa za kuwawajibisha watu hatuwezi kuchukua, basi tuchukue hatua ya kupiga kura na kuchagua viongozi ambao ni bora.

Wahi kapige kura yako asubuhi hii, na mhamasishe kila unayekutana naye nae akapige kura.

Hapa ndipo mabadiliko ya nchi yetu yanapoanzia.

Sunday, November 2, 2014

Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Ni Muhimu Sana. Tuzingatie Mambo Haya Matano.

Tarehe 14/12/2014 itakuwa siku muhimu sana katika miaka mitano ijayo. Siku hii itakuwa ni siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa. Watu wengi sana hawaupi uchaguzi huu nafasi kubwa na wameelekeza macho na masikio yao kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Hili ni kosa kubwa sana ambalo tunafanya watanzania wenzangu. Uchaguzi wa serikali za mitaa ni muhimu kama ilivyo uchaguzi mkuu. Ni kupitia serikali za mitaa ambapo tunakuwa na demokrasia ya moja kwamoja. Yaani kama kuna jambo lolote la kufanya maamuzi kwenye mtaa au kijiji basi wananchi wote watafanya maamuzi kwenye vikao na mikutano mbalimbali.

Pia serikali hizi za mitaa zina mamlaka ya kutunga sheria ndogo ndogo ambazo zinaweza kuwa na athari chanya au hasi kwetu sisi wananchi.

Serikali za vijiji zina mamlaka makubwa sana kwenye ardhi na hivyo zinaweza kufanya maamuzi ya kuuza ardhi kwa watu mbalimbali. Hivyo unapokuwa na serikali ya kijiji ambayo sio imara mnaweza kujikuta mnapoteza ardhi yenu.

Mwisho kabisa naamini mabadiliko na maendeleo ya nchi hii yanaweza kuanzia kwenye ngazi ya mitaa, vitongoji au vijiji. Hii ni kwa sababu matatizo yoyote tunayokumbana nayo kama taifa yanaanzia katika ngazi ya familia na hatimaye mitaa. Kwa mfano wahalifu wote wanaishi kwenye mitaa yetu, wauzaji wa madawa ya kulevya na hata watumiaji wanakaa kwenye mitaa yetu. Hivyo tukiweza kuwa na serikali zamitaa ambazo zipo imara tunaweza kujenga misingi mizuri kama taifa.

Baada ya kuona umuhimu huo mkubwa wa serikali za mitaa sasa naomba nikushirikishe mambo matano muhimu ya kuzingatia kwenye uchaguzi huu wa serikali za mitaa.

1. Hakikisha unapiga kura na hamasisha wengine nao wapige kura.

Ule utamaduni wetu watanzania wa kutokupiga kura halafu tunakuwa wa kwanza kulalamika kwamba viongozi ni wabovu sio utaratibu mzuri. Hakikisha unapiga kura siku hiyo ya uchaguzi na pia washawishi ndugu jamaa na marafiki zako nao wapige kura siku hiyo. Kura yako moja ina thamani kubwa sana, usiidharau.

uchaguzi

2. Chagua kiongozi mwenye maono na mwenye historia nzuri.

Kwanza kabisa mtu ambaye mtamchagua awe mtu ambaye mnamjua vizuri. Awe ni mtu ambaye amekaa kwenye mtaa huo na mna historia yake nzuri ya namna ambavyo amekuwa akihamasisha mambo mbalimbali kwenye mtaa au kijiji chenu. Awe ni mtu mwenye maono na anayefikiria na kukubali mabadiliko. Kiongozi wa aina hii ataweza kushirikiana nanyi kuleta maendeleo kwenye eneo lenu.

Kujua zaidi kuhusu tabia za viongozi bonyeza maandishi haya.

3. Mtu yeyote atakayotoa rushwa usifikirie mara mbili, usimpigie kura na hamasisha wengine wasimpigie kura.

Uongozi wa serikali za mitaa ni uongozi ambao hauna manufaa makubwa kifedha zaidi ya posho ndogo ndogo. Sasa mtu ambaye anatoa rushwa lili kupata nafasi hiyo, jiulize ananufaikaje? Kwa vyovyote vile atahakikisha akipata nafasi analipa fedha yake aliyowekeza kwa kutoa rushwa hivyo atawaingiza kwenye matatizo.

4. Chagua mtu, usichague chama.

Kwa siasa zetu za Tanzania bado haturuhusu mgombea binafsi hivyo unalazimika kuchagua mgombea anayeletwa na chama fulani. Chama kinaweza kuwa na sera nzuri sana ila kama kitakuwa na mgombea ambaye hana uwezo mzuri wa uongozi sera hizo ni kazi bure. Hivyo hudhuria mikutano ya kampeni, wafatilie vizuri wagombea wote na mchague mtu ambaye unaona anaweza kuleta mabadiliko kwenye mtaa au kijiji chenu. Hata kama wewe ni mkereketwa wa chama fulani ila ukaona mgombea wa chama kingine ana sifa zaidi ya mgombea wa chama chako, mpigie kura. Mwisho wa siku maendeleo yatakuwa ni kwa mtaa wenu na sio chama chenu.

5. Tuoneshe ushirikiano na kuwawajibisha viongozi tuliowachagua.

Baada ya uchaguzi na viongozi kupatikana ni vyema kuweka tofauti za kisiasa pembeni na kupeana ushirikiano ili kiongozi mliyemchagua aweze kutekeleza majukumu yake. Kwa kuonesha ushirikiano mzuri italeta mafanikio makubwa kwa mtaa au kijiji chenu.

Pia pale ambapo kiongozi mliyemchagua anakwenda kinyume na ahadi zake ni vizuri kumwajibisha. Kwenye serikali za mitaa tupo karibu sana na viongozi wetu na hivyo ni rahisi kuhoji mambo mbalimbali ambayo mnaona hayaendi sawa.

Nichukue nafasi hii kuwatakia watanzania wote uchaguzi mwema na twende tukafanye maamuzi sahihi kwa mitaa na vijiji vyetu kwa miaka mitano ijayo.

Tanzania ni yetu sote, tushirikiane kuijenga.

Sunday, September 14, 2014

Hili Ndilo Kosa Kubwa Tunalokwenda Kufanya Watanzania 2015.

Mwaka 2015 ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu sana na watanzania wengi umekaribia kabisa kufika. Huu ni mwaka ambao uchaguzi mkuu wa nchi yetu utakwenda kufanyika na hivyo wananchi kupata nafasi ya kuchagua diwani, mbunge na raisi ambaye tunaona anatufaa.

Mwaka 2015 umekuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu kwa sababu wananchi wengi tumeaminishwa na kuamini kwamba baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 na chama tawala kuondoka madarakani maisha yetu yatakuwa mazuri sana. Ni imani nzuri sana ambayo tumekuwa nayo hasa ukizingatia hali ya nchi kiuchumi ipo chini sana ukilinganisha na rasilimali tulizonazo.

Pamoja na kuwa na imani hii nzuri, kuna kosa kubwa sana ambalo watanzania tutakwenda kulifanya mwaka huo 2015. Kosa hili litatugharimu tena miaka mingine mitano au hata zaidi ya hapo kama hatutaendelea kujifunza.

Kosa hili kubwa ni kutokuwa na vigezo vya kiongozi tunayemtaka sisi wananchi. Na kwa kukosa vigezo hivi tutarudia makosa ambayo tuliyafanya nyuma kwa kuchagua watu kutokana na umaarufu wao. Kutokana na kuangalia umaarufu tumechagua viongozi wengi ambao wameishia kutuangusha na kushindwa kutimiza ahadi zao wenyewe.

Ni lazima sisi kama wananchi bila hata ya kuambiwa na wanasiasa, tuwe na vigezo vya aina ya kiongozi tunayemtaka. Na hii ni kuanzia udiwani, ubunge na uraisi. Lazima sisi tuwe na vigezo vyetu kisha wale watakaojitokeza kuomba nafasi hizo tuwachuje kwa kutumia vigezo vyetu.

SIASA

Ilivyo sasa ni kwamba wananchi hatuna vigezo vyetu, ila tunatumia vigezo vya wagombea watakavyotuletea na hivyo tunaweza kulinganisha baina ya mgombea na mgombea na kuamua kumchagua mmoja wao. Hapa ina maana kama wagombea wote ni wabovu tutamchagua ambaye ni ahueni. Na hapa ni kwa sehemu ndogo, shemu kubwa itatumia kigezo cha umaarufu.

Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu sasa hivi kuitisha mikutano ya waandishi kila kukicha kutangaza nia zao za kugombea uongozi. Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu kuzunguka huku na kule kutoa misaada ili waonekane wanajali sana.

Sasa watanzania tuache kufanya kosa hili ambalo litaendelea kugharimu maisha yetu.

Katika makala zijazo tutazungumzia ni vigezo gani tunaweza kuvitumia katika kila nafasi ya uongozi ili tuweze kupata viongozi bora.

Tanzania ni nchi yetu sote, unapopata ujumbe huu wajulishe na wenzako wote unaowafahamu ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.

Usisahau kuweka email yako ili upate makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

TUKO PAMOJA.

Hili Ndilo Kosa Kubwa Tunalokwenda Kufanya Watanzania 2015.

Mwaka 2015 ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu sana na watanzania wengi umekaribia kabisa kufika. Huu ni mwaka ambao uchaguzi mkuu wa nchi yetu utakwenda kufanyika na hivyo wananchi kupata nafasi ya kuchagua diwani, mbunge na raisi ambaye tunaona anatufaa.

Mwaka 2015 umekuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu kwa sababu wananchi wengi tumeaminishwa na kuamini kwamba baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 na chama tawala kuondoka madarakani maisha yetu yatakuwa mazuri sana. Ni imani nzuri sana ambayo tumekuwa nayo hasa ukizingatia hali ya nchi kiuchumi ipo chini sana ukilinganisha na rasilimali tulizonazo.

Pamoja na kuwa na imani hii nzuri, kuna kosa kubwa sana ambalo watanzania tutakwenda kulifanya mwaka huo 2015. Kosa hili litatugharimu tena miaka mingine mitano au hata zaidi ya hapo kama hatutaendelea kujifunza.

Kosa hili kubwa ni kutokuwa na vigezo vya kiongozi tunayemtaka sisi wananchi. Na kwa kukosa vigezo hivi tutarudia makosa ambayo tuliyafanya nyuma kwa kuchagua watu kutokana na umaarufu wao. Kutokana na kuangalia umaarufu tumechagua viongozi wengi ambao wameishia kutuangusha na kushindwa kutimiza ahadi zao wenyewe.

Ni lazima sisi kama wananchi bila hata ya kuambiwa na wanasiasa, tuwe na vigezo vya aina ya kiongozi tunayemtaka. Na hii ni kuanzia udiwani, ubunge na uraisi. Lazima sisi tuwe na vigezo vyetu kisha wale watakaojitokeza kuomba nafasi hizo tuwachuje kwa kutumia vigezo vyetu.

SIASA

Ilivyo sasa ni kwamba wananchi hatuna vigezo vyetu, ila tunatumia vigezo vya wagombea watakavyotuletea na hivyo tunaweza kulinganisha baina ya mgombea na mgombea na kuamua kumchagua mmoja wao. Hapa ina maana kama wagombea wote ni wabovu tutamchagua ambaye ni ahueni. Na hapa ni kwa sehemu ndogo, shemu kubwa itatumia kigezo cha umaarufu.

Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu sasa hivi kuitisha mikutano ya waandishi kila kukicha kutangaza nia zao za kugombea uongozi. Ni kigezo hiki cha umaarufu ambacho kinawafanya watu kuzunguka huku na kule kutoa misaada ili waonekane wanajali sana.

Sasa watanzania tuache kufanya kosa hili ambalo litaendelea kugharimu maisha yetu.

Katika makala zijazo tutazungumzia ni vigezo gani tunaweza kuvitumia katika kila nafasi ya uongozi ili tuweze kupata viongozi bora.

Tanzania ni nchi yetu sote, unapopata ujumbe huu wajulishe na wenzako wote unaowafahamu ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.

Usisahau kuweka email yako ili upate makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

TUKO PAMOJA.

Sunday, September 7, 2014

Je Vijana Wanaoingia Kwenye Siasa Wanaweza Kuwa Wakombozi Wetu?

Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana hapa Tanzania ambao wanaingia kwenye siasa. Na kwanzia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambapo baadhi ya vijana waliogombea ubunge walipata kuchaguliwa kumekuwa na mwamko mkubwa sana wa vijana kuingia kwenye siasa.

Na hata kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 vijana wengi wameonesha nia ya kugombea nafasi mbalimbali za udiwani na ubunge katika maeneo mbalimbali. Na kwa kuwa mpaka sasa hatuna sheria inayoruhusu mgombea binafsi, vijana hawa wote ambao wana nia ya kugombea inawalazimu kupitia vyama vya siasa. Kwa sasa tuna vijana wengi sana ambao wameingia kwenye vyama mbalimbali vya siasa na wengine wamepata nafasi kubwa kwenye vyama hivi.

siasa

Swali kubwa la kujiuliza ni je vijana wengi kuingia kwenye siasa wanaweza kuwa wakombozi wa nchi yetu Tanzania? Natumia neno ukombozi kwa sababu naamini nchi yetu inahitaji ukombozi ili kutoka hapa ilipo. Inahitaji ukombozi kwa sababu tumefika hapa tulipo kutokana na uongozi mbovu na siasa na sera mbovu zilizowekwa na viongozi hawa wabovu. Na ukiangalia viongozi hao umri wao umekwenda sasa na hivyo vijana ndio watakwenda kuchukua nafasi zao siku za mbeleni.

Najiuliza swali hili kwa sababu tumeona baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye siasa hizi wakiishia kutumiwa na baadhi ya watu na hivyo kujikuta wakishindwa kuleta mabadiliko yoyote. Tumeona baadhi ya vijana ambao walikuwa wakilalamikia uongozi mbovu ila wamepewa uongozi kwenye sehemu mbalimbali na kushindwa kuleta mabadiliko yoyote. Na vibaya zaidi wanaishia kuwa sehemu ya kitu walichokuwa wanakipinga.

Sina tatizo na kijana ambaye ameingia kwenye chama chochote cha siasa alichopenda yeye. Iwe ameingia CCM, CHADEMA, CUF au hata CHAUSTA. Kikubwa ambacho wananchi wanataka kuona ni mabadiliko ya kweli katika siasa zetu na hatimaye uongozi wa nchi yetu. Naamini mabadiliko haya yanawezekana kupitia vijana kama watajua ni kitu gani wanakwenda kufanya kwenye siasa hizi na kuepuka kutumika na wale ambao wapo kwenye mifumo hii kwa muda mrefu.

Wewe kama ni kijana ambaye umeingia kwenye siasa jiulize swali hili mara kwa mara na hakikisha unakuwa sehemu ya mabadiliko popote unapokuwepo.

Nakutakia kila la kheri katika harakati za kuleta mabadiliko katika taifa letu Tanzania.

TUKO PAMOJA.

Hakikisha hukosi makala mpya kila inapowekwa kwenye blog hii. Weka email yako hapo juu ili upate makala moja kwa moja kwenye email yako.

Je Vijana Wanaoingia Kwenye Siasa Wanaweza Kuwa Wakombozi Wetu?

Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana hapa Tanzania ambao wanaingia kwenye siasa. Na kwanzia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambapo baadhi ya vijana waliogombea ubunge walipata kuchaguliwa kumekuwa na mwamko mkubwa sana wa vijana kuingia kwenye siasa.

Na hata kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 vijana wengi wameonesha nia ya kugombea nafasi mbalimbali za udiwani na ubunge katika maeneo mbalimbali. Na kwa kuwa mpaka sasa hatuna sheria inayoruhusu mgombea binafsi, vijana hawa wote ambao wana nia ya kugombea inawalazimu kupitia vyama vya siasa. Kwa sasa tuna vijana wengi sana ambao wameingia kwenye vyama mbalimbali vya siasa na wengine wamepata nafasi kubwa kwenye vyama hivi.

siasa

Swali kubwa la kujiuliza ni je vijana wengi kuingia kwenye siasa wanaweza kuwa wakombozi wa nchi yetu Tanzania? Natumia neno ukombozi kwa sababu naamini nchi yetu inahitaji ukombozi ili kutoka hapa ilipo. Inahitaji ukombozi kwa sababu tumefika hapa tulipo kutokana na uongozi mbovu na siasa na sera mbovu zilizowekwa na viongozi hawa wabovu. Na ukiangalia viongozi hao umri wao umekwenda sasa na hivyo vijana ndio watakwenda kuchukua nafasi zao siku za mbeleni.

Najiuliza swali hili kwa sababu tumeona baadhi ya vijana ambao wameingia kwenye siasa hizi wakiishia kutumiwa na baadhi ya watu na hivyo kujikuta wakishindwa kuleta mabadiliko yoyote. Tumeona baadhi ya vijana ambao walikuwa wakilalamikia uongozi mbovu ila wamepewa uongozi kwenye sehemu mbalimbali na kushindwa kuleta mabadiliko yoyote. Na vibaya zaidi wanaishia kuwa sehemu ya kitu walichokuwa wanakipinga.

Sina tatizo na kijana ambaye ameingia kwenye chama chochote cha siasa alichopenda yeye. Iwe ameingia CCM, CHADEMA, CUF au hata CHAUSTA. Kikubwa ambacho wananchi wanataka kuona ni mabadiliko ya kweli katika siasa zetu na hatimaye uongozi wa nchi yetu. Naamini mabadiliko haya yanawezekana kupitia vijana kama watajua ni kitu gani wanakwenda kufanya kwenye siasa hizi na kuepuka kutumika na wale ambao wapo kwenye mifumo hii kwa muda mrefu.

Wewe kama ni kijana ambaye umeingia kwenye siasa jiulize swali hili mara kwa mara na hakikisha unakuwa sehemu ya mabadiliko popote unapokuwepo.

Nakutakia kila la kheri katika harakati za kuleta mabadiliko katika taifa letu Tanzania.

TUKO PAMOJA.

Hakikisha hukosi makala mpya kila inapowekwa kwenye blog hii. Weka email yako hapo juu ili upate makala moja kwa moja kwenye email yako.

Sunday, August 31, 2014

Sababu Mbili Kwa Nini Tanzania Ni Nchi Masikini.

Kwa nini Tanzania ni nchi masikini? Pamoja na rasilimali nyingi tulizonazo, mlima mrefu, mbuga za wanyama, madini na hata ardhi kubwa kwa nini tunaendelea kuwa masikini?
Hili ni swali gumu sana maana hata raisi wa nchi mheshimiwa Jakaya Kikwete alikiri kwamba hajui kwa nini nchi yetu ni masikini. Sasa leo nataka tujadiliane nini kinatufanya tuendelee kuwa kati ya nchi masikini sana duniani licha ya rasilimali nyingi tulizonazo.
Katika moja ya vitabu vyake Mwalimu Nyerere aliwahi kuandika kwamba ili tuendelee tunahitaji vitu vinne. Vitu hivyo ni WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UONGOZI BORA. Katika vitu hivi vinne kuna viwili ambavyo tunavyo vya kutosha na viwili ambavyo tumekosa na ndio maana tunaendelea kuwa masikini.

Vitu viwili tulivyonavyo.

Katika vitu hivi vinne tunavyohitaji ili kuendelea, viwili tayari tunavyo, vitu hivyo ni;
1. Ardhi. Tunayo ardhi kubwa sana ya kutosha. Sehemu kubwa ya ardhi ya tanazania bado haijatumika kabisa. Na sehemu kubwa ya ardhi yetu ina rutuba na hivyo inafaa kwa kilimo cha kila aina. Nenda katika kila mkoa utakuta kuna mazao fulani yanayokubali sana. Hata maeneo ya katikati ya nchi ambayo yana asili ya ukame bado kuna mazai yanakubali vizuri.
Lakini ardhi hii sasa iko hatarini kutoweka kutokana na ukosefu mwingine tutakaouona baadae.
2. Watu. Katika sensa ya mwaka 2012 tanzania ina watu zaidi ya milioni 45. Na wengi katika watu hawa ni vijana. Kwa watu wote hawa tulionao, kama wangeweza kutumiaka vizuri tungeweza kufikia maendeleo makubwa sana.

Vitu viwili ambavyo tumekosa.

1. Siasa safi. Kila nchi duniani inaendeshwa kwa siasa. Tanzania tuliwahi kuwa na siasa ya UJAMAA NA KUJITEGEMEA, ambayo ilikwenda vizuri sana mpaka pale ilipouliwa, tumewahi pia kuwa na SIASA NI KILIMO ambapo kilimo kilipewa kipaumbele kwa sababu ndio sehemu kubwa ya wananchi wanategemea kilimo. Lakini nayo haikudumu muda mrefu. Tuliwahi pia kuwa na SIASA YA UWEKEZAJI NA UBINAFSISHAJI ambapo tulishuhudia mashirika ya umma yakipewa watu binafsi na wengi wao kutoka nje ya nchi. Sasa hivi sina hakika tunaendeshwa na siasa gani.
Tumekosa siasa safi na ndio maana tumeshindwa kutumia rasilimali zetu na hata watu wengi tulionao kuweza kufikia maendeleo kama taifa.
2. Uongozi bora. Hili ndio tatizo kubwa sana na ndio linazaa matatizo mengine yote. Tumekosa uongozi bora ambao unaweza kuwatengeneza na kuwatumia watu tulionao kuweza kufikia mafanikio. Tumekosa uongozi bora ambao utatengeneza siasa safi ambayo itatuwezesha kutumia watu wetu na rasilimali zetu vizuri.
Tunao watu wengi ambao wanashikilia nafasi za uongozi ila wamekosa sifa za uongozi. Watu hawa ndio wanafanya maamuzi mabovu na hivyo kutufanya tuendelee kuwa masikini.
Hii ndio sababu kubwa iliyonifanya niwe naandika kuhusu uongozi kwenye blog hii kila siku ya jumapili. Kama umekosa kusoma makala za uongozi zilizopita, bonyeza maandishi haya ili uweze kuzisoma.

Tufanye nini ili kuondoka kwenye umasikini huu?

Kwa kuwa tumeshajua mambo mawili muhimu tunayokosa ili kufikia maendeleo na kwa kuwa tumeshajua ukosefu wa uongozi bora ndio tatizo kubwa zaidi nashauri sisi wananchi tuchukue hatua ya kujua na kuchagua viongozi bora. Na nashauri hasa vijana tujifunze sana kuhusu uongozi na kisha tugombee nafasi mbalimbali za uongozi ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.
Kukaa tu na kulalamika kila siku hakutakuwa na msaada kwetu binafsi na hata kwa vizazi vijavyo. Kuna chaguzi zinakuja mwaka huu na mwaka ujao, tutumie nafasi hii kujua ni viongozi wapi wanaotufaa na wapi wasiotufaa. Tukiendelea kufanya makosa haya katika uchaguzi wa viongozi tutaendelea kuwa masikini siku zote.
TANZANIA NI NCHI YETU SOTE, TUSHIRIKIANE KUIJENGA.

Sababu Mbili Kwa Nini Tanzania Ni Nchi Masikini.

Kwa nini Tanzania ni nchi masikini? Pamoja na rasilimali nyingi tulizonazo, mlima mrefu, mbuga za wanyama, madini na hata ardhi kubwa kwa nini tunaendelea kuwa masikini?
Hili ni swali gumu sana maana hata raisi wa nchi mheshimiwa Jakaya Kikwete alikiri kwamba hajui kwa nini nchi yetu ni masikini. Sasa leo nataka tujadiliane nini kinatufanya tuendelee kuwa kati ya nchi masikini sana duniani licha ya rasilimali nyingi tulizonazo.
Katika moja ya vitabu vyake Mwalimu Nyerere aliwahi kuandika kwamba ili tuendelee tunahitaji vitu vinne. Vitu hivyo ni WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UONGOZI BORA. Katika vitu hivi vinne kuna viwili ambavyo tunavyo vya kutosha na viwili ambavyo tumekosa na ndio maana tunaendelea kuwa masikini.

Vitu viwili tulivyonavyo.

Katika vitu hivi vinne tunavyohitaji ili kuendelea, viwili tayari tunavyo, vitu hivyo ni;
1. Ardhi. Tunayo ardhi kubwa sana ya kutosha. Sehemu kubwa ya ardhi ya tanazania bado haijatumika kabisa. Na sehemu kubwa ya ardhi yetu ina rutuba na hivyo inafaa kwa kilimo cha kila aina. Nenda katika kila mkoa utakuta kuna mazao fulani yanayokubali sana. Hata maeneo ya katikati ya nchi ambayo yana asili ya ukame bado kuna mazai yanakubali vizuri.
Lakini ardhi hii sasa iko hatarini kutoweka kutokana na ukosefu mwingine tutakaouona baadae.
2. Watu. Katika sensa ya mwaka 2012 tanzania ina watu zaidi ya milioni 45. Na wengi katika watu hawa ni vijana. Kwa watu wote hawa tulionao, kama wangeweza kutumiaka vizuri tungeweza kufikia maendeleo makubwa sana.

Vitu viwili ambavyo tumekosa.

1. Siasa safi. Kila nchi duniani inaendeshwa kwa siasa. Tanzania tuliwahi kuwa na siasa ya UJAMAA NA KUJITEGEMEA, ambayo ilikwenda vizuri sana mpaka pale ilipouliwa, tumewahi pia kuwa na SIASA NI KILIMO ambapo kilimo kilipewa kipaumbele kwa sababu ndio sehemu kubwa ya wananchi wanategemea kilimo. Lakini nayo haikudumu muda mrefu. Tuliwahi pia kuwa na SIASA YA UWEKEZAJI NA UBINAFSISHAJI ambapo tulishuhudia mashirika ya umma yakipewa watu binafsi na wengi wao kutoka nje ya nchi. Sasa hivi sina hakika tunaendeshwa na siasa gani.
Tumekosa siasa safi na ndio maana tumeshindwa kutumia rasilimali zetu na hata watu wengi tulionao kuweza kufikia maendeleo kama taifa.
2. Uongozi bora. Hili ndio tatizo kubwa sana na ndio linazaa matatizo mengine yote. Tumekosa uongozi bora ambao unaweza kuwatengeneza na kuwatumia watu tulionao kuweza kufikia mafanikio. Tumekosa uongozi bora ambao utatengeneza siasa safi ambayo itatuwezesha kutumia watu wetu na rasilimali zetu vizuri.
Tunao watu wengi ambao wanashikilia nafasi za uongozi ila wamekosa sifa za uongozi. Watu hawa ndio wanafanya maamuzi mabovu na hivyo kutufanya tuendelee kuwa masikini.
Hii ndio sababu kubwa iliyonifanya niwe naandika kuhusu uongozi kwenye blog hii kila siku ya jumapili. Kama umekosa kusoma makala za uongozi zilizopita, bonyeza maandishi haya ili uweze kuzisoma.

Tufanye nini ili kuondoka kwenye umasikini huu?

Kwa kuwa tumeshajua mambo mawili muhimu tunayokosa ili kufikia maendeleo na kwa kuwa tumeshajua ukosefu wa uongozi bora ndio tatizo kubwa zaidi nashauri sisi wananchi tuchukue hatua ya kujua na kuchagua viongozi bora. Na nashauri hasa vijana tujifunze sana kuhusu uongozi na kisha tugombee nafasi mbalimbali za uongozi ili tuweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.
Kukaa tu na kulalamika kila siku hakutakuwa na msaada kwetu binafsi na hata kwa vizazi vijavyo. Kuna chaguzi zinakuja mwaka huu na mwaka ujao, tutumie nafasi hii kujua ni viongozi wapi wanaotufaa na wapi wasiotufaa. Tukiendelea kufanya makosa haya katika uchaguzi wa viongozi tutaendelea kuwa masikini siku zote.
TANZANIA NI NCHI YETU SOTE, TUSHIRIKIANE KUIJENGA.

Sunday, February 23, 2014

Lengo Langu Kubwa Kwenye Maisha; Kuwa Rais wa Tanzania.

  Leo nakushirikisha lengo kubwa sana kwenye maisha yangu. Lengo hilo ni kuwa rais wa nchi yangu Tanzania. Kama ilivyo kwenye kuweka lengo lolote kuna hatua muhimu za kufuata ili kuweza kufikia lengo unaloweka.   Katika lengo langu mimi ninachotaka ni kuwa rais wa nchi yangu Tanzania.

  Kwa nini nataka kuwa rais wa tanzania?

Kuna sababu nyingi zinazonisukuma kutaka kuwa rais wa nchi yangu. Hapa nitaeleza sababu chache na kadiri muda unavyokwenda nitazidi kueleza sababu nyingine.

1. Naipenda nchi yangu na ninatamani kuleta mabadiliko makubwa kwenye maisha ya wananchi na taifa kwa ujumla. Naamini nina mchango mkubwa sana kwenye mabadiliko ya nchi yangu na njia nzuri ya kutoa na kutekeleza mchango huo ni kupata nafasi kubwa kwenye uongozi wa nchi hii.

2. Naamini matatizo mengi tuliyonayo Tanzania yanaweza kutatulika kama tukiwa na viongozi ambao wana uzalendo.

3. Naamini viongozi wengi tulionao sasa hivi hawana sifa za uongozi na wengi wapo kwa maslahi binafsi hivyo wanazidi kuwa tatizo kwenye nchi yetu.

4. Naamini maendeleo ya nchi yanatokana na maendeleo ya wananchi ambao wamejengewa uwezo na sio kutokana na misaada ama mikopo.

5. Naamini mifumo mingi ni mibovu na hatuwezi kubadili nchi hii bila kubadili kabisa mifumo hiyo. Kwanza ni mfumo mzima wa uongozi, pili mfumo wa utumishi wa umma, tatu mfumo wa elimu. Mifumo hii hasa wa elimu na uongozi imekuwa kikwazo kikubwa kwetu kupata taifa ambalo linajielewa.

 

Ni lini nategemea kuwa rais wa nchi hii?

Nategemea kuwa rais wa nchi hii ifikapo mwaka 2040. Ni mbali sana lakini nina sababu za msingi za kuweka muda huo mwingi mpaka niwe raisi. Kuanzia leo mwaka 2014 mpaka kufika mwaka 2040 ni miaka 26 kuna mambo mengi sana nahitaji kuyafanya katika miaka hiyo ndio niwe rais wa Tanzania.

 

Kwa nini nimetangaza mapema na kwa nini nakuambia wewe?

1.Nimetangaza mapema na nimeweka wazi ili kupata muda wa kutosha kujiandaa. Najua kazi ya urais sio kazi lele mama, ni kazi inayohitaji busara kubwa na uwezo mkubwa wa kuamua na kutenda. Hivyo kwa miaka 26 ijayo nitajifunza mambo mengi sana ya uongozi ili niwe kiongozi bora na ninayejua ni kitu gani ninafanya.

2. Nataka nijue ni watu gani ninaoweza kufanya nao kazi. Kama rais wa nchi nitahitaji wasaidizi ambao nitawachagua mimi. Nitakapokuwa rais nitatumia vigezo vikali sana kuchagua watu watakaoshika sehemu za uongozi. Sitotumia kujuana au urafiki, nitatumia uwezo wa mtu. Naamini kwenye miaka hii 26 nitakutana na watu wengi na nitaweza kupima uwezo wao hasa kwenye matendo. Kama wewe ni rafiki yangu na unasoma hapa ni vyema ukawa unaonesha uwezo wako kwenye mambo yako binafsi unayofanya. Hata kama tumewahi kulala kitanda kimoja usishangae ukija kukosa nafasi hata ndogo sana wakati nitapokuwa rais.

3. Nahitaji mchango wako ili niweze kuwa kiongozi bora. Nahitaji ushauri wako, na nahitaji kupingwa ninapotoa hoja ambazo haziendani na mahitaji yetu. Naamini haya yote yatanijenga kuwa kiongozi bora.

 

Kwa sasa nitatumia blog hii kama sehemu ya kujifunza uongozi. Nakukaribisha twende pamoja kama na wewe una ndoto ya kuwa kiongozi kwenye maisha yako. Kila siku ya jumapili nitakuwa naweka makala moja inayohusisha UONGOZI, SIASA AU RAIS KIVULI. Pia nitakuwa nashirikisha watu vitabu mbalimbali vya uongozi nitakavyokuwa navisoma.

Karibu tujiandae kulijenga taifa letu.

Nategemea maoni yako hapo chini.