Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, July 16, 2015

UKURASA WA 197; Una Sababu Moja Tu, Nyingine Zote Ni Kuchagua.

Umekuwa ukisikia mara nyingi kwamba kosa sio kutenda kosa, bali kosa ni kurudia kosa. Hii ikiwa na maana kwamba unapofanya jambo kwa mara ya kwanza na ukapata majibu ambayo hukutegemea kupata, tunaweza kukusamehe. Ila tunatarajia kwamba uwe umejifunza kwamba njia uliyotumia mwanzo haileti majibu unaotaka.
Sasa kama wewe utarudia tena kufanya vile vile na ukapata majibu yale yale ambayo hukuyataka ndio tunasema kwamba wewe unafanya makosa. Nafikiri tumeelewana vizuri hapo kwenye kosa, na unajua ni makosa gani ambayo umechagua kuwa unayafanya tena na tena.
Sasa leo nataka nikuambie kitu kingine kizuri ambacho kinaweza kuendana na hiko. Una sababu moja tu, nyingine zote ni kuchagua mwenyewe. Kwa maana nyingine unaweza kuwa na kisingizio mara moja tu, baada ya hapo umeamua mwenyewe na huna sababu au kisingizio chochote.
Kwa mfano; kwa nini kila siku unasema utaanza biashara ila huanzi? Sababu ya kweli, sina mtaji. Swali hilo tena miaka mitano baadae, kwa nini mpaka sasa hujaanza biashara... hapa ukisema tena huna mtaji sio sababu tena, maana yake unajua kabisa kwamba huna mtaji na hufanyi jitihada zozote kutafuta mtaji huo.
Usipende kutafuta sababu(visingizio), ila kama haikwepeki, basi sababu iwe mara moja tu. Kama utaendelea kutuambia sababu ile kila siku sio sababu tena bali umeamua kuishi maisha hayo. Hivyo tafadhali sana, usitupigie tena kelele, tumeshasikia sababu yako na umeshatuambia kwamba umekubali kuishi nayo.
TAMKO LA LEO;
Najua nina nafasi moja tu ya kuwa na sababu au kisingizio. Ila baada ya hapo siwezi tena kutumia kisingizio hiko kwa sababu nitakuwa nimeamua mwenyewe. Kuanzia leo nitakwepa kutoa sababu na kama sababu haikwepeki nitatoa mara moja tu.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment