Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, July 11, 2015

UKURASA WA 192; Tatizo La Kuweka Kipimo Cha Furaha, Na Kwa Nini Hukifikii.

Kuna watu ambao huwa wanaweka furaha kwenye kipimo. Mtu anafikiri nikishapa kitu fulani basi nitakuwa na furaha sana.
Kwa hiyo huwa inaanza hivi;
Uko mtoto mdogo unatamani sana kwenda shule unasema nikianza darasa la kwanza nitafurahi sana. Unaanza na unagundua hakuna kitu cha tofauti sana.
Unaendelea na shule kwa miaka saba, unapokaribia mwisho unasubiri kwa hamu sana ukisema nikimaliza darasa la saba tu, nitakuwa na raha sana. Unamaliza na unaona kumbe kilikuwa kitu cha kawaida sana.
Unaanza sekondari unasoma na kufikiria nikimaliza tu, nitakuwa na raha, unamaliza na maisha ni yale yale.
SOMA; Ndege Wa Angani Hawalimi Ila Wanakula, Kuna Mambo Haya Matano(5) Pia Wanakuzidi Ujanja.
Hivyo hivyo mpaka unaingia chuoni, unafikiria nikimaliza na nikapata kazi, maisha yangu yatakuwa ya furaha sana. Unamaliza na labda unapata kazi na unakuta ni kawaida tu na huenda ukakutana na changamoto nyingi zaidi.
Hivyo pia inakuwa kwenye kila kitu unachofanya kwenye maisha yako, unafikiri ukipata kitu fulani utakuwa na furaha, ila unakifanya na unagundua kuna kingine zaidi cha kufanya.
Ni vigumu sana kupima furaha kwa vipimo hivi hasa pale unaposogeza kipimo kila unapokifikia.
Wakati sahihi kwako kuwa na furaha ni sasa hivi, hapo ulipo na unaposoma hii. Na utakapotoka hapo kila wakati kuwa na furaha. Kama unafikiria utaipataje furaha chukua kalamu na karatasi na andika vitu kumi unavyoshukuru kuwa navyo hapo ulipo. Huenda ni kazi au biashara inayokupatia fedha za kuendesha maisha, huenda ni familia inayokupenda, huenda ni marafiki mnaopendana na kadhalika.
Huwezi kupima furaha na ukaipata, furaha ipo ndani yako, ni wewe kuifikia na kuiishi.
TAMKO LA LEO;
Kuanzia sasa naacha kupima furaha kwa sababu nimegundua kwamba kuweka kipimo kwenye furaha ni sababu namba moja ya kushindwa kuifurahia. Hapa nilipo nina furaha kwa sababu nina vitu hivi vifuatavyo(soma orodha yako ya vitu kumi).
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment