Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, July 10, 2015

UKURASA WA 191; unalipwa kwa sababu unaonekana au kwa sababu unatoa thamani?

Swali muhimu sana hilo kujiuliza kama hujawahi kufanya hivyo. Ngoja nikuulize tena vizuri ili twende sawa,
Je unalipwa mshahara kwa sababu unaonekana kazi au kwa sababu una thamani unayotoa kwenye kazi yako?
Je mteja wa biashara yako ananunua kutoka kwako kwa sababu amekuona na wewe unafanya biashara au kwa sababu kuna thamani anaifuata?
Jipe muda wa kujibu swali hili, maana ndio msingi wako wote wa mafanikio umelala hapo.
Kulipwa kwa kuonekana.
Hapa ni pale unapotegemea malipo kwa sababu tu umeonekana kazini, au kwa sababu tu na wewe unauza. Hivyo kinachotokea ni wewe kujionesha kwamba na wewe upo. Kama ni kazini basi unahakikisha unaonekana una kazi nyingi na upo bize kumbe hakuna thamani kubwa unayotengeneza. Ukiwa mtu wa aina hii inakubidi uonekane una juhudi sana kumbe ukweli sio hivyo.
Kama ni biashara unakazana kutangaza ili uonekane na wewe upo.
Tatizo la kutegemea kipato kwa njia hii ni kwamba huwezi kupata kipato kizuri na huwezi kujiamini.
SOMA; Ukiendelea Na Maisha Haya Watu Watakunyanyasa Sana…
Kulipwa kwa kuongeza thamani.
Hiki ndio wanachofanya watu wote wenye mafanikio. Hawaendi kazini ili waonekane na wao wamekuja, ila wanakwenda pale kuleta mabadiliko. Kuongeza thamani kwenye kile wanachofanya na hivyo kuwanufaisha wengi zaidi.
Kama ni wafanyabiashara wanakazana kutatua matatizo yanayowasumbua wengi. Na kwa kuwa suluhisho lao ni bora watu wanakuwa wanawatafuta wenyewe.
Na kwa upande wa kipato, watu hawa wao wenyewe ndio wanaamua walipwe kiasi gani, wakitaka kuongezwa kipato wanaongeza thamani wanayotoa.
Je umeshajua uko wapi? Kazana kuongeza thamani na sio kukazana kuonekana. Unapokazana kuonekana maana yake unapiga kelele. Unapokazana kuongeza thamani umuhimu wako pia unaongezeka. Na kila mtu atataka kufanya kazi na wewe. Na utaanza kupanga ulipwe kiasi gani.
TAMKO LA LEO;
Najua njia bora ya kutengeneza kipato sio kwa kuonekana bali kwa kuongeza thamani. Kuanzia sasa nitakuwa nakazana kuongeza thamani na sio kuwapigia watu kelele ili wajue kama nipo. Najua nitakapotoa thamani kubwa na kipato changu pia kitaongezeka.
Tukutane kwenye ukurasa wa 192 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment