Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, December 20, 2014

Hawa Ndio Watu Unaoishia Kuwa Nao...

Unaishia kuwa na watu ambao unawavumilia...
Marafiki ulionao ni wale ambao unawavumilia, wenye tabia ambazo unazivumilia na hakuna aliyekulazimisha uwe nao.
Wafanyakazi ulionao ni wale ambao unawavumilia, wenye ufanisi ambao unauvumilia na hakuna aliyekulazimisha kuendelea kuwa nao.
Wateja ulionao ni wale ambao unawavumilia, wenye tabia ambazo unazivumilia na hakuna aliyekulazimisha kuendelea kuwa nao.
Mwajiri uliyenaye ni yule unayemvumilia, mwenye tabia unazozivumilia na anayekupa kipato unachokivumilia, hakuna aliyekulazimisha uendelee kuwa naye...
Yote hii ina maana gani?
Maana kubwa ni kwamba MAISHA NI UCHAGUZI, unachagua nani awe rafiki yako, nani awe mwajiri wako, nani awe mfanyakazi wako na nani awe mteja wako.
Kama kuna ambaye unaona hafai kuwa mmoja kati ya hao, unamfukuza, unaachana nae na kujumuika na yule unayeendana nae.
Maisha yako, uchaguzi wako.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment