Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, December 30, 2014

Matatizo Yote Kwenye Maisha Yako Yanatokana Na Kitu Hiki.

Kila mmoja wetu anapitia matatizo au changamoto mbalimbali kwenye maisha yake. Inawezekana unapitia matatizo ya kuumwa, au mwingine anapitia changamoto ya madeni na pia inawezekana unapitia changamoto ya migogoro kwenye familia.
Sasa matatizo yote haya huwa yanaanza na kitu kimoja.
Kabla sijakuambia kitu hiko naomba nikuoe mfano mmoja mzuri sana.
Ukitaka kumuua chura kwa maji ya moto huwezi kumuua kwa kumweka kwenye maji ya moto. Chura ni mnyama ambaye anavyopata joto kali anakuwa na nguvu ya kuweza kuchukua hatua haraka. Hivyo ukimweka kwenye maji ya moto ataruka haraka sana kuondoka kwenye maji hayo.
Sasa hapa kuna njia rahisi ya kumuua chura kwa maji ya moto. Unachukua maji ya baridi kabisa, tena yenye barafu halafu unamweka chura. Kwenye baridi chura hana nguvu ya kuondoka. Baada ya hapo unaanza kupasha maji yale taratibu, kadiri maji yanapata joto chura anakuwa anafurahia, anaona utamu. Akija kustuka maji yanakaribia kuchemka na mwili mzima umesaishiwa nguvu.
Hivi ndivyo matatizo uliyonayo yalivyoanza;
Hukujikuta siku moja unaumwa tu, bali zilianza dalili ndogo ndogo ukazipuuzia.
Hukujikuta kwenye madeni tu, bali ulianza uzembe mdogo mdogo kwenye fedha na ukapuuzia,
Hukujikuta kwenye mgogoro mkubwa wa kifamilia kwa mara moja tu, bali vilianza vitu vidogo vidogo ukavipuuzia.
Hatimaye mambo yamekuwa mambo na sasa upo katikati ya matatizo.
Kupuuzia dalili ndogo ndogo ambazo zingeweza kushughulikiwa ndio kunakufikisha kwenye matatizo makubwa.
Kama waswahili wanavyosema; usipoziba ufa....

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment