Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, January 16, 2015

Habari Za Kusikitisha; Kila Kitu Kinabadilika…

Leo nilipanda dala dala ambapo nilikaa kiti cha nyuma ya dereva, dereva alikuwa na mazungumzo na mtu mmoja aliyekaa mbele, anaonekana ni kondakta au dereva ila sio wa gari hiyo niliyopanda. Hivyo kwa sehemu yote ya safari walikuwa wakihadithiana ni jinsi gani anzi hizo kazi ya daladala inalipa. Waliongea sana kwamba kabla ya ujio wa madaladala makubwa ya kampuni ya uda hapa dar, walikuwa wakipata fedha nyingi sana. Wakawa wanalalamika vile mabasi ya uda yanavyobeba watu wengi na yanavyoweza kutumia bara bara nyingi kushinda daladala za kawaida

SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.

Kwa muda ambao nilifuatilia maongezi yao, walionekana kukatishwa tamaa sana na mabadiliko haya makubwa yaliyotokea na yanayoendelea kutokea.

Ukweli ni kwamba mabadiliko yanatokea kila sehemu sasa. Hata zile sehemu ambazo watu walifikiri wataendelea kunufaika milele mambo ni magumu sana. Na huu ni mwanzo tu wa mabadiliko, mabadiliko yataendelea kuja na kwa kasi ya ajabu sana.

SOMA; Vitu Vitatu Vinavyoathiri Kipato chako Kwenye Chochote Unachofanya.

Nasema hizi ni habari za kusikitisha kwa sababu watu wengi hawapendi mabadiliko. Watu wanapenda kuendele akufanya kile alichkuwa wanafanya, wapate kile walichokuwa wanapata. Lakini dunia haiendi hivi, dunia inabadilika kila siku.

Na katika mabadiliko haya ya dunia yanatengeneza makundi matatu ya watu.

1. Kuna wale ambao wanabadilika haraka na hivyo kunufaika sana na mabadiliko.

2. Kuna wale ambao hawajui kama mabadiliko yanatokea na hivyo kuburuzwa na mabadiliko', hawa huendelea kuwa na maisha magumu.

3. Kuna wale ambao wanayagomea mabadiliko na hivyo wanaachwa nyuma.

Je wewe unataka kuwa katika kundi lipi?

Maisha ni yako, Chaguo ni lako.

Najikuta nikikusanya hadithi nyingi sana zinazohusiana na mabadiliko kwa sababu sasa hivi naandika kitabu cha jinsi ya kukabiliana na mabadiliko yanayotokea kwa kasi. Kama ungependa kuwa wa kwanza kukipata(katika softcopy) tuma ujumbe huu kwa watu wa tano kwenye email zao halafu nikopy mimi kwenye email hizo, tumia email makirita@kisimachamaarifa.co.tz kama hujui jinsi ya kukopi, wakati unaweka email ya unayemtumia chini yake kuna cc, hapo weka email yangu. Nitakupa zawadi ya kitabu hiki pale kitakapokamilika.

SOMA; Maswali 12 Muhimu Ya Kujiuliza Ili Kuweza Kufikia Mafanikio.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment