Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, January 27, 2015

#HADITHI_FUNZO; Kijana Aliyeiba Shoka..

Mtu mmoja alipoteza shoka lake na akawa anahisi mtoto wa jirani yake ndio amemuibia. Kila alipokuwa anamwangalia kijana yule, jinsi alivyotembea, jinsi alivyoongea alionekana kabisa ndiye mwizi wa shoka lake.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

Siku moja mtu yule akiwa anafanya usafi kwenye banda lake aliliona shoka alilofikiri limeibiwa. Alipomuona kijana yule tena hakuna tabia yake yoyote ambayo ilimuonesha kwamba ni mwizi.

Tunajifunza nini hapa?

Ukishahukumu mtu au kitu, utajitengenezea mazingira ya kukushawishi wewe ukubaliane na hukumu yako. Ni vyema kuangalia jambo katika uhalisia wake badala ya kuongozwa na hisia ambazo mara nyingi sio za kweli.

SOMA; Hizi Ndio Siri 21 Za Mafanikio

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment