Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, January 2, 2015

Kuwa Kawaida Ni Kupoteza Muda Wako Na Siri Moja Ya Mafanikio Mwaka 2015

Ukipanda ndege kutoka sehemu moja kwenda nyingine na ukafika hilo sio jambo la kushangaza, ndio ulichotegemea.
Lakini ukipanda ndege na ukapata huduma nzuri sana, ukapewa vyakula na vinywaji ya bei ghali kama upo kwenye hoteli ya nyota tano utafurahia na huenda utamsimulia kila mtu utayekutana naye.
Hii inamaanisha nini?
Ukifanya kile ambacho unategemewa kufanya hakuna atakayegundua kwa sababu ni kawaida, kwa sababu ndicho walichotegemea.
Ila unapofanya cha ziada zaidi, unapoweka ubunifu zaidi, unapoweka jitihada zaidi hapo ndio watu wanagundua, wanaona tofauti, wanawaambia wengine na ghafla kazi yako au huduma yako inakuwa bora na maarufu sana.
Mara zote fanya kwa ziada, nenda maili ya ziada, utasimama kwa tofauti.
Hii ndio siri ya mafanikio kwenye jambo lolote unalofanya, iwe ni baba/mama, mume/mke, mwanafunzi, mfanyakazi, mfanyabiashara, msanii.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment