Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, January 13, 2015

Una Mdomo Mmoja Na Masikio Mawili Kwa Sababu Hii Kubwa.

Kila mtu ana mdomo mmoja na masikio mawili kwa sababu kuu moja; unatakiwa kusikiliza zaidi ya unavyoongea.
Kwa bahati mbaya sana watu tunapenda sana kuongea badala ya kusikiliza.
Unapokuwa muongeaji sana, unakosa kujifunza kutoka kwa wengine.
Unapokuwa msikilizaji unajifunza mengi sana kutoka kwa wengine.
Na kama una upumbavu mwingi ndani yako(kila mtu ana upumbavu kiasi) kwa kuongea sana utaonesha upumbavu wako wote. Ila ukiwa msikilizaji utaonekana una busara.
Pia ukiwa muongeaji sana utajikuta unaongea na ya wengine na hatimaye unaanza umbea na majungu.
Sikiliza zaidi ya unavyoongea, utajifunza mengi na pia kuficha upumnavu wako.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment