Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, January 27, 2015

Unataka Kuiona Dunia? Vua Miwani…

Unachokiona sasa hivi sio dunia halisi, bali ni dunia unayotaka kuiona wewe.

Hii ni kwa sababu kila mtu ni kama amevaa miwani yake ambayo inamuonesha kile anachotaka kuona.

Umewahi kuvaa miwani ya rangi? Unaonaje kitu unapokiangalia? Je unaonaje kitu kile unapovua miwani?

Hiko ndio kinachotokea kweye maisha yako ya kila siku. Unaona vitu kutokana na mtazamo wako, mawazo yako na hata matamanio yako.

SOMA; Njia Kumu(10) Za Kupata Utajiri Na Mafanikio.

Hali yoyote inayotokea, jinsi unavyoichukulia na jinsi utakavyokwenda nayo itategemea wewe unaionaje dunia .

Kama unataka kuiona dunia ya uhalisia, vua miwani, ondoa matarajio yote, ondoa hisia zinazoegemea upande mmoja na iangalie dunia kama vile ilivyo.

Utajifunza mengi na utaona fursa nyingi ambazo kwa sasa huzioni.

SOMA; Maswali 12 Muhimu Ya Kujiuliza Ili Kuweza Kufikia Mafanikio.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment