Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, January 31, 2015

UKURASA WA 31; Umetoka Wapi, Upo Wapi Na Unaelekea Wapi?

Ili kufikia mafanikio makubw akwenye maisha yako ni lazima uwe na njia ya kuweza kujipima. Ni lazima uweze kujipima kama kweli upo kwenye njia sahihi ya kukufikisha kwenye mafanikio.

Ni muhimu sana kujua unakotoka, hii itakufanya ujue ni kazi kiasi gani unahitaji kufanya ili kufika unakotaka.

Ni muhimu pia kujua ulipo, hii itakusaidia kuweza kupanga na kutekeleza mipango ya kukutoa hapo ulipo na kukufikiahsa unakotaka.

Ni muhimu sana kujua kule unakokwenda ili malengo na mipango utakayoweka iweze kukufikisha huko.

Pamoja na kujua unakotoka, ulipo na unapokwenda ni lazima uwe na njia ya kujipima. Katika wakati wowote ule ni lazima uweze kujifanyia tathmini kama kweli uko kwenye njia sahihi na itakayokufikisha kwenye malengo yako.

SOMA; Njia KUMI Za Kuboresha Maisha Yako Ya Kibiashara.

Kama leo ni siku ya 31 ambayo ni siku ya mwisho ya mwezi wa kwanza. Tumia siku ya leo kufanya tathmini ya mwezi mzima. Ni vitu gani ambavyo umefanikiwa kuvifanya, ni vitu gani ambavyo umeshindwa kufanya na ni changamoto gani umekutana nazo.

TAMKO LA LEO;

Najua ya kwamba ni muhimu sana kupima kile ninachofanya na kule ninakokwenda. Kitu chochote ambacho hakiwezi kupimwa hakiwezi kufanyika kwa ukamilifu. Kila mara nitakuwa najitathmini ili kujua kama nipo kwenye njia sahihi na nafanya jambo sahihi la kunifikisha kwenye mafanikio. Leo nitafanya tathmini ya siku 30 za mwezi huu wa kwanz ana kuweka au kubadili baadhi ya mipango ambayo haiendi vizuri.

Tukutane kwenye ukurasa wa 32 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Sababu 10 Kwa Nini Hutafikia Malengo Yako 2015.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment