Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, January 24, 2015

UKURASA WA 24; Kila Kitu Kina Gharama…

Mtu mmoja mwenye mafanikio aliwahi kuulizwa ni ipi siri ya mafanikio ambayo unaweza kumshauri mtu yeyote na yeye akafanikiwa?

Mtu yule alijibu ili kuwa na mafanikio kwenye maisha, bila ya kujali unaanzia wapi unahitaji vitu viwili;

1. Kujua ni nini unataka.

2. Kujua gharama unayotakiw akulipa na kuwa tayari kuilipa.

SOMA; Mambo Kumi Muhimu Kuhusu Maisha

Kama umekuwa ukifuatilia kurasa hizi tokea siku ya kwanza, tayari unajua ni nini unataka kwenye maisha yako. Najua mpaka sasa una malengo yako na hivyo unayafanyia kazi. Kama mpaka sasa hujui ni nini unataka kwenye maisha yako au hujaweka malengo yoyote nakushauri uachie kusoma hapa na ufanye mambo mengine yatakayoendana na maisha magumu utakayoendelea kuwa nayo.

Kitu cha pili muhimu ili uweze kufikia malengo yako na mafanikio ni lazima ujue gharama ya mafanikio unayotaka. Na ukishaijua uwe tayari kuilipa. Gharama inaweza kuwa muda, nguvu, kusema hapana kwa mambo mengine na kadhalika.

Wewe jua gharama unayotakiwa kulipa na anza kuilipa, usichelewe hata sekunde moja.

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba chochote ninachotaka kupata kwenye maisha yangu kuna gharama ninayotakiwa kulipa. Ili kufikia malengo niliyojiwekea niko tayari kulipa gharama zifuatazo(ziorodheshe kulingana na malengo yako na hali uliyonayo). Nitatumia muda wangu vizuri katika kulipa gharama hizi ili niweze kupata kile ninachotaka.

Tukutane kwenye ukurasa wa 25 hapo kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Kitu Hiki Kimoja Kitakufanya Uweze Kujiajiri, Uishie Kuwa Mwajiriwa Au Uishie Jela.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment