Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, January 29, 2015

Nafasi Ya Wewe Kuwa Bora Kila Siku… NA ZAWADI YA TSH 365,000/=

Kama mpaka sasa huna utaratibu wa kujifunza kila siku, tayari upo nyuma sana katika kufikia mafanikio kwenye jambo lolote unalofanya kwenye maisha yako.

Kujifunza kila siku ni hitaji la chini sana la wewe kuweza kufikia mafanikio. Na tunaposema kujifunza kila siku ni kila siku kweli, jumatatu mpaka jumapili na kurudia tena na tena na tena.

Pamoja na umuhimu wa kujifunza kila siku, bado tunaishi kwenye jamii ambayo haitupi nafasi kubwa ya kujifunza. Hii ni kutokana na kuzungukwa na mazingira yenye changamoto nyingi zinazozuia kujifunza kila siku.

Kutokana na changamoto hizi ndio kulikonisukuma kutumia muda wangu kukupatia wewe nafasi ya kujifunza zaidi. Kupitia blog ya MAKIRITA AMANI utaweza kupata nafasi ya kujifunza kila siku, jumatatu mpaka jumapili.

Kila siku utaianza siku yako kwa neno la siku, hili ni neno ambalo litakupa hamasa ya kuweza kuifanya siku yako kuwa bora zaidi. Na pia kila siku kwa mwaka huu 2015 utapata ukurasa mmoja katika safu ya kurasa 365 za mwaka 2015. Kama bado hii haitoshi, unapata nafasi ya kupata kauli za kuhamasisha kutoka kwa viongozi na watu mashuhuri ambao wamefanikiwa sana. Na pia utaweza kupata hadithi za mafunzo ambapo utawez akujifunz akupitia visa mbalimbali.

Pamoja na haya yote utakuwa ukipata makala zenye fikra za kukuchokoza. Hizi ni zile ambazo zinaniingia kwenye fikra zangu kutokana na mawazo mbalimbali yanayonifikia katika kutafuta njia za kufanya maisha yangu na ya wewe msomaji kuwa bora zaidi kila siku.

Kwa kifupi wewe kutembelea blog hii ni sawa na kuwa na mimi pembeni yako, kwani utapata kitu kizuri kutoaka kwangu pale unapokihitaji.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za mbalimbali za kukufundisha na kukuhamasisha kila siku bonyeza hapa na uweke email. Kila siku kwenye email yako utapata mambo haya moja kw amoja.

Siku yako itakuwa bora sana kwa kuwa karibu na blog hii nzuri kwako.

Kama ningekuwa natoza wasomaji fedha kulingana na elimu ninayoitoa hapa, kila msomaji angetakiw akulipa tsh elfu moja kila siku. Hivyo kwa mwaka ungetakiw akulipa tsh 365,000/= ili kupata elimu hii muhimu sana kwako. Lakini sijataka wewe uingie gharama yoyote, gharama yako ni wewe kufungua blog, kusoma makala na kufanyia kazi yale unayojifunza.

Ombi moja muhimu sana kwako ni wewe kuwaalika watu wengi zaidi kusoma blog hii. Haina gharama yoyote na wala haitakuja kuw ana gharama yoyote. Tafadhali tuma makala hii kwenye email za watu watano, itume kama ilivyo halafu nikopy kwenye email hiyo utakayotuma, tumia email makirita@kisimachamaarifa.co.tz kama hujui jinsi ya kukopi, wakati unaweka email ya unayemtumia chini yake kuna cc, hapo weka email yangu. Na mimi nitakupa zawadi nzuri sana ya kitabu cha mabadiliko ambacho bado nakiandika.

Nakutakia kila la kheri katika safari hii ya kuboresha maisha yako.

TUPO PAMOJA SANA.

 

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment