Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, January 22, 2015

Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Nelson Mandela.

Nelson Mandela alikuwa mpingaji wa sera za kibaguzi nchini Afrika ya kusini. Pia alikuwa raisi wa Afrika kusini kati ya mwaka 1994 mpaka mwaka 1999. Alifungwa jela miaka 27 kutokana na harakati zake ila hakukata tamaa, alipotoka jela aliendelea na harakati na hatimaye kuweza kuwa raisi wa taifa ambalo halina ubaguzi.

mandela

Leo tutajifunza kauli kumi kutoka kwake ambazo zitatuhamasisha kuboresha maisha yetu na ya jamii inayotuzunguka.

1. To deny people their human rights is to challenge their very humanity.

Kuwanyima watu haki zao ni kutoa changamoto kwa ubinadamu wao.

2. It always seems impossible until its done.

3. Money won't create success, the freedom to make it will.
Fedha haitatengeneza mafanikio, uhuru wa kutengeneza fedha ndio utakaoleta mafanikio.

SOMA; Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Martin Luther King

4. If you want to make peace with your enemy, you have to work with your enemy. Then he becomes your partner.
Kama unataka kuleta amani na adui yako, unahitaji kufanya naye kazi na hapo mnakuwa washirika.

5. There is no passion to be found playing small - in settling for a life that is less than the one you are capable of living.
Hakuna hamasa kwenye kufanya vitu vidogo, kwa kukubali maisha ya chini kuliko ambayo una uwezo wa kuyaishi.

6. We must use time wisely and forever realize that the time is always ripe to do right.

Ni lazima tutumie muda kwa akili na tuelewe kwamba mara zote ni muda sahihi kufanya jambo sahihi.

SOMA; Lengo Langu Kubwa Kwenye Maisha; Kuwa Rais wa Tanzania.

7. Even if you have a terminal disease, you don't have to sit down and mope. Enjoy life and challenge the illness that you have.

Hata kama una ugonjwa ambao hauwezi kupona, hutakiwi kukaa chini na kukata tamaa. Furahia maisha na toa changamoto kwa ugonjwa ulionao.

8. No country can really develop unless its citizens are educated.
Hakuna nchi inayoweza kuendelea kweli mpaka wananchi wake wawe wameelimika.

9. When the water starts boiling it is foolish to turn off the heat.
Wakati maji yanaanza kuchemka ni upumbavu kuzima moto.

10. Only free men can negotiate. A prisoner cannot enter into contracts.

Ni mtu huru pekee anayeweza kujadili. Mfungwa hawezi kuingia mkataba.

Pitia kauli hizi kumi na zitakuhamasisha kufanya zaidi ili uweze kufikia mafanikio.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment