Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, January 27, 2015

Unataka Kujifunza Kitu Chochote Unachoona Ni Kigumu? Fanya Hivi...

Njia bora kabisa ya kujifunza ni kufanya, kutenda.
Utasoma vitabu vyote, utafundishwa na walimu waliobobea ila kama hutatendea kazi yale uliyojifunza ni kazi bure.
Hakuna mtu aliyewahi kujifunza na akajua kuendesha baiskeli kwa kusoma vitabu tu. Hata baada ya maelekezo ulihitaji kuipanda baiskeli, kuanguka na hata kuumia ndio ukajua kuendesha baiskeli.
Sasa nini kinakuzuia wewe kuchukua hatua sasa? Hujajifunza? Anza kufanya.
Unataka kujifunza biashara, anza kufanya biashara, anza kidogo kidogo.
Unataka kujifunza kuandika makala nzuri anza kuandika, anza maneno matano nenda kumi, ishirini, mia...
Unataka kujifunza kilimo, nenda tafuta shamba, anza kulima.
Unataka kujifunza maisha, anza kuishi, sio kuishi kama kila mtu anavyoishi, bali kuishi kama ambavyo unataka kuishi.
Mwaka huu ni JUST DO IT.
Chochote unachotaka kwenye maisha yako, anza kukifanyia kazi. Hakuna kitakachokushinda.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment