Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, January 26, 2015

UKURASA WA 26; Lazima Kuna Atakayekuwa Zaidi Yako.

Katika jambo lolote unalofanya kwenye maisha, lazima kuna mtu ambaye anafanya zaidi yako.

Kama ni biashara kuna ambaye atakuwa anafanya zaidi yako. Kama ni kazi kuna ambaye atakuwa anafanya zaidi yako.

SOMA; Mambo Matatu Muhimu Ya Kufanya Siku Ya Jumapili Ili Kuwa Na Wiki Yenye Mafanikio

Ukinunua gari utakutana na wengine wenye magari mazuri zaidi yako.

Kitu kibaya sana kwenye maisha ni kujilinganisha na wengine. Ukifanya hivi kila siku utaishia kuumia kwa sababu utaona watu ambao wanacho zaidi ya ulicho nacho.

Wewe ni wa tofauti, wewe ni wa pekee na una uwezo ambao hakuna mtu mwingine anao.

Badala ya kupoteza nguvu nyingi kujilinganisha na wengine, tumia nguvu hizo kujiboresha zaidi. Hakikisha siku ya leo unakuwa bora zaidi ya ulivyokuwa jana.

Hakikisha kazi unayofanya leo ni bora kuliko uliyofanya jana.

Kwa njia hii utaona mabadiliko makubwa kila siku kwenye maisha yako.

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba katika jambo lolote ninalofanya kuna mtu anayefanya zaidi yangu. Najua mimi ni wa pekee na hakuna mtu ninayefanana naye kwa kila kitu. Sitajilinganisha na mtu yeyote. Nitahakikisha nakuwa bora kila siku inayokuja.

Tukutane kwenye ukurasa wa 27 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Hii Hapa Ni Tsh 604,000/= Utakayokabidhiwa Leo Usiku. Utaitumiaje?

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment