Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, January 30, 2015

Je Upo Tayari Kupata Unachotaka? Siri Ni Hii Moja…

Unataka nini kwenye maisha yako?

Maana kama hujui unachotaka tayari umeshakikosa.

Je upo tayari kupata hiko unachotaka?

Ni nini kinakuzuia mpaka sasa hujakipata?

Haya ni maswali muhimu sana ya kujiuliza. Maana kuna kitu ambacho kimekufanya mpaka sasa hujapata unachotaka na kushindwa kujua kitu hiko kitaendelea kukuzuia.

Jua kikwazo ni nini na anza kukishughulikia.

Anza na vikwazo hivi;

Kwa watanzania waliowengi, vikwazo vinafanana na baadhi ya vikwazo hivyo ni;

1. Kutokujiamini.

2. Hofu

3. Kulalamika

4. Kutegemea kuna mtu atakuja kukutoa hapo ulipo.

5. Matumizi mabaya ya hela.

6. Uvivu, kutokuwa na ubunifu. Kuiga

7. Kukosa uvumilivu na kukata tamaa mapema.

8. Kutafuta njia ya mkato

9. Kukosa uaminifu

10. Kupanga malengo na mipango ila kushindwa kuchukua hatua.

Anza kufanyia kazi mambo hayo kumi na utaona ilivyo rahisi kupata chochote unachotaka.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment