Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, February 24, 2015

UKURASA WA 55; Usikubali Kirahisi…

Maisha yako hivi, unaweza kuwa unahitaji kitu fulani na ili kupata kitu hiko inabidi umwombe mtu mwingine. Unapoendakumwomba mtu huyo anakupa jibu rahisi, HAPANA, HAIWEZEKANI.

Wewe unachofanya ni nini? Unakubali, unarudi nyuma na kuwa shahidi mzuri, kwamba ulijaribu sana, lakini haikuwezekana, uliambiwa hapana, uliambiwa haiwezekani.

Hapo ndio unapokosea, unakubali kirahisi, kwamba hupewi, kwamba haiwezekani, kwamba hutaweza.

SOMA; UKURASA WA 07; Uvumilivu Ni Nguzo Muhimu.

Leo nakwambia acha kabisa kukubali kirahisi. Ni marufuku kukubali majibu rahisi rahisi tu. Kwa sababu mtu amekwambia hawezi kufanya unachomwambia afanye haimaanishi hawezi kweli, huenda hujampa sababu za kutosha kwa nini inabidi afanye hiko unachotaka afanye.

Kwa sababu umefungua biashara na wateja hawanunui haimaanishi biashara yako haina wateja, bali unahitaji kuwashawishi zaidi kuwapa huduma bora zaidi ili waridhike na kile wanachotoa na kile wanachopokea pia.

SOMA; UKURASA WA 47; Kuwa Na Subira, Hakuna Unachopoteza.

Vyovyote vile usikubali majibu rahisi, chimba ndani zaidi, komaa na utaona vikwazo vyote vilivyokuwa vinajitokeza vilikuwa vinakupima tu kama una kiu kweli ya kupata unachotaka.

TAMKO LA LEO;

Sitakubali tena kupokea majibu rahisi na kukubaliana nayo kirahisi. Nitaendelea kushinikiza, nitaendelea kuhoji na nitaendelea kuchunguza mpaka nipate sababu inayonizuia kupata ninachotaka. Kwa sababu najua vikwazo ninavyokutana navyo haviwezi kunizuia kamwe.

Tukutane kwenye ukurasa wa 56 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA

SOMA; Je Upo Tayari Kupata Unachotaka? Siri Ni Hii Moja…

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment