Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Showing posts with label WATU MASHUHURI. Show all posts
Showing posts with label WATU MASHUHURI. Show all posts

Thursday, February 5, 2015

Kauli KUMI Za Confucius Zitakazokuhamashisha Kuboresha Maisha Yako.

Confucius alikuwa mwalimu, mwandishi, mwanafalsafa na mwanasiasa wa China. Alikuwa akiandika falsafa zinazohusu maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla.

Leo utajifunza kauli kumi kutoka kwake zitakazokuhamasisha kuchukua hatua na kuboresha maisha yako.

1. Choose a job you love and you will never have to work a day in your life.

Chagua kazi unayoipenda na hutofanya kazi tena kwenye maisha yako.

2. I hear and I forget. I see and I remember. I do and I understand.

Nikisikia nasahau. Nikiona nakumbuka. Nikifanya naelewa.

SOMA; Sheria Kumi Za Familia Za Kuzingatia

3. By three methods we may learn wisdom: first, by reflection which is noblest; second, by imitation, which is the easiest; and third, by experience, which is the bitterest.

Kwa njia tatu unaweza kujifunza hekima; kwanza kwa kutafakari ambayo ni bora; pili kwa kuiga, ambayo ni rahisi; tatu kwa uzoefu ambayo ni chungu.

4. A man who has committed a mistake and doesn't correct it is committing another mistake.

Mtu aliyefanya makosa na kutoyasahihisha anafanya makosa mengine.

5. It is man that makes truth great, not truth that makes man great.

Ni mtu anayeufanya ukweli kuwa mkuu, na sio ukweli unaomfanya mtu kuwa mkuu.

6. The will to win, the desire to succeed, the urge to reach your full potential... these are the keys that will unlock the door to personal excellence.

Utashi wa kushinda, hamu ya kufanikiwa, wito wa kufikia uwezo wako mkubwa… hizi ni funguo zitakazofungua milango ya ubora wako.

7. Real knowledge is to know the extent of one's ignorance.

Maarifa ya kweli ni kujua kiwango cha ujinga wako.

SOMA; NENO LA LEO; Uwekezaji Unaolipa Riba Kubwa Sana

8. You don't love someone for their looks, or their clothes, or for their fancy car, but because they sing a song only you can hear.

Humpendi mtu kwa muonekano wake, au nguo zake, au gari lake bali kwa sababu anaimba wombo ambao ni wewe tu unayeweza kuusikia.

9. Everything has its beauty, but not everyone sees it.

Kila kitu kina uzuri wake, lakini sio kila mtu anauona.

10. In a country well governed, poverty is something to be ashamed of. In a country badly governed, wealth is something to be ashamed of.

Kwenye nchi ambayo ina utawala mzuri, umasikini ni kitu cha aibu. Kwenye nchi ambayo ina uongozi mbovu, utajiri ni kitu cha aibu.

NYONGEZA…

11. To see the right and not to do it is cowardice.

Kuona ukweli na kutoufanya ni woga.

12. Wherever you go, go with all your heart.

Popote unapoenda, nenda na moyo wako wote.

SOMA; Njia TATU Za Kufanya Moto Wa Ujasiriamali Uendelee Kuwaka Kwenye Nafsi Yako…

Tuesday, February 3, 2015

Kauli KUMI Za Marcus Aurelius Zitakazokufanya Uyaone Maisha Kwa Utofauti.

Marcus Aurelius (26 April 121 – 17 March 180 AD)  alikuwa mfalme wa Roma kuanzia mwaka 161 mpaka mwaka 180. Alikuwa mmoja wa wafalme watano wa mwisho wa Roma ambao walikuwa na mafanikio makubwa sana. Alipitia vipindi vigumu kwenye utawala wake lakini aliweza kufanya mambo makubwa. Pia Marcus ni mmoja wa wanafalsafa wakubwa waliowahi kuishi duniani.

SOMA; Matatizo Yote Kwenye Maisha Yako Yanatokana Na Kitu Hiki.

Leo hapa utajifunza kauli kumi kutoka kwa mwanafalsafa huyu ambazo zitakufanya uyaone maisha kwa upande tofauti na kukuwezesha kufanya makubwa.

1. When you arise in the morning, think of what a precious privilege it is to be alive - to breathe, to think, to enjoy, to love.

Unapoamka asubuhi, fikiria jinsi ulivyo upendeleo wa kipekee wa wewe kuwa unaishi, kupumua, kufikiri, kufurahia, kupenda.

2. Very little is needed to make a happy life; it is all within yourself, in your way of thinking.

Unahitaji vitu vichache sana ili kuwa na maisha yenye furaha; vyote viko ndani yako, kwa jinsi unavyofikiri.

SOMA; Mambo Kumi Muhimu Kuhusu Maisha

3. Everything we hear is an opinion, not a fact. Everything we see is a perspective, not the truth.

Chochote unachosikia ni maoni, sio uhalisia. Chochote unachoona ni mtazamo, sio ukweli.

4. Accept the things to which fate binds you, and love the people with whom fate brings you together, but do so with all your heart.

Kubali vitu ambavyo vinakutokea, penda watu ambao unakutana nao, na fanya hivyo kwa moyo wako wote.

5. The happiness of your life depends upon the quality of your thoughts: therefore, guard accordingly, and take care that you entertain no notions unsuitable to virtue and reasonable nature.

Furaha ya maisha yako inategemea ubora wa mawazo yako; hivyo yalinde mawazo yako, na kuwa makini usikubali mawazo ambayo hayatakuletea furaha.

6. Waste no more time arguing about what a good man should be. Be one.

Usipoteze muda wako kubishana mtu bora anatakiwa kuwaje. Kuwa mtu huyo.

SOMA; Kitu Hiki Kimoja Kitakufanya Uweze Kujiajiri, Uishie Kuwa Mwajiriwa Au Uishie Jela.

7. The object of life is not to be on the side of the majority, but to escape finding oneself in the ranks of the insane.

Lengo la maisha sio kuwa upande wa wengi, ila kuepuka kujikuta kati ya wapumbavu.

8. He who lives in harmony with himself lives in harmony with the universe.

Mtu anayeishi kwa kuelewana na nafsi yake, anaishi kwa kuelewana na ulimwengu wote.

9. Never let the future disturb you. You will meet it, if you have to, with the same weapons of reason which today arm you against the present.

Usikubali kesho ikusumbue. Utakutana nayo kama itatokea, na utatumia silaha zilizokuwezesha kuivuka leo.

10. Life is neither good or evil, but only a place for good and evil.

Maisha sio mazuri wala sio mabaya, ila ni sehemu ya mazuri na mabaya.

SOMA; NENO LA LEO; Hapa Ndio Pa Kuanzia, Hasa kwa mwaka 2015…

NYONGEZA;

Kutokana na kauli nyingi nzuri za Marcus kuhusu maisha hapa nimeongeza nyingine mbili muhimu za kuzingatia.

We ought to do good to others as simply as a horse runs, or a bee makes honey, or a vine bears grapes season after season without thinking of the grapes it has borne.

Tunahitaji kufanya mema kwa wengine kama ambavyo farasi anakimbia, au nyuki anavyotengeneza asali, au mzabibu unavtotengeneza zabibu msimu baada ya msimu bila ya kufikiria ni zabibu gani unatoa au zitaliwa na nani.

Do every act of your life as if it were your last.
FANYA KILA UNACHOFANYA KAMA VILE NDIO KITU CHAKO CHA MWISHO KUFANYA.

Kama utaamua kupuuza vyote na kuishi kwa kauli hizo mbili za nyingeza tu, utakuwa na maisha yenye mafanikio makubwa sana.

Nakutakia kila la kheri

SOMA; Adui Yako Anaanzia Hapo Ulipo Na Anaanza hivi.

Friday, January 30, 2015

Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Robert Mugabe.

Robert Mugabe (kuzaliwa 21 February 1924) ni mwanamapinduzi na raisi wa Zimbabwe. Robert Mugabe aliweza kupambana na kuondoa walowezi ambao walikuwa wanashikilia sehemu kubwa ya ardhi ya zimbabwe. Ni kiongozi shujaa sana ambaye ameweza kushindana na vikwazo vya mataifa makubwa.

Leo tutapata kauli kumi kutoka kwake ambazo zitatuhamasisha na kutufanya tuchukue hatua kwenye maisha yetu.

1. There are things one must do for oneself.

Kuna vitu ambavyo mtu anahitaji kufanya kwa ajili yake mwenyewe.

2. We of Africa protest that, in this day and age, we should continue to be treated as lesser human beings than other races.

Sisi waafrika tunakataa kwamba, mpaka sasa tunaendelea kuchukuliwa kama watu wa hali ya chini ukilinganisha na watu wengine.

SOMA; Dalili Kumi Kwamba Tayari Wewe Ni Kiongozi.

3. We don't mind having sanctions banning us from Europe. We are not Europeans.
Hatujali kama ulaya wanatuwekea vikwazo, sisi sio wazungu.

4. Countries such as the U.S. and Britain have taken it upon themselves to decide for us in the developing world, even to interfere in our domestic affairs and to bring about what they call regime change.
Nchi kama marekani na uingereza wamechukua nafasi ya kutuamulia sisi nchi zinazoendelea, wanadiriki hata kuingilia mambo yetu ya ndani kwa kile wanachodai ni mabadiliko.

5. It may be necessary to use methods other than constitutional ones.
Kuna wakati inakuwa muhimu kutumia njia nyingine tofauti na za kikatiba.

6. Our party must continue to strike fear in the heart of the white man, our real enemy!
Chama chetu lazima kiendelee kuingiza hofu kwenye mioyo ya wazungu, ambao ndio maadui zetu.

SOMA; Naomba Ufanye Changamoto Hii Ya Siku Kumi, Utabadili Sana Maisha Yako.

7. The white man is not indigenous to Africa. Africa is for Africans. Zimbabwe is for Zimbabweans.
Watu weupe sio wazawa wa Africa, Africa ni ya waafrika, Zimbabwe ni ya wazimbabwe.

8. The only white man you can trust is a dead white man.

Mtu mweupe pekee unayeweza kumwamini ni yule aliyekufa.

9. We are no longer going to ask for the land, but we are going to take it without negotiating.

Hatutaendelea tena kuomba ardhi, tunakwenda kuichukua bila ya kukubaliana.

10. If the choice were made, one for us to lose our sovereignty and become a member of the Commonwealth or remain with our sovereignty and lose the membership of the Commonwealth, I would say let the Commonwealth go.

Ni maamuzi tumefanya, kama ni kupoteza utaifa wetu ili kuwa wanachama wa jumuia ya madola au kubaki na utaifa wetu na kupoteza uanachama wa jumuia ya madola, tuko tayari kuacha uanachama wa jumuia ya madola.

Tumia kauli hizi kufikiri zaidi na kuhamsika kuchukua hatua ya kuboresha maisha yako na ya wale wanaokuzunguka.

SOMA;  Wajasiriamali Wenye Mafanikio Hufanya Mambo Haya Matano Kila Siku.

Wednesday, January 28, 2015

Kauli Kumi Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Abraham Lincoln

Abraham Lincoln (February 12, 1809 – April 15, 1865) alikuwa raisi wa 15 wa marekani. alianza kipindi chake cha uraisi March 1861 mpaka alipouawa April 1865. Lincoln aliongoza marekani katika kipindi cha vita ambayo ilikuwa changamoto kubwa kwake. Katika vita hii aliweza kuimarisha muungano wa majimbo ya marekani, kutokomeza utumwa na kuimarisha uchumu.

Leo utajifunza kauli kumi kutoka kwake ambazo zitakuhamasisha wewe kuchukua hatua na kuboresha zaidi maisha yako na ya wale ambao wanakuzunguka.

1. In the end, it's not the years in your life that count. It's the life in your years.
Mwishoni sio miaka ya maisha yetu itakayohesabika bali maisha ya miaka yetu ndio itakayohesabika.

SOMA; Viongozi 100 Walioibadili Dunia.

2. Most folks are as happy as they make up their minds to be.
Watu wengi wanafuraha kama walivyozifanya akili zao kuwa hivyo.

3. Nearly all men can stand adversity, but if you want to test a man's character, give him power.
Karibu kila mtu anaweza kuvumilia matatizo, ila kama unataka kupima tabia ya mtu, mpe nguvu(uongozi)

4. Always bear in mind that your own resolution to succeed is more important than any other.
Kila mara kumbuka kwamba uamuzi wako wa kufanikiwa ni muhimu kuliko kitu kingine chochote.

abraham-lincoln-quote-5

SOMA; Watu Watatu(3) Waliofukuzwa Kwenye Kampuni Walizoanzisha Wenyewe.

5. The best thing about the future is that it comes one day at a time.
Uzuri wa baadae ni kwamba inakuja siku baada ya siku.

6. Give me six hours to chop down a tree and I will spend the first four sharpening the axe.
Nipe masaa sita ya kukata mti na nitatumia masaa manne ya mwanzo kunoa shoka langu.

7. Whatever you are, be a good one.
Chochote utakachoamua kuwa, kuwa bora.

SOMA; Mambo 10 Usiyojua Kuhusu Vatican.

8. No man is good enough to govern another man without the other's consent.
Hakuna mtu mwenye uwezo wa kumtawala mwingine bila ya uamuzi wake.

9. Better to remain silent and be thought a fool than to speak out and remove all doubt.
Ni bora kukaa kimya na kufikiriwa kwamba ni mpumbavu, kuliko kuongea na kudhihirisha kwamba kweli ni mpumbavu.

10. Things may come to those who wait, but only the things left by those who hustle.
Vitu vinaweza kuja kwa kwa wale wanaosubiri, ila vitakuwa ni vitu ambavyo vimeachwa na wale wanaopambana.

NYONGEZA… NA AMBAYO NAIPENDA SANA…

The things I want to know are in books; my best friend is the man who'll get me a book I ain't read.
Vitu ninavyotaka vipo kwenye vitabu; rafiki yangu wa kweli ni yule atakayenipa kitabu ambacho sijakisoma.

Fanyia kazi kauli hizi kumi na uweze kuboresha maisha yako zaidi.

SOMA; Mambo Matano Yatakayotokea Utakapoanza Tabia Ya Kujisomea.

Monday, January 26, 2015

Kauli Kumi Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Mahatma Gandhi.

Mahatma Gandhi alikuwa mpigania uhuru wa nchi ya India. Aliweza kuongoza harakati za kuipatia India uhuru kutoka kwa waingereza na alikuwa akitumia njia za amani katika harakati zake.

Mahatma Gandhi amekuwa akiwahamasisha wengi sana kwa maisha aliyoishi na harakati alizofanya na jinsi alivyoleta mabadiliko makubw akwenye nchi yake na dunia kwa ujumla.

Leo hapa utazipitia kauli kumi za kukuhamasisha kutoka kwake.

1. Happiness is when what you think, what you say, and what you do are in harmony.
Furaha ni pale ambapo mawazo yako, maneno yako na matendo yako yanaendana.

2. You must be the change you wish to see in the world.
Kuwa mabadiliko unayotaka kuyaona duniani.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

3. We may stumble and fall but shall rise again; it should be enough if we did not run away from the battle.

Tunaweza kukwama na kuanguka lakini tutainuka tena; na inatosha kama hatutayakimbia mapambano.

4. It is health that is real wealth and not pieces of gold and silver.

Afya ndio utajiri wa kweli, sio sarafu na dhahabu.

5. First they ignore you, then they laugh at you, then they fight you, then you win.

Kwanza wanakudharau, kisha wanakucheka, halafu wanakupinga, mwisho unashinda.

6. I suppose leadership at one time meant muscles; but today it means getting along with people.

Kuna kipindi uongozi ulikuwa ni nguvu; ila leo uongozi ni uwezo wa kuweza kushurikiana na watu.

SOMA; Dalili Kumi Kwamba Tayari Wewe Ni Kiongozi. 

7. You can chain me, you can torture me, you can even destroy this body, but you will never imprison my mind.

Unaweza kunifunga, unaweza kuniumiza, unaweza kuharibu mwili wangu, lakini huwezi kufunga akili yangu.

8. Live as if you were to die tomorrow. Learn as if you were to live forever.

Ishi kama utakufa kesho. jifunze kama utaishi milele.

9. You must not lose faith in humanity. Humanity is an ocean; if a few drops of the ocean are dirty, the ocean does not become dirty.

Usipoteze imani kwenye ubinadamu. Ubinadamu ni bahari, kama matone machache ya bahari hii ni machafu haimaanishi bahari nzima ni chafu.

10. The best way to find yourself is to lose yourself in the service of others.

Njia bora ya kujijua ni kujipoteza kwenye kuwahudumia wengine.

Soma kauli hizo kumi na zitumie katika maisha yako na shughuli zako za kila siku ili uweze kuboresha maisha yako.

SOMA;
Vitu VITATU Vinavyoathiri Kipato Chako Na Jinsi Ya Kukiongeza.

Thursday, January 22, 2015

Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Nelson Mandela.

Nelson Mandela alikuwa mpingaji wa sera za kibaguzi nchini Afrika ya kusini. Pia alikuwa raisi wa Afrika kusini kati ya mwaka 1994 mpaka mwaka 1999. Alifungwa jela miaka 27 kutokana na harakati zake ila hakukata tamaa, alipotoka jela aliendelea na harakati na hatimaye kuweza kuwa raisi wa taifa ambalo halina ubaguzi.

mandela

Leo tutajifunza kauli kumi kutoka kwake ambazo zitatuhamasisha kuboresha maisha yetu na ya jamii inayotuzunguka.

1. To deny people their human rights is to challenge their very humanity.

Kuwanyima watu haki zao ni kutoa changamoto kwa ubinadamu wao.

2. It always seems impossible until its done.

3. Money won't create success, the freedom to make it will.
Fedha haitatengeneza mafanikio, uhuru wa kutengeneza fedha ndio utakaoleta mafanikio.

SOMA; Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Martin Luther King

4. If you want to make peace with your enemy, you have to work with your enemy. Then he becomes your partner.
Kama unataka kuleta amani na adui yako, unahitaji kufanya naye kazi na hapo mnakuwa washirika.

5. There is no passion to be found playing small - in settling for a life that is less than the one you are capable of living.
Hakuna hamasa kwenye kufanya vitu vidogo, kwa kukubali maisha ya chini kuliko ambayo una uwezo wa kuyaishi.

6. We must use time wisely and forever realize that the time is always ripe to do right.

Ni lazima tutumie muda kwa akili na tuelewe kwamba mara zote ni muda sahihi kufanya jambo sahihi.

SOMA; Lengo Langu Kubwa Kwenye Maisha; Kuwa Rais wa Tanzania.

7. Even if you have a terminal disease, you don't have to sit down and mope. Enjoy life and challenge the illness that you have.

Hata kama una ugonjwa ambao hauwezi kupona, hutakiwi kukaa chini na kukata tamaa. Furahia maisha na toa changamoto kwa ugonjwa ulionao.

8. No country can really develop unless its citizens are educated.
Hakuna nchi inayoweza kuendelea kweli mpaka wananchi wake wawe wameelimika.

9. When the water starts boiling it is foolish to turn off the heat.
Wakati maji yanaanza kuchemka ni upumbavu kuzima moto.

10. Only free men can negotiate. A prisoner cannot enter into contracts.

Ni mtu huru pekee anayeweza kujadili. Mfungwa hawezi kuingia mkataba.

Pitia kauli hizi kumi na zitakuhamasisha kufanya zaidi ili uweze kufikia mafanikio.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

Tuesday, January 20, 2015

Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Martin Luther King

Martin Luther King Jr alikuwa mpigania haki za watu weusi nchini marekani. Huyu ni mmoja wa watu ambao walikufa wakipigania usawa baina ya binadamu wote. Kazi yake kubwa liyoifanya imeacha alama kubwa na leo tunaishi kwenye dunia ambayo ubaguzi wa rangi sio tatizo kubwa tena.

images

Hapa nimekukusanyia kauli Kumi za Martin Luther King ambazo zitakuhamasisha kuchukua hatua;

1. Darkness cannot drive out darkness; only light can do that. Hate cannot drive out hate; only love can do that.

Giza haliwezi kuondoa giza; ni mwanga pekee unaoweza kuondoa giza. Chuki haiwezi kuondoa chuki; upendo ndio unaoweza kuondoa chuku.

2. Faith is taking the first step even when you don't see the whole staircase.

Imani ni kupiga hatua ya kwanza hata kama huoni ngazi nzima.

SOMA; UKURASA WA 18; Hakuna Anayejali Maisha Yako Zaidi Yako Mwenyewe.

3. The ultimate measure of a man is not where he stands in moments of comfort and convenience, but where he stands at times of challenge and controversy.

Kipimo kizuri cha mtu sio pale aliposimama wakati wa raha na mafanikio bali pale aliposimama wakati wa shida na kushindwa.

4. The time is always right to do what is right.

Mara zote muda ni sahihi kufanya kile ambacho ni sahihi.

SOMA; Naomba Ufanye Changamoto Hii Ya Siku Kumi, Utabadili Sana Maisha Yako.

5. In the End, we will remember not the words of our enemies, but the silence of our friends.

Mwisho hatutakumbuka maneno ya maadui zetu, bali ukimya wa rafiki zetu.

6. I have decided to stick with love. Hate is too great a burden to bear.
Nimeamua kung’ang’ania upendo. Chuku ni mzigo mzito sana ambao siwezi kuvumilia.

7. We must learn to live together as brothers or perish together as fools.

Ni lazima tujifunze kuishi pamoja kama ndugu au tuangamia pamoja kama wapumbavu.

8. Our lives begin to end the day we become silent about things that matter.

Maisha yetu yanaanza kuisha pale tunapokaa kimya kwa mambo ambayo ni muhimu kwetu.

SOMA; Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.

9. Freedom is never voluntarily given by the oppressor; it must be demanded by the oppressed.

Uhuru kamwe hautolewi kwa hiari na mkandamizaji; bali unachukuliwa kwa kutaka kwa kandamizwaji.

10. Law and order exist for the purpose of establishing justice and when they fail in this purpose they become the dangerously structured dams that block the flow of social progress.

Sheria na taratibu zimewekwa kwa ajili ya kuanzisha haki na usawa na zinaposhindwa kutimiza lengo hilo zinakuwa hatari na kuzuia maendeleo ya kijamii.

Naamini umejifunza vitu muhimu kuhusu maisha kupitia kauli hizi kumi. Anza kufanyia kazi ili kuboresha maisha yako.

Makirita Amani,

makirita@gmail.com