Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, July 15, 2015

UKURASA WA 196; Kama Huwezi Kujibu Swali Hili Hujui Maisha Yako Yanakoelekea.

Siku zote huwa nasema kwamba kuna ‘emergency’ chache sana kwenye maisha. Ile hali kwamba jambo limetokea na watu wanashangaa limetokeaje ni kuamua tu kutumia unafiki wetu wenyewe.
Ni sawa na shimo ambalo lipo njiani kwa muda mrefu lakini watu wanaliangalia tu, siku moja linasababisha vifo watu wanasema ni ajali. Hapana sio ajali, ni watu wamechagua kufa kwa njia hiyo. Kwa sababu shimo lilikuwa linaonekana siku zote, lakini hakuna aliyejali.
Hivyo hivyo kwenye maisha yako, kuna vitu vingi sana ambavyo unavipuuzia kwa sasa lakini kuna siku vitakukaba sana. Na wakati huo ndio utaanza kuhangaika, utaanza kusumbua wengine kwamba kwa nini hawachukulii hali yako kwa tahadhari. Bila ya wewe kujua na kukubali kwamba hakuna tahadhari kubwa ila ni kitu ulichotengeneza wewe mwenyewe.
Kila siku inayoanza jiulize swali hili muhimu sana, je mambo haya ninayofanya leo hayatengenezi tahadhari siku ya kesho? Au siku zijazo? Mambo ninayoyapuuza leo hayajitengenezi na kuwa makubwa halafu siku moja yakanizidi?
Ni kawaida ya binadamu kufanya vitu kwa mazoea ila mambo yanapokuwa magumu tunasahau kwamba tumeyatengeneza wenyewe. Na kama wewe ni mtu wa kulaumu utaanza kulaumu na uzuri ni kwamba hutakosa mtu wa kumlaumu.
Hakuna kitu kinachokea kwa ajali kwenye maisha yako, kila kitu kinasababishwa na wewe mwenyewe ndiye unayesababisha. Kuwa makini na yale yote unayofanya, yanaweza kukusababishia matatizo makubwa siku za mbeleni.
TAMKO LA LEO;
Najua chochote ninachofanya leo kina madhara kwenye maisha yangu siku za baadae. Madhara haya yanaweza kuwa chanya au kuwa hasi. Nitahakikisha maamuzi ninayofanya hayanipelekei kwenye madhara hasi ili niepuke kuwa na dharura zisizo za msingi kwenye maisha yangu.
Tukutane kwenye ukurasa wa 196 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment