Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, January 3, 2015

Hii Ni Kazi Yenye Malipo Makubwa Sana Ambayo Unaweza Kujifunza Kuifanya

Kazi yenyewe ni kufikiri vizuri(GOOD THINKER)
Kwa nini ni muhimu sana wewe kuwa mtu wa kufikiria(GOOD THINKER)
1. Watu wanaofikiria wanahitajika sana, mtu anayejua JINSI YA KUFANYA hakosi kazi, ila anayejua KWA NINI INAFANYWA anakuwa bosi wake.
2. Watu wanaofikiri wanatatua matatizo na hawakosi mawazo ya kujenga taasisi.
3. Watu wanaofikiri ni vigumu kujikuta kwenye matatizo yanayosababishwa na watu wengine. Ni vigumu watu kuweza kuwatumia kwa faida zao wenyewe.
Adolf Hitler amewahi kunukuliwa akisema; ni raha iliyoje kwa watawala kwamba watu hawafikiri.
Kuna aina kumi na moja za kufikiri ni muhimu sana kuzingatia zote maana kila moja ina umuhimu wake ili uweze kufikia mafanikio.
1. Kufikiria kwa pica kubwa
2. Kufikiria kwa kuepuka usumbufu
3. Kufikiria kwa ubunifu
4. Kufikiria kwa uhalisia
5. Kufikiria kimkakati
6. Kufikiria kwa uwezekano
7. Kufikiria kwa kutafakari yaliyopita
8. Kufikiria kwa umaarufu
9. Kufikiria kwa kushirikiana
10. Kufikiria kwa kuepuka ubinafsi
11. Kufikiria kwa undani.
Uanzie wapi ili na wewe uwe mtu wa kufikiri
1. Soma vitabu, majarida na vitu vingine vitakavyokuongezea ufahamu.
2. Kaa na watu ambao nao wanafikiria.
3. Andika mawazo yanayokuja kichwani kwako. Njia rahisi ni kuandika mawazo kumi kila siku.
Ukifanya hivi utakuwa kiwanda cha kuzalisha mawazo mazuri na utakuwa wa thamani sana.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment