Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, January 30, 2015

Hakuna Kitu Chenye Maana...

Hakuna kitu chenye maana duniani,
Ila sisi wenyewe ndio tunavipa vitu maana.
Ukiweza kulijua hili, utajipunguzia matatizo mengi sana.
Kwa mfano kama unaona dhahabu ina maana, kuliko shaba, kumbuka vyote hivi ni madini ambayo yanapatikana kwenye ardhi. Tumeweka maana kubwa kwenye dhahabu kwa sababu haipatikani kirahisi kama shaba.
Kama nyama choma ni chakula cha maana, kumbuka huyu ni mnyama ambaye ameuawa na kuchomwa, hiyo maana nyingine tumeweka wenyewe.
Kama unaona pombe na mivinyo ya bei kali ni vitu vya maana, kumbuka haya ni matunda yaliyochachishwa, lakini sisi tumevipa maana.
Kitu chochote ambacho kina maana au kina thamani kubwa, hakijajipa thamani hiyo chenyewe.
Thamani hiyo tumevipa sisi wenyewe, hivyo usikubali kuteseka kwa sababu unaona huna vitu hivyo.
Chagua ni vitu gani cya maana kwako na vifanyie kazi.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment