Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, January 20, 2015

Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Martin Luther King

Martin Luther King Jr alikuwa mpigania haki za watu weusi nchini marekani. Huyu ni mmoja wa watu ambao walikufa wakipigania usawa baina ya binadamu wote. Kazi yake kubwa liyoifanya imeacha alama kubwa na leo tunaishi kwenye dunia ambayo ubaguzi wa rangi sio tatizo kubwa tena.

images

Hapa nimekukusanyia kauli Kumi za Martin Luther King ambazo zitakuhamasisha kuchukua hatua;

1. Darkness cannot drive out darkness; only light can do that. Hate cannot drive out hate; only love can do that.

Giza haliwezi kuondoa giza; ni mwanga pekee unaoweza kuondoa giza. Chuki haiwezi kuondoa chuki; upendo ndio unaoweza kuondoa chuku.

2. Faith is taking the first step even when you don't see the whole staircase.

Imani ni kupiga hatua ya kwanza hata kama huoni ngazi nzima.

SOMA; UKURASA WA 18; Hakuna Anayejali Maisha Yako Zaidi Yako Mwenyewe.

3. The ultimate measure of a man is not where he stands in moments of comfort and convenience, but where he stands at times of challenge and controversy.

Kipimo kizuri cha mtu sio pale aliposimama wakati wa raha na mafanikio bali pale aliposimama wakati wa shida na kushindwa.

4. The time is always right to do what is right.

Mara zote muda ni sahihi kufanya kile ambacho ni sahihi.

SOMA; Naomba Ufanye Changamoto Hii Ya Siku Kumi, Utabadili Sana Maisha Yako.

5. In the End, we will remember not the words of our enemies, but the silence of our friends.

Mwisho hatutakumbuka maneno ya maadui zetu, bali ukimya wa rafiki zetu.

6. I have decided to stick with love. Hate is too great a burden to bear.
Nimeamua kung’ang’ania upendo. Chuku ni mzigo mzito sana ambao siwezi kuvumilia.

7. We must learn to live together as brothers or perish together as fools.

Ni lazima tujifunze kuishi pamoja kama ndugu au tuangamia pamoja kama wapumbavu.

8. Our lives begin to end the day we become silent about things that matter.

Maisha yetu yanaanza kuisha pale tunapokaa kimya kwa mambo ambayo ni muhimu kwetu.

SOMA; Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.

9. Freedom is never voluntarily given by the oppressor; it must be demanded by the oppressed.

Uhuru kamwe hautolewi kwa hiari na mkandamizaji; bali unachukuliwa kwa kutaka kwa kandamizwaji.

10. Law and order exist for the purpose of establishing justice and when they fail in this purpose they become the dangerously structured dams that block the flow of social progress.

Sheria na taratibu zimewekwa kwa ajili ya kuanzisha haki na usawa na zinaposhindwa kutimiza lengo hilo zinakuwa hatari na kuzuia maendeleo ya kijamii.

Naamini umejifunza vitu muhimu kuhusu maisha kupitia kauli hizi kumi. Anza kufanyia kazi ili kuboresha maisha yako.

Makirita Amani,

makirita@gmail.com



Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment