Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, January 19, 2015

Naomba Ufanye Changamoto Hii Ya Siku Kumi, Utabadili Sana Maisha Yako.

Binadamu tunapenda kulalamika sana na hata kuwalaumu wengine. Hakuna mtu anayependa aonekane kwamba yeye ndio amechangia kusindwa kwa jambo fulani. Hivyo katika jambo lolote lile linalotokea watu hukimbilia kumtafuta mchawi, yaani mtu wa kulaumu.

SOMA; Haya Ni Maajabu Ya Dunia Ambayo Unayafanya Kila Siku.

Sasa kwa tabia hii ya kulalamika na kulaumu inakurudisha sana wewe nyuma katika maendeleo ya maisha yako.

Huwezi kufikia mafanikio kama kila mara wewe ni mtu wa kulalamika na kulaumu wengine.

Leo hii nataka ufanye changamoto moja ambayo itakuwezesha kuondokana na tabia hii ili uweze kufikia mafanikio.

SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.

Kwa siku kumi kuanzia leo, jiepushe kulalamika au kumlaumu yeyote. Hakikisha siku nzima imesiha bila ya kulalamika au kulaumu. Ikitokea umefanya siku ya kwanz aila ya pili ukajisahau na kulalamika, unafuta na kuanz atena upya. Endelea hivi mpaka siku kumi ziishe bila ya kulalamikia kitu chochote.

Pia katika siku hizi kumi usimseme mtu kwa jambo lolote baya, yaani usisengenye, usishiriki majungu na wala usifanye umbea. Hizi ni tabia ambazo zinakurudisha sana nyuma.

SOMA; Huu Ndio Ushauri Muhimu Sana Wa Kuishi Nao Kila Siku Kwenye Maisha Yako.

Fanya changamoto hii na kama ukifanikiwa kukamilisha siku kumi nitumie email kwenye makirita@kisimachamaarifa.co.tz kunijulisha umeionaje hali hiyo na pia nitakuwa na zawadi nzuri kwako.

Na changamoto ianze, tutakutana upande wa pili, KARIBU SANA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

1 comments:

  1. japhetandrea@688gmail.com.fone+255755057039.0735557039

    ReplyDelete