Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, January 28, 2015

Kauli Kumi Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Abraham Lincoln

Abraham Lincoln (February 12, 1809 – April 15, 1865) alikuwa raisi wa 15 wa marekani. alianza kipindi chake cha uraisi March 1861 mpaka alipouawa April 1865. Lincoln aliongoza marekani katika kipindi cha vita ambayo ilikuwa changamoto kubwa kwake. Katika vita hii aliweza kuimarisha muungano wa majimbo ya marekani, kutokomeza utumwa na kuimarisha uchumu.

Leo utajifunza kauli kumi kutoka kwake ambazo zitakuhamasisha wewe kuchukua hatua na kuboresha zaidi maisha yako na ya wale ambao wanakuzunguka.

1. In the end, it's not the years in your life that count. It's the life in your years.
Mwishoni sio miaka ya maisha yetu itakayohesabika bali maisha ya miaka yetu ndio itakayohesabika.

SOMA; Viongozi 100 Walioibadili Dunia.

2. Most folks are as happy as they make up their minds to be.
Watu wengi wanafuraha kama walivyozifanya akili zao kuwa hivyo.

3. Nearly all men can stand adversity, but if you want to test a man's character, give him power.
Karibu kila mtu anaweza kuvumilia matatizo, ila kama unataka kupima tabia ya mtu, mpe nguvu(uongozi)

4. Always bear in mind that your own resolution to succeed is more important than any other.
Kila mara kumbuka kwamba uamuzi wako wa kufanikiwa ni muhimu kuliko kitu kingine chochote.

abraham-lincoln-quote-5

SOMA; Watu Watatu(3) Waliofukuzwa Kwenye Kampuni Walizoanzisha Wenyewe.

5. The best thing about the future is that it comes one day at a time.
Uzuri wa baadae ni kwamba inakuja siku baada ya siku.

6. Give me six hours to chop down a tree and I will spend the first four sharpening the axe.
Nipe masaa sita ya kukata mti na nitatumia masaa manne ya mwanzo kunoa shoka langu.

7. Whatever you are, be a good one.
Chochote utakachoamua kuwa, kuwa bora.

SOMA; Mambo 10 Usiyojua Kuhusu Vatican.

8. No man is good enough to govern another man without the other's consent.
Hakuna mtu mwenye uwezo wa kumtawala mwingine bila ya uamuzi wake.

9. Better to remain silent and be thought a fool than to speak out and remove all doubt.
Ni bora kukaa kimya na kufikiriwa kwamba ni mpumbavu, kuliko kuongea na kudhihirisha kwamba kweli ni mpumbavu.

10. Things may come to those who wait, but only the things left by those who hustle.
Vitu vinaweza kuja kwa kwa wale wanaosubiri, ila vitakuwa ni vitu ambavyo vimeachwa na wale wanaopambana.

NYONGEZA… NA AMBAYO NAIPENDA SANA…

The things I want to know are in books; my best friend is the man who'll get me a book I ain't read.
Vitu ninavyotaka vipo kwenye vitabu; rafiki yangu wa kweli ni yule atakayenipa kitabu ambacho sijakisoma.

Fanyia kazi kauli hizi kumi na uweze kuboresha maisha yako zaidi.

SOMA; Mambo Matano Yatakayotokea Utakapoanza Tabia Ya Kujisomea.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment