Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, January 31, 2015

Huu Ni Mwaka Wa Kuacha Unafiki...

Umefika wakati wa kuacha unafiki..
Maana kuendelea na unafiki huu hakuwezi kukusaidia tena.
Swali la msingi; wakati unazaliwa au unakua ni nani alikuambia maisha yatakuwa rahisi? Kwamba utapata kila kitu kwa urahisi? Kwamba kutakuwa na njia za mkato za wewe kupata unachotaka?
Hakuna popote umewahi kuambiwa hivi.
Lakini kwa unafiki umeamua kulalamikia mambo hayo.
Kwamba maisha ni magumu, kwamba hupati njia ya mkato ya kufikia mafanikio.
Achana na unafiki huu,
Maisha ni magumu ndio, lakini ugumu wa maisha ndio unayafanya yawe mazuri kuishi.
Hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio, na kutokuwepo kwa njia hii ndio kunafanya safari ya kuelekea kwenye mafanikio kuwa nzuri.
Furahia kila hatua ya maisha yako.
Jifunze kutokana na changamoto unazopitia.
Acha kulalamika.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment