Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, July 17, 2015

UKURASA WA 198; Tuko Upande Mmoja.

Katika shule moja kulikuwa na kundi la wanafunzi watukutu ambao walikuwa wakionea wanafunzi wenzao. Wanafunzi hao walikuwa wakikuta mwanafunzi mwingine wanamlazimisha achague wa kupigana naye na akikataa wanampiga wote.
Siku moja kundi hili walikutana na mwanafunzi mmoja aliyeonekana kuwa mnyonge sana. Wakamwambia achague wa kupigana naye. Yule mwanafunzi akachora mstari na kusema yule ambaye anajiona ndio mbabe kuliko wote avuke huu mstari. Yule ambaye ndio alikuwa mbabe alivuka mstari ule na alipofika upande wa pili yule mwanafunzi mnyonge alimwambia sasa tupo upande mmoja, tuungane kupambana na hao wengine.
Maisha ndivyo yalivyo, sisi wote tuko upande mmoja. Na watu wote wanaokuzunguka mpo nao upande mmoja. Sema watu hatuelewi hili na ndio maana tumekuwa tunashindana lakini hatufiki mbali.
Kama wanandoa wangejua kwamba wapo upande mmoja, wa kutaka maisha yao wote kuwa bora basi matatizo mengi sana ya ndoa yasingekuwepo na ndoa zingedumu.
Kama mwajiri na mwajiriwa wangejua wapo upande mmoja, kunufaisha kazi yao na maisha yao kwa ujumla, basi kungekuwa na ufanisi mkubwa sana kwenye eneo la kazi.
Kama mfanyabiashara na mteja wake wangejua kwamba wapo upande mmoja basi biashara zingeendeshwa kwa mafanikio makubwa kwa wote wawili.
Lakini mara nyingi tunafikiri kwamba tuko pande tofauti na hivyo kuishia kushindana, mashindano ambayo hayamfaidishi hata mmoja wetu.
TAMKO LA LEO;
Najua kwamba wale wote ambao wamenizunguka tupo upande mmoja. Mwenza wangu, wateja wangu, mwajiri/mwajiriwa wangu wote tupo upande mmoja. Kila mara nitajitahidi kuelewa upande tuliopo ili iweze kutusaidia kuboresha maisha yetu sote.
Tukutane kwenye ukurasa wa 199 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment