Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, July 14, 2015

UKURASA WA 195; Dunia Inapenda Washindi, Usiumizwe Na Hilo.

Wakati unaweka juhudi za ziada zaidi ya wengine hakuna atakayekutukuza, na wengine wengi watakukatisha tamaa.
Wakati wewe unafanya kazi wakati wengine wamepumzika, wanastareheka hakuna atakayekuwa anakumulika, na wanaojua watakuwa wanakubeza na kukuona hujui unachofanya.
Kama utaendelea kung’ang’ana na kuweka juhudi licha ya watu kukususa na wengine kukukatisha tamaa, unajua ni nini kitatokea?
Mambo yako yatakuwa mazuri, utaanza kupata majibu tofauti na wengine wanayopata, kila mtu ataanza kuona mafanikio yako. Na wakati huu unajua ni kitu gani kitatokea?
Kila mtu ataanza kukutukuza, kukusifu, huyu hakukata tamaa. Na wanaokujua wataanza kusema tulijua tu atafika mbali, wakati hakuna hata siku moja wamekutia moyo.
Je utawachukia watu hawa kwa sababu ni wanafiki, wanakusifia wakati tu umefikia mafanikio? Hapana usifanye hivyo, sio kosa lao, ndivyo dunia ilivyowatengeneza. Dunia inapenda washindi, dunia haina muda na wanaoteseka, wanaokazana na ukishindwa ndio kabisa utakuwa mfano wa kuwatisha wengine.
Ufanye nini sasa? Endelea kuweka juhudi, endelea kushinda. Hata pale wanapokusifia usione ndio umefika mwisho, wacha wao waendelee kutoa sifa, na wewe endelea kuweka juhudi.
TAMKO LA LEO;
Najua dunia inapenda washindi. Hainisumbui kama sasa hivi hakuna anayeniona pamoja na juhudi kubwa ninazoweka. Na hata nitakapofikia mafanikio na waliokuwa wa kwanza kunicheka wakawa ndio wa kwanza kusema walijua nitafanikiwa pia halitakuwa tatizo kwangu. Mimi nitaendelea kuweka juhudi bila ya kujali watu wanasema nini.
Tukutane kwenye ukurasa wa 196 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment