Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, February 13, 2015

UKURASA WA 44; Usiondoe Macho Kwenye Zawadi…

Vikwazo ni kile unachokiona pale unapoondoa macho yako kwenye malengo yako.

Kauli hii ni ya kweli kabisa. Unapoacha kuangalia kile unachotaka, unapoacha kuweka msisitizo kwenye kile unachotaka kupata ndio unaanza kuona vikwazo, ndio unapoanza kuona changamoto na ndio unapoanza kupata mawazo ya kukata tamaa.

Kama kweli unataka kupata unachotaka, fanya maamuzi ya kutoangalia kitu kingine chochote, angalia kile unachotaka tu. Kwa kufanya hivi hata utakapokutana na vikwazo itakuwa rahisi kwako kupata ufumbuzi na kuendelea kusonga mbele.

Maana hakuna kikwazo kisichokuwa na ufumbuzi, hakuna mafumu yasiyokuwa na mwisho.

SOMA; Huu Ndio Ushauri Muhimu Sana Wa Kuishi Nao Kila Siku Kwenye Maisha Yako.

Lakini kama utaanzakupepesa macho yako, na kuangalia vitu vingine, utaanza kuona vitu vingine ni bora kuliko unachofanya na utashawishika kuacha unachofanya na kwenda kufanya hivyo ulivyoangalia.

Utastuka pale utakapoanza kuvifanya na kugundua kwamba vina changamoto pia.

TAMKO LA LEO;

Nitaweka macho yangu, akili yangu na nguvu zangu zote kwenye malengo yangu. Sitapoteza muda wangu kuangalia mambo mengine maana kwa kifanya hivi naweza kushawishika kuacha malengo yangu na kuparamia vitu vingine ambavyo vitanifanya nishindwe.

SOMA; UKURASA WA 20; Geuza Changamoto Kuwa Fursa.

Tukutane kwenye ukurasa wa 45 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

 

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment