Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, February 15, 2015

UKURASA WA 46; Kuwa Mtaalamu Uliyebobea..

Katika fani yoyote ile, watu wanaolipwa sana au wanaopata kipato kikubwa ni wale ambao ni wataalamu sana na waliobobea.

Hawa ni watu ambao wamechagua kufanya kitu na kujifunza kuhusu kitu hiko nje ndani.

Wanajua mbinu zote za kuweza kufanya kazi iliyobora na wakitoa kazi yao kila mtu anaifurahia na kuipenda.

Hawa ni watu ambao wakigusa kitu kinabadilika, kama ni jiwe linakuwa dhahabu.

SOMA; UKURASA WA 14; Kataa Kupokea Chochote Kizuri, Na Kubali Hiki…

Hawa ni watu ambao mtu yeyote mwenye shida hafikirii kutafuta mtu mwingine bali wao.

Unapokuwa mtaalamu, unapobobea kila mtu atataka kufanya kazi na wewe, kila mtu atataka kupata huduma au bidhaa unayotoa.

Kwa chochote unachofanya, iwe ni kazi au biashara hakikisha unaijua vizuri kushinda mtu mwingine yeyote duniani, na unaifanya kwa ubora wa kipekee kuliko mtu yeyote alivyowahi kuifanya dunia nzima. Sitanii, namaanisha dunia nzima uwe wewe tu unayetoa unachotoa, na inawezekana kama ukianza leo.

SOMA; KAWAIDA Ni Tafsida Ya HOVYO…

TAMKO LA LEO;

Naamua kuwa mtaalamu niliyobobea kwenye hiki ninachofanya. Nitaijua kazi/biashara hii kwa undani na nitatumia ujuzi wangu kutoa huduma/bidhaa ambayo ni bora sana kwa yule anayekwenda kuitumia. Nitahakikisha mtu hawezi kupata huduma hii sehemu nyingine yoyote, ila kwangu tu.

Tukutane kwenye ukurasa wa 47 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment