Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, February 16, 2015

UKURASA WA 47; Kuwa Na Subira, Hakuna Unachopoteza.

Wenye busara walisema; haraka haraka haina baraka.

Hawakuishia hapo, waksema tena, pole pole ndio mwendo.

Lakini dunia ya sasa inatufanya tuone tuna busara zaidi, kwamba hatuna muda wa kusubiri, nataka hiki na nakitaka sasa hivi. Huku ni kujidanganya.

Kwa sababu mwaka huu 2015 umeamua kubadili maisha yako haimaanishi utaanza kuona matokeo mara moja, itakuchukua miezi na hata miaka ndio uone kile ambacho unakitaka.

SOMA; UKURASA WA 07; Uvumilivu Ni Nguzo Muhimu.

Usilazimishe mambo, kwa kufanya hivyo utajiondoa kabisa kwenye njia inayokupeleka kwenye mafanikio.

Kama ambavyo mwanamke atachukua ujauzito kwa miezi tisa ndio aweze kuzaa mtoto mwenye afya nzuri na anayeweza kuhimili hali ya dunia. Na kama ilivyo kwmaba huwezi kuharakisha mchakato wote huu wa ujauzito mpaka kupatikana kw amtoto. Ndivyo ilivyo kwmaba mafanikio yanakuja kwa wakati sahihi, kama utaendelea kufanya kile kilicho sahihi bila ya kuacha.

Unahitaji subira kubwa na uvumilivu pia ili uweze kupata unachotaka.

TAMKO LA LEO;

Najua ninahitaji subira ili niweze kupata kile ninachotaka. Najua siwezi kuharakisha sana bila ya kuleta madhara. Nitaendelea kufanya kile ambacho ni sahihi, nitaendelea kuweka juhudi na maarifa, nitaendelea kuwa mwaminifu na nitaendele akupenda kile ninachofanya. Kwa kufanya hivi bila kuchoka najua ya kwamba mafanikio yatakuja kwa wakati wake yenyewe.

Tukutane kwenye ukurasa wa 48 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Njia TATU Za Kufanya Moto Wa Ujasiriamali Uendelee Kuwaka Kwenye Nafsi Yako…

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment