Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, February 2, 2015

#HADITHI_FUNZO; Dakika Ya Mwisho Kabla Ya Kufa…

Mtu mmoja alikuwa akipita msituni na hamadi akakutana na chui mkali.  Ili kuokoa maisha yake alikimbia sana. Kwa mbio zake alijikuta kwenye kona ya mteremko mkali sana. Palikuwa na mzabibu uliokuwa unaning’inia kwenye mteremko ule na hivyo akaninginia nao.

SOMA; Kitu Kimoja Cha Kufanya Kila Siku Ili Ufikie Malengo Yako 2015…

Akiwa pale na kujua ndio mwisho wa maisha yake aliona panya wakimega mzabibu ule. Alipoangalia kwa karibu aliziona zabibu, alichuma chache na kuweka mdomoni mwake. Zilikuwa zabibu tamu sana.

Tunajifunza nini kwenye hadithi hii?

1. Hata pale unapofikia wakati wa mwisho kabisa na ukaona hakuna tumaini tena, endelea kuishi maisha yako.

2. Tafuta kitu kizuri hata kama upo katika hali ngumu kiasi gani.

Unaweza kuongeza vingine ulivyojifunza kwenye maoni hapo chini.

SOMA; Je Upo Tayari Kupata Unachotaka? Siri Ni Hii Moja…

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment