Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, February 1, 2015

Kitu Kimoja Cha Kufanya Kila Siku Ili Ufikie Malengo Yako 2015…

Mpaka sasa umeshajifunza mbinu nyingi sana za kukuwezesha kufikia malengo uliyojiwekea kwa mwaka huu 2015.

Kama una malengo na mipango tayari ni muhimu sana kutumia yale unayojifunza ili uweze kufikia malengo yako.

Mpaka kufikia leo kuna watu ambao tayari wameshasahau malengo waliyokuwa wamejiwekea kwa mwaka huu 2015. Hii inatokana na kuweka malengo kishabiki na kutokufuata kanuni muhimu z akuweza kuyafikia.

SOMA; Sababu 10 Kwa Nini Hutafikia Malengo Yako 2015.

Ili uweze kufikia malengo yako unahitaji kuyafanya yawe kwenye akili yako kila siku na kila mara. Bila ya kujali ni hali gani unayopitia hutakiwi kuondoa mawazo yako kwenye malengo yako.

Leo utajifunza mbinu moja muhimu sana itakayokuwezesha kuyaweka malengo yako kwenye akili yako kila mara.

Mbinu hii ni kujiwekea utaratibu wa kuandika malengo yako kila siku asubuhi kabla ya kuianza siku yako. Yaani kila siku unapoamka andika malengo yako makubwa kwenye karatasi(ni vyema ukawa na kitabu) na tarehe ambazo utakuwa umefikia malengo hayo.

SOMA; Kozi 1100 Unazoweza Kujifunza Bure Kupitia Mtandao.

Kwa kufanya hivi utaianza siku yako kwa kufikiria ni nini cha kufanya ili uweze kufikia malengo hayo. Malengo yako yanakuwa kwenye akili yako muda wote na inakuwa rahisi kwako kuziona fursa za kukuwezesha kufikia malengo hayo.

Kumbuka kila siku kuandika malengo yako, haitakuchukua muda mrefu, dakika chache tu ila itakuletea faida kubwa. Usione ni kitu kidogo, kina matokeo makubwa kwako.

Nakutakia kila la kheri katika kufikia malengo yako kwa mwaka huu 2015.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Naomba Ufanye Changamoto Hii Ya Siku Kumi, Utabadili Sana Maisha Yako.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment