Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, February 25, 2015

UKURASA WA 56; Unajaribu Kumdanganya Nani?

Unajua kwamba maisha yako ni yako, na wewe mwenyewe ndio utaishi maisha hayo mpaka utakapokufa, sasa unajaribu kumdanganya nani?

Unajua kabisa kwamba kazi unayofanya huifurahii, kipato unachopata hakikutoshi, lakini unapokuwa na watu unakazana uonekane unafanya kazi muhimu, na inakupa kipato cha kutosha, unajaribu kumdanganya nani?

SOMA; UKURASA WA 18; Hakuna Anayejali Maisha Yako Zaidi Yako Mwenyewe.

Unajua kabisa kwamba biashara unayofanya inakupa changamoto kubwa, unakazana sana lakini faida unayopata ni kidogo, huna mbinu zozote za kubadili hali hiyo lakini unapokuwa na watu unakazana kuwaonesha kwamba biashara yako ni nzuri, unajaribu kumdanganya nani?

Unavaa nguo nzuri, uonekane umependeza. Unakaa na marafiki mnapiga soga, mnakunywa, unatembelea sehemu nzuri na za kifahari lakini ukirudi nyumbani hakuna amani, ukilala usiku bado unajiona ni mpweke, mtupu. Unajaribu kumdanganya nani?

SOMA; Kauli KUMI Za Kukuhamasisha Kutoka Kwa Martin Luther King

Imetosha sasa, acha kujaribu kudanganya watu, maana ukweli ni kwamba unajidanganya mwenyewe na hali hiyo haitakufikisha mbali. Maisha yako yataendele akuwa magumu na kuigiza kutakuchosha.

TAMKO LA LEO;

Naamua leo kuacha kuendelea kujaribu kuwadanganya wengine na kujidanganya mwenyewe pia. Naamua kuacha kuishi maisha ya maigizo. Naamua kuishi maisha yangu, kufanya kile ambacho napend akufanya, ambacho ni sahihi kwangu na kwa wanaonizunguka. Sitajaribu tena kuwafanya watu wanikubali, maana nitakuwa nawadanganya na kujidanganya mwenyewe.

SOMA; Katika Kula Ujana Usifanye Mambo Haya Matano, Utajutia Maisha Yako Yote.

Tukutane kwenye ukurasa wa 57 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment