Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, February 11, 2015

Mambo Yamebadilika, Hatari Sio Hatari Tena, Salama Ndio Hatari...

Kuna wakati ambapo ilikuwa inaonekana kuacha kazi na kuingia kwenye ujasiriamali ni hatari kubwa sana.
Ajira zilikuwa na usalama, angalau mtu alikuwa na uhakika wa kupata kipato cha kumtosha kuendesha maisha yake.
Ila sasa hivi mambo yamebadilika kabisa, hatari sio hatari tena, na salama imekuwa hatari, tena hatari kweli kweli.
Sasa hivi kukaa kwenye ajira na kuitegemea ajira tu ni hatari kubwa saba.
Kwanza kipato hakitoshelezi, gharama za maisha zinaongezeka kila siku.
Pili nafasi zenyewe ni finyu hivyo hakuna wa kukung'ang'ania.
Tatu hata ukiongeza juhudi kipato chako bado kinaamukiwa na mtu mwingine.
Nne unaweza kufukuzwa na ukabaki mikono mitupu.,,
Lakini ujasiriamali umekuwa salama sana.
Kwanza unakuwa na uhuru kwenye matumizi ya muda wako
Pilu unafanya kitu unachokipenda
Tatu ukiongeza juhudi na maarifa na kipato chako nacho kinaongezeka.
Nne, hakuna wa kukufukuza, labda uamue kujifukuza mwenyewe.
Je unaamua kuchagua hatari au salama?
Jibu unalo mwenyewe,
Nakutakia kila la kheri kwenye kuchagua ili uchague kilicho chema kwako.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment