Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, February 20, 2015

UKURASA WA 51; Uadilifu, Kioungo Muhimu Cha Kufikia Mafanikio.

Viungo vingine muhimu sawa na uadilifu ni KUFANYA KAZI KWA BIDII NA MAARIFA na UAMINIFU. Ukibonyeza hizo hapo chini unajifunza zaidi kuhusu viungo hivyo viwili.

SOMA; UKURASA WA 06; Kazi Ndio Msingi Wa Maendeleo.

SOMA; UKURASA WA 38; Uaminifu, Kitu Muhimu Kitakachokuwezesha Kupata Unachotaka.

Uadilifu ni kiungo muhimu sana cha wewe kuweza kufikia mafanikio katika jambo lolote unalolifanya. Kukosa uadilifu ni hatari kubwa sana kwenye maisha yako. Hii ni kwa sababu hata ukifanya kazi kwa juhudi kiasi gani unajikuta unaingia kwenye matatizo au huoni mafanikio yoyote.

Uadilifu ni pale ambapo wewe mwenyewe unakuwa na misingi yako uliyojiwekea na kuisimamia kwenye kila jambo na kila wakati. Uadilifu ni pale ambapo unafanya jambo kwa manufaa ya wengi na sio kwa manufaa yako tu.

Kama hujui uanzie wapi kuwa mwadilifu basi anza kuishi kauli hii; USIMFANYIE MWINGINE KILE AMBACHO HUNGEPENDA KUFANYIWA.

Watu wengi ambao wanaingia kwenye matatizo, watu wengi ambao wanatapeliwa, watu wengi ambao wanaua na kuuawa ukichunguza vizuri matatizo yote yanaanzia kwenye uadilifu.

Kuwa mwadilifu, weka mising yako na isimamie.

SOMA; Mwongozo Wa Kujijengea Misingi Yako Ya Kimaisha Ili Kufikia Mafanikio Makubwa.

TAMKO LA LEO;

Najua UADILIFU ni kiungo muhimu sana kwangu kufikia mafanikio. Najua kwa kukosa uadilifu hata nikiweka jitihada kiasi gani nitaendelea kuingia kwenye matatizo makubwa zaidi. Kuanzia leo naishi kwa kauli hii; SITAMFANYIA MTU MWINGINE KILE AMBACHO MIMI SIPENDI KUFANYIWA. Na kazi au biashara yoyote nitakayoifanya itakuwa ya kuwanufaisha wote wanaohusika nayo na sio kuninufaisha mimi tu.

Tukutane kwenye ukurasa wa 52 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment