Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, February 28, 2015

NENO LA LEO; Akili Ndogo, Akili za Kawaida Na Akili Kubwa.

Great minds discuss ideas; average minds discuss events; small minds discuss people. -Eleanor Roosevelt

Akili kubwa zinajadili mawazo; akili za kawaida zinajadili matukio; akili ndogo zinajadili watu.

SOMA; UKURASA WA 40; Amua Kuwa Wewe…

Je wewe unajadili nini?

Ukijikuta unajadili watu, fulani kafanya hiki, fulani kafanya kile na mengine mengi ambayo hayawezi kukusaidia jua una akili ndogo. Kwa kutumia akili hii ndogo sahau kabisa kufikia mafanikio makubwa.

Kama muda mwingi unajadili matukio, nini kimetokea, kimetokeaje, kwa nini kimetokea halafu mara nyingi matukio hayana msaada wowote kwenye malengo yako ujue unatumia akili ya kawaida. Na kama tulivyosema, KAWAIDA = HOVYO. Hivyo ukitumia akili ya kawaida unakuwa hovyo.

SOMA; KAWAIDA Ni Tafsida Ya HOVYO…

Kama muda mwingi unajadili mawazo, wazo gani zuri, jinsi gani ya kuboresha wazo lako ni wazo gani linaweza kuendana na mazingira uliyopo, unatumia akili kubwa. Na mafanikio lazima yawe yako kwa sababu mawazo ndio yanaleta mabadiliko.

Kuanzia leo amua kutokujadili watu wala matukio, JADILI MAWAZO.

Nakutakia siku njema.

SOMA; NENO LA LEO; Hapa Ndio Pa Kuanzia, Hasa kwa mwaka 2015…

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment